Mshana Jr Yuko Sahihi kusema kuwa Roho ni nishati hai (Living energy)....
Roho pia kwakuwa ni nishati inaweza kukuconnect na Malimwengu mengine yoyote na ndo maana katika biblia (Naitumia kama refference) utakuta katika yohana 4;24...
.
Yohana 4:24
"Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."
Pia unaweza ukafanya Rejea Ya
1 Wakorintho 15:29-53
Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania
ruʹach au neno la Kigiriki,
pneuʹma waliporejelea “roho.” Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo.
Kwa mfano, andiko la
Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho [
ruʹach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.”
Andiko la
Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho [
pneuʹma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno
ruʹach halitafsiriwi tu “roho” bali pia “nguvu” au kani ya uhai.
Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [
ruʹach] za uhai ndani yao.” (
Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.
Na Ndo maaana Muhubiri anatuambia kuwa kwa upande wa Roho na maumbile ya Roho Binadamu na Mnyama ni sawa....
Muhubiri 3:18-22
View attachment 2795289