Umejifunza nini katika picha hii ambayo Dkt Tulia amepakatwa na Mama Yake Mzazi?

Umejifunza nini katika picha hii ambayo Dkt Tulia amepakatwa na Mama Yake Mzazi?

Hoja yako nimeshajibu nashangaa wewe bado huelewi.sasa unataka nini tena.maana nimekwambia kuwa hayo unayoyasema na kuyapendekeza tayari yalishafanyika kitambo sana.
Usiruke post yangu imeuliza haya:

"Hujajibu swali, andiko lako limefanikisha nini hasa? Ulikuwa unalenga kupata nini hasa? Je, majibu haya ya wachangiaji ambayo kwa kiasi kikubwa ni hasi ndiyo ulikuwa umepania kuyapata juu ya mhusika mkuu wa andiko lako Spika Tulia?"

Jibu bwana Mwashambwa!
 
Sio Kila mtoto anapakatwa!kwani huyo mama mbona hapakati watoto wake wengine?we kuwa Hali Jojo mbe uone kama mama yako atakupakata,ukimpigia hata simu utasikia keshaanza usumbufu huyu nae!.....Tafuta mpunga baba
 
Ndugu zangu Watanzania,

Hapa chini ni picha ya Mama mzazi wa Mheshimiwa Dkt Tulia Acksoni Mwansasu ,speaker wa Bunge letu pamoja na Rais wa umoja wa mabunge Duniani yaani IPU. Tukio hili la kugusa hisia za watu na ambalo liliteka hisia za watu wengi sana mitandaoni na DUNIA nzima kwa ujumla wake lilitokea mara baada ya Dkt Tulia kurejea Nchini kama Rais mpya wa IPU.

Ambapo ni katika tukio hilo ambapo Dada wa Taifa,fahari ya nyanda za juu kusini,msomi Nguli wa sheria kuwahi kutokea nyanda za juu kusini na chaguo la wana Mbeya alionyeshwa upendo wa kipekee kabisa kutoka kwa Mama yake huyu Mzazi aliyeamua kumpakata Mwanae kwa upendo na hisia kali sana na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake na kuiheshimisha Mbeya na Tanzania nzima kwa ujumla wake..

Bila shaka Mama huyu na mama yetu aliyemleta DUNIANI speaker wetu kijana kabisa na mwenye akili kubwa ,mfano wa kuigwa kwa watoto wengi wa kike wanaosoma na mwenye moyo wa ukarimu,huruma,upendo, unyenyekevu,utu na ucha Mungu alimkumbusha mama yake na kumrejesha mbali sana kimawazo.

Bila shaka Mama yetu aliwaza mapito na magumu aliyopitia kimaisha katika kumlea mwanae mpaka kufika hapo alipofika ,mahali ambapo Dunia ikakubali uwezo wake na kumpatia Urais wa IPU kwa kishindo.bila shaka alikuwa anajionea kwa macho yake matendo makuu ya Mungu,bila shaka alikuwa anaona maneno yaliyoandikwa katika kitabu cha Samweli kuwa Mungu humuinua mnyonge kutoka mavumbini na kumpandisha mhitaji kutoka jaani ili kumketisha pamoja na wakuu , yakitimia kama ndoto machoni pake.

Bila shaka mama yetu ndani ya moyo wake alikuwa akibubujikwa na machozi ya furaha na shukurani kwa Mungu wake ,kwa kumkumbuka na kumuinulia Mwanae kama Nuru katikati ya giza kama ambavyo Mungu alimkumbuka Hana ambaye alikuwa ni Tasa na ambaye alikuwa akilia kila siku ili Mungu ampatie mtoto na hatimaye Mungu akajibu Maombi ,kwa kumpatia watoto na miongoni mwake ni Samweli aliyekuja kuwa mfalme.

Akina Mama wanapaswa kupewa heshima yao na kuheshimiwa sana.tunapaswa kuwapenda Mama zetu.jiulize ni mangapi amepitia Mama huyu katika kumsomesha mwanae mpaka kumfikisha alipofika? Ikumbukwe ya kuwa mama huyu na familia yake hakuwa tajiri wala kumiliki utajiri.lakini kwa uweza wa Mungu alihakikisha mtoto wake anatimiza ndoto zake za kielimu mpaka mwisho.

Ni kupitia tumbo la Mama huyu mpole na mkarimu leo Dunia inafaidika na akili na kipawa cha uongozi cha Mwanae Dkt Tulia,leo watu wanapata tabasamu na matumaini katika maisha yao baada ya kusaidiwa na kufikiwa na mkono wa huruma wa mwanae Dkt Tulia,leo mabinti wa kike mkoani mbeya wanasoma huku mfano wao ukiwa Dkt Tulia.

leo yatima ,wajane na wazee wasio jiweza mkoani Mbeya wanapata matumaini na kuishi kwa furaha kwasababu ya kusaidiwa kwa hali na mali na Dkt Tulia,leo maelfu ya watu mkoani Mbeya wanaishi bila wasiwasi na kuwa na uhakika wa kupata matibabu wakiumwa baada ya kuwa wamegawiwa bure kabisa Bima za afya, na wengine kujengewa nyumba huku wengine wakipewa na kuwezeshwa mitaji ya kufanyia biashara zao za kuwapatia na kuwaingiza kipato cha kila siku.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mtoto kwa mama hakui.
 
Ata mimi mawe ya ephen nipigwe , mpka kufa ,bora ata wewe hayo mawe unashambuliwa na unapona ,mimi nataka niuwawe kabisa kwa ajili ya ephen 😊
😃😃😃😃Mimi nimehiyari kubeba hata dhambi na makosa yote ya ephen.nimekubali kubeba mzigo wowote wa ephen,nimekubali kuteswa hadi mwisho bila kumkataa wala kumgeuka zaidi ya kusema mimi nipo tayari kwa lolote kwa ajili ya ephen.nimekubali na kuruhusu watu wanitukane matusi yote yanayoandikika na yasiyo andikika lakini asiwepo wa kumgusa ephen. ephen ndio mboni yangu .ni ephen ephen ephen kwangu.
 
😃😃😃😃Mimi nimehiyari kubeba hata dhambi na makosa yote ya ephen.nimekubali kubeba mzigo wowote wa ephen,nimekubali kuteswa hadi mwisho bila kumkataa wala kumgeuka zaidi ya kusema mimi nipo tayari kwa lolote kwa ajili ya ephen.nimekubali na kuruhusu watu wanitukane matusi yote yanayoandikika na yasiyo andikika lakini asiwepo wa kumgusa ephen. ephen ndio mboni yangu .ni ephen ephen ephen kwangu.
Mkuu angalia usije ukajiua pale ambapo utaona ephen akipeperushwa kama njiwa manga ,yangu macho😁😁
 
Back
Top Bottom