Mahondaw
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 67,252
- 168,563
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
hahahaha, dah.Me nilipomwambia nimeipigia kura CCM
Watoto wa mom and dad Hao..Basi ukute wewe na kudeka
Ujue umenifanya nicheke kwa nguvu sana..eti nataka kuzimia[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Mi baba aliwah nipiga mpaka kuhisi kuzimia ,hadi nikawa namuambia baba nataka kuzimia ,,tokea hapo hakunipiga tena ,nimekumbuka nimejisikia vibaya lo
Duh!!bora utuambie tu. I'm curious,ulifanya nn[emoji13] [emoji13] [emoji13]Dah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
Maskini,pole sana. Ni kweli muda mwingine watoto wanapigwa kwa sababu ya stress za wazazi..wanatafuta kwa kumalizia hasira. Nmehuzunika sana[emoji20]Mmh... mi nimechapwa hadi niliwachukia. Tena saingine kosa la mmoja tunapigwa wote watatu. Mdogoetu alikua mdogo.
Nilichokuja kugundua baadae ni kua wazazi walikua na stress mno.
Watu na ndugu walitamani maisha yetu ila hawakujua tu yanayoendelea. Migogoro yao ya ndoa ilitutesa sana sana.. SANA!
Mkisikia ukatili kwa watoto ndio ule. Kila siku Nilitamani kuihama ile nyumba. Nilivyomaliza six tu nikabahatisha kibarua cha hela nzuri halafu mkoa wa mbali. Nilishukuru
Mdogoangu anaenifatia ni wa kiume. Yeye alifaulu mkoani kuanza kidato cha kwanza ikawa sababu. Hakurudi tena hata likizo.
Nimepigwa hadi form 6 nachapwa vikosa vyenyewe sasa. Saingine kutoa Radio Tumaini kuweka radio One.
Pole sana Mkuu, nimecheka sana. Kwa adhabu hiyo hilo kosa lilikuwa ni kali sana.Dah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Nilikuwa mtundu sana nilipokuwa primary, kuna siku mzee alirudi na radio mpya, nikaifungua yote, nikashindwa kuifunga, na hii ilikuwa radio ya tatu kuiharibu. Sasa mzee aliporudi toka job alipa bakora nne za maana, na adhabu ikaendelea kwa wiki nzima kila akitoka job ni salam na fimbo moja then tunaendelea na mambo mengine.
[emoji23] [emoji23] [emoji23]Nilikula kwa watu... Mama akatandika stiki nyingi sana.. Imepita miaka 18 sijarudia tena
dah mkuu ulikua na roho mbaya sana.Mimi nilikuwa Mtundu sana. Hii ilisababisha mpaka nikapelekwa shule ya boarding nikiwa na miaka minne pekee.
Siku moja ambayo mama na baba walinichangia ni siku ambapo nilienda kumtega mzee kipofu na kumwangusha. Nilitengeneza kamba alafu nikaitegesha njiani, mzee kipofu alipokuja anatembea na mkongojo wake nikainyanyua na kumuangusha. Nikabaki hapo pembeni nacheka kwa nguvu.
Asee, hiyo kipigo nilichopata sitakaa nisahau asee. Nilichapwa fimbo za kutosha maana nilishakuwa sugu kwenye mkanda.
Mungu anisamehe kwa niliyomtendea yule Mzee. Naamini hata huyo mzee kanisamehe pia, nilikwenda jumuomba msamaha kabla hajafariki, RIP.
Inaonekana ww ulikuwa zaid ya mafia jina lako tu ni jibu toshaDah... Mie kosa nililofanya sisemi.....ila mshua alinipa kipondo cha kufa mtu... Magumi, mateke na vibao....kisha akanining'iniza mtini kichwa chini miguu juu siku2 bila kunywa wala kula [emoji13] [emoji13]
Daah!!! Poleni sana!Mmh... mi nimechapwa hadi niliwachukia. Tena saingine kosa la mmoja tunapigwa wote watatu. Mdogoetu alikua mdogo.
Nilichokuja kugundua baadae ni kua wazazi walikua na stress mno.
Watu na ndugu walitamani maisha yetu ila hawakujua tu yanayoendelea. Migogoro yao ya ndoa ilitutesa sana sana.. SANA!
Mkisikia ukatili kwa watoto ndio ule. Kila siku Nilitamani kuihama ile nyumba. Nilivyomaliza six tu nikabahatisha kibarua cha hela nzuri halafu mkoa wa mbali. Nilishukuru
Mdogoangu anaenifatia ni wa kiume. Yeye alifaulu mkoani kuanza kidato cha kwanza ikawa sababu. Hakurudi tena hata likizo.
Nimepigwa hadi form 6 nachapwa vikosa vyenyewe sasa. Saingine kutoa Radio Tumaini kuweka radio One.
Hahaha! Pole!!!Jamaniiii.
Mimi nakumbuka kisa changu,nilivyokuwa mtoto age ya miaka 7-10 nilikuwa nasumbuliwa sana na kifua cha kikohozi. Yaani nilikuwa nikipigwa na kaubaridi kidogo tu naanza kukohoa. Sasa nikawa Nina Tabia ya kuogelea mvua zikinyesha. Siku moja bimkubwa akanibamba akaniambia wewe una tatzo la kifua,haifai uogelee mvua. Na nilikuwa nikiogelea mvua tu mpaka naumwa kabisa siku zingine ila nikawa sisemi tatzo la homa ni nini. A couple of days baada ya kupewa warning nikarudia kuogelea halafu mama alikuwa anatoka kazini,kapita na mwavuli wake si akanibamba nipo kwenye mvua tena kwenye vidimbwi vya maji machafu pia,jamani nilivyorudi nyumbani,alinizabua maana nikisema kupigwa haitoshi. Alinizabua vya kutosha sana mpaka akaanza kulia yeye mwenyewe. Duh!!! Sitokaa nisahau kile kipigo a.k.a mkong'oto heavy
Jamani!!! Waliziua ndoto zako kwa kibanooo!!!Enzi hizo nipo la tano napenda sana Mpiraa bhanaa.. Nyumbani nachelewa kurudi!! Yakaja matokeo nimekuwa mtu wa 9 akati kawaida ni 1 mpak 4 mwisho...khaaa Nadhani siku ilee Hata Baba wa mbinguni alisikia kilio changu...Nilikula kibanoooo toka kwa bi maza mpka mkono wake ulivimba..!! Tulipofungua shule uwanja wa mpira ulikuwa kituo cha Polisi yani....na ndoto za kuwa mcheza mpira zikafutika jumla.