Umepata somo gani la maisha 2022?

Umepata somo gani la maisha 2022?

Somo kubwa nililopata ni kuwa ili upate mafanikio uwe tofauti na wetu wengine hasa kiuchumi ni lazima upitie mateso kweli kweli hadi hatua ya kupoteza matumaini vinginevyo wazazi wako waliteseka sana kuandaa future zao na watoto wao na wakati wako wa kuteseka teseka we mwenyewe usitake kuwashirikisha watu wengine mateso yako kwani hata wao mpaka unaona wanamafanikio na wanakula bata waliteseka tena sana.Nashukuru maisha mapya baada ya kula msoto wa kutosha mambo yameanza kufunguka najiona kweli nipo tofauti na nilipotoka na ninaimani watoto wangu hawatakula msoto kivile sababu baba yao kikombe nilikibeba na njia nimewatengenezea.
Kweli mkuu,hapa kuna ukweli mkuu,tatizo watu wengi tunapenda kufanikiwa bilakupitia msoto ,ndio kazi ilipo
 
Nimejifunza usikopeshe mtu pesa yako na ukimpatia uwe tu umemsaidia usidai

Kuna jamaa mmoja nilimsaidia kiroho safi kabisa baadaye akawa hapatikani kwenye simu nikajitahidi kuulizia kwa rafiki yake akanitumia namba nyingine napiga akapokea mke wake nikamuuliza "bro yupo" akasema yupo ngoja ampatie bro akagoma kuongea kisha akatuma bonge la meseji nusu daftari eti nimkome mke wake cha ajabu ni kwamba ni kuwa hata mke niliongea naye maneno mawili " bro yupo" na simjui
 
Ukiona kila anaekuomba hela unafanya namna yoyote umpatie basi ujue kupiga hatua itakuwa ngumu.

Kusaidia ni jambo zuri lakini wema usizidi uwezo. Thamini kila shilling moja yako.
Upo sahihi sana nilikuwa namsaidia mtu kuzidi uwezo wangu miezi mitatu mfululizo mpka nikaona hapa wema umezid uwezo nikamwambia hali yangu ngumu, nililambwa block kila sehemu hadi kesho alooh ,popte alipo Mungu azid kumfanya awe omba omba
 
Usikubali wakakukuta kama walivyokuacha .

Usiwaambie watu mipango yako, fanya kimya kimya itekelezeke.

Kamwe hakuna mtu ambae atakuja kukusaidia kuishi maisha yako, wajibika.

Kuweka akiba na kujiimarisha kiuchumi.

Hata wajinga huzeeka.

Never beg for attention

Yanga bingwa
 
Hakuna ataependa ufanikiwe zaidi ya wazazi wako....acha kuchekea watu wanaoingilia njia zako za maisha, chunga sana chunga sana kuruhusu watu waingiee kihivooo Kwenye maisha yako(usiamini kiumbe kinaitwa binadamu)...watakuumiza.

Kwenye safari ya mafanikio sio kila mtu ni wa kumuamini... kwani umdhaniaye ndiye kumbe siye!!!
Usimpende mtu kupita kiasi huenda baadae akawa adui yako na Usimchukie mtu kupita kiasi huenda baadae akawa rafikiyo.

Duh! Watu mnatema tu madini ya ukweli.
 
Back
Top Bottom