Ulitumia kiasi gani cha fedha ama umepanga kutumia kiasi gani cha fedha kugharamia harusi yako?

Ulitumia kiasi gani cha fedha ama umepanga kutumia kiasi gani cha fedha kugharamia harusi yako?

Suala la Kuoa ama kuolewa bado litaendelea kuwa ni hitaji muhimu miongoni mwa Jamii ya watu wengi Ulimwenguni.

Kwa Tanzania, tunazo Ndoa za aina mbalimbali ambazo zinatambulika kisheria ambazo ni Ndoa za Kidini, Kimila na Kiserikali.

Mara baada ya kufunga Ndoa, maharusi wengi Kwa kushirikiana na jamii zao, hupenda kufanya sherehe. Sherehe hizo huambatana na michango Kwa walio wengi kupitisha Kadi kwaajili ya kuomba kuchangiwa kufanikisha sherehe za harusi zao.

Japo baadhi hufanya sherehe za harusi zao pasipo kuomba michango Kwa ndugu/jamaa na marafiki. Wao hugharamia Kila kitu wao wenyewe na hao ndugu/jamaa na marafiki hupewa Kadi za mwaliko kuweza kuhudhuria sherehe tu.

Kwa utafiti usio rasmi, sherehe za harusi hupendwa zaidi na Wanawake kuliko Wanaume. Wanaume wako tayari kufunga Ndoa za kimya kimya lakini sio Wanawake.

Je, ulitumia fedha kiasi gani kufanikisha harusi yako ama umepanga kutumia fedha kiasi gani kwaajili ya harusi yako na mwenzi wako?

Binafsi, nilitumia kiasi cha shilingi milioni 10 kuweza kufanikisha harusi yangu na Bibi yenu miaka kadhaa iliyopita 🤗🙏

Sikuhitaji kuchangiwa fedha kufanikisha sherehe ile, bali niliweza kujipanga mwenyewe Kwa muda wa miaka 5.

Nilifungua akaunti maalumu Benki (Fixed deposit account) ambayo nilikuwa nina ruhusiwa kuweka fedha pasipo kutoa Kwa muda wa miaka 5 hivi, japo nilikuwa napata interest kidogo za Benki.

Baada ya miaka 4 hivi, nilikwenda kuchungulia fedha nikakuta nina milioni 9.35 so nikaanza maandalizi kujiandaa na harusi Mwaka unaofatia.

Mind you, tayari nilikuwa nina Cheti cha Ndoa ya Serikali na mwenzangu lakini yeye Kiu yake ni lazima tukafunge ile ya Kanisani 🙌

Kuna wakati nilikuwa nafanya biashara ya kununua na kuuza mazao ya nafaka. Nilikuwa naenda Mashambani, nawakopesha fedha Wakulima then wakati wa mavuno nilikuwa naenda kukusanya mazao hasa zao la Mpunga.

Kwahiyo kwenye ile harusi, sikuwa na hofu ya Chakula maana tayari nilikuwa nina stock ya magunia ya kutosha ya Mpunga.

Wanasema harusi ni kula na Kunywa. Kwahiyo nilijiandaa kwenye eneo hili.

Kwenye upande wa Chakula niliandaa wali mweupe,Pilau, chips, mtori, nyama za kukaanga, kachumbali

Vinywaji niliandaa Soda na Maji tu.

Niliandaa Kadi za Mwaliko za watu 300 lakini walifika watu 358 japo hili nilijua lazima lingetokea maana harusi yenyewe niliifanyia Kijijini kwahiyo wengi ni wale watu mnajuana. Kwahiyo niliweka chakula na Vinywaji Kwa zaidi (excess budgeting)

Pamoja na Wageni waalikwa, usiku ule nilikuwa na Mchungaji pamoja na Mwinjilisti ambao walishiriki kuanzia mwanzo wa harusi hadi tunamaliza tukio majira ya saa 9 usiku.

Gharama za mavazi za Wapambe niligharamia mwenyewe kuanzia mavazi ya Kanisani hadi Ukumbini 🙌

Niliamua kukodisha Ma-MC wawili ili kunogesha sherehe 🤗

Pete nilinunua zenye ppt ya dhahabu, kuogopa zisije kupauka.

Mchanganuo wa Bajeti yangu kufanikisha sherehe ile, nimeambatisha kwaajili ya wengine kujifunza.

Kumbukeni, hata kama umeoa bado unaweza kuja kuozesha watoto wako miaka ijayo. Baadhi yetu mnaweza kuwa Wanakamati kwenye harusi za wengine pia

Kwahiyo Harusi zitaendelea kufanyika hata baada ya kufa kwetu maana tutakuwa tumeacha Kizazi chetu kinaendelea Kuoa na kuolewa.
Ni benki gan hiyo ambayo ulifungulia hiyo fixed account
 
Kwa ile video ya equatorial guinea 🇬🇶 bado mna mpango wa kutoa mamilioni ya fedha kwa ajili ya sherehe ya harusi mi nafkiri mahari inatosha
Hiyo ni ajali Kazini

Unaweza kupewa Mke bure usitoe hata shilingi 10, lakini ukaja kuchapiwa.

Wanasema kuchapiwa hakuepukiki.

Muhimu ikifika zamu yako, kula kama vile kesho huletewi Tena😜
 
Hiyo ni ajali Kazini

Unaweza kupewa Mke bure usitoe hata shilingi 10, lakini ukaja kuchapiwa.

Wanasema kuchapiwa hakuepukiki.

Muhimu ikifika zamu yako, kula kama vile kesho huletewi Tena😜
Bora nipewe bure haitaniuma kma nikiwa nimetumia mapesa mengi
 
Inaonekana suala la Kuoa hujalipa kipaumbele, nashauri ujipe muda wa kutosha uweze kutafakari.

Nina uhakika ukifika above 40 unaweza kuanza kuona umuhimu wa Kuoa na kuwa na familia yako
Nakubaliana na mahari ila kufanya sherehe hilo kwangu halipo
 
Nilijiwekea lengo la kutosumbua watu kwenye michango, na nilifanikiwa
Ila cha kushangaza unasumbuliwa, harusi ni mambo ya kijamii si mbaya kushiriki na wenzako maana na wao watashiriki yako, mwisho wa siku hutachangia wenzako maana hukuomba support zao.
 
Dah sidhani kama nitafanya sherehe, sina hobby na hizo harakati japo mama ndio anaforce, mimi ni msabato nimemwambia wife, nikishatoa mahali mimi nakubeba tutaenda kufunga ndoa kwa mchungaji baadae, asipotaka basi.
Shida ni kwamba wazo la sherehe huanza kuwa organised na wengine kabisa mwishoni unaingizwq mzima mzima kwa ahadi kuwa unafanyiwa harusi ndogo tu.
 
Ila cha kushangaza unasumbuliwa, harusi ni mambo ya kijamii si mbaya kushiriki na wenzako maana na wao watashiriki yako, mwisho wa siku hutachangia wenzako maana hukuomba support zao.
Hii tabia imekuwa kubwa mno miongoni mwetu.

Yaani michango ya harusi inakuwa kama ni lazima, na usipotoa watu wanakununia

Kama hautakuwa makini hadi Mwaka unaisha, unaweza kujikuta unachangia zaidi ya harusi 20 ama zaidi, wakati huo harusi yako uliifanya pasipo kuomba hata shilingi 10 ya mtu🙌
 
Shida ni kwamba wazo la sherehe huanza kuwa organised na wengine kabisa mwishoni unaingizwq mzima mzima kwa ahadi kuwa unafanyiwa harusi ndogo tu.
Hatari sana 🙌
 
Ila cha kushangaza unasumbuliwa, harusi ni mambo ya kijamii si mbaya kushiriki na wenzako maana na wao watashiriki yako, mwisho wa siku hutachangia wenzako maana hukuomba support zao.
Mimi nachangia tu nikiona kuna ulazima/umuhimu wa kuchangia, sio zote lazima uchangie.

Lakini, mtazamo wangu ni kuwa kama unajiweza hamna haja ya kusumbua watu kwa kuwaomba michango, fanya jambo kiasi watakaoamua kukusupport wafanye hivyo bila kusukumwa na wale ambao hawataki napo isiwe case.

Imagine harusi inaandaliwa ndani ya miezi 6 kisa mtu unakomaa kuomba watu michango ilihali una uwezo, its chaos!
 
Mimi nachangia tu nikiona kuna ulazima/umuhimu wa kuchangia, sio zote lazima uchangie.

Lakini, mtazamo wangu ni kuwa kama unajiweza hamna haja ya kusumbua watu kwa kuwaomba michango, fanya jambo kiasi watakaoamua kukusupport wafanye hivyo bila kusukumwa na wale ambao hawataki napo isiwe case.

Imagine harusi inaandaliwa ndani ya miezi 6 kisa mtu unakomaa kuomba watu michango ilihali una uwezo, its chaos!
Miezi 6 ya kuwakomalia ndugu na jamaa wakuchangie harusi, wakati huo huo unataka harusi ya shilingi milioni 20 halafu muhusika ana shilingi milioni 1 kama kianzio

Milioni 19 zote zinategemea wadau 🙌
 
Kuna kijana wa jirani yangu yeye binafsi hakutaka makuu kutokana na hali aliyonayo,nia yake afunge ndoa kanisani kisha jioni awatoe wanafamilia wa karibu kwa chakula cha jioni
Ndugu sasa Oh hiyo kitu haiwezekani lazima tufanye sherehe,Dogo akamwambia sawa kama ndiyo hivyo andaeni hiyo sherehe
Mie ni mmoja wa wanakamati ninavyoandika hapa tumeshafanya vikao viwili ...... sioni dalili ya kufanikiwa kwani hao waliokuwa wanataka sherehe siwaoni vikaoni na ukiwapigia simu za ahadi ya michango....hizo ahadi zao sasa😞
 
Kuna kijana wa jirani yangu yeye binafsi hakutaka makuu kutokana na hali aliyonayo,nia yake afunge ndoa kanisani kisha jioni awatoe wanafamilia wa karibu kwa chakula cha jioni
Ndugu sasa Oh hiyo kitu haiwezekani lazima tufanye sherehe,Dogo akamwambia sawa kama ndiyo hivyo andaeni hiyo sherehe
Mie ni mmoja wa wanakamati ninavyoandika hapa tumeshafanya vikao viwili ...... sioni dalili ya kufanikiwa kwani hao waliokuwa wanataka sherehe siwaoni vikaoni na ukiwapigia simu za ahadi ya michango....hizo ahadi zao sasa😞
Ndiyo maana kwenye utangulizi wa hii mada hapo juu, nimeelezea kwamba mara zote wanaoshinikiza sherehe za harusi ni ndugu either wa kikeni ama kiumeni bila kujali uwezo uliopo.

Usipo tafakari vyema, unaweza kujikuta unalazimika kuingia Kwenye madeni ili kuwafurahisha ndugu na jamaa kufanya sherehe kubwa, lakini baada ya hiyo sherehe ukajikuta unaishi kwenye ukata na madeni yasiyoisha wewe na Mkeo hadi mkajikuta mnakonda kwasababu hizo 🙌
 
Kuna kijana wa jirani yangu yeye binafsi hakutaka makuu kutokana na hali aliyonayo,nia yake afunge ndoa kanisani kisha jioni awatoe wanafamilia wa karibu kwa chakula cha jioni
Ndugu sasa Oh hiyo kitu haiwezekani lazima tufanye sherehe,Dogo akamwambia sawa kama ndiyo hivyo andaeni hiyo sherehe
Mie ni mmoja wa wanakamati ninavyoandika hapa tumeshafanya vikao viwili ...... sioni dalili ya kufanikiwa kwani hao waliokuwa wanataka sherehe siwaoni vikaoni na ukiwapigia simu za ahadi ya michango....hizo ahadi zao sasa😞
Watu kama hao ningewanyoosha. Ikifika siku ya siku baada ya church, picha, afu tunaenda kwa shishifood au buhetifood ndo nimemaliza. Kila mtu na mipango yake, nini kuchoshana. Watu tuliolewa kimya kimya na maisha yanasonga, mi nialikwe kwenye kamati naenda na plan ya harusi ndogo, na yeyote atakaetaka sherehe aahidi kuanzia laki tano esp kama bwana harusi choka mbaya.
 
Watu kama hao ningewanyoosha. Ikifika siku ya siku baada ya church, picha, afu tunaenda kwa shishifood au buhetifood ndo nimemaliza. Kila mtu na mipango yake, nini kuchoshana. Watu tuliolewa kimya kimya na maisha yanasonga, mi nialikwe kwenye kamati naenda na plan ya harusi ndogo, na yeyote atakaetaka sherehe aahidi kuanzia laki tano esp kama bwana harusi choka mbaya.
Hizo gharama za kuwapeleka maharusi na waalikwa ShishiFood nani atagharamia?
 
Back
Top Bottom