Umewahi kufanyiwa kituko gani na Fundi Nguo (Cherehani) mpaka ukatamani msingefahamiana?

Umewahi kufanyiwa kituko gani na Fundi Nguo (Cherehani) mpaka ukatamani msingefahamiana?

Mimi mwamuzi wa Tanzania ila wajinga wakizingua nawalisha makonde.
Kuna level ya ujinga haiwezi kuondoka bila fimbo au ngumi .
Mtu namwambia nipe nguo yangu anasema it's impossible kwakuwa nimeshaikatakata . Nikamwambia nipe tu nitakulipa pesa tuliyokubaliana anatoa nguo iko vilevile kama nilivyompa
Wewe kumbe mgomvi alaaah
 
Mpuuzi sana yule fundi,miaka ya nyuma kidogo suruali za vitambaa za kushona zilikuwa dili,sasa nami nikaona nianze kuvaa za kushona baada ya kuelekezwa kwa fundi mmoja mzuri,nilipeleka kitambaa cha suruali moja akatoa suruali moja nzuri sana hivyo nikaamua kununua vitambaa vya suruali tano.Kumbe yule fundi akampa mwanafunzi wake kushona suruali zangu.Kwa namna zile suruali zilivyo ilinilazimu kuzigawa zote maana nilikuwa nakasirika kila ninapoziona.Ni zaidi ya miaka 25 sijawahi kushona suruali kwa fundi kwa sababu ya yule mpuuzi.
 
Sista aliambiwa na fhndinkushona nguo 25000. Akaenda kwa fundi kamseleleko akamabia kushona 12000.
Basi akampa advanve 10000 ibakie 2000. Siku anaenda kuichukua sound za kutosha akashona. Asubuhi anatest nguo ile zipu imetatuka pyaaa. Hahahahahaha na fundinhapatikani hewani hahahahahaha.
 
Fundi ambaye alikuwa ananishoneaa nguo Kwa zaidi ya miaka kumi hatimayeee nimemwaga rasmi...dharau alizonionesha zilinitoshaa nikasemaa no enough is enough 🙌 imagine nguo nguo nilimpa Kwa makubalioano ya one week na nguo ilikuwa nivae kwenye tukio na nisare...kabla ya siku ya kuchukuaa siku mbili kabla nikampigia cm akasema usijari sister naelewaa hiloo nguo itakuwa tayari,siku tayari...siku mojaa kabla nikampigia tenaa akaniambia sawaa usijali😅😅siku ya kwenda kuchukuaa kwanza sikumkutaaa kbsa ofisini nampigia cm akaniambia nashonea nyumbanii sister nikasemaa hiii... nikamwambia nguo naivaa keshoo kwenye tukiooo.. Akasema uwahii asubuhii itakuwaa tayari... asubuhii by saa nne nikawa tenaa hapoo ofisini sikumkutaa tenaaa nikampigia tenaa hakupokea cm tenaa na nguoo sikuvaa hiyooo..nilipanic hatarii nikaiziraa hiyoo nguooo nimemuamaa kbsaaaa...Im done na yeye🙌🙌🙌
 
Mie pia si mvaaji sana wa nguo za kushona kwa mafundi wetu hawa, basi siku hiyo nikashawishiwaaa nikaona poa, nikabeba kitenge kwa fundi nikampa mshono rahisi kweli kweli maana sivai nguo fupi, siku nafika kuchukua nguo nakuta kitukooo,nilichukia na hivi nina kigugumizi hata kuongea nilishindwa, nikamlipa na nguo nikamuachia kenge yule...!
🤣🤣
 
Mafundi wanazingua sana.
Kuna mahali nilikuwa napeleka nguo kushonewa, mmiliki wa ofisi alikuwa na mafundi wazuri sana kwa kushona nguo.

Nguo ya 1, ya 2 hakuna usumbufu, kuna siku nikapeleka vitambaa 2 na kumkuta fundi mwenyewe, boss wake hakuwepo (Mara zote ulikuwa ukipeleka nguo unafanya mawasiliano na boss). Nikawasiliana nae vizuri akampatia maelekezo fundi wake.

Siku ya kufuata nguo imefika nguo hazionekani wala vitambaa..😁
Tafuta tafuta wapi! Kapigiwa simu fundi kuulizwa fundi hapokei simu (Kumbe walikorofishana na boss wake akahama ofisi pamoja na vitambaa vya wateja alivyokuwa amekabidhiwa kushona.

Nikaona hapa nisipokuwa mkali hawa watanichukulia poa. Nikawaambia sitoki hapa ofisini mpaka nikabidhiwe nguo/vitambaa vyangu.

Mwisho wa siku nikapatiwa namba ya fundi nideal naye mwenyewe.
Aisee, nilideal nae kwa vitisho vingi sana mwisho wa siku akafunguka na kunielekeza mahali alipo. Kajichimbia Sinza, humo ndani huwezi kujua kama kuna ofisi. (Nyumba ofisi).

Muda wote huo hata nguo ilikuwa haijashonwa, zile heka heka ndo zikamfanya akate vitambaa. Nilikaa kusibiri amalize nikaondoka na nguo zangu.

Mafundi hawana tofauti na madalali.
 
Nakumbuka nimefauri kwenda form One,enzi izo tnavaa makaptura polyester gly,basi mzee akanipa pesa nikanunue kitambaa kariakoo ni duka Moja nyuma ya sok kuu karibu na tafifu aina ya vitambaa Ivo vilikiwa vinapatikana.Tukaenda tulikuwa wanafunzi kama watano wote tulifauru kutoka shule Moja.Nimerudi direct kwa fundi hakuwa mbali sana na nyumbani,kanipima Kila kitu akasema baada ya sk nne zitakuwa tayar.Mie Sasa mchchto kibao katika chezacheza pitapita nachungulia kwambali naona anaendelea na kazi nikawa nashtuka mbona kaptura anayoshona ni ndogo au ya mwingine.Nikajipa moyo nikajisemea labda wasiwasi wangu tu.Siku ikafika nikaenda kujaribu nyumbani aisee ni skin tight, zinanibana sana.Nikaridisha kwa fundi huku machozi yananilengalenga .Hairekebishiki hakuna hata kipande cha kuongeza.Kibaya zaidi kabla sijanunua yy ndoalinipima na akasuggest kitanbaa cha 2.5m.Mzuka wote wakureport shule ukaisha kabisa.Kilichosaidia Kuna mwwnzetu mmoja yy alikuwa hajashonesha Bado,nikampa zangu akafit zikakubali akanirudishia pesa .Nilitaka pensi nyanya lenye kufika magoti pia aweke Malinda,ingawa kwa Sasa neno Malinda ni balaaa
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 nimevuta picha lipensi nyanya afu lina marinda 🤣🤣🤣🤣🤣 bro umenivunja mbavu
 
Nimekumbuka Miaka kadhaa iliyopita Wiki mbili kabla ya Siku yangu ya Uchumba na kutolewa mahari nikapeleka kitambaa kwa fundi anitolee Gauni nzuri na mshono ulikuwa simple tu

Akanipa na siku ya kurudi kuchukua nguo bhana, me nikajiongeza nikasogeza siku kadhaa (akamilishe vizuri nguo) nikaenda siku 2 kabla ya uchumba, yoooh nimefika pale kuchukua nguo fundi ananiuliza ulileta kitambaa cha aina gani?

Heeeeeeee Jaman nilitamani kuzimia, nilimwangalia kama vile nimnyongeeeee, niliongea mpaka machozi yakanitoka mwenzenu. Nilikaa hapohapo kitambaa kikaanza kutafutwa kwenye manguo huko ndani ndio aanze kushona huku nasubiria, nguo ilikamilika saa 4 usiku aisee kuanzia saa 9 mchana

Kuna mwingine nilimpa Kitenge ashone koti, siku naenda kuchukua nakuta natoa Gauni, nikagundua Mafundi watakuwa sababu ya miye kwenda Jela aiseeee

Kuanzia hapo mzuka na Nguo za kushona uliisha, mimi na nguo za dukani mpaka Yesu arudi
Nakumbuka nilipokuwa form six niliibiwa suruali nikabakiwa na pea moja na kwenye mkoa niliokuwa nasoma kulikuwa na baridi Kali kiasi cha nguo kutokauka mapema ukiifua, niliamua kwenda kwa fundi akanishonee suruali nyingine nilimpa robo tatu ya hela yake akaniambia niende kuchukua baada ya siku tatu.
Basi siku ya tatu nilienda kuchukua mzigo wangu nilipofika sikumkuta funda bali nilimkuta rafiki yake mmoja ambaye kila siku anakuwa naye pale anakoshona, nilimwuliza huyo rafiki yake iwapo anafahamu aliko fundi akaniambia ametoka kidogo atarudi baada ya masaa mawili kwa hiyo nikaondoka. Siku ya pili nikarudi na mambo yalikuwa yale yale ya nne nikarudi sikumkuta tena ila nilianza kuchunguza nyumba aliyokuwa anafanyia kazi kama aliweka CCTV Camera ama la lakini nikagundua ameweka bonge la kioo mithili ya ile ya kwenye saluni. Kumbe kile kioo kinaonesha Kila anayekuja kuleta ama kuchukua nguo yake na akiona mtu anaenda kuchukua nguo anajificha.
Nilivyogundua hivyo siku nyingine nilienda ila nikabadili njia yeye kuja kugundua nimeshabisha hodi alipotambua sauti alikumbia chumbani akasimama, kama kawaida yangu nikamwuliza rafiki yake niliyemkuta pale.
MIMI:Fundi yuko wapi
RAFIKI WA FUNDI:Ametoka ila atarudi siyo mda mrefu.
(Kwa sababu jamaa nilimshtukiza hakujificha vizuri, miguu alikuwa inaonekana kupitia chini ya pazia la chumba.)
MIMI:Mwambie siku nyingine akiondoka asisahau kuondoka na miguu yake naona kayaacha pale chini ya pazia la chumba.
Nikaondoka zangu na siku nyingine niliporudi nikakuta ameshamaliza kushona na akanisamehe hela iliyobaki maana alijua nitamwaibisha zaidi.

NI ngori!
 
Mm nilipeleka kitenge anishonee suruali na blause.. siku nimeichukua ile suruali iliishia juu ya magoti haikupita..nikamwambia si ulinipima jamani vzr tuu sasa hiki kiuno kinachoishia miguuni ni kiuno cha nani...
Wanaboa sana..
 
Enzi hizo nipo kwenye ubora wangu, mechi haichezwi mpaka niwepo, tuna game saa 10, jana yake mazoezini kiatu kikazingua kidogo, asubuhi nikadamkia kwa fundi,
Mimi "fundi eeh, kiatu kinahitajika saa 9, si unajua leo ndio nusu fainali yetu"
Fundi" hapo 1000 tu, saa 7,8 njoo uchukue."
Nikampa buku 2 chenji hana, nikamwambia sio kesi, tufanye yote hiyo yake..
Saa 9 tupo kambini namtuma mtu akachukue kiatu, hajamkuta fundi, naenda mwenyewe fundi hayupo, jamaa wa pale wananijua, wakanipa ruksa ya kupekua, nakuta kiatu hakijashonwa..
Sipendi kumuwazia mtu mabaya, japo tayari nishaumuka, nikajisemea huenda kapata dharura kubwa.
Rudi kambini, tafuta sana kiatu cha kuazima, mie navaa 10.5 ama 11.. Tafuta saana, ikabidi apigiwe mtu simu alete toka karume.. Tukaingia gahara ya kununua kiatu kipya.

Yule kumer saa 5 usiku analeta viatu huku anafoka, nimeenda ofisini kwake nimemuharibia, kumsogelea ana kaharufu kapombe, namuelekeza kuwa nilifanya vile kwa sababu hivi na hivi haelewi yupo juu, namuuliza mbona hukufanya kama nilivyokuelekeza na badala ya buku nilikupa buku 2, mie nahangaikia viatu kumbe umeenda kwenye ulabu, akanijibu nisimpamgie...
Aisee kilinitoka kibao kimoja maridadi, nikapiga kelebu saafi kabisa, kuninuka nikamjaza na ndoo, hajakaa sawa nikalima mtama, kisha nikachukua fimbo ilikuwepo maeneo yale charaza sana, wati wakaja kuamua yakaisha..

Asubuhi polisi hawa hapa, kutizama namuona fundi na maaskari, fundi kavimba uso, alama za mikwaju kibao.
Tukaenda kituoni, kufika tunamkuta mkuu wa kituo, ambae ni number 1 fan wangu kwenye suala zima la kudananda soka.
Afande "Makaveli vipi tena kijana wangu,
Mimi. :sifahamu mkuu, nimeletwa na polisi, kwamba fundi kanisihtaki.
Akaniuliza ilikuwaje, nikamuelezea vizuri tu,
Jamaa akaulizwa ayasemayo makaveli yana ukweli, akajibu ndio yupo sahihi, akaambiwa umekosea wewe, na mimi kosa langu ni kushambulia, jamaa akakiri akasema yeye anataka elfu 30 tu kwenda jitibia, nikakubali ila pale sijabeba hela wala simu sijachukua, twende home nikampe, fundi akagoma, akiogopa ya jana yake, mkuu wa kituo akatoa elfu 10 pale, jamaa akasema hiyo inatosha.
Akaondoka zake, nikabaki na mkuu wa kituo, tukiongea na kunipongeza kwa kiwango kizuri cha jana, akaniambia alipanga kuwa atanipa zawadi yangu na ilikuwa ni 30, sasa pale kaishatoa 10, basi ananipa 20, akanipa 20.
Akaniahidi fainali ikiwa fresh kwa kiwango kile basi kuna 50 yangu, fainali ikawa nyepesi zaidi kuliko nusu fainali, nikajaga kupata 50 yangu.
Yule fundi ikawa heshima na adabu.

Yule mkuu wa kituo alihamishwaga pale, na nikapata taarifa za umauti wake, apumzike kwa amani.
😄😄😄😄
 
Kuna hao wa nguo halafu wengine wa furniture😁😁😁.

Dada yangu alikuwa fundi cherehani,siku moja amekusanya vitambaa vya watoto wa watu wa ubarikio awashonee wavae christmass,kajibaraguza weee,mpaka tareh 24 hajamaliza nguo 3,wale watoto wanazifata usiku nguo bado,waliangua kilio mpaka nikaanza kufeel namna wanavyojisikia,ilibidi akomae na mwanga wa torch ya simu mpaka saa sita usiku maana waligoma kabisa kuondoka..
 
Nakumbuka nimefauri kwenda form One,enzi izo tnavaa makaptura polyester gly,basi mzee akanipa pesa nikanunue kitambaa kariakoo ni duka Moja nyuma ya sok kuu karibu na tafifu aina ya vitambaa Ivo vilikiwa vinapatikana.Tukaenda tulikuwa wanafunzi kama watano wote tulifauru kutoka shule Moja.Nimerudi direct kwa fundi hakuwa mbali sana na nyumbani,kanipima Kila kitu akasema baada ya sk nne zitakuwa tayar.Mie Sasa mchchto kibao katika chezacheza pitapita nachungulia kwambali naona anaendelea na kazi nikawa nashtuka mbona kaptura anayoshona ni ndogo au ya mwingine.Nikajipa moyo nikajisemea labda wasiwasi wangu tu.Siku ikafika nikaenda kujaribu nyumbani aisee ni skin tight, zinanibana sana.Nikaridisha kwa fundi huku machozi yananilengalenga .Hairekebishiki hakuna hata kipande cha kuongeza.Kibaya zaidi kabla sijanunua yy ndoalinipima na akasuggest kitanbaa cha 2.5m.Mzuka wote wakureport shule ukaisha kabisa.Kilichosaidia Kuna mwwnzetu mmoja yy alikuwa hajashonesha Bado,nikampa zangu akafit zikakubali akanirudishia pesa .Nilitaka pensi nyanya lenye kufika magoti pia aweke Malinda,ingawa kwa Sasa neno Malinda ni balaaa
Pole sana mkuu. Huyo fundi wako ni nyoko
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣huu uzi bana
 
Back
Top Bottom