Umewahi kuchapwa/kupigwa na mzazi/mlezi?

Umewahi kuchapwa/kupigwa na mzazi/mlezi?

Mi baba aliwah nipiga mpaka kuhisi kuzimia ,hadi nikawa namuambia baba nataka kuzimia ,,tokea hapo hakunipiga tena ,nimekumbuka nimejisikia vibaya lo
Ujue umenifanya nicheke kwa nguvu sana..eti nataka kuzimia[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Dah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
Duh!!bora utuambie tu. I'm curious,ulifanya nn[emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
Mmh... mi nimechapwa hadi niliwachukia. Tena saingine kosa la mmoja tunapigwa wote watatu. Mdogoetu alikua mdogo.
Nilichokuja kugundua baadae ni kua wazazi walikua na stress mno.
Watu na ndugu walitamani maisha yetu ila hawakujua tu yanayoendelea. Migogoro yao ya ndoa ilitutesa sana sana.. SANA!
Mkisikia ukatili kwa watoto ndio ule. Kila siku Nilitamani kuihama ile nyumba. Nilivyomaliza six tu nikabahatisha kibarua cha hela nzuri halafu mkoa wa mbali. Nilishukuru

Mdogoangu anaenifatia ni wa kiume. Yeye alifaulu mkoani kuanza kidato cha kwanza ikawa sababu. Hakurudi tena hata likizo.

Nimepigwa hadi form 6 nachapwa vikosa vyenyewe sasa. Saingine kutoa Radio Tumaini kuweka radio One.
Maskini,pole sana. Ni kweli muda mwingine watoto wanapigwa kwa sababu ya stress za wazazi..wanatafuta kwa kumalizia hasira. Nmehuzunika sana[emoji20]
 
Jamaniiii.
Mimi nakumbuka kisa changu,nilivyokuwa mtoto age ya miaka 7-10 nilikuwa nasumbuliwa sana na kifua cha kikohozi. Yaani nilikuwa nikipigwa na kaubaridi kidogo tu naanza kukohoa. Sasa nikawa Nina Tabia ya kuogelea mvua zikinyesha. Siku moja bimkubwa akanibamba akaniambia wewe una tatzo la kifua,haifai uogelee mvua. Na nilikuwa nikiogelea mvua tu mpaka naumwa kabisa siku zingine ila nikawa sisemi tatzo la homa ni nini. A couple of days baada ya kupewa warning nikarudia kuogelea halafu mama alikuwa anatoka kazini,kapita na mwavuli wake si akanibamba nipo kwenye mvua tena kwenye vidimbwi vya maji machafu pia,jamani nilivyorudi nyumbani,alinizabua maana nikisema kupigwa haitoshi. Alinizabua vya kutosha sana mpaka akaanza kulia yeye mwenyewe. Duh!!! Sitokaa nisahau kile kipigo a.k.a mkong'oto heavy
 
Enzi hizo nipo la tano napenda sana Mpiraa bhanaa.. Nyumbani nachelewa kurudi!! Yakaja matokeo nimekuwa mtu wa 9 akati kawaida ni 1 mpak 4 mwisho...khaaa Nadhani siku ilee Hata Baba wa mbinguni alisikia kilio changu...Nilikula kibanoooo toka kwa bi maza mpka mkono wake ulivimba..!! Tulipofungua shule uwanja wa mpira ulikuwa kituo cha Polisi yani....na ndoto za kuwa mcheza mpira zikafutika jumla.
 
Dah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
Pole sana Mkuu, nimecheka sana. Kwa adhabu hiyo hilo kosa lilikuwa ni kali sana.
 
Nilikuwa mtundu sana nilipokuwa primary, kuna siku mzee alirudi na radio mpya, nikaifungua yote, nikashindwa kuifunga, na hii ilikuwa radio ya tatu kuiharibu. Sasa mzee aliporudi toka job alipa bakora nne za maana, na adhabu ikaendelea kwa wiki nzima kila akitoka job ni salam na fimbo moja then tunaendelea na mambo mengine.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mimi nilichapwa na baba tena kwenye zizi LA ng'ombe dada alikuwa mtoro shuleni tulikuwa tukisoma shule Moja Alf mimi sikuwa nasema nilikuwa namtunzia siri waalimu wakiniuliza namtetea lbd anaumwa au anauguza,,,, sasa siku mama alipoitwa shuleni mmmh nilijuta kuzaliwa makosa ya mtu mwingine nikachapwa mm
 
Mimi nilikuwa Mtundu sana. Hii ilisababisha mpaka nikapelekwa shule ya boarding nikiwa na miaka minne pekee.

Siku moja ambayo mama na baba walinichangia ni siku ambapo nilienda kumtega mzee kipofu na kumwangusha. Nilitengeneza kamba alafu nikaitegesha njiani, mzee kipofu alipokuja anatembea na mkongojo wake nikainyanyua na kumuangusha. Nikabaki hapo pembeni nacheka kwa nguvu.

Asee, hiyo kipigo nilichopata sitakaa nisahau asee. Nilichapwa fimbo za kutosha maana nilishakuwa sugu kwenye mkanda.

Mungu anisamehe kwa niliyomtendea yule Mzee. Naamini hata huyo mzee kanisamehe pia, nilikwenda jumuomba msamaha kabla hajafariki, RIP.
dah mkuu ulikua na roho mbaya sana.
 
Dah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
Inaonekana ww ulikuwa zaid ya mafia jina lako tu ni jibu tosha
 
Mmh... mi nimechapwa hadi niliwachukia. Tena saingine kosa la mmoja tunapigwa wote watatu. Mdogoetu alikua mdogo.
Nilichokuja kugundua baadae ni kua wazazi walikua na stress mno.
Watu na ndugu walitamani maisha yetu ila hawakujua tu yanayoendelea. Migogoro yao ya ndoa ilitutesa sana sana.. SANA!
Mkisikia ukatili kwa watoto ndio ule. Kila siku Nilitamani kuihama ile nyumba. Nilivyomaliza six tu nikabahatisha kibarua cha hela nzuri halafu mkoa wa mbali. Nilishukuru

Mdogoangu anaenifatia ni wa kiume. Yeye alifaulu mkoani kuanza kidato cha kwanza ikawa sababu. Hakurudi tena hata likizo.

Nimepigwa hadi form 6 nachapwa vikosa vyenyewe sasa. Saingine kutoa Radio Tumaini kuweka radio One.
Daah!!! Poleni sana!
 
Jamaniiii.
Mimi nakumbuka kisa changu,nilivyokuwa mtoto age ya miaka 7-10 nilikuwa nasumbuliwa sana na kifua cha kikohozi. Yaani nilikuwa nikipigwa na kaubaridi kidogo tu naanza kukohoa. Sasa nikawa Nina Tabia ya kuogelea mvua zikinyesha. Siku moja bimkubwa akanibamba akaniambia wewe una tatzo la kifua,haifai uogelee mvua. Na nilikuwa nikiogelea mvua tu mpaka naumwa kabisa siku zingine ila nikawa sisemi tatzo la homa ni nini. A couple of days baada ya kupewa warning nikarudia kuogelea halafu mama alikuwa anatoka kazini,kapita na mwavuli wake si akanibamba nipo kwenye mvua tena kwenye vidimbwi vya maji machafu pia,jamani nilivyorudi nyumbani,alinizabua maana nikisema kupigwa haitoshi. Alinizabua vya kutosha sana mpaka akaanza kulia yeye mwenyewe. Duh!!! Sitokaa nisahau kile kipigo a.k.a mkong'oto heavy
Hahaha! Pole!!!
Kuzabua na kukong'otwa ndo inaeleze vizuri vipigo vingine.
 
Enzi hizo nipo la tano napenda sana Mpiraa bhanaa.. Nyumbani nachelewa kurudi!! Yakaja matokeo nimekuwa mtu wa 9 akati kawaida ni 1 mpak 4 mwisho...khaaa Nadhani siku ilee Hata Baba wa mbinguni alisikia kilio changu...Nilikula kibanoooo toka kwa bi maza mpka mkono wake ulivimba..!! Tulipofungua shule uwanja wa mpira ulikuwa kituo cha Polisi yani....na ndoto za kuwa mcheza mpira zikafutika jumla.
Jamani!!! Waliziua ndoto zako kwa kibanooo!!!
 
Nilipigwa mara ya mwisho na baba nikiwa la tano.

Kaondoka zake mjini kaniambia nifanye kazi za nyumbani, nioshe vyombo na kufanya usafi ikiwa ni pamoja na kuteka maji.

Kidume nikapiga chai nikaaenda misele ile narudi nakuta mzee kafika alikuwa na boot moja imeandikwa chini ya unyayo BASE basi bhna nikasalimia mzee na kuingia ndani.

Ile naingia ndani naona giza la ghafla kumbe milango imefungwa nipo na mzee ndani hakuna kazi imefanyika, stiki zikaanza za rejareja hadi shingoni.

Duh BASE ikanikalia shingoni nikapewa stiki za kutosha ili kujiokoa nikavunga nimezimia anapiga silii wala kutikisika.

Mzee anahisi ameua akafungua milango wee nilitoka nduki kama Hamorapa.
 
Back
Top Bottom