Mshangazi dot com
JF-Expert Member
- Nov 19, 2011
- 1,345
- 3,503
Mapenzi Shikamoo!
Usiku huu nimeshuhudia mkaka anarudisha gari na fremu ya biashara kwa mmama aliyekua anadate naye sababu amepata msichana anayempenda na anataka kumuoa. Huyu mkaka amekua na mahusiano na huyu mmama ambaye ni rafiki yetu kwa zaidi ya miaka mitatu. Aliacha ajira serikalini, akafunguliwa biashara, akapewa gari na mwaka huu kalipiwa fremu yake ya pili kodi mwaka mzima apanue biashara zake.
Nyuma ya pazia kumbe alikutana na msichana, akampenda na akamwambia kila kitu kuhusu mmama wake anayefadhili lifestyle yake. Msichana akamwambia achague kati ya yeye au mmama na kama anampenda arudishe vitu vyote alivyopewa na waanze maisha upya wao kama wao.
Leo kijana kaja na karudisha kila kitu including gari lilikokua na jina lake na umiliki wake halali. Rafiki yetu naye anaugulia maumivu na hataki vitu vilivyorudishwa anasema yule kijana avichukue tu, upande wa pili mkaka hawezi kwa sababu demu wake mpya hataki.
Vipi, ushawahi kukataa hela au kuachia kitu chenye gharama kwa sababu ya mapenzi?
Usiku huu nimeshuhudia mkaka anarudisha gari na fremu ya biashara kwa mmama aliyekua anadate naye sababu amepata msichana anayempenda na anataka kumuoa. Huyu mkaka amekua na mahusiano na huyu mmama ambaye ni rafiki yetu kwa zaidi ya miaka mitatu. Aliacha ajira serikalini, akafunguliwa biashara, akapewa gari na mwaka huu kalipiwa fremu yake ya pili kodi mwaka mzima apanue biashara zake.
Nyuma ya pazia kumbe alikutana na msichana, akampenda na akamwambia kila kitu kuhusu mmama wake anayefadhili lifestyle yake. Msichana akamwambia achague kati ya yeye au mmama na kama anampenda arudishe vitu vyote alivyopewa na waanze maisha upya wao kama wao.
Leo kijana kaja na karudisha kila kitu including gari lilikokua na jina lake na umiliki wake halali. Rafiki yetu naye anaugulia maumivu na hataki vitu vilivyorudishwa anasema yule kijana avichukue tu, upande wa pili mkaka hawezi kwa sababu demu wake mpya hataki.
Vipi, ushawahi kukataa hela au kuachia kitu chenye gharama kwa sababu ya mapenzi?
