Ulishawahi kutengwa na rafiki yako wa karibu baada ya yeye kufanikiwa? Toa kisa chako ilikuwaje

Ulishawahi kutengwa na rafiki yako wa karibu baada ya yeye kufanikiwa? Toa kisa chako ilikuwaje

Zero Conscious

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2022
Posts
254
Reaction score
519
Wakuu habari za wakati huu! Nina Imani mu wazima wa afya na mnaendelea kupambana na maisha ya Kila siku. Mungu atusaidie sana.

Kama ambavyo title inajieleza, Mimi ni mtu ambae sina marafiki wengi, si kwakuwa ninajiskia sana, hapana ila ni aina ya watu ambao ninaweza kusema ni introvert. Nina marafiki wachache tu ambao nina amani sana kuwa nao.

Sasa kuna mmoja ambae ndio mtu wa karibu zaidi, jambo lake ni langu na langu ni lake, tumesaidizana kwenye nyakati ngumu na hatukuwahi kutengana kote tulikopita kama marafiki. Hatuna maisha mazuri kwakuwa bado ni vijana na tunapambana kutafuta angalau siku moja tuwe kwenye nafasi nzuri pia kimaisha.

Sasa changamoto imekuja kuonekana baada ya huyu mwenzangu kuwa amebahatika kupata chaka sehemu, yaani imekuwa si yeye ninaemfahamu tena. Kwa ukaribu wangu na yeye sidhani hata kama ni kubanana inaweza kuwa kwa mwenendo huu anaouonyesha.

Imekuwa ni mara chache sana siku hizi kuonana tena involuntarily ingawa najua yupo, na baadhi ya watu anakutana nao anapokuwa nje ya majukumu yake ila si mimi tena. Unaweza kumtumia ujumbe usijibiwe kabisa na tangu aanze kazi nakumbuka alinitumia ujumbe siku mbili tu za kwanza tangu alipoanza kazi.

Kiufupi sijapendezwa na mwenendo huo, muda mwingine asiponijibu ujumbe au simu yangu najisikia unyonge sana. Najiona kama nimepoteza nafasi kama rafiki kwake kutokana na aidha anahisi ntamlilia shida au sina msaada tena kwake. Silaumu yeye kupata kazi sababu mwisho wa siku haya ni maisha, tunatakiwa kukua kuelekea hatua nyingine. Mwenzangu katangulia ilhali wakati wangu wa milango kufunguka Bado..

It pains, kwa nyakati tulizifanikiwa kukutana tangu apate kazi anaonyesha kabisa he doesn't care about me and not interested with me anymore,, even jokes we used to make Hana response nazo kabisa. Mnaweza kuwa kwenye maongezi ghafla tu utaiskia anasema nataka niende kwa akina flani, like he's escaping me. Nimeamua kuacha kumtafuta pia sababu nishakuwa inferior kwa jinsi asivyojali tena kuhusu Mimi.

Ndipo nimepata kujifunza kuwa vitu vidogo sana huua urafiki.Si kwamba nahitaji pesa Toka kwake, it's all about value of friendship (THAMANI YA URAFIKI), Sawa naweza kukwama nikahitaji msaada kwake kama kawaida lakini si kudepend moja kwa moja kwenye kile alichonacho. Mara nyingi tu nimemshika mkono kipindi mambo yangu yanakwenda sawa, nimenusuru mahusiano yake zaidi ya mara moja, nimemvusha kifedha kipindi Mwanamke wake kalazimisha kuja ilhali hakuwa na pesa, nilimkabidhi sehemu ninayokaa Ili aenjoy na Mwanamke wake as a best friend of me. Treatment nayoipata sasa ndio inayoninyima furaha, sitegemei kama atajali tena lolote kati yangu naye. Nadhani kakutana na watu wapya, wa category yake ndio maana imekuwa hivi.

Anyway, Mi bado muangaikaji ambae siijui kesho yangu inakucha vipi ila naamini Mungu atanionyesha mlango pia. Tusiwapuuze watu tunaokuwa nao kwenye kipindi kigumu pindi tunapofunguliwa njia za mafanikio. Japo kuna ubize lakini si mbaya tukajuliana Hali tu..

Asanteni wakuu🙏, dondosha pia kisa chako
 
Kwa upande wangu wapo ambao walipofanikiwa hawakunitafuta ila kabla walikuwa nilipo wapo, na mm huwa siwakumbuki kiwepesi.

Sijui kwanini, labda kwa sababu walinitegemea zaidi ya mimi kuwategemea hivyo wanavyofanikiwa na kuondoka nakuwa sioni upungufu. Ila kwa % kubwa baada ya muda kupita huwa kunakuwa na mawasiliano yale ya hapa na pale.
 
Kaona huna jambo la msingi kaamua kuku-cut off. Unakuta story zako asubuhi hadi jioni ni mampira, pisi, pombe, movies, story za kusadikika na mambo mengine yasiyo na tija hata Mimi nakupunguza hata kama wewe mwanangu. Badala ya kumlaumu jitafakari.
 
Sasa unalalamika nini bwashee,we mwenyewe umesema kuwa ulikuwa selective kupata marafiki kwa kuwa unajiona uko kwenye rank fulani hivyo na yeye ameingia kwenye rank fulani kwa sasa hivyo ni haki yake kuwa selective na ameona wewe humfai kwa sasa.

Malipo hapa hapa duniani usikute na wewe kuna waliokuwa rafiki zake na hatimaye ukawatenga na pengine waliugulia maumivu kama unayopata wewe sasa hivi. KWENYE MAISHA JIJENGEE MAZINGIRA YA KUTAFUTWA WEWE SIO WEWE UANZE KUTAFUTA URAFIKI NA WATU.
 
Kaona huna jambo la msingi kaamua kuku-cut off. Unakuta story zako asubuhi hadi jioni ni mpira, pisi, pombe, movies, story za kusadikika na mambo mengine yasiyo na faida hata Mimi nakupunguza hata kama wewe mwanangu. Badala ya kumlaumu jitafakari.
Sawa mkuu, ila ujue katika maisha kuna vipindi pia, kama muda Bado hata mtu upambane vipi Bado kupanda inaweza kuwa ngumu. Unadhani nafanya nini hata ukinipunguza? Yaani nakosa kuwa na maana kwakuwa wewe umetangulia kupata kabla yangu?

Ni vizuri lakini Pia kwa upande wa pili ngoja nijitafakari upya mkuu
 
Mimi pia yameshanikuta hayo na sijakoma ujue now kuna mshikaji pia naishi nae gheto nikimuangalia naona ni wale wale tu
Mkuu usimfikirie vibaya, nenda nae vizuri tu kikubwa unafahamu jinsi tulivyo wanadamu. Do not expect anything from anyone to avoid disappointment. Tenda nafasi yako tu
 
Wala simalumu jamaa, wewe move on wacha kulia lia mtoto wa kiume.

Ni kawaida watu akipata nafasi mahala atakutana na watu wanao speak the same language, watu wa haiba yake. Hata sehemu za kuonana hazitakua sawa na huko awali. Kiufupi mtu akipata (hata wewe) utabadili mfumo mzima wa maisha.

Kipindi yuko maskini story zilikua za level yako na jokes za level ya kimaskini, now story zitakua tofauti tu, akija hapo aanze kuongelea story za magari, ujenzi wa nyumba na biashara zake utakuja kufungua uzi hapa kuwa jamaa anajidai (kumbe mwenzio ndio maisha yake saa hizi)

Hapo option na wewe pambana utusue, hapo mkionana mtaongea lugha moja
 
Wala simalumu jamaa, wewe move on wacha kulia lia mtoto wa kiume.

Ni kawaida watu akipata nafasi mahala atakutana na watu wanao speak the same language, watu wa haiba yake. Hata sehemu za kuonana hazitakua sawa na huko awali...
Ni kweli mkuu, sikuwahi kujua hili labda kwakuwa ndio nakutana nalo mara ya kwanza. Nitazidisha jitihada pia mkuu🙏
 
Back
Top Bottom