Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji3]
 
Umenena sahihi
 
Unaesema huwezi kukaa kwa ndugu,nani anakaa akiwa anajielewa? Na kumbuka,haya ni baadhi ya mambo yanayomfanya mtu akomae kiakili. Ukisikia hujafa hujaumbika,ndo hayo sasa.
Niliwahi kukaa kwa mama mdogo,tena ugenini(nchi nyingine). Kumbe yeye,ni kunguru. Ila mmewe,mstaarabu sana. Kajimama kakawa kanachepuka,na mambo ya ajabu. Haikuwa tabu,maana yalikuwa hayanihusu.
Siku moja,kakabeba hela(za Kenya),mwenyewe kuja kutafuta,hazionekani. Jama alibadilika,japo hakuwa muongeaji. Basi jimama likawa na vituko,mara hutoki ndani,mara kazini umechelewa,mara huku ugenini utapotezwa hupaswi kwenda kupanga,mara we ndo ndugu yangu tuu aliyepo karibu. Sasa,kipindi hicho mi hata sijawahi kumvua chupi mtu. Akawa ana marafiki zake wanawake,af watu wazima. Acha alianzishe kwamba mmoja kamwambia namtaka. Hasira ninazo za uhakika mie. Nina ka akiba kidogo,nilibeba begi langu huku ananiangalia,mambo ya kubembelezwa sitaki. Nikaenda,badae nikapiga simu kwa mmewe nikamuaga,hakufurahia,na sikutaka kumwambia shida ilikuwa nini. Majuzi tu mmewe,tunapiga stori weeee, kumbe miaka hiyo,alimwambia pesa nilichukuwa mimi. Mungu si Athuman,kumbe alipochukuwa,alipeleka kuchange, mmewe kufatilia,aliambiwa na kiasi kilicholetwa kuombewa chenji. Means mmewe hakuwa na shida na mimi,maana ukweli aliupata mapema,nae akakausha.

Wapo waliopitia mengi,lakini kumbukeni. Kama ndugu ndo ameomba au wazazi,huwezi kujitia wazimu kwamba siendi, au kama upo eti naondoka.
 
Nimekumbuka
Nilienda kwa ndugu nikafika saa 8 usiku picha linaanza siku ya kwanza nafika huo mkoa kanipokelea na melekezo ya bodaboda bar af mimi sio mnywaji kivile aloo niliteseka

Kila usiku yupo kushtua afu alivoona nipo pale akawa anakamua kweli kweli funguo anakuachia utaendesha bomu lake mwenyewe

Ule mkoa mwezi tu nikajuana na mabaamedi wote wa bar maarufu na wanywaji maana jamaa nae alikua sio wapolepole


Nilikaa mpaka shida yangu ilipoisha ila ndo niliona starehe ikizidi mara nyingine ni mbaya
 
Ni kazi kwelikweli sijawahi kwa kweli🤣🤣🤣 nakwepakwepa tu
 
Wewe ni dikteta
 
Pole sana mkuu
 
Duuh
 
Ulimkosea bhana. Ungefuatilia ukamstili, au hata ukamcheck bro ukaongea nae. Wanawake wengi wao unajua akili zao zishahama!! Na bro haukuwa na ubaya nae,na alijua we ni kidume tu lazima ukaze sehemu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…