Ulimwengu wa roho ni timilifu

Ulimwengu wa roho ni timilifu

Vyovyote iwavyo Khantwe wote tunazaliwa mara ya pili
Ufafanuzi wake huu hapa
Kwa sisi waamini wa Mungu mmoja tukifa tunaenda ama jehanam peponi(rebirth) ama kusubiri kiama (nitakufafanulia )
Na wenzetu waabudu miungu waamini katika hilo unalotaka kujua( reincarnation
Naomba upitie mada hii rebirth na reincarnation ni kitu kilekile nitakutag pia
Uncle Naona Unaongea Kwa Ushahid
 
Wacha weeehh, lkn sidhani kabla ya kuzaliwa roho ijue itazaliwa wapi, ni roho gani atakayependa aishi Tanzania, ni roho gani atapenda awe masikini, ni roho gani atapenda ainuke kimaisha na kupotea tena, ni roho gani atapenda afiwe na wazazi akiwa angali mdogo, nk nk nk. Kama roho wangekuwa na uwezo huu basi leo hii hakuna mtu ambae angekuwa anaishi maisha ya tabu kama ilivyo kwa binadamu sasa, kwani zingekataa kuingia katika miili ambayi itataabika maana hakuna apendae kuiumiza roho yake. Kama haizana uwezo huo basi tayari roho zipo limited na modificated.

Ni mawazo tu
 
Kuna watu wanaamini ukifa unazaliwa mara nyingine tena..unaweza kuzaliwa mtu yuleyule na sura ileile au kiumbe kingine. Wanadai maisha uliyoishi ndo yana-determine next life utazaliwa katika mazingira gani. Hili nimelisikia siku nyingi ila sijawahi kulitilia maanani maana mimi kwa imani yangu mtu akifa ndo mwisho wake anasubiria hukumu ni either uzima wa milele au moto wa milele lakini naona kadri siku zinavyoenda natamani kujua zaidi kuhusu hili..hii imekaaje mshana jr

ni kweli fuatilia mafundisho ya pythagoras ya transmigration of soul na re incarnation.
 
Hauna makosa! Hauna mawaa kwa kizungu tunaweza kusema no errors no faults. ...najua utasema kuwa Mungu kasema hakuna mkamilifu!

Kumbuka kasema hakuna mkamilifu la hata mmoja akimaanisha mwanadamu sio roho. Makosa ya kiutendaji,makosa binafsi, makosa ya kukusudia na kutokusudia , habari za bahati mbaya na maneno kama heri ningejua....! Haya yote si ya kiroho ni ya kimwili

Ukisoma habari za jicho la tatu, machale ,ndoto taarifa ufunuo na maono unaona kwa usahihi kabisa ulimwengu wa roho ulivyotutangulia kufahamu yajayo kabla ya nafsi zetu kupata taarifa rasmi

Kila tukio liko preplanned. Hakuna bahati mbaya, ni limitations za ufahamu tu wa kibinadamu ndio umezuiwa kuona haya
Maisha yako na yangu yako kwenye mchoro kamili tangu kuzaliwa mpaka kufa...........

Utazaliwa lini na nani utapitia nini na wapi utakutana na nani! Utakuwa nani, utafanya nini, utaanguka wapi na kusimama wapi! Yote haya hayatokei kwa bahati mbaya

Jee huu ni ubaguzi?
Kwamba mmoja tangu kuzaliwa mpaka kufa yeye ni mafanikio tu?
Kwamba tangu kuzaliwa mpaka kufa ni yeye na matatizo matatizo na yeye?

Kwamba wengine husimama na kushamiri kisha huanguka na kupotea kabisa?
Kwamba wengine hukulia kwenye shida nyingi na matatizo lakini huja kutoboa na kutoka kimaisha?

Ulimwengu wa roho hauyumbishwi...formula zake ziko kama zilivyo michoro yake ni kamili na kamilifu unapojaribu kuisahihisha na ishu za waganga nyota na ngekewa unajitafutia dhahama usiyoiweza

Utafanikiwa kwa kipindi tu lakini asili itakurudisha kwenye shina lako kiroho..pale ulipotakiwa kuwa na hapo ni sawa na kujaribu kunyoosha bati lililopinda na kupondeka

Ulimwengu wa roho hauna modifications! Ishi maisha yako ukijibidiisha na ufanyayo katika mstari sahihi...usijaribu kutoka nje ya mstari kwa kuchanganya ya rohoni na ya kidunia ...hutafika mbali
Mkuu nakufuatilia sana na upo vizuri aisee
 
YESU pekee anaweza vunja hiyo mikataba[/NI
NI KWELI NI YESU PEKEE ILA SPECIFICALLY DAMU YAKE, MAANA KATIKA MAAGANO NA MIUNGU ZILITUMIKA DAMU AITHA ZA WANYAMA, DAMU YA YESU ILIYOMWAGIKA MSALABANI NDIO NI DAMU ILETAYO UKOMBOZ(Kutoka kwenye mikataba ya laana ) na Kuweka agano jipya lililo bora zaidi.
 
Anachosema mshana jr ni kweli kulingana na bible. Biblia imeelezea predestination/kukusudiwa kimbele. Ndio maana Mungu alisema shukuruni kwa kila jambo. Liwe jema au baya tushukuru tu kwa sababu yeye ndiye kila kitu.

Ukitaka kuangalia pre destination kwenye Maisha yako chunguza hili. Ulipokuwa mtoto mdogo wakati ukikua uliwa na kupanga mambo mengi nanpengine kufikiria ungekuwa nani baadaye. Ungeoa mke yupi, watoto fulani, nyumba fulani etc.
Lakini leo almost mambo sivyo yalivyo salaaleh! Mahali ulipo hukuwahi kupawazia, status uliyonayo hukuwahi kuifikiria kabla, mke, watoto, mali na maisha kwa ujumla siyo yale uliyowazia zamani. Hii inaashiria nini??? PREDESTINATION.
Tangu unakuja Duniani ulishapangiwa njia ya kupita na huwezi kuikwepa. Hapa chini ni mfano wa pre destination unaoongelewa na Biblia:
Waefeso 1:3-5
[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;
[4]kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.
[5]Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake.

Kwa hiyo ukijiona ni mkristo leo hujifanyi hivyo, bali ulishakusudiwa hilo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Maana yake alikujua na kukuchangua kimbele ili uwe hivyo. Kwakuwa anajua mwisho kabla ya mwanzo ndio maana alikuwekea njia ya wewe kufikia kile alichokukusudia. Hilo ni kweli kabisa

kuna uchaguzi wakufanya aither uchague path of destruction (mauti) au uzima(baraka, mafanikio n.k), yote mawili yako kwenye maagano kwa hilo unapochagua agano la mauti/laana/shetani usitegee unaweza kutumia nguvu zako kubalisha chochote hata ufanye nini hutoweza, ukichagua uzima utafanikiwa tu, lakini uchaguzi unaweza kuwa ulifanya na mababu zetu na tayari uliingizwa kwenye huo mkataba hatua muhimu ni kujitoa kwenye huo mkataba ndipo uingie mkataba mpaya.
 
Bado nina safari ndefu ya nikufahamu Mshana jr, ila niaanza kukuelewa kidogo, na kama niko sahihi utakuwa mtu mzuri
 
Bado nina safari ndefu ya nikufahamu Mshana jr, ila niaanza kukuelewa kidogo, na kama niko sahihi utakuwa mtu mzuri
[emoji3] Agynasa mpendwa sijawahi kuwa mbaya ila perception ya watu kwenye hizi makala imenijengea image tofauti kabisa ....nashukuru kama umeanza kunielewa[emoji6] [emoji6]
 
Ulimwengu wa roho hauyumbishwi...formula zake ziko kama zilivyo michoro yake ni kamili na kamilifu unapojaribu kuisahihisha na ishu za waganga nyota na ngekewa unajitafutia dhahama usiyoiweza

Utafanikiwa kwa kipindi tu lakini asili itakurudisha kwenye shina lako kiroho..pale ulipotakiwa kuwa na hapo ni sawa na kujaribu kunyoosha bati lililopinda na kupondeka

Ulimwengu wa roho hauna modifications! Ishi maisha yako ukijibidiisha na ufanyayo katika mstari sahihi...usijaribu kutoka nje ya mstari kwa kuchanganya ya rohoni na ya kidunia ...hutafika mbali


Mkuu hapo nimekuelewa sana,kwa hiyo hata wale wanajitahidi kukufanyia ushirikina ili usifanikiwe maana yake wanajidanganya tu,[emoji2] [emoji2] [emoji2][emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Ulimwengu wa roho hauyumbishwi...formula zake ziko kama zilivyo michoro yake ni kamili na kamilifu unapojaribu kuisahihisha na ishu za waganga nyota na ngekewa unajitafutia dhahama usiyoiweza

Utafanikiwa kwa kipindi tu lakini asili itakurudisha kwenye shina lako kiroho..pale ulipotakiwa kuwa na hapo ni sawa na kujaribu kunyoosha bati lililopinda na kupondeka

Ulimwengu wa roho hauna modifications! Ishi maisha yako ukijibidiisha na ufanyayo katika mstari sahihi...usijaribu kutoka nje ya mstari kwa kuchanganya ya rohoni na ya kidunia ...hutafika mbali


Mkuu hapo nimekuelewa sana,kwa hiyo hata wale wanajitahidi kukufanyia ushirikina ili usifanikiwe maana yake wanajidanganya tu,[emoji2] [emoji2] [emoji2][emoji120] [emoji120] [emoji120]
Mwisho wako utasimama wewe na wao kuanguka vibaya...ila tu kama utasimama ulipo bila kujiunga katika mahangaiko yao ya visasi vijicho husuda na kutesana
 
Usiende kwa waganga! Usitafute ufumbuzi wa matatizo yako nje ya utaratibu wa kusahihisha uumbaji kama kusafisha nyota na kufanya kafara na matambiko
Laana za ukoo zinatokana na kutaka kusahihisha michoro yetu
Hapo kwenye laana za ukoo sasa mbona imani inatuambia kuwa kuna laana tulizorithi kutoka kwa mababu zetu...... utaratibu wa kujitakasa ukoje?
 
Hapo kwenye laana za ukoo sasa mbona imani inatuambia kuwa kuna laana tulizorithi kutoka kwa mababu zetu...... utaratibu wa kujitakasa ukoje?
Hizo walishamkasirisha Mungu na zitaondoka baada ya kizazi cha tatu ama cha nne.... Sanasana kinachofanyika ni kupozapoza tu kwa ibada na matambiko ya kawaida...kuendelea kufanya kafara za kuchinja ni sawa na kuzidi kuzilisha zile roho
 
Back
Top Bottom