Umbali kati ya Misri na Israel ni KM 613, lakini wana wa Israel walisafiri kwa miaka 40

Hii mada ilishajadiliwa humu kitambo omba moderators wakusaidie kuipata, Unaleta mada ambayo humu imejadiliwa sana acha kuleta story za whatsapp group humu JF, Tafuta jukwaa soma hiyo story yako ipo
 
Hii mada ilishajadiliwa humu kitambo omba moderators wakusaidie kuipata, Unaleta mada ambayo humu imejadiliwa sana acha kuleta story za whatsapp group humu JF, Tafuta jukwaa soma hiyo story yako ipo
Wacha tuijadili tena huo muda mrefu wengine hatukufanikiwa kujadili
 
Hayo ni msuala ya kiroho kamanda maana kwa hesabu za kibinadamu hutapata jibu Mkuu.
 
Kwanza hizo stories hakuna wa kuzithibitisha.

Pili, usi assume kwamba walisafiri moja kwa moja, ukizunguka zunguka jangwani safari ya siku moja inaweza kutumia siku mia moja.
 
Nitakujibu kama upo tayari kujifunza.Kwanza umesoma kitabu kimoja alafu unakuja kujenga hoja si sawa kabisa.Nakushauri usome na Qur'an kwanza maybe uta learn kitu.
Safari ya Musa(a.s) na ban Israel ilianzia Misri kuelekea nchi ya ahadi(Kanani) iliwachukuwa miaka 40 katika safari hii lakini walikuwa wanaweka makazi na kuanzisha shughuli mbalimbàli kama kilimo na n.k
 
Hawakua na compass huko jangwani inawezekana walipotea njia wakatangatanga kwa miaka kadhaa huku wakitia kambi hapa na pale kwa miaka kadhaa
 
Hapa hapa bongo kuna watu walikuwa wanatokea mikoa ya nyanda za juu kusini hadi Tanga kukata mkonge kwa miezi sita.
Kwa siku walikuwa wanatembea kama kutoka pale Magomeni usalama hadi Ubungo mataa, ni umbali ambao walinionesha ambao mimi nilikuwa natembea nusu saa tu tena nikiwa na mzigo wa kuni.
 
Me nahisi labda miaka 40 walikuwa wanatafuta makazi wanakaa hata mwaka kisha wanaondoka yaani kama wahamiaji afu pia watu wa zamani walikuwa wanaishi miaka mingi.pia kumbuka ile ni kale sana inawezekana waandishi walikuwa wana vipimo vyao vya siku kukamilisha mwaka.yaani labda miezi 4 wenyewe walikuwa wanaita mwaka.
 
Eh yamekuwa hayo tena?? Kwani ulichokisema ni sehem ya jibu au inatusaidiaje kufikia jibu??

Wee si ni Kadinali. Halaf hujui jibu.

Jibu hakuna kwenye hiko kitabu na siwezi kutoa jibu kutokana na kitabu kisicho na muelekeo.

Tumia ukadinali wako umpe jibu mleta mada tuone nawe kama unafit kwa hilo jina au nawe unapelekwa pelekwa tu kama kondoo.
 
Kwanza hizo stories hakuna wa kuzithibitisha.

Pili, usi assume kwamba walisafiri moja kwa moja, ukizunguka zunguka jangwani safari ya siku moja inaweza kutumia siku mia moja.
Kama walikua wanazunguka zunguka tu jangani, maana yake hawakua na kiongozi, hawakua wanajua wanaenda wapi. Lakini Biblia inasema Mungu alikua anawaongoza na kumuelekeza Musa njia salama ya kupita, je Mungu ndio alikua anawaongoza kuzunguka zunguka na kuzurula jangawani bila malengo au uelekeo wowote?
 
Hawakua na compass huko jangwani inawezekana walipotea njia wakatangatanga kwa miaka kadhaa huku wakitia kambi hapa na pale kwa miaka kadhaa
Ila Biblia inadai kua Mungu ndio alikua anawaongoza, au yeye pia hana au hakua na compass na hakujua alikua anawaingoza kuelekea wapi, au alikua anawaongoza njia ya uongo kwa maksudi?
 
1. Mimi siamini kwamba habari hizo ni factual. Siamini kwamba hata huyo Mungu yupo. Kwa hiyo huu si utetezi. Ni logical explanation kwamba habari ya wao kuzunguka haiko logically inconsistent. Naelezea biblia kama plot ya Shakespeare.

2. Ukishakubali kwamba Mungu yupo, maelezo ya kibiblia ni kwamba Mungu aliwazungusha jangwani kwa makusudi kwa sababu hawakuwa na imani naye walikuwa wanalialia kulilia nyama za kwa Farao. Akafanya kizazi kile kilichoongozwa na Musa kisifike nchi ya ahadi, mpaka kizazi kikichofuata kilichoongozwa na Joshua.
 
Tumia Magajizuto kaka,
Hesabu rahisi sana hizi
 
Tatizo watu mnapenda kutafuniwa kila kitu, mbona jibu la swali liko ndani ya bible na imeelezwa wazi kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…