Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Duh ila ndugu wa mume jamani kuishi nao yataka moyo.nimekuja kugundua kwanini watu wengi wanaishi na ndugu zao kuliko ndugu wa mume.nikiishi na mdogo wangu namtuma nitakavyo hata nguo zangu nampa anifulie hutomsikia kunung'unika, ndugu wa mume mtume hata mara moja ukoo wao mzima watajua . Nako hapa naishi na wifi yangu kaachika kwa mume wake yaani ni kero jamani nyumba imekuwa kama na wanawake wawili mimi napanga kipikwe hiki yeye anapika kile mavyakula anapika mengi anaishia kumwaga yaani ilimradi fujo.hapa napanga na mimi niondoke niende kuishi kwa kakaangu
Huna lolote zaid ya roho mbaya unaona ana faidi sana kukaa hapo.. wanawake asilimia ni mashetani
 
Nimesoma comment zote watu wamenyanyasika.ila kiukweli mimi nilienda kuishi kwa mjomba wangu kipindi hicho najitafuta niliishi vizur miaka 5 sikuwahi kunyanyaswa hata siku moja wala kufokewa au kusemwa.

Nakumbuka niliishi maisha mazuri nikiwa hom tu pale kulikua na beki 3 yeye na aunty ndo walikua wanamaliza kila kitu, labda kazi kiume labda kubeba kitu ndo nilikua nawasaidia tu.

Niliishi kama nyumbani, nakula vizur hadi uhuru kama nyumbani, nilipewa mpaka ufunguo wa geti la nje ili nikitoka huko nisigonge geti, yule aunty yangu ana moyo wa ajabu sana yaani sijawai kuona mtu ana roho hiyo. Yaani mtu unaishi mpaka unasema hivi huyu mbona ananijali hivi.

Mpaka leo huwa namkumbuka sana na fadhila zake huwa simalizi mwezi bila kwenda kumuona na zawadi kidogo.

Kwahyo ndugu zangu wapo watu wana roho nzuri ni wachache tu ndo wanasahau kama haya ni maisha tunapita tu.
Hongera sana,
 
Hahahaaaa haya maisha yasikie Tu Kwa watu Mimi nilikaa Kwa uncle Kama wewe Ila nilitimiliwa usiku wa Saa sabaa tukiwa tunaishi mabibo kwenye Kota za jeshi chanzo nilipata mishe super market ya kuwa auditor wao wa muda duh shangazi yangu alilipuka Kwa kusema mbona hujasema kuwa unafukuzia KAZI kwendraaa niliumia Sana Kwa kuwa sikuwa na mshahara hata mmoja but now days mwamba alitumbuliwa pale MSD na magu yupo Kama muokota makopo
Kwahyo magu alitenda mkuu[emoji1787]
 
Vituko vya Junior tu vinatosha
IMG_20230723_172800.jpg
 
Enzi najitafuta nilienda kupambana mkoa Fulani nyanda za juu kusini, mkoa huo unabaridi sana na ilikuwa mwezi wa 5 kwenda 6.
Basi Kuna mwanangu mmoja ni classmate yeye alisoma akiwa tayari ameajiliwa ( in-service), akanipokea maisha yakaanza. Ghetto alinipeleka kwa mshakaji wake pot alikuwa anaishi mwenyewe ( single) lakini misosi naenda kula nyumbani kwake.

Basi bwana life likaenda week ya kwanza na Mimi natafuta fursa tukazungumza na mshkaji tukaona tutafute mabanda ya kuku tufuge kipindi tunaendelea kujitafuta kama ninachochote chakuanzia basi tuchange.
Tukapiga hesabu ilikuwa inaitajika mil.1 kama kianzio, basi kwakumuamini mwenyeji wangu nitatoa laki 3 nikamwambia tuanze. Asee nilipigwa chenga mwamba nikimuuliza anasema Bado. Muda ukaenda asee mara gafla ya huduma ya chakula kwake ikawa ya kusuasua. Kuna siku nimeenda usiku kula nagonga mlango wapo ndani hawataki kunifungulia. Wakajifanya hawanisikii.

Nikaondoka kwa hasira nikaenda kulala, mwamba akaninawa ugenini Sina ndugu namtegemea yeye, pesa imekata halafu amenidhulumu na Sina Cha kumfanya. Pot nae akapata short course Moshi anatakiwa aende akataka kufunga ghetto lake maana hata mwenyeji wangu na yeye hamuelewe. Nashukuru Mungu kwa muda niliokaa nae jamaa alinikubali sana alikuwa ananiachia Hadi ATM yake nitoe pesa niandae misosi maana nilianza kula kwake Sasa
Ikanibidi niishi kwa akiba yangu ya mwisho iliyobakia huku nikipambana kupata pakujishikiza. Nashukuru tu kipindi pot anataka kwenda Moshi alikuwa Hana nauli kama unavyojua maisha ya mapoti, basi akaniomba nimkopeshe nikampa elfu 30 ikawa hamna namna basi aniachie ghetto mpaka atakaporudi.

Baada msela kuninawa nikaanza kupambana pekeangu, Kuna msela alikuwa manager kwenye NGO moja ya kilimo na Mimi niliomba nafasi humo nikawa nikimkuta nambembeleza anisaidie , ila anasema nafasi Bado. Baada ya kumuomba sana akasema yeye ana bar kama Sina mishe nikajishikize kuwa manager kwenye bar yake, nikakubali maisha ya umanager mchwara yakaanza asee, jamaa alivyosikia nimepata kazi ya bar akawa anakuja anakunywa bia halafu halipi nikiitwa anasema huyu nimemleta Mimi. Akawa ananikwaza sana, mara alete fujo da! Boss akafuatilia jamaa akamwambia yeye ameniajiri vp bila yeye kukubali ananijua nimetoka wapi, nikikimbia na pesa zake atanitoa wapi.
JAMAA AKAOGOPA NIKAFUKUZWA KAZI BILA KUPEWA SABABU.
Ilinibidi nitafute nauli nirudi nyumbani nikajipange upya.

Nashukuru Mungu hayo mapito yamepita kwasasa ninamaisha yangu naishi kwangu na nipo jijini dar es salaam maisha yanasonga. Nashukuru mwanangu kwa yote uliyonifanyia Mungu akulinde na akupe unachostahili.
 
Mi ukikaa kwangu ni lazima uende kanisani au msikiktin mzee. Tena jion kabla ya kulala lazima tusali pamoja wote na kila mmoja ana siku yake ya kutoa tafakar. Mi sina mbingu ya kukupeleka kaka kwahiyo maadamu unaishi kwangu utasali hutaki unaondoka simpo. Kwangu kila jmos tuna lisaa la kUdiscus kuongea kinachokukera na nini kifanyike ili maisha yawe mazur. Umeamua kuja kuish kwa mtu lazima ujue kila nyumba ina utaratibu wake na muhim kwako kuuheshim huwez then tembea cnaga mbambamba. Cwez kuja kufanya watoto wangu wa kisasa bila displin kwasababu yako. Ikitokea ni nyumban day aisee wote kila mtu anafanya usafi cnaga cha House girl wala house boy cku hiyo wote ni front kuanzia watoto mpaka baba. Haya maisha bila ukuda kidogo mitoto inaharibika sana.
Huu nauita ukuda Pro max [emoji1787][emoji1787][emoji119][emoji119]
 
Habari za muda huu, ni siku tulivu sana hapa. Jiji la Dar es Salaam kumekucha salama, ingawa kulikuwa na upepo wa baridi sana, poleni na natumaini kila mmoja wetu ni mzima kabisa. Nawatakia kila la kheri katika pilika za kuijenga Tanzania kuwa kubwa tena, yenye amani na upendo. Twende kwenye mada.

Kuna kipindi kwenye Life cycle ya kimaisha ilinifanya nihamie kwa uncle wangu kuishi nae ili kuangalia uwezekano wa kufanya maisha. Enzi zile ndio nimemaliza masomo nipo home tu nikapata mchong huo, nilikuwa very excited sana na hili, maana nilikuwa ninavuta picha fulani hivi kabla ya kufika kwa uncle Dar.

Siku mbili baada ya kupewa taarifa ya safari nilijiandaa lakini ilikuwa ghafla sana kutokana na uchu wa safari ya kuja huku hata watu niliokuwa nawadai pesa zangu wengi niliwapotezea, kitu ninachojutia sana.

Siku ya safari ikawadia, panda nikapanda basi safari mpaka Dar, nifika mida ya saa moja hivi enzi za ubungo terminal pale, akaja mshakaji aliyekuwa anakaa kwa huyo uncle, wakanichukua freshi mpaka home.

Hapo nipo so excited na wishes nying sana how it's going to be in the up coming day's, nikachil, nikafika home. Yale mapokezi tuu yakanidropisha point. Yule mke wake alikuwa anagubu sana, nilivyofika nikaona hapa chakike.

Picha linaanza kulipokucha tunaamshwa saa kumi na moja tufanye usafi, duuhh nilichoka. Kumbe wanafuga mbwa, sehemu padogo mbwa wanajisaidia, morning ni kuzoa na kusafisha kumwaga maji, nilichoka. Ila nikajikaza kumbe bado kuna kuosha magari usiku unaamshwa uoshe, kibaya zaidi ni kila siku iwe mvua au jua.

Kibaya zaidi ni huyo mke wake alikuwa na visa na maneno ya shombo, mara hataki watu watoke nje ya geti anafunga, mara hataki watu wakae sebuleni, hata kunywa maji ya kwenye friji jau, akinunua matunda mpaka akupe yeye na atakupa wakati linaanza kuharibika ukila atakuja kuongea mpaka ujute.

Kwa kipindi kile ilikuwa ni mateso sana, sabuni ya kuogea unajinunilia, mafuta ya kujipaka pia, tulikuwa tunajitegemea kama tumepanga hata kipindi tunaenda K/Koo ilikuwa ni taabu sana.

Ilinipasa kuishi kama mtoto wa miaka kumi kushuka chini, maana ni kama sikuwa najielewa. Maana watu walikuwa wanakuja pale wanashangaa tunawezaje kuishi na hawa, hata wadogo zake na yule mama walishindwa kukaa nae, wengine walikimbia na kutoroka. Ila ndo changamoto tunazokutana nazo katika maisha ya wengi wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi naishi mjini na nimekuwa nilipokea watu kama wewe kwa muda mrefu. Nilichogundua ni hata mtu umfanyie wema upi.bado wanaongea maneno ya jinsi hawakuthaminiwa. Na kibaya zaidi ni kwamba watu wenyewe wanaoishi kwa watu hawana appreciation hata kidogo. Unakuta wao walikuja kwa ajili ya shida zao na wewe unakuwa kama daraja tu. Kwa maana hiyo hata mimi sikubali mtoto wangu aishi kwa mtu hata kama ni ndugu. Atapitia siku moja kisalimia na ya pili aondoke. Ushauri wangu epuka kuishi kwa watu usije kusimulia mabaya na kusahau mazuri uliyotendewa.
 
We jamaa umenichekesha sana [emoji16][emoji16][emoji16]

Ila we ndie ulikuwa na tatizo wala sio hao mbwa, kwa kifupi mbwa ni mnyama mwenye akili ukiwa unabehave km una hatia lazima wakushambulie.

Mbwa ukiwa unamuogopa kwa kawaida huwa ana sense na kujua kwamba huyu sio mtu mzuri kwa hyo anakuwa anajihami.

Ulichopaswa kufanya kuanzia mwanzo ni kufanya juu chini wakuzoee na hili lingewezekana km ungekuwa una act upo cool mbele yaani huna wasiwasi, hili la kuwa na wasiwasi kila mara unapowaona ndio lilifanya muwe maadui wa kudumu.
Ndugu, unaongea uonekane Mjuba ama namna gani!?

Kiustaarabu kabisa, kama una wageni nyumbani kwako na unafuga mbwa unapaswa kuwataarifu uwepo wa hao wanyama wako, usimwambie mgeni wako kuwa hawana Tabu ilihali hawamjui wala hawajamzoea. Na unataka mbwa wamzoee ili iweje ikiwa ni mgeni na kibaya zaidi choo ni cha nje au unakuta ni nyumba ya kupanga ila mwenye nyumba anafuga mbwa! Think Twice even Thrice aisee
 
Ndugu, unaongea uonekane Mjuba ama namna gani!?

Kiustaarabu kabisa, kama una wageni nyumbani kwako na unafuga mbwa unapaswa kuwataarifu uwepo wa hao wanyama wako, usimwambie mgeni wako kuwa hawana Tabu ilihali hawamjui wala hawajamzoea. Na unataka mbwa wamzoee ili iweje ikiwa ni mgeni na kibaya zaidi choo ni cha nje au unakuta ni nyumba ya kupanga ila mwenye nyumba anafuga mbwa! Think Twice even Thrice aisee
Hayo mambo ya mjuba mi hta siyajui! Nilichotaka ni kumfundisha jinsi ya ku survive kwenye mazingira yenye mbwa km alipofikia

Kwa mbwa wetu hawa wa uswahilini siku tatu tu zinatosha kufanya wakuzoee.
 
Kukaa na ndugu sitaki kabisa wala kukusikia tumekaa na ndugu toka tunazaliwa ila sahizi tunalipwa mabaya ila ndugu upande wa baba [emoji23][emoji23][emoji23] ni hatari kabisa tuombee maisha tusiwe mafiwi ,shangazi, mama wakubwa na wadogo wabaya kwa vizazi vyetu
Ndugu upande wa baba [emoji2090][emoji2090][emoji2090][emoji2090][emoji23][emoji23] kwangu msije kabisa
Sisi undugu yaani ushangazi na ubaba uliisha baada ya Baba yetu kufariki. Toka 2018 hakuna hata mmoja amewahi nipigia simu wala nijulia hali kama mtoto wa kaka yao.

Katika kitu ambacho namshukuru Mungu kwa ajili ya Baba yetu ni kufariki sisi tukiwa watu wazima wenye watoto na tunaojitambua. Katika maombi yangu ya kila siku mbele za Mungu ni anipe uhai na afya njema ili nione wanangu wakijua na kujitambua then anichukue nikapumzike. Duniani kuna shida na changamoto nyingi sana. Eehhh Mungu tusaidie.
 
Kuna mwaka nilienda mkoa nikafikia kwa blaza alikua anaishi na mke wake, watoto wawili na beki tatu, mimi na blaza tulikua tunaenda vzr kabisa, nilikua nawahi kurudi home nakuta wenye nyumba hawajarudi yuko dada tu na watoto, kusema kweli yule mtt wa kirangi alikua vizuri sana slowly tukaanza kujenga mazoea nikirudi namzingua mixer kumshika manyonyo demu anafurahi hatari, siku moja nikawahi kurudi nikasema leo lazima nimtombe kweli kufika nikamzingua mtt kaelewa nikaweka palepale sitting room, kuanzia siku hiyo wenye nyumba wakiingia kulala mimi naenda chumba cha dada natomba, sasa siku hiyo nikaenda kama kawaida yangu tukaanza mizamuano kumbe shem alikua hajalala akawa amekuja ghafla chumba cha dada kuchukua nguo ya mtoto kanikuta juu ya kifua cha dada yule shem alipiga kelele hadi majirani wakasikia, akawa anamuita mume wake njoo uone mdogo wako anambaka dada, nilijaribu kumpliz akae kimya ila ndo kama namwambia aongeze sauti nilichofanya nilitoka fasta chumbani nikaenda kwangu nikavaa viatu nikatoka nikasepa, hapo ni kama saa tano usiku nikaenda kulala nyumba ya jirani kuna jamaa alikua amepanga, asubuhi nikasepa sikutaka kukutana na ile aibu, sasa ni zaidi ya miaka 15 sijarudi pale hata nikienda huo mkoa wanasikiaga tu kuwa nipo mjini, kifupi yule shem alizingua na sijui nini kilimtokea beki3 huko nyuma.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Shem alikuwa na wivuu kiufupiii...
 
Sisi undugu yaani ushangazi na ubaba uliisha baada ya Baba yetu kufariki. Toka 2018 hakuna hata mmoja amewahi nipigia simu wala nijulia hali kama mtoto wa kaka yao.

Katika kitu ambacho namshukuru Mungu kwa ajili ya Baba yetu ni kufariki sisi tukiwa watu wazima wenye watoto na tunaojitambua. Katika maombi yangu ya kila siku mbele za Mungu ni anipe uhai na afya njema ili nione wanangu wakijua na kujitambua then anichukue nikapumzike. Duniani kuna shida na changamoto nyingi sana. Eehhh Mungu tusaidie.
Kama nakusoma vile
 
Back
Top Bottom