Umepata somo gani la maisha 2022?

Umepata somo gani la maisha 2022?

1 Nimejifunza kwamba kumsubiri Yesu aje akukute ukiwa hai na akakutwaa ni jambo jema na Imani nzuri, Ila jua unaweza kuzeeka na ukafa hajarudi Ila wewe ndie umemfuata huko. Kwa hiyo jambo la muhimu Ni kujiweka tayari hata ukifa uwe mmoja wa watakaofufuliwa kuingia uzima na milele. Mimi nikiwa kijana nilijua angerudi mapema tu ila Sasa Nina miaka 70 bado hajarudi, labda nitakufa na hajaja.

2. Nimejifunza kwamba aliyedhulumiwa lazima atashinda japo inawezakuwa baada ya muda mwingi kupita, lakini haki yake haitapotea kamwrme

3. Nimejifunza kwamba Ni ngumu sana mtu kukupiga kofi umgeuzie lingine....nadhani Kuna maana ingine isiyo hiyo.

4. Nimejifunza? kwamba maisha yanaweza kumalizika wakati wowote huku tukiwa hatujatimiza ndoto zetu hata robo.....Mtu aliyempokea Yesu lazima atimize kusudi kwa sehemu kubwa.

5. Nimejifunza kwamba maneno matamu na uso wenye bashasha na ukarimu ni afya njema sana kwa mtu Ila uso uliokunjamana na hasira hupunguza sana siku za mtu.

6. Nimejifunza kwamba tajiri mkubwa kuliko matajiri wote duniani ni yule ambaye anamiliki afya na amani.
7. Nimejifunza Chochote kinaweza kutolea muda wowote ule kwahyo nipunguzie mategemeo
 
Huu mwaka nimejifunza
1: kuongeza kukaa kimya sana nikiwa na jambo ni heri nikakae bar nitakaemkuta kaunta ntaongea nae yataishia hapo hapo sitoshare na mtu nnaejuana nae.

Watu mafriji hayagandishi kabisa yani hata kwa ishu zisizokuwa habari wao wanazifanya habari kumaaaaaninaaah sana
 
Be a millionaire, billionaire it doesn't bite, they say money can't buy happyness but i say to you that say 's a scam
No limits on what you can achieve let no body tell you that you can't do it the last person you can trust if you are a men it's your mom and your sister
 
Huu mwaka nimejifunza
1: kuongeza kukaa kimya sana nikiwa na jambo ni heri nikakae bar nitakaemkuta kaunta ntaongea nae yataishia hapo hapo sitoshare na mtu nnaejuana nae.

Watu mafriji hayagandishi kabisa yani hata kwa ishu zisizokuwa habari wao wanazifanya habari kumaaaaaninaaah sana
Haaaaaaaaah Eti mafrigi hayagandishi
 
Somo kubwa nililopata ni kuwa ili upate mafanikio uwe tofauti na wetu wengine hasa kiuchumi ni lazima upitie mateso kweli kweli hadi hatua ya kupoteza matumaini vinginevyo wazazi wako waliteseka sana kuandaa future zao na watoto wao na wakati wako wa kuteseka teseka we mwenyewe usitake kuwashirikisha watu wengine mateso yako kwani hata wao mpaka unaona wanamafanikio na wanakula bata waliteseka tena sana.Nashukuru maisha mapya baada ya kula msoto wa kutosha mambo yameanza kufunguka najiona kweli nipo tofauti na nilipotoka na ninaimani watoto wangu hawatakula msoto kivile sababu baba yao kikombe nilikibeba na njia nimewatengenezea.
 
Back
Top Bottom