Ulimwengu aliponzwa na kujitapa Utustsi!!

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2009
Posts
7,375
Reaction score
6,958
Katika mambo ya kinywaji nyakati za mwanzo za utawala wa awamu ya tatu, Jeneral Twaha Ulimwengu alikuwa amekaa mahali akinywa katika kikao chake hicho alionekana kumlaumu sana Raisi wa wakati huo Ben Mkapa kwa kutomteua kuwa waziri wakati kwani wao ni marafiki wakubwa kwani hata kwenye harusi ya mtoto wa Ulimwengu, B Mkapa alikuwa MC!

Sasa kutokana na kuumia kwa kuwekwa benchi au sijui nini... Akaanza kutamka maneno haya;

Kwamba yeye hajali kitu kwani anaamini wao watutsi kunasiku wataiongoza tu dunia, kwani hata mtaji wa Magazeti yake alipewa na ndugu yake (mtutsi mwenzie) Museven rais wa Uganda kama njia ya wao kujiimarisha kutaka kuitawala kwanza Afrika mashariki.... akaenda mbali zaidi kwakusema hata jina la gazeti lake RAI lina maana ya "RWANDESE AGENCIES INTERNATIOALE"!

Sasa, kama mnavyojua bwana... kumbe UWT walikuwepo wakampelekea mkanda mzima bwana Ben Mkapa!

Nasikia Ben ali-mind mno!! Akaamua kuunyofoa uraia wa Ulimwengu!

Haya wengine kwamba ooh, waligombana kwenye pombe nasikia sio kweli... hili ndiyo msingi wa Bifu lisiloisha kati Jenerali na Ben.
Na eti Ulimwengu hatamsamehe Ben ataendelea kumponda lakini msingi wake ni kuharibiwa mpago wake wa RWANDESE AGENCIES INTERNATIOALE!! hapa Tanzania maana alikuwa karibu kabisa kuaminika hadi watu kuanza kumfikiria kuwa raisi ambalo lilikuwa lengo lake kuu!

Story ndefuee!? sorryy

........Jamani hii nimeishawahi kuisikia kama mara mbili tatu hivi kutoka kwa watu wazito tu.....kuna ukweli??!
 
RWANDESE AGENCIES INTERNATIONALE sio lazima awe mtutsi anaweza kuwa mhutu au muhtwa....huu ni udaku.Period
 
RWANDESE AGENCIES INTERNATIONALE sio lazima awe mtutsi anaweza kuwa mhutu au muhtwa....huu ni udaku.Period

Mkuu, mbona unachukulia mambo kirahisirahisi!? Ben na Ulimwengu hawajawahi kuwa marafiki? ukichunguza kwa asili Ulimwengu ni mtutsti kama alivyo raisi wa Uganda siyo mhutu. Kwani msukuma ukienda kuishi Malawi si ataitukuza Tanzania!? Vipi mzee?
 
Kwa hiyo na wewe unaendeleza ukabila. Mahakama ya Arusha inakusubiri.
 
Mimi pia ninewahi kusikia kuwa Jenerali kweli alikuja TZ na wazazi wake akiwa mdogo, ila hayo malengo yake labda wakuu wa JF watufunulie.
 
Tatizo la Jenerali Ulimwengu ni kujaribu kuicheza ngoma ambayo hakujua kiitikio chake.Ni dhahiri alikuwa na weakness zake ambazo wengine bado wanazifahamu fika.
Alimshambulia sana Ben mwanzoni mwa utawala wake akitegemea kuwa anamsingi imara nchini.
Kumuondolea uraia si tu ilishangaza wengi lakini vile vile watu kujiuliza huyu Ulimwengu ni nani?
 
Mkuu badili Nick yako uitwe MZIZI wa FITINA...
Kama unabisha basi leta proof ya hiyo narrative story yako shekhe
 
Mkuu badili Nick yako uitwe MZIZI wa FITINA...
Kama unabisha basi leta proof ya hiyo narrative story yako shekhe

Jamaa si tayari kasema kasikia mara mbili tatu kutoka kwa wakuu mtaani na akaileta hapa ili wenye data wamwage. Sasa mbona unataka kumsakama bila kosa au kosa lake hapa ni nini???? Au Ulimwengu kwenye awamu ya nne haguswi?????????????
 
Hapa ndo waafrika wenzangu wananiacha hoi...Leo wahindi, wazungu na wengineo....wanaikamua nchi/bara letu no body speaks..but somebody is busy telling us sijui wahutu..siji watutsi..and what not..Hivi hii dhambi ya sisi waafrika kuchukiana tuliitoa wapi na tutaitibu vipi? Mpaka leo tunapandikiza chuki za kubaguana kwa kutumia kigezo cha urefu wa pua zetu? if you are a mhutu, mtusi, mmatumbi, mzigua..so what? And sadly..its all over Africa..huu ubaguzi sijui utaisha vipi. But What I can be sure of: Hautusadiii lolote na unazidi kutudidimiza.

An African is the only person who is neither respected at home nor abroad. Yaani tupo tupo tuu! Hivi hii ngozi nyeusi ililaaniwa na nani? Sidhani kama Mungu alifanya hiki kitu. No way, it must be somebody else. Huyo ndo inabidi tumtafute. Ndo mbaya wetu.

Kweli inasikitisha sana kuona mpaka leo watu bado tuna mawazo mgando kama haya..Hivi mtu anayefanana na Obama anaweza kweli kuja hata kugombea ukatibu tarafa kwetu Africa?..cha kwanza tutamhukumu kwa kuangalia sura yake...Ila akiwa ngozi nyeupe..I believe he stands a better chance..ila akiwa na asili yetu..his/her chances are doomed!

Kweli wazungu wametuzidi. Africa and Africans are just a lost case! no matter how we spin it. I said it...kusudi bara letu lisonge mbele..hatuna budi wote kuteketea...vizazi vichipuke upya!

Masanja,
 

Looks like a frustrated lot!
 
Watutsi wapo Rwanda, Burundi, Tanzania, DR Congo, Uganda kama vile wadholuo (wajaluo) walivyo Tz na Kenya, wamakonde walivyo Tz na Msumbiji, wamasai walivyo Tz na Kenya, wasomali walivyo Somalia, Kenya na Ethiopia.

Ila ni kama vile unajaribu ku-justify Mkapa alivyomnyang'anya Ulimwengu uraia wa Tz. There's no such a justification in your thread.

Kweli hizo ni tetesi. Nothing else. Period.
 
Mkuu, mbona unachukulia mambo kirahisirahisi!? Ben na Ulimwengu hawajawahi kuwa marafiki? ukichunguza kwa asili Ulimwengu ni mtutsti kama alivyo raisi wa Uganda siyo mhutu. Kwani msukuma ukienda kuishi Malawi si ataitukuza Tanzania!? Vipi mzee?
tofauti ya watusti na wahutu ni ipi?
 
..inasemekana Jenerali alikuwa kwenye timu ya Kikwete wakati wa kampeni za Uraisi za 95.

..baada ya Mkapa kushinda Jenerali akahamia kambi ya ushindi ya Mkapa.

..baada ya Mkapa kuingia Ikulu, akaanza kumzawadia Jenerali kwa kumteua mjumbe ktk Tume mbalimbali zilizokuwa na ulaji mzuri kwelikweli.

..wananchi wakaanza kulalamika kulikoni Jenerali ateuliwe kwenye kila Tume ya Raisi?

..Mkapa kwa kusikiliza malalamiko hayo akaacha kumpa ulaji Jenerali.

..wakati huohuo Mkapa akaanza kucheza dili za ulaji yeye mwenyewe na washirika wake wengine.

..Jenerali akaamua kumlipizia kisasi Mkapa kwa kuanza kumshambulia kwenye magazeti yake.

..Mkapa naye akachukia akiona kwamba Jenerali hana shukurani kwa ulaji wote aliokuwa akimpa. kwa hiyo Mkapa akaamua kumlipua Jenerali ktk masuala yake ya uraia.

NB:

..kwa upande mwingine Jenerali Ulimwengu ni nani?

..hili jina halina tofauti na majina tunayotumia hapa Jamii Forums. inashangaza kidogo.

..amezaliwa wapi, amesomea wapi?

..amefanya kazi gani tangu amalize shule na ktk taasisi zipi?
 

Tatizo hapa si chuki dhidi ya kabila la kitutsi ...tatizo la watutsi ni pale wanapojifanya wao ni bora kuliko waafrika wengine..eti wao ni wazuri..wana-maumbo mazuri..pua nzuri na pia wanaasili ya wayahudi ..kwa hiyo wanapasa kutawala waafrika wengine!!...HAPO NDIYO CHUKI DHIDI YAO INAPOANZA!..na kama wataweza kulielewa hilo na kutambua kuwa ututsi ni kabila kama makabila mengine Afrika basi mambo yatakuwa mswano na yote yatatulia tuli...
 
..kwa upande mwingine Jenerali Ulimwengu ni nani?

..hili jina halina tofauti na majina tunayotumia hapa Jamii Forums. inashangaza kidogo.

..amezaliwa wapi, amesomea wapi?

..amefanya kazi gani tangu amalize shule na ktk taasisi zipi?
kuna mtu mmoja anajiita Born Agai Pargan(BAP) nadhani aanweza kuwa hata humu JF kasoma na m7,ulimwengu? na wengine nadhani atakuwa na jibu la uhakika.....

btw sidhani kama uraia wa uliwmengu kwa sasda una maana yoyote....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…