Umbali kati ya Misri na Israel ni KM 613, lakini wana wa Israel walisafiri kwa miaka 40

Umbali kati ya Misri na Israel ni KM 613, lakini wana wa Israel walisafiri kwa miaka 40

Miaka 40 ya Waisrael kutoka Misri kwenda Kanaani waiona mingi mno kiasi cha kuwa na mashaka. Ukimwasi MUNGU na kuigiza kama vile unamtumikia na yeye amekuchagua lazima akurudi kama baba amrudivyo mwanawe anayempenda. Nitakupa mfano rahisi wa kibinadamu unaoujua au waweza kuutafuta na kuupata. Miaka Tanganyika iliyojitawala (pamoja na muda wa muungano) ni miaka 53 sasa. Huu ni muda mrefu kuliko safari ya wana wa Israel na vikwazo vyake. Pima kiwango cha maendeleo na mafanikio yetu. Kufikia mwaka 1971 tulifanya makubwa mno ambayo tumeibomoa na sasa tunaanza upya. Tuliweza kutengeneza nguo zetu,viberiti vyetu,viatu vyetu. Tukaviharibu.Tunashangaa hakuna ajira. Tunatamani kuvifufua wengine wanaona bora Mwingereza arid I( kama Waisrael walivyokumbuka nyama Misri)
Ni kanuni ya MUNGU Taifa lisipomtii litazunguka tu. Walipoisha kizazi cha kuasi kwa kuabudu Ndama na kujitukuza fahamu zikafunguliwa. Joshua akakiongoza kizazi kipya kuingia kanaani.

Afu hili tatizo nilidhani ni mimi tu naliona ! Yaani unaweza safiri toka Mtwara hadi Mwanza usione serious production activity afu viongozi wetu wanafunga tai tu ! Sijui wamepigwa na pepo . Yaani hamna hata kiwanda kimoja njiani duh!
 
....Ni kama Tanzania tu mwaka wa 50 bado hatujaweza kujivunia utaifa wetu siku tukipata ukombozi wa kweli kifikra na tukaweka kwenye historia wajukuu zetu kipindi hicho wataumiza vichwa sana ilikuwaje babu na bibi zetu wakaishi maisha ya ukoloni mambo leo miaka yote hiyo?

Watu mmejaliwa ucheshi.
Nilikuwa nime-concentrate kuutafakari umbali toka Misri mpaka Israeli, mara Boom...!!
Namna lyinga alivyo oanisha mada na huu mfano wa Tanzania.... duh, nimecheka sana.
Yaani sikutegemea; mwanzo wa hiyo paragraph ni noma!
 
Tunasoma katika bibilia kuwa wana wa israel walichukua muda wa miaka 40 kufika nchi ya ahadi wakitokea utumwani misri. Hapa najiuliza sana. Miaka 40 kutoka hapo kairo kwenda yerusalemu? Mbona ni miaka mingi sana? Au walikuwa hawajui njia? Mimi napata mashaka, miaka waliyokuwa wanahesabu cyo hii tunayohesabu sisi.

Hivi kuna umbali gani kutoka misri (cairo) kwenda israel (yerusalemu)?
Hii hadithi ya miaka 40 umeitoa wapi? Kama ni kwenye biblia basi hicho ni kitabu cha
Riwaya kama vile vya shigongo
 
Miaka ya zamani nfmi tofauti na sasa.
Mwezi mmoja wa sasa ni sawa na miaka 10 ya zamani.
so hao walitumia Miezi Minne tu kutoka Misri hadi Israel.
 
Misri ya Leo sio Misri ya enzi za Musa, pia haimaanishi kuwa walikuwa wakisafiri kwa miaka yote hiyo, Kuna process kuweza kuachiliwa kutoka mtumwa hadi kwa huru

Ehhh makubwa misri ya Leo Sio ile ya akina musa??? Naomba ufafanuzi
 
Hiyo 40 years ni kwa hesabu ya kalenda ya sasa ya Papa Gregory.....? Huenda labda kulikuwa na hesabu ya siku kwa kipindi hiko...
 
kwani kuna safari ya kwenda mbinguni toka duniani.? Aaah, story za mbinguni zipo kiimani zaidi. Kwenda mbinguni lazima kufa kwanza.

Safi sana. good idea, napenda sana ulivyojiongeza kimawazo. sio watu wengine wanafuata mkumbo tu bila kuwaza zaidi
 
Ni kama Tanzania tu mwaka wa 50bado hatujaweza kujivunia utaifa wetu siku tukipata ukombozi wa kweli kifikra na tukaweka kwenye historia wajukuu zetu kipindi hicho wataumiza vichwa sana ilikuwaje babu na bibi zetu wakaishi maisha ya ukoloni mambo leo miaka yote hiyo?

We jamaa una akili sana..natamani ningekua nakufahamu weekend ijayo tungekula bia nyingi sana na fursa ya kuzipata busara zako kwa ukaribu
 
Miaka 40 ya Waisrael kutoka Misri kwenda Kanaani waiona mingi mno kiasi cha kuwa na mashaka. Ukimwasi MUNGU na kuigiza kama vile unamtumikia na yeye amekuchagua lazima akurudi kama baba amrudivyo mwanawe anayempenda. Nitakupa mfano rahisi wa kibinadamu unaoujua au waweza kuutafuta na kuupata. Miaka Tanganyika iliyojitawala (pamoja na muda wa muungano) ni miaka 53 sasa. Huu ni muda mrefu kuliko safari ya wana wa Israel na vikwazo vyake. Pima kiwango cha maendeleo na mafanikio yetu. Kufikia mwaka 1971 tulifanya makubwa mno ambayo tumeibomoa na sasa tunaanza upya. Tuliweza kutengeneza nguo zetu,viberiti vyetu,viatu vyetu. Tukaviharibu.Tunashangaa hakuna ajira. Tunatamani kuvifufua wengine wanaona bora Mwingereza arid I( kama Waisrael walivyokumbuka nyama Misri)
Ni kanuni ya MUNGU Taifa lisipomtii litazunguka tu. Walipoisha kizazi cha kuasi kwa kuabudu Ndama na kujitukuza fahamu zikafunguliwa. Joshua akakiongoza kizazi kipya kuingia kanaani.

Kweli mkuu huenda Mungu anasubiri kizazi cha wakina Wasira na Lukuvi kipite kwanza ndio atubariki.
 
Tunasoma katika bibilia kuwa wana wa israel walichukua muda wa miaka 40 kufika nchi ya ahadi wakitokea utumwani misri. Hapa najiuliza sana. Miaka 40 kutoka hapo kairo kwenda yerusalemu? Mbona ni miaka mingi sana? Au walikuwa hawajui njia? Mimi napata mashaka, miaka waliyokuwa wanahesabu cyo hii tunayohesabu sisi.

Hivi kuna umbali gani kutoka misri (cairo) kwenda israel (yerusalemu)?
Kwa kweli siyo mbali ki vile siku hizi huwa nawaona watu wanaenda kwa mguu tu mkuu, yaani unakatisha tu mfereji wa Suez unajikuta uko Israel. Kuhusu wana wa Israel kuchukua muda mrefu hivyo nafikri inabidi tukumbuke kuwa hawakupita njia inayotumika sasa hivi, wao walikatisha bahari ya Shamu na kujikuta wako ilipo Yemen ya sasa hivi.

Pia ikumbukwe kuwa humo njiani walikuwa wanamkorofisha Mungu naye anaamua kuwapa adhabu ya kupotea humo jangwani ndo maana walikuwa wanachukua muda mrefu sana. Pia humo njiani kulikuwa kunatokea mapigano na makabila mengine waliyoyakuta humo njiani hivyo wakati mwingine wanaenda mbele wakati mwingine wanarudishwa nyuma, ndo maana walikaa miaka 40.
 
Ni kama Tanzania tu mwaka wa 50bado hatujaweza kujivunia utaifa wetu siku tukipata ukombozi wa kweli kifikra na tukaweka kwenye historia wajukuu zetu kipindi hicho wataumiza vichwa sana ilikuwaje babu na bibi zetu wakaishi maisha ya ukoloni mambo leo miaka yote hiyo?

you are deserving my like
 
Kwa kweli siyo mbali ki vile siku hizi huwa nawaona watu wanaenda kwa mguu tu mkuu, yaani unakatisha tu mfereji wa Suez unajikuta uko Israel. Kuhusu wana wa Israel kuchukua muda mrefu hivyo nafikri inabidi tukumbuke kuwa hawakupita njia inayotumika sasa hivi, wao walikatisha bahari ya Shamu na kujikuta wako ilipo Yemen ya sasa hivi. Pia ikumbukwe kuwa humo njiani walikuwa wanamkorofisha Mungu naye anaamua kuwapa adhabu ya kupotea humo jangwani ndo maana walikuwa wanachukua muda mrefu sana. Pia humo njiani kulikuwa kunatokea mapigano na makabila mengine waliyoyakuta humo njiani hivyo wakati mwingine wanaenda mbele wakati mwingine wanarudishwa nyuma, ndo maana walikaa miaka 40.

ahsante kwa maelezo. Miaka 40 ya enzi hizo ni sawa na 40 ya sasa? Ufafanuzi tafadhali.
 
Back
Top Bottom