Umasikini ni tabia inayotakana na uwezo wako wa kufikiri

Umasikini ni tabia inayotakana na uwezo wako wa kufikiri

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kama uwezo wako unafikiri kidogo, ata katika kutatua changamoto zako zinazokuzunguka utazitatua kidogo; na hatimaye utakuwa masikini.

Kama wewe ni muajiriwa, na umerizika kuwa na chanzo kimoja cha mapato; yaani mshahara, mfano wa laki 5; na unautumia mshahara huo wote na kuishia kwenye matumizi ya kawaida, ndani ya mwezi; huo ni umasikini.

Njia pekee ya kukuondoa kwenye umasikini, ni kubadili mtazamo wako wa kufikiri, na kuanza kuchukua hatua za kuutafuta utajiri.

Na utajiri, unataka uwe na vyanzo kadhaa vya mapato; na si lazima kuanza na vyanzo vikubwa vya mapato.

Mfano mdogo tu; wewe ni mwalimu wa shule ya msingi, nunua baiskeli 3, nunua deli 3 za barafu; tengeneza barafu nyumbani, na chukua vijana 3 kutoka vijijini wanaochunga ng'ombe, waje wakuuzie barafu.

Uwezo wa kufikiri ukibadilika, mafanikio yataonekana.
 
Wapi bhanaaa...kuwa na uwezo wa kufikiri kama beberu na wewe urushe satellite angani badala ya kurusha ungo ambao wengine hatuuoni....
 
Back
Top Bottom