Umeshawahi kuletewa nyodo na mhudumu wa kike?

Mwenge ndiyo chuo changu umemaliza mwaka gani?,
 
Niliwahi ila Moto nilio muwashia mbona ilibidi BOSI wake ajizoezoe kuomba msamaha ! Lakini halikuishia Happ nikaendeleza kichambo Nika mobilize WATEJA letu likawa moja hahahaaaa Kilichowakuta hawana hamu na Mimi na hawatafanya hivyo Tena
Ulikuwa unakunywa kinywaji gani?
 
Unakunywa maji ya jero unataka wahudumu wakukimbilie mkuu?
Mkuu Kama ilifikiri kuhusu wahudumu wa baa SIPO HUKO NA SIJAWAHI ENDA MAENEO HAYO!
Mimi nimekuja Petro station kujaza gari mafuta halafu uniletee nyodo,au nimekuja benki,hospitali au ofisi ya umma halafu uniletee nyodo kisa nina kunywa maji ya bomba hakika sikuachi nyodo zako lazima zikutokee masikioni!!!!
 
Mkuu Mimi NIMEKUJA Petro station kujaza gari mafuta halafu uniletee nyodo,au nimekuja benki,hospitali au ofisi ya umma halafu uniletee nyodo kisa nina kunywa maji ya bomba hakika sikuachi nyodo zako lazima zikutokee masikioni!!!!
🤣🤣🤣🤣
 
tatizo la madada wengi kwenye customer care na utoaji wa huduma huko maofisini ni namna walivyozipata hizo kazi... kwa binadamu aliyefuata taratibu za ajira na kupata ajira kwa haki hawezi kudharau mtu yeyote....
 
Jamani Babe pole sana.,
 
Vihudumu vya bank hasa visichana vinakuaga na dharau sana. Mimi sehemu ninayokua mpole ni hospital na polisi tena kama ninayemfahamu hayupo. Sehemu nyingine moto nauwasha saa yoyote
Hivi vihudumu vya bank vinadharau zaidi ya kawaida.Siku moja bana nipo zangu huko kanda ya magharibi mwanchi nikaaenda tawi la Crdb ili nikalipie nusu ya malipo ya manunuzi ya gari niliyoagiza huko Japani,basi bana kale kadada kalileta nyodo sana yani kalinidharau jinsi nilivyo,wearing style..akanambia unataka kulipa hizi hela unazo kweli! Utaweza kununu hii gari ya hivi.![emoji1][emoji1]Ila alipochek balance yangu sasa kulikuwemo mzigo wamaana,heshima ikamjia.
 
Juzi yupo mmoja hivi nimeenda kutoa pesa akaleta nyodo na dharau akizani nimetumwaa na sio mwenye akaunti husika ya benki. Nilimponda sana mjinga yule
Kwamba account yako haina picha? Alafu nani anatumwa kutoa pesa za mtu benki?
 
Hii ndio yenyewe.
Sasa naweza kuacha kusoma zingine.
Haibanetingii.........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…