Umasikini wa mtu unaanzia kichwani pake. Kama utani nilivyopoteza mtaji wangu wote kizembe

Umasikini wa mtu unaanzia kichwani pake. Kama utani nilivyopoteza mtaji wangu wote kizembe

Mkuu umeandika ukweli sana aseee,

Mimi pia nimepoteza sana pesa kwa mambo ya kijinga japo si sana ila pesa nyingi nimepoteza kwa kuamini watu kwenye bzness nimekuwa mtu wa kuchukua risk sana ila tatizo linakuja kwenye suala la uaminifu aseee wabongo tunafeli hapo, madeni nayodai watu ni million za shilingi na sioni dalili za kurejesha hizo pesa manake mtu mnadaiana mwisho wa siku unaamua kumuacha kama alivyo maana ni kupoteza muda na kuongeza stress tu, sometime unapata shida unaikumbuka pesa yako unabaki kumlaani tu.

Ila sijawahi kukata tamaa manake kila hatua nayochukua naona mafanikio na kujifunza zaidi (ukipoteza pesa kwenye jambo la maendeleo si sawa na kupoteza pesa kwenye anasa)... Akili yako ndio utajiri wako ila wabongo tunafelishana sana aseeeee.
Ndio mkuu kikubwa nikuziba myanya ya pesa zinapo potelea
 
Ndio mkuu kikubwa nikuziba myanya ya pesa zinapo potelea
Yaani maswala ya pesa Mkuu ni changamoto sijui kwa wengine lakini naamini hata waliofanikiwa sana ukifuatilia utagundua changamoto kama hizi walikutana nazo,

Mimi kipindi cha nyuma iliwahinitokea sikuwa na pesa lakini nilikuwa na plan nzuri sana, nilikuja pata pesa tena ya mkopo 7m aseee plan zote ziliyeyuka hewani zikaja zingine, Nimekuja kupata akili tayari nimepoteza Zaidi ya 70%.
Nikachukua risk kwa tahadhari nikawekeza kwenye moja ya plan zangu za awali japo kwa kusua sua na mtaji huku nikitegemea mshahara kulipa marejesho aseeee biashara na yenyewe ikawa haileti hesabu ni hasara tu (yaani msimamizi akawa mjanja mjanja)

Nikaachana nae nikatafuta mwingine, kidogo ikawa afadhali nikaona mwanga biashara ikakua nikamaliza deni.
Nikachukua tena mkopo tena mkubwa kidogo zaidi ya awali, nikaongeza mtaji kwenye bzness, nikaanzisha zingine mbili,

Bahati mbaya zile biashara mpya zote zilikufa na mtaji, nikajifunza kitu sikufanya tathmin ya kutosha pia usimamizi mbovu.
Kupitia biashara ya kwanza nikapata tena kianzio nikaanzisha ujasiriamali na bizness ndogo ndogo nyingine.

Bado naendelea kulipa deni, Nili apa nikimaliza sichukui tena pesa ya mkopo bila kuwa na tathmin ya kutosha.

Pesa ya mkupuo si yakutegemea sana, kwanini matajiri ni wachache kuliko maskini ni kwa sababu ya nidham ya pesa, Wote tunapata pesa ila inategemea unainvest wapi pia uwezo wa kuifanya igenerate hata kama ikiyumba unakuwa na uelewa wa kuifanya ikue tena sasa pesa ya pamoja(mkupuo) ukiipoteza kuirudisha ni mtihani mwingine.
 
Yaani maswala ya pesa Mkuu ni changamoto sijui kwa wengine lakini naamini hata waliofanikiwa sana ukifuatilia utagundua changamoto kama hizi walikutana nazo,

Mimi kipindi cha nyuma iliwahinitokea sikuwa na pesa lakini nilikuwa na plan nzuri sana, nilikuja pata pesa tena ya mkopo 7m aseee plan zote ziliyeyuka hewani zikaja zingine, Nimekuja kupata akili tayari nimepoteza Zaidi ya 70%.
Nikachukua risk kwa tahadhari nikawekeza kwenye moja ya plan zangu za awali japo kwa kusua sua na mtaji huku nikitegemea mshahara kulipa marejesho aseeee biashara na yenyewe ikawa haileti hesabu ni hasara tu (yaani msimamizi akawa mjanja mjanja)

Nikaachana nae nikatafuta mwingine, kidogo ikawa afadhali nikaona mwanga biashara ikakua nikamaliza deni.
Nikachukua tena mkopo tena mkubwa kidogo zaidi ya awali, nikaongeza mtaji kwenye bzness, nikaanzisha zingine mbili,

Bahati mbaya zile biashara mpya zote zilikufa na mtaji, nikajifunza kitu sikufanya tathmin ya kutosha pia usimamizi mbovu.
Kupitia biashara ya kwanza nikapata tena kianzio nikaanzisha ujasiriamali na bizness ndogo ndogo nyingine.

Bado naendelea kulipa deni, Nili apa nikimaliza sichukui tena pesa ya mkopo bila kuwa na tathmin ya kutosha.

Pesa ya mkupuo si yakutegemea sana, kwanini matajiri ni wachache kuliko maskini ni kwa sababu ya nidham ya pesa, Wote tunapata pesa ila inategemea unainvest wapi pia uwezo wa kuifanya igenerate hata kama ikiyumba unakuwa na uelewa wa kuifanya ikue tena sasa pesa ya pamoja(mkupuo) ukiipoteza kuirudisha ni mtihani mwingine.
Uzoefu murua ndugu, shukrani sana.
 
Natumai wote mnaendelea poa na miangaiko ya hapa na pale.

Wataalam wa mambo wanasema umri wa kufanya makosa na kujifunza vitu mbali mbali ni ule ambao bado mtu yupo kijana maana ni umri ambao unaweza kusahihisha makosa na kurudi kwenye mstari

Kwakweli mimi kama kijana kuna makosa mengi sana ambayo nimesha yafanya ambayo kuna muda nikikaa huwa nawaza nasema pengine nisinge fanya ule ujinga pengine ningekuwa mbali sana kiuchumi lakini ndio unakuta opportunity imeshapita.

Kwa kweli huwa muda mwingine nakaa nafikiria wale wazee ambao umri umeenda na wako bado kwenye umasikini wa kutupwa sipatii picha maumivu ya majuto walionayo maana unakuta umri umeenda hawawezi tena kupindua meza

Sasa kuna kisa ambacho kimenisukuma kuandika huu uzi , kama mnavyo fahamu maisha ya jiji la dar es salaam kwa wale ambao hawana ajira rasmi na pia hawana mitaji mikubwa ya kufanya biashara maisha yao yanavyokuwa, unakuta ni kuangaika sana kama kuku wa kienyeji na kazi ndogo ndogo ili mkono uende kinywani na ulipe bili kama maji na umeme.

Kuna siku rafiki yangu mmoja alinipigia simu akaniambia njoo makumbusho karibia na stand kuna dili la maana litanifaa niachane na mambo ya uchinga niliokuwa nafanya ilala boma .

Kweli nilienda nikakutananae akanipeleka kwa jamaa yake flani akaniambia huyu rafiki yangu amabahatika kupata kazi sasa anauza hii sehemu yake ya biashara kama nitakuwa na pesa aniuzie maana mzunguko wa biashara pale ulikuwa mzuri.

Jamaa alikuwa amechongesha banda kubwa sana la kisasa alikuwa anauza juisi za matunda pamoja na kupaki matunda ndani ya hilo banda alikuwa na freezer kubwa, friji moja ndefu, blender za kisasa na vitu vingine vidogo vidogo,mbele kaweka banda la chips na mishikaki pia mpesa kazi alikuwa anapiga hadi saa 6 usiku .

Vitu vyote alikuwa anataka million 2 kuanzia banda hadi vifaa hapo mfukoni nilikuwa na shillingi laki mbili tu, ikabidi niongee na yule jamaa yangu kama anaweza kunikopesha kiasi kadhaa kweli alikubali kuniongezea laki 4 nije nimrudishie laki 4.5

Baada ya mazungumzo tulielewana baada ya wiki nitampelekea ile pesa maana ilibidi nitafute kama millioni 1.4 ili itimie 2 million. Wakati narudi nimepanda kwenye daladala nikaanza kujilaumu na kumlaumu mungu nitapata wapi mtaji nikachukue ile sehemu kiukweli mawazo yalikuwa mengi sana lakini sikupata jibu wapi nitatoa 1.4m

Baada ya siku kama 3 nikapiga dili kwenye maswala haya ya upatu kwa bahati nikapata kama million 5 hapo ndio akili ikapotea kichwani .kumbuka hapo jamaa yangu yule alikuwa kakubali kunipa laki 4, mm nilikuwa tayari na laki 2 ilikuwa kwenye ile pesa nilioipata nilikuwa natakiwa kutoa 1.4 million ili nikamilishe kuchukua lile eneo.

Kiukweli akili yangu ilibadilika nikaona nikitoa ile pesa kuchukua ile sehemu nikama pesa yote itaisha, yaani nikawa naona kama naenda kudhulumiwa. Wazo nililolipata niakona nitoe pesa yote niitunze getto. Kisha nikampigia yule rafiki yangu nikamwabia amwabie yule mwenye eneo atafute mtu mwingine mimi jamaa niliokuwa natarajia anipe pesa amegoma.

Kiukweli baada ya kushika ile pesa mkononi niliiona ni nyingi mno zaidi ya millioni 5 mabunda manne ya elfu kumi kumi na mawilli ya elfu tano tano.

Uone sisi masikini tulivyowajinga kwanza shughuli nilizokuwa nafanya ilala boma pale nikasitisha nilikuwa mvivu balaa maana ile kazi nilikuwa nawahi saa 9 hadi saa kumi asubuhi nikaona kama nauchosha mwili bure.

Nikaacha kabisa kwenda kufanya kazi kule ilala , kaziniliokuwa nafanya nikula kucheki gemu za mpira mixer, mieleka tamthilia, nilikuwa sitoki njee nikitoka asubuhi naenda kuchukua tray nzima ya mayai kila siku nakaanga mayai 10, maziwa yale fresh ya asas kila siku nachukua mifuko miwili. Matunda yalikuwa hayakauki getto, mikate, juice zile za Ceres ndio yalikuwa maji yangu ya kunywa.

Pale riverside kuna mama mchaga anafuga kuku wa kisasa kila siku nilikuwa nimeweka order kuku mzima ananitengenezea kabisa kisha ananiletea nakaanga vyakula vilijaa getto ikabidi ninunue kale ka friji kadogo kabisa used boss laki na hamsini nikawa natunza mazaga zaga humo.

Pale riverside sehemu ya starehe iliozoeleka ni mikasa kila siku nilikuwa naenda kula raha pale usiku kisha naondoka na demu napeleka getto .

Akili yangu ilikuwa kama imeruka kuna siku nilikuwa nalala naamka hata saa 7 usiku kutoka usingizini najiandaa naingia bar kunywa pale mikasa yaani kwa muda mfupi wahudumu wa pale wakanizoea maana mm kila siku kuanzia J3 hadi jpili sijui usiku wa kareoke vyote nilikuwa nahudhuria kisha nikiona demu mkali lazima nijikoshe na vipesa kisha niondeke nae.

Ikifika asubuhi kabla demu hajaondoka namwambia atoe kuku kwenye kale ka freezer akaange mixer mayai, maziwa kisha nampatia na pesa kisha ndio anaondoka.

Nakumbuka kunasiku nilikuwa counter nimekunywa kweli siunajua watoto wa dar walivyo mara akaja manzi flani akakaa karibu yangu bila kuuliza nikaanza kumnunulia bia kunywa sana bia zangu na unajua mule ndani bia yenye bei ndogo kabisa 3000 . Nakambuka niliondokanae kufika getto kumbe ni malaya aliekubuu ananiambia kabla ya kila kitu naomba changu kabisa.

Asee nilikasirika sana kwa ile kauli nilifungua begi kwa hasira nikatoa burungutu moja la million moja nikahesabu elfu 30 mbele yake nikamwambia chukua kisha usepe na hapo huyo manzi alikuwa ameomba 20k.

Yaani kiukweli zile pesa zilinipa kiburi kuna demu mmoja slay queen amekula sana pesa zangu pale Mcity piza heat, nilimmnunlia hadi samsung A30

Kiukweli nilifanya mambo mengi ya kufuja pesa yaani sitaki kukumbuka maana nilikuwa sipigi hesabu nilikuwa naingiza mkono nachukua burungutu lolote sitoi hata labberband navuta tu noti kadhaa mpaka kunasiku noti kama 3 ziichanika

Siku akili yangu ilirudi kukaa sawa niliingiza mkono kwenye lile begi nikakuta kuna labberband nyingine hazina kitu kupiga hesabu nikakuta nimebaki kama na laki moja na elfu ishirini asee niliogopa, hapo ndio nikakumbuka mwezi unaokuja natakiwa kulipa kodi ya nyumba yaani nilichanganyikiwa .

Nalitawanya zile pesa zote ndani ya kama mwezi na nusu nikarudi sifuri yaani ilifika muda nikawa naongea mwenyewe barabarani wazo ndio likaniijia kwanini nisinge chukua lile eneo la biashara tena rafiki yangu alikuwa kajitolea kunisaidia .Nilikuwa nikitembea barabarani naona kila mtu kanizidi akili kuanzia boda boda, wale wanaouza maji pembeni ya barabara, sehemu za mpesa, hadi mamantilie

Nilichojifunza ukiona anapata pesa badala ya kuwekeza unaogopa unakaanayo ndani nakupa pole sana unauwezekano mkubwa wa kufa masikini. Masikini tunaogopa sana kuwekeza hapo ndio matajiri wanatuzidia.

Now mtu hanidanganyi nilivyosota hadi kukaa sawa nibora pesa yangu iteketee kwenye biashara kuliko kwenye mambo ya kijinga. Mfano bora anaewekeza kwenye jambo fulani mfano kilimo pesa ikapotea kuliko kuharibu kwenye mambo ya kihuni wote ndio watakuwa wamepoteza lakini kunautofauti mkubwa sana kati ya hao watu wawili

Ogoba sana wale jamaa wakatisha tamaa wekeza pesa yako kwenye biashara yoyote ilimradi umeona inaweza kulipa anaekukatisha tamaa anataka uharibu pesa kwenye mambo ya kujinga.

Pia nilichojifunza vitu ambavyo ni hatari kwa pesa za vijana wengi watafutaji cha kwanza upatu/gambling, wanawake, pombe, ukiangalia vizuri vyote vinaambatana na tamaa

Uzi tayari
Hahaahahahah dah aisee sijui nikutafute nikupe story yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
uliona wapi pesa ya kamari ikafanya la maana...
pesa n pesa tu mzee hakunaga pesa ya kamari, ya mshahara wala ya sadaka. na ndio maana ukiwa na sh 1000 hata iwe ya kamari au ya sadaka au ya kuiba au ya kupewa ukienda dukan utapata vocha ya 1000 haijalish hyo pesa umeipataje.....kinachomata n thaman na sio chanzo cha pesa
 
pesa n pesa tu mzee hakunaga pesa ya kamari, ya mshahara wala ya sadaka. na ndio maana ukiwa na sh 1000 hata iwe ya kamari au ya sadaka au ya kuiba au ya kupewa ukienda dukan utapata vocha ya 1000 haijalish hyo pesa umeipataje.....kinachomata n thaman na sio chanzo cha pesa
Hayo maelezo umeyaelekeza kwa mtu hasiye sahihi. Mimi pia nina uelewa kama huo kwamba pesa ni pesa
 
pesa n pesa tu mzee hakunaga pesa ya kamari, ya mshahara wala ya sadaka. na ndio maana ukiwa na sh 1000 hata iwe ya kamari au ya sadaka au ya kuiba au ya kupewa ukienda dukan utapata vocha ya 1000 haijalish hyo pesa umeipataje.....kinachomata n thaman na sio chanzo cha pesa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kweli mkuu. Unakuta mtu kafanya kazi miaka 40 anapewa mafao million zaidi ya 100 baada ya miaka 2 unakuta kazitumbua zote
 
Back
Top Bottom