Ulishawahi kukutana na mtu aliyevaa nguo zinazofanana na zako? How did you react to it?

Ulishawahi kukutana na mtu aliyevaa nguo zinazofanana na zako? How did you react to it?

Kuna jamaa alinipa kaunda suti yake bure anayotokelezea ofisini akasema inambana. Siku mbili badae nikasikia kwa mshikaji eti jamaa kanipa suti baada ya kuniona eti nimevaa suti kama yake halafu nimekaa chini nasuka mkeka (nabeti). Jamaa hajui kama kazi yangu ni sawa tu na yake tofauti yeye anatumia elimu. Kwa hasira na mimi nikaigawa bure suti yake kwa muuza juice ya miwa. GG ikawa imetoa tayari.
Kwani kubeti hutumii akili hahaaa
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Sio kila muda tunapaswa kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya Cold War, jeshi na ujasusi wa KGB. Leo ngoja tujadili kidogo changamoto za maisha katika jamii tunamoishi.

Eti ndugu zangu Watanzania;

HUMAN BEHAVIORAL PSYCHOLOGY.
============
Ulishawahi kukutana na mtu ghafla (kwenye sherehe, daladala au njiani) aliyevaa nguo zinazofanana na za kwako? How did you react to it? mlipungia mkono, mlipeana tabasamu, mlimfuata kumsalimia au ulikwepesha macho?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher

Huwa nguo hizo sizivai tena, hasa mashati; sasa hivi nina rekodi ya mashati zaidi ya 30 ambayo nilikumbana na mkasa huo. Huwa ninayatoa kwa ndugu zangu wa kijijini ambao zinawafit; ni nadra sana wao kukumbana na adha hiyo huko kijijini kuliko huku mijini.
 
Licha ya kukutana na mtu wa mfanano wa nguo na kuamua kuifanya nguo ya kushindia, nilipata bahati mbaya zaidi ya kuwa nakutana na watu wawili tofauti nikiwa nimevaa nguo hizo hizo mara kadhaa kwa nyakati tofauti (japo nguo hazikufanana na zao) ila watakuwa walibakiwa na maswali kadhaa vichwani mwao....
Jamaa huu ndio mtoko pekee anaoaminia?
Jamaa hii ndio kauka nikuvae?
Jamaa anafua muda gani?

Kuepusha utata Nikaamua kuzigawa kabisa nguo zenyewe.
 
nilipata bahati mbaya zaidi ya kuwa nakutana na watu wawili tofauti nikiwa nimevaa nguo hizo hizo mara kadhaa kwa nyakati tofauti (japo nguo hazikufanana na zao) ila watakuwa walibakiwa na maswali kadhaa vichwani mwao....
Jamaa huu ndio mtoko pekee anaoaminia?
Jamaa hii ndio kauka nikuvae?
Jamaa anafua muda gani?
Daaah hatari sana mkuu...
 
nlikuwa nmevaa jezi ya manchester nkakutana na jamaa kavaa jez kama yangu japo yake ilikua mikono mifupi. Nlijikuta kuna ktu kwa ndan kinanisukuma kumsalimia. mpaka leo ni jamaa yangu
 
Sikuivaa tena niligawa tangia siku hiyo sivai special ni mtumba tu.
hv maeneo/masoko gan hapa dar wana tshet & jeans/kardet orijinoza mtumba?? mana hz tshet za dukan nikifua mara 2 basi inapauka kabisa.the same to cardet/jeans
 
Mimi nina kigari changu Ki Starlet cha kunivusha hapa na pale. Basi kila nikikutana na Ki starlet njiani lazima tupigiane honi nisipoanza mimi basi mwenzangu ataanza. Sijui hii ni kwa sisi wenye starlet tu au kwa wote!!
hata ss tunaomiliki Land rover Discovery 4 na Range rover huwa tunapigiana honi pia.

-just joking-[emoji2]
 
Nafananishwa sana, nilienda polisi pale kariakoo yaani niliitwa jina afande ...... na nilihudumiwa haraka mno.

Polisi tena hapo loliondo niliitwa jina la mama fulani na kuulizwa habari za dodoma, nilihudumiwa na nauli walinipa, mmh nilivyoondoka nakasema wasije shituka duuu,

Nafananishwa siyo kawaida.
miaka ya nyuma mm ilikuwa kila nkienda mkoa fulan lazma nfananishwe na mtu. cku moja nko kwny basi kuna jamaa seat ya pemben yangu ananiuliza "ww ni fulan mwanafunz wa shule X? akat sjawah fika hata hyyo shule.
 
Back
Top Bottom