Ulishawahi kudate na mtu ambaye hata iweje hutamani kurudiana naye?

Binti Sayuni03

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2025
Posts
1,075
Reaction score
1,913
Katika pita pita zangu nilibahatika kuwa na huyo kijana wa kisukuma kwa jina namuhifadhi, huyu kijana aliniambia yeye amesoma chuo lakini alikosa ajira kaamua kuwa dereva boda boda, mara nyingi alikuwa anafanyia online hizi uber na bolt.

Basi huyu kijana alikuwa na wivu sana nilikuwaga naenda kwake then jioni naondoka sasa nikiondoka hizo simu zitapigwa mno nikiwa njiani, hadi sasa nikaanza kumchukiaga.

Kuna siku moja nakumbuka tulipishana kitu akawa amenunua mboga kaniambia nipike mimi nikagoma nataka kuondoka eeeh! Si akanifungia mlango, nilijua utani aisee, nikawa nimekaa tukajibishana hapo akaniambia najua yeye ni nani au namchukulia poa tu anaweza akaniua na mtu yoyote asijue, kama nabisha niwaulize majirani.

Akawa amepika amekula, mimi niligoma kula, usiku tukawa tumelala si nikawa nareplay vimeseji natumiwa na watu huko online akataka kunipokonya simu nikamg'ata alooo nilipigwa bao moja zito sana hadi jicho lilivimba. Akauchukua mkono akaunyonga kwa nyuma aloooh! Nilihisi kufa hii siku na nilijuta kuzaliwa, alivyo mshenzi sasa nilikuwaga sijampa kama wiki1 hivi nilimwambia tusubiri siku hatari zipite, hii siku alitumia kama fursa akanibaka bila ridhaa yangu.

Nilimchukia mno, kulivyopambazuka nikaenda home, nilikuwa na funguo za hapo kwake kuna siku hakuwepo nikaenda nikachukuaga nguo zangu nikamwambia atafute mwengine atakaevumilia vipigo kama vile. Alilia mno meseji kama zote alinisumbua sana hata mwaka jana nakumbuka alinitafutaga, ila kamwe siwezi kurudi nyuma kwa huyu mtu hata iweje.

Sitaki kusema kuwa wasukuma wote wana tabia ya kupiga ila binafsi mwanaume kisukuma siwezi kuwa nae nawaogopa mno.

Ex, yupi huwezi kurudi kwake na kwanini??
 
Alimwagia ndani na kukukojoza? Au alikuwa goigoi kitandani
 
Siwezi kurudi kwa sababu alikuja maishani mwangu kuangamiza Maono yangu ya maisha. Nilimuacha na urembo wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…