Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Naomba usinifuatane PM

Niliambiwa sema chochote unachotaka... Utapata

Nikashindwa kusema na ile chance ime-nicost mpaka leo maana wengine waliambiwa waseme wanachotaka wakasema kweli wamepata...

Kuna waliosema wanataka ndoa wameoa na wengine wameolewa mpaka sasa,

Kuna waliosema wanataka kazi wamepata kazi na wanafanya kazi mpaka sasa,

Kuna waliosema wanataka biashara wamepata biashara na wana biashara zao mpaka sasa,

Mimi sikusema chochote maana sikua naamini katika kile kinachofanyika Ila sasa daaah haya Mambo yapo na watu wanafanikiwa kweli.. ukipuuza unakuja kujilaumu mbele
 
sijawai kusikia ana mizimu wala majini
Yeye hutuambia ni dawa za asili alifundishwa akiwa mdogo kusaidia kupata mifungo iliopotea , kuikinga mifugo dhidi ya wanyama wakali
na kujua mtu aliekwenda safari ya mbali kama bado yupo hai ama alishakufa

Dawa hizo pia hutumika kuwaita watoto waliokwenda mjini kutafta maisha na kusahau kurudi kijijn kusalmia wazee ,unambiwa ukifanyiwa hizo dawa utatafta kila njia urudi kwenu hata kwa mkopo ama kutembea kwa mguu

Na kuna ingine alinambia ikitokea hataki mtoto wake aende kutafuta maisha mbali na nyumban anachota unyayo wake anamix dawa na kwenda kuufunika na chungu
kuanzia hapo aliefunikwa hawez hata kufikiria kusafiri wala kwenda kuishi mbali na nyumbani.
Mkuu nipe huo mchongo basi mimi nikutane na huyo bibi anifundishe hizo dawa
 
Kwa kuwa ni shuhuda ntatoa yangu ,Ila staki pm au judgement, haya ni mambo yaliyopita tulifanya ,tusiaemane vibaya.

Kisa Cha kwanza kilitokea 2010 hapo, nlikuwa kijana Sana Ila mganga huyo yupo Ila jina wala namba sitoi. Nlikuwa nauza spare parts za Mercedes ,Faw ,Howo n.k kwa duka la jamaa kutoka turkey hapa dar,nenda keko uulize jina la Mchopa wa spare parts utapewa story ucheke uanguke .
Ss nlikuja kujua kazi nikataka kumpiku boss, mshkaji wangu akanieleza kuhusu mganga fulani Chipu, Sumbawanga mpaka namba nikapewa. Yule mshkaji alipofatlia nkajidai mambo ya mganga staki Ila kimya kimya weekend moja nlisepa kwenda kule mwenyewe .
Ikumbukwe mkoa wa rukwa wala sumbawanga nlikuwa sijawahi kanyaga, nliposhuka stendi nkaulizia kuulingana na maelezeo ya yule braza mpaka kijiji nkakipata , nikiwa almost kufika kwa yule mganga (sitaki kumtaja jina) nlipatana na mbwa alikaa Kama amechizika hvi ,aisee nlitoka mbio akinifukuza ,nliingia ndani ya compound nkihema nikipiga kelele ,kukatokea yule mganga akamfukuza tule mbwa Kisha kunipa karibu .
Kufupisha, Mzee aliniongoza kwa kichaka chake nkapata jiwe limeegemea mti kando Kuna kijumba kidogo na hapo tulipokaa nakumbuka kulikuwa na kisu kina damu Yaani kichafu ,dhahiri kuonyesha kafara watu walikuwa wanafnya pale.
Kimbunga kilianza pale Mzee aliponiuliza ntakacho nkamwambia nataka kumzidi boss niwe tajiri, akaongea mambo yake Kisha lile jiwe likageuka bibi kikongwe ,alinipa kile kisu akaniambia Kama mm ni jasiri na nataka Mali nichukue kisu kile kisha nifuate kinjia fulani kulikuwa hapo ,kile ntapata kife.
Kushika njia Ile nlipatana na kuku nkampita sikushkanisha ,nilipoendelea mbele bila kupata kitu nkakumbuka nliambiwa kile ntapatana nacho ,nilirudi faster Sana.
Mzee yule kuku tulikimbizana ktk ya nyasi ile kumshika nlikata bawa ila akapepea na hio moja mbali sikumpata ,hii tukio ilipita Kama 2 hours hvi nikimkimbiza kuku yule.
Kurudi nlipata kile kibibi kinacheka balaa,nlirudi nimeshika pande LA bawa nlilokata natoka jasho sana ,akaniambia mwanangu una roho ngumu ,nenda mambo yako yatakuwa sawa ,Ila nisiwai kula kitimoto.
Long story short pale keko nilichakata mbususu nyingi Sana Tena Sana ,yule bosi alipanda ndege na familia Yao hawajarudi mpaka leo aisee .
Aliyopo pale kwa ss nijamaa anaitwa shafa ,anauza matunda kando Kuna stationary ya jamaa anaitwa dula wananikumbuka Sana tu .
Nlikuja jisahau nkala sausage one day nkiwa na Dem fulani kisu ,wanawake Yaani wapuzi ,aliponilisha tu moyo ulipasuka nkakumbuka vile nliambiwa , kila kitu kilienda na hewa mpaka zile pisi nlizokuwa zanikimbiza ...Ila nlijenga nyumba moja kubwa Sana mpaka Leo wazazi na dada zangu wanaifaidi , ujana aisee stosahau .
Leo hii nishamaliza masomo nina Mali Ila sijafikia enzi zile .
Walioko keko nenda kwa dula , au Rick Ross bonge fulani anaendesha bajaji pale ,muulize jina Mzee wa mbususu au Mchopa wa spare utapewa bonge LA story kunihusu enzi hizo .
Kwa nliowakosea enzi zile ,nisameheni Bure ni kiburi cha pesa tu na ujana , uchawi upo Ila Kama unajua kuplay smart nao
 
Kisa Cha pili ndio balaa kabisa ,nlirudi kule ,waliponiona walicheka sana yule Mzee na yule kibibi ,nliwapa zawadi Ila bwana uchawi usikie tu ,Kama unasali Sali Sana tu ,Kama ww ni mchawi ,chawika kabisa , Dunia hii Ina mambo mengi Sana .
Nlisaidika Sana mpaka Leo hii Ila sikushauri ww uende kule.
Mie ni a bahati hamna yyte kwetu ashawai kufa Ila wengi nimewapata kule wanamwaga watu Kama upepo ...
Kila mtu na lake
Daaah very interesting wallah
Lakini maisha yana definition pana na fumbo gumu sana kulitambua yahitaji akili kubwa na hekima ya hali juu.

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Kwa kuwa ni shuhuda ntatoa yangu ,Ila staki pm au judgement, haya ni mambo yaliyopita tulifanya ,tusiaemane vibaya.

Kisa Cha kwanza kilitokea 2010 hapo, nlikuwa kijana Sana Ila mganga huyo yupo Ila jina wala namba sitoi. Nlikuwa nauza spare parts za Mercedes ,Faw ,Howo n.k kwa duka la jamaa kutoka turkey hapa dar,nenda keko uulize jina la Mchopa wa spare parts utapewa story ucheke uanguke .
Ss nlikuja kujua kazi nikataka kumpiku boss, mshkaji wangu akanieleza kuhusu mganga fulani Chipu, Sumbawanga mpaka namba nikapewa. Yule mshkaji alipofatlia nkajidai mambo ya mganga staki Ila kimya kimya weekend moja nlisepa kwenda kule mwenyewe .
Ikumbukwe mkoa wa rukwa wala sumbawanga nlikuwa sijawahi kanyaga, nliposhuka stendi nkaulizia kuulingana na maelezeo ya yule braza mpaka kijiji nkakipata , nikiwa almost kufika kwa yule mganga (sitaki kumtaja jina) nlipatana na mbwa alikaa Kama amechizika hvi ,aisee nlitoka mbio akinifukuza ,nliingia ndani ya compound nkihema nikipiga kelele ,kukatokea yule mganga akamfukuza tule mbwa Kisha kunipa karibu .
Kufupisha, Mzee aliniongoza kwa kichaka chake nkapata jiwe limeegemea mti kando Kuna kijumba kidogo na hapo tulipokaa nakumbuka kulikuwa na kisu kina damu Yaani kichafu ,dhahiri kuonyesha kafara watu walikuwa wanafnya pale.
Kimbunga kilianza pale Mzee aliponiuliza ntakacho nkamwambia nataka kumzidi boss niwe tajiri, akaongea mambo yake Kisha lile jiwe likageuka bibi kikongwe ,alinipa kile kisu akaniambia Kama mm ni jasiri na nataka Mali nichukue kisu kile kisha nifuate kinjia fulani kulikuwa hapo ,kile ntapata kife.
Kushika njia Ile nlipatana na kuku nkampita sikushkanisha ,nilipoendelea mbele bila kupata kitu nkakumbuka nliambiwa kile ntapatana nacho ,nilirudi faster Sana.
Mzee yule kuku tulikimbizana ktk ya nyasi ile kumshika nlikata bawa ila akapepea na hio moja mbali sikumpata ,hii tukio ilipita Kama 2 hours hvi nikimkimbiza kuku yule.
Kurudi nlipata kile kibibi kinacheka balaa,nlirudi nimeshika pande LA bawa nlilokata natoka jasho sana ,akaniambia mwanangu una roho ngumu ,nenda mambo yako yatakuwa sawa ,Ila nisiwai kula kitimoto.
Long story short pale keko nilichakata mbususu nyingi Sana Tena Sana ,yule bosi alipanda ndege na familia Yao hawajarudi mpaka leo aisee .
Aliyopo pale kwa ss nijamaa anaitwa shafa ,anauza matunda kando Kuna stationary ya jamaa anaitwa dula wananikumbuka Sana tu .
Nlikuja jisahau nkala sausage one day nkiwa na Dem fulani kisu ,wanawake Yaani wapuzi ,aliponilisha tu moyo ulipasuka nkakumbuka vile nliambiwa , kila kitu kilienda na hewa mpaka zile pisi nlizokuwa zanikimbiza ...Ila nlijenga nyumba moja kubwa Sana mpaka Leo wazazi na dada zangu wanaifaidi , ujana aisee stosahau .
Leo hii nishamaliza masomo nina Mali Ila sijafikia enzi zile .
Walioko keko nenda kwa dula , au Rick Ross bonge fulani anaendesha bajaji pale ,muulize jina Mzee wa mbususu au Mchopa wa spare utapewa bonge LA story kunihusu enzi hizo .
Kwa nliowakosea enzi zile ,nisameheni Bure ni kiburi cha pesa tu na ujana , uchawi upo Ila Kama unajua kuplay smart nao

Kuna siri gani kuhusu kitimoto,mana waganga wanaikataa na huku kwenye dini za wazungu na waarabu wanaikataa,
 
Waganga wazushi tu niliibiwa simu ktk mazingira ya kutatanisha simu kala na gharama sn.

Ss mm sio mtu wa ulozi kama mshana jr, akaja mwanangu mmoja na kuniambia anipeleke kwa mganga hiyo simu aliyeiba atarudisha.

Tumefka kwa sangoma baada ya kuelezea shida zetu mixer akasaga majanimajani si jui ni ya aina gani akasema nichemshe ninywe simu itarudi.

Sasa nipo njiani najiuliza simu aibe mwingine mijani ya dawa ninywe mie, halafu kuna uhusiano gani Kati ya kurudi kwa simu na mm kunywa Yale majani

Aahh kudadeki niliitupilia mbali ile mijani na mpaka ss siamini ulozi na hiyo simu nishasamehe[emoji3061]

Sent from my itel W4001P using JamiiForums mobile app
Ingejaribu ndio uanze kulalamika
 
TRUE STORY

Miaka ya nyuma kidogo kipindi tupo secondary shule moja ya bweni. Siku moja tulikua tumeenda kukusanyika katika moja ya jengo la shule kulikua na kikao.

Kama unavyojua wale madoja hua hawakosekani. Sasa ile kurudi bwenini tumemaliza kikao tulikua tunatabia ya kuficha simu sehemu mbalimbali kwa sababu tulikua tunazitumia kwa magendo.

Bwana we wa kwanza akaanza kulalamika haoni simu yake ndipo kilamtu akaanza kuhakikisha kama je! Yake imesalimika? Kwakweli simu zote zilikua zimeibiwa nyuso zetu zikawa zenye huzuni sana.

Mmoja wetu akashauri twende kwa mganga kwa changamoto ile na umuhimu wa simu kwa wakati ule hakuna aliepinga lile wazo.

Safari ya kwenda kwa mganga inaanza kwa idadi tulikua takribani watu sita (6). Tukafika kwa mganga tukaambiwa wanaoruhusiwa kuingia ni watatu tu. (3)

Basi Mganga akatuamuru tueleze kilichotupeleka baada ya maelezo akatuuliza chumba chenu mnaishi watu wangapi tukampa idadi akatupa karatasi na peni akatuambia niandikieni majina ya watu wote wanaoishi katika hicho chumba.

Baada ya kumpatia karatasi ya majina akafanya mambo mambo pale baadae akatupa majibu kwamba simu zenu zipo salama sasa nendeni nyuma ya chumba chenu kunashimo limechimbwa usawa wa dirisha fukueni mtazikuta simu zenu zimetiwa kwenye mfuko.

Kabla hatujaondoka akatutajia jina la mtu aliefanya kitendo hicho lakini ONYO alilotupatia ni kwamba huyo mtu alofanya kitendo hiko tusithubutu kabisa kumpiga bali kesho yake turudi nae kwa mganga.

Hili ndo tukio langu pekee nililoshuhudia kutoka kwa Mganga.
Hujaendeleza kuwa mlipata au?...
 
Mimi nina sheikh wangu mmoja hapo Magomeni Mwembe Chai, ni noma kishenzi. Yeye hakopeshi, ukitaka kuua mtu au kumpa mtu laana ya kuokota makopo anakuambia niletee kuku tu au nyama kilo mbili ale na familia yake.....anadedisha mtu bila hata huruma.
Huruma itoke wapi kuna watu wanastaili kukutana na hasira ya mnyama na si hasira ya kibinadamu. Huyo mganga awadedishe tu kwakweli na tena awauwe sana kuna watu wanajikuta wao ni Mungu kumbe ni wapumbavu wakubwa
 
Nilikuwa nasafirisha mkaa mpaka dar bila vibali!

Nikikaa mbele ya gari trafiki na watu wa maliasili hawaioni gari mpaka Dar.

Kwa nin niliacha....with time mganga aliniambia kwa sasa nadaiwa sadaka ya damu ya mbuzi watatu, nikatoa
Baadae akaniambia nipate mimba niitoe nimpelekee.

NIKACHAPA LAPA ILA NILIZULUMIWA HELA, VIWANJA, GARI nikabaki kama mwanafunzi wa secondary

Namshukuru MUNGU nimeanza upya bila ndumba
Nyongeza: Kwa huyo mganga nilikutana na vigogo kadhaa wa mashirika na idara za serikali na NGO ...wakuu wa vyombo vya usalama.

UNAJUA KWA NIN WATU WANANUNUA VX?

UKIONA mtu ana Vx posta anatoka kazini saa 9:30 anakimbia kwa mganga , anajigangua asubuhi saa tisa ,kumi anaanza Safari kurudi kazini.

Nilishangaa kuona VX kibao zikiingia usiku nikawauliza hawa wote ni watoto wa hiki kijiji, mmebarikiwa...jibu hawa ni mabosi na vigogo wa posta.
Kama ni kweli, Basi better late than never [emoji137][emoji137][emoji137][emoji1787][emoji1787]
 
Naomba hapa wale watembea kwa sangoma mtoe shuhuda zenu mliyokutana nayo kwa waganga na toka umeanza kwenda Mganga.

Alikusaidia nini ukaona kabisa shida yako imetatuliwa kwa nguvu ya mganga.

Ikiwezekana mtaje mganga alipo na wengine wakauone uwezo wake.
Ni story kweli ya jamaa yangu wa karibu sana.

Mkewe alianza kuumwa pressure akiwa na ujauzito wa miezi 6.

Wiki nyumbani, wiki hospitali yalikuwa ndiyo maisha yake.

Tulifikia wakati tulishauri daktari atoe mimba mama apone. Daktari alikataa kabisa. BP ilikuwa inapanda hadi 180.

Huwezi amini, alijifungua salama japokuwa mtoto alikuwa njiti.

Cha ajabu, baada ya kujifungua tu, tumbo lilijaa mara mbili ya alipokuwa na mimba. Alivimba miguu kiasi cha kushindwa hata kusimama. Daktari anasema licha ya hali hiyo, hawaoni tatizo lolote katika kupima na hata BP imerudi hadi 110.

Ikawa mshikemshike, hali tete. Si mgonjwa wala watunzaji na daktari mwenyewe tumekata tamaa. Ndipo mmoja wa ndugu akasema nitatenda dhambi mgonjwa apone.

Alikuwa mkristo wa imani ya juu. Wale wa kusali na kulala kanisani. Alikwenda kwa witch doctor. Hakupewa chochote zaidi ya kuambiwa arudi hospitali na kwamba atajua yeye cha kufanya na mgonjwa baada ya saa 3 atasimama.

Alipofika hospitali mgonjwa alishazima. Anasubiriwa tu akate moto.

Baadaye akawa kama ameshtuka fulani, akafungua macho. Akaonekana kurejea uzimani.

Kweli baada ya saa 4 hivi, mgonjwa aliweza kusimama kwa kujitegemea. Akawa mzima tena.

Sote tulimwamini yule witch doctor. Shemeji yetu mzima hadi leo, tena kwa gharama ya sh. 30000/= tu.
 
Kuna rafiki yangu alikuwa ana mapepe sana na mdadisi. Siku moja usiku tukiwa msibani akamwona mtu anachoma ganja, akataka kujaribu kwani hakuwahi kuvuta ktk maisha yake. Sasa sina hakika kama ni madhara ya ganja au lah, ila baada ya siku kama mbili hivi akaanza kuwehuka taratibu. Wehu wake ukawa unamtuma kuhubiri neno la Mungu na kuombea watu. Hali ilivyozidi kuwa mbaya akaanza kuwa mchafu na hatimaye kuokota makopo kabisa. Mama yake alitutuhumu marafiki zake kwa kumloga mwanaye kwa kuwa alikuwa ametuzidi maendeleo. Akaanza kupambana kwenda kwa waganga mbali mbali hadi kufikia kufilisika katika biashara zake na kuuza nyumba. Baadaye alivyoishiwa pesa akakata tamaa na kumwacha mwanaye aendelee kurandaranda tu mtaani. Sasa kuna rafiki yetu alikuwa ndio amehitimu masomo yake ya udaktari wa maswala ya afya ya akili, alipomuona akasema tumpelekee akajaribu kumtibu. Na kweli alifanikiwa na jamaa yetu akapona kabisa, mpaka leo yupo sawa kabisa.
Alimtibuje huyo jamaaa
 
Back
Top Bottom