Umewahi kuachwa na Basi au Treni? Ulifanya nini kuliwahi

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Nyie usiombe kuachwa na Mabasi ya Mikoani hasa kipindi kile Stendi kuu ilikua Ubungo πŸ˜….

Kuna siku nilikua naenda Mbeya sasa nimefika ubungo kumbe nimesahau Tiketi, ikanibidi nirudi kufuata. Nimefika stendi Basi ndo kwanza linatoka nililia kama mtoto mdogo ikabidi watu wanisaidie kulisimamisha. Nilisemwa hadi nilijuta.
Vipi wewe umewahi kuachwa na mabasi au Treni?
 
Nataja na jina kabisa kwa jinsi nilivyoadhirika. Esther, nilikata tiketi ya kuondoka kesho yake, kwenye kituo alinipita makusudi, nilichukuwa bodaboda kumbe mwendeshaji alikuwa ameweka ganja, nusura hiyo siku nipoteze maisha. Bahati tulilikuta kwenye follen ya upimaji uzito.
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…pole
 
ukiona mtu anachwa na bus basi akili zake hazichaji wengi wanakua na uzezeta au vimelea vya usonjo
 
Nimefika tu custom ya bukoba na meli naiona ile inaondoka kuelekea mwanza kwa kweli nilipatwa na kimuhe muhe maana ilikuwa ni lazima asubuhi niwe mwanza,ndipo wenyeji wa pale waliponishauri niiwahi eneo la kemondo nami fasta nikapanda kipanya ili kusogea kemondo,njiani naona kama gari haiendi basi nikajua nimeshafeli kuiwahi CHA AJABU NIMEFIKA KEMONDO IKABIDI MIMI NDIO NIISUBIRI MELI KWA ZAIDI YA SAA ZIMA[emoji23][emoji23]
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Nshawah kuachwa msamvu on my way to arusha......nlkua natoka school!!! Pesa yote ya kula nkamlipa bodaboda kuifkuzia.....
 
Tuliakata tickets, then alfajiri nikamuamsha asema alale kidogo....
Nilipo maliza kujiandaa nikaenda kupanda bus.
Baafa ya hapo tuliachana tu, maana she wasn't care about time management blood hell....☹️
Lakini watako soma heading kwa haraka, watasema walisha achwa na Kalekwa, Mwajabu, Kaundime, Kalunde nk:
 
Tulio achwa na ndege za kimataifa tuna comment wapi?
 
Kuna wajinga wa Super feo Mwanza to Songea. Walinambia wanatoka stendi Nyegezi saa 11 alfajiri ila 10 na nusu niwe barabarani kumbe wanatoka saa 10. Bahati mbaya nilikuwa napandia kituo mbele ya stand. Saa 11 nipo kituoni naambiwa imeosha tayari. Nilizama mfukoni tena ili safari iendelee.
 
Ni zamani kidogo, niliwahi kuachwa na bus la Exercutive, nilikuwa naenda Harare kwenye summit fulani. Bus lilikuwa linaondoka saa 11 alfajiri. Gari ya kwanza.

Nikapitiwa na usingizi, nikaamshwa na simu yao. Nikapiga hesabu nikaona siwezi kuwahi, nikadanganya kuwa niliahirisha safari na nilitoa taarifa ofisini kwao kwa simu.

Hiyo ilileta mgogoro wa kwenye simu na jamaa wao aliyenipigia, mimi nilishikilia msimamo wangu, hadi akakata simu kwa hasira.

Kulipokucha nikaenda ofisini kwao Kisutu, nikaenda kushikilia msimamo wangu. Huko nako ilikuwa balaa, nikashikilia kuwa nilipiga simu kuahirisha safari.

Wao waling'ang'ania kuuliza nilipiga namba ipi, nami nikawaambia sikumbuki, ila ni moja ya namba iliyo kwenye ticket.

Kitu kilichoniokoa ni kwamba ticket yangu ilikuwa na ya kurudi, maana waliniambia nina bahati nilikuwa na ticket ya kurudi. Wakanipa ticket nyingine, nikaondoka baada ya siku mbili.

Ova
 
Boti ya kwenda zenji Iliniacha kisa papuchi

Nikaona aibu kurudi home nikalala lodge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…