Poor Brain
JF-Expert Member
- Jul 5, 2019
- 19,644
- 40,546
Wewe kumbe mgomvi alaaahMimi mwamuzi wa Tanzania ila wajinga wakizingua nawalisha makonde.
Kuna level ya ujinga haiwezi kuondoka bila fimbo au ngumi .
Mtu namwambia nipe nguo yangu anasema it's impossible kwakuwa nimeshaikatakata . Nikamwambia nipe tu nitakulipa pesa tuliyokubaliana anatoa nguo iko vilevile kama nilivyompa
Nilisusa 😂😂😂 maana ilikuwa fupi na haiingii maeneo mengine yani ni kama hakuchukua vipimo...!Sasa uliichukua ukaenda kuivaa, uligawa au uliitupa? 😀😀😀
Kwa jinsi ulivyo sipendi uwe unasaula mitumban emu hit my PM tupitie LC Waikiki jioni hii ya leo.Mimi niliacha kuvaa nguo za kushona tangu nipo chuo...fundi alinishonea vituko nguo hata kuvaa huwezi...bora nikasaule mtumbani
🤣🤣Mie pia si mvaaji sana wa nguo za kushona kwa mafundi wetu hawa, basi siku hiyo nikashawishiwaaa nikaona poa, nikabeba kitenge kwa fundi nikampa mshono rahisi kweli kweli maana sivai nguo fupi, siku nafika kuchukua nguo nakuta kitukooo,nilichukia na hivi nina kigugumizi hata kuongea nilishindwa, nikamlipa na nguo nikamuachia kenge yule...!
Kwa sbb sio waaminifu ndo maana Wana njaaHivi hiyo kazi Ina pesa kweli, maana kuna watu wanaifanya miaka nenda rudi Ila Wana njaa sio poa.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 nimevuta picha lipensi nyanya afu lina marinda 🤣🤣🤣🤣🤣 bro umenivunja mbavuNakumbuka nimefauri kwenda form One,enzi izo tnavaa makaptura polyester gly,basi mzee akanipa pesa nikanunue kitambaa kariakoo ni duka Moja nyuma ya sok kuu karibu na tafifu aina ya vitambaa Ivo vilikiwa vinapatikana.Tukaenda tulikuwa wanafunzi kama watano wote tulifauru kutoka shule Moja.Nimerudi direct kwa fundi hakuwa mbali sana na nyumbani,kanipima Kila kitu akasema baada ya sk nne zitakuwa tayar.Mie Sasa mchchto kibao katika chezacheza pitapita nachungulia kwambali naona anaendelea na kazi nikawa nashtuka mbona kaptura anayoshona ni ndogo au ya mwingine.Nikajipa moyo nikajisemea labda wasiwasi wangu tu.Siku ikafika nikaenda kujaribu nyumbani aisee ni skin tight, zinanibana sana.Nikaridisha kwa fundi huku machozi yananilengalenga .Hairekebishiki hakuna hata kipande cha kuongeza.Kibaya zaidi kabla sijanunua yy ndoalinipima na akasuggest kitanbaa cha 2.5m.Mzuka wote wakureport shule ukaisha kabisa.Kilichosaidia Kuna mwwnzetu mmoja yy alikuwa hajashonesha Bado,nikampa zangu akafit zikakubali akanirudishia pesa .Nilitaka pensi nyanya lenye kufika magoti pia aweke Malinda,ingawa kwa Sasa neno Malinda ni balaaa
Enzi izooo,pensi linafika magitini fundi anakuwekea solobroshen a.k.a Marinda🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 nimevuta picha lipensi nyanya afu lina marinda 🤣🤣🤣🤣🤣 bro umenivunja mbavu
Nakumbuka nilipokuwa form six niliibiwa suruali nikabakiwa na pea moja na kwenye mkoa niliokuwa nasoma kulikuwa na baridi Kali kiasi cha nguo kutokauka mapema ukiifua, niliamua kwenda kwa fundi akanishonee suruali nyingine nilimpa robo tatu ya hela yake akaniambia niende kuchukua baada ya siku tatu.Nimekumbuka Miaka kadhaa iliyopita Wiki mbili kabla ya Siku yangu ya Uchumba na kutolewa mahari nikapeleka kitambaa kwa fundi anitolee Gauni nzuri na mshono ulikuwa simple tu
Akanipa na siku ya kurudi kuchukua nguo bhana, me nikajiongeza nikasogeza siku kadhaa (akamilishe vizuri nguo) nikaenda siku 2 kabla ya uchumba, yoooh nimefika pale kuchukua nguo fundi ananiuliza ulileta kitambaa cha aina gani?
Heeeeeeee Jaman nilitamani kuzimia, nilimwangalia kama vile nimnyongeeeee, niliongea mpaka machozi yakanitoka mwenzenu. Nilikaa hapohapo kitambaa kikaanza kutafutwa kwenye manguo huko ndani ndio aanze kushona huku nasubiria, nguo ilikamilika saa 4 usiku aisee kuanzia saa 9 mchana
Kuna mwingine nilimpa Kitenge ashone koti, siku naenda kuchukua nakuta natoa Gauni, nikagundua Mafundi watakuwa sababu ya miye kwenda Jela aiseeee
Kuanzia hapo mzuka na Nguo za kushona uliisha, mimi na nguo za dukani mpaka Yesu arudi
😄😄😄😄Enzi hizo nipo kwenye ubora wangu, mechi haichezwi mpaka niwepo, tuna game saa 10, jana yake mazoezini kiatu kikazingua kidogo, asubuhi nikadamkia kwa fundi,
Mimi "fundi eeh, kiatu kinahitajika saa 9, si unajua leo ndio nusu fainali yetu"
Fundi" hapo 1000 tu, saa 7,8 njoo uchukue."
Nikampa buku 2 chenji hana, nikamwambia sio kesi, tufanye yote hiyo yake..
Saa 9 tupo kambini namtuma mtu akachukue kiatu, hajamkuta fundi, naenda mwenyewe fundi hayupo, jamaa wa pale wananijua, wakanipa ruksa ya kupekua, nakuta kiatu hakijashonwa..
Sipendi kumuwazia mtu mabaya, japo tayari nishaumuka, nikajisemea huenda kapata dharura kubwa.
Rudi kambini, tafuta sana kiatu cha kuazima, mie navaa 10.5 ama 11.. Tafuta saana, ikabidi apigiwe mtu simu alete toka karume.. Tukaingia gahara ya kununua kiatu kipya.
Yule kumer saa 5 usiku analeta viatu huku anafoka, nimeenda ofisini kwake nimemuharibia, kumsogelea ana kaharufu kapombe, namuelekeza kuwa nilifanya vile kwa sababu hivi na hivi haelewi yupo juu, namuuliza mbona hukufanya kama nilivyokuelekeza na badala ya buku nilikupa buku 2, mie nahangaikia viatu kumbe umeenda kwenye ulabu, akanijibu nisimpamgie...
Aisee kilinitoka kibao kimoja maridadi, nikapiga kelebu saafi kabisa, kuninuka nikamjaza na ndoo, hajakaa sawa nikalima mtama, kisha nikachukua fimbo ilikuwepo maeneo yale charaza sana, wati wakaja kuamua yakaisha..
Asubuhi polisi hawa hapa, kutizama namuona fundi na maaskari, fundi kavimba uso, alama za mikwaju kibao.
Tukaenda kituoni, kufika tunamkuta mkuu wa kituo, ambae ni number 1 fan wangu kwenye suala zima la kudananda soka.
Afande "Makaveli vipi tena kijana wangu,
Mimi. :sifahamu mkuu, nimeletwa na polisi, kwamba fundi kanisihtaki.
Akaniuliza ilikuwaje, nikamuelezea vizuri tu,
Jamaa akaulizwa ayasemayo makaveli yana ukweli, akajibu ndio yupo sahihi, akaambiwa umekosea wewe, na mimi kosa langu ni kushambulia, jamaa akakiri akasema yeye anataka elfu 30 tu kwenda jitibia, nikakubali ila pale sijabeba hela wala simu sijachukua, twende home nikampe, fundi akagoma, akiogopa ya jana yake, mkuu wa kituo akatoa elfu 10 pale, jamaa akasema hiyo inatosha.
Akaondoka zake, nikabaki na mkuu wa kituo, tukiongea na kunipongeza kwa kiwango kizuri cha jana, akaniambia alipanga kuwa atanipa zawadi yangu na ilikuwa ni 30, sasa pale kaishatoa 10, basi ananipa 20, akanipa 20.
Akaniahidi fainali ikiwa fresh kwa kiwango kile basi kuna 50 yangu, fainali ikawa nyepesi zaidi kuliko nusu fainali, nikajaga kupata 50 yangu.
Yule fundi ikawa heshima na adabu.
Yule mkuu wa kituo alihamishwaga pale, na nikapata taarifa za umauti wake, apumzike kwa amani.
Pole sana mkuu. Huyo fundi wako ni nyokoNakumbuka nimefauri kwenda form One,enzi izo tnavaa makaptura polyester gly,basi mzee akanipa pesa nikanunue kitambaa kariakoo ni duka Moja nyuma ya sok kuu karibu na tafifu aina ya vitambaa Ivo vilikiwa vinapatikana.Tukaenda tulikuwa wanafunzi kama watano wote tulifauru kutoka shule Moja.Nimerudi direct kwa fundi hakuwa mbali sana na nyumbani,kanipima Kila kitu akasema baada ya sk nne zitakuwa tayar.Mie Sasa mchchto kibao katika chezacheza pitapita nachungulia kwambali naona anaendelea na kazi nikawa nashtuka mbona kaptura anayoshona ni ndogo au ya mwingine.Nikajipa moyo nikajisemea labda wasiwasi wangu tu.Siku ikafika nikaenda kujaribu nyumbani aisee ni skin tight, zinanibana sana.Nikaridisha kwa fundi huku machozi yananilengalenga .Hairekebishiki hakuna hata kipande cha kuongeza.Kibaya zaidi kabla sijanunua yy ndoalinipima na akasuggest kitanbaa cha 2.5m.Mzuka wote wakureport shule ukaisha kabisa.Kilichosaidia Kuna mwwnzetu mmoja yy alikuwa hajashonesha Bado,nikampa zangu akafit zikakubali akanirudishia pesa .Nilitaka pensi nyanya lenye kufika magoti pia aweke Malinda,ingawa kwa Sasa neno Malinda ni balaaa