Uliwahi kutamkiwa neno gani baya na Mwalimu wako?

Uliwahi kutamkiwa neno gani baya na Mwalimu wako?

Mimi naingia form one tu siku ya ya kurupoti nikaambiwa DOGO WEWE HUMALIZI SEKONDARI NAKUAPIA na sijamkosea kitu yaani anakuja kijambulisha na kufahamiana na wanafunzi kashaanza tayari maneno. Lakini LEO NIPO OFISINI. Cha kushauri tu ni kuwa waalimu kiufupi waachane na tabia hizo za kuwatamkia wanafunzi manene ambayo kwa wengine umri alio nao mwanafunzo anashindwa kustahimili uzito. Japo kuwa mimi ndio yakinifanya nikomae ili ajue kwamba hawezi kuamua hatima yangu bali ni mungu.
 
Baadhi ya walimu kuanzia Shule ya Awali na Msingi,Sekondari na hadi Chuo wamekuwa na tabia ya kutamkia watoto maneno makali na yenye kukatisha tamaa.

Mojawapo ya Maneno hayo ni kama “Hutaweza kufanikiwa hata siku moja”.

Wakati mwingine maneno hayo huwafanya wanafunzi kujiona wanyonge na kukata tamaa katika masomo yao na kusababisha baadhi yao kushindwa kutimiza ndoto zao.

Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida wanafunzi wengi wakimaliza masomo baadhi yao hufanikiwa na kuajiriwa katika Taasisi, idara, Mashirika na sehemu nyingine kama hizo.

Walimu hufika kuhitaji msaada na kuwakuta wanafunzi wao waliowatamkia maneno makali wakitoa huduma katika sehemu hizo.

Wakati mwingine husaidiwa lakini pia wakati mwingine hukutana na Vikwazo kutokana na yale waliyoyatenda nyuma.

Walimu tujifunze tuache kuwa wakatili na kutoa kauli kali kwa Mtoto ili kesho yenu iwe Bora zaidi.
Baba yako anauza ng'ombe ili alete ng'ombe nyingine shulee🏃‍♂️🏃‍♂️💭💭💭
 
Sijawahi kutamkiwa neno lolote Baya na mwalimu KATIKA maisha yangu yote ya shule.Kwanza nilikua muoga Sana WA fimbo hivo kunikuta kwenye makosa ilikua mara chache Sana.Nakumbuka nilipokua darasa la pili mwalimu WA hesabu alikua anachapa walokosa baadhi ya maswali,hivyo kabla ya kuchapa alikua anasema "Leo nitawachapa Hadi muombe ardhi ifunguke muingie".Dah haya maneno yalikua yananifanya nilie Sana kabla ya kuchapwa.Nilikua nadhani ardhi inafunguka kweli tunadumbukia😭😭😭
 
Niliambiwa na second master hapo Tarime Sec, wewe unavyotusumbua hivi sababu baba ako anakupa pesa nyingi


Tutakufukuza shule, na kweli nilifukuzwa form four nikarudi kukamilisha ratiba ya necta
 
Back
Top Bottom