Umewahi kuingilia ugomvi usiokuhusu halafu yakakukuta makubwa?

Umewahi kuingilia ugomvi usiokuhusu halafu yakakukuta makubwa?

Kuna watu hatupendi wengine waonewe hivyo tunaingilia ingilia sana ugomvi wa watu. Magu anasema 'Kuwashwa washwa' anyway wakati mwingine show unayoiingilia jukwaa ni kubwa show ndefu halafu wewe pumzi ndogo.

Nina visa vingi vingi (si unajua ukiwa mlinzi wa club eeh? Au kuishi uswazi?) Basi nitaandika kimoja kimoja kadri nitakavyokumbuka.

Nilipanga chumba maeneo fulani hivi kulia napakana na mshkaji bachela kama mimi kushoto yupo jamaa na mkewe na kachanga nahisi kama miezi miwili haizidi minne.

Basi siku hiyo usiku kama saa nane nikawa nasikia mwanamke anamwambia mwanaume (hakuna ceiling board)
"Mi sitaki bwana niache" nasikia jamaa akinong'ona kwa besi akili yangu ikaniambia jamaa anataka tendo.
Kisha nikasikia kilio cha binti kile chembamba cha chini chini lakini cha kwikwi.

Akili yangu ikaniambia jamaa anaomba jicho nini analila kilazima. Kisha sauti ikaongezeka halafu nikasikia chombo cha udongo kinavunjika halafu zikafuatia purukushani na mwanaume akitukana, hapo nikashtuka.
Nikafungua mlango, nafika sebuleni nakuta wapangaji wengine walikua hapo muda tu, wamama wawili na yule mshkaji wa kulia kwangu.

Basi nikajitia ujasiri nikaenda kugonga mlango purukushani zikakoma nasikia kilio tu cha binti. Nikazidi kugonga mara mlango ukafunguliwa akatoka yule mwanamke mbio jamaa akaja mlangoni kufunga mlango.
Tukakutanisha macho, hakusema kitu na mimi kimya tunatazamana tu. Akafunga mlango.

Wamama wakasema yule binti atakua kakimbilia ukweni kwake.

Nikarudi kulala..........
Mi niliamulia ugomvi wa gelofriendi wangu na shosti yake enzi hizo. Baada ya wiki mbili shosti wa gelofriendi wangu akanizawadia papuchi kama shukrani ya wema wangu.

Tangu siku hiyo niko makini sana kufuatilia gomvi za jinsia KE. Huwezi jua mipango ya shetani, naweza nikalamba bingo tena

Mzigua90 na Shunie mtagombana lini nije niwaamulie?
 
Mi niliamulia ugomvi wa gelofriendi wangu na shosti yake enzi hizo. Baada ya wiki mbili shosti wa gelofriendi wangu akanizawadia papuchi kama shukrani ya wema wangu.

Tangu siku hiyo niko makini sana kufuatilia gomvi za jinsia KE. Huwezi jua mipango ya shetani, naweza nikalamba bingo tena
Hahaha kwahiyo ugomvi wa Humble na CCNP kwako hauna faida?
 
Kuna mpangaji mwenzangu ana mke na mtoto mmoja nahisi ni wa miaka minne yule mtoto.

Jamaa shughuli zake ni ufundi, kwahiyo akitoka kurudi usiku sana. Siku hiyo kawahi kurudi akakuta mkewe kapakatwa na kinyozi mmoja hivi barabarani. Jamaa hakuongea kitu.

Alfajiri ya saa 10 kelele za 'Nakufaaaaa' zikaanza. Mimi nakaa chumba cha nje miongoni mwa vyumba vitatu vya nje hawa mke na mume wanakaa vyumba vya ndani.
Hadi uingie ni lazima ufunguliwe mlango.

Basi washkaji wa vyumba vitatu wote tumetoka tunamsihi jamaa amuache binti. Huku tukwapigia kelele wa vyumba vingine wafungue. Mmoja wetu akaenda dirisha la mwenye nyumba ili afungue mlango.

Nikaona wanachelewa nikaanza kupiga mateke mlango. Bwana muvi zinadanganya kumbe mlango ni mgumu baada ya mateke kama nane nikaona nitajivunja nisubiri kwanza.
Mwenye nyumba akafungua mlango nikatangulai kufika mlango wa chumba cha jamaa. Kama kawaida yangu mateke tu, nabadilisha miguu tu.

Yule jamaa alivyofungua mlango akatoka ni kisu akanichana kwenye triceps kidogo coz niliwahi kutoa mkono. Binti akapata upenyo wa kukimbia mi nikamtight mshkaji akanyang'anywa kisu.

Mchana nimelala nagongewa na watu kama wanne natoka askari kanzu watatu, mmoja ana sare na yule jamaa. Jamaa anadai nimempiga asubuhi. Nikabebwa hadi kituo kidogo.

Mwisho askari wakasema ok huna kosa unatuachaje? Ikanitoka 20K narudi nyumbani mwenye nyumba ananiambia mateke yangu yamemharibia milango hivyo natakiwa nigharamie ama milango mipya au ile iboreshwe.

Mie hoi.
 
nakumbuka mwaka 2013 life la chuo na ujana damu inachemka kila weekend club..

tulikuwa washkaj watatu mimi gatsby..bruno..na masai mmoja tulikuwa tunamuita pede

tumekula bia za kutosha pale Club Wantansh kwa nje mida ya saa saba na nusu usiku tukasema ngoja tuzame ndani kubambia na ikiwezekana kung'oa wadada wa masaki (maana kama mara mbili mimi na bruno tulitunukiwa na wadada wakubwa wakubwa kiumri baada ya kudance nao)

ile tumezama ndani tukaanza kucheza huku tunaendelea kula bia ikafika mida ya saa 8 na nusu yule mwenzetu masai pede akazima tukamuweka kwenye sofa sisi tukaendelea kula maisha

gafla tunaenda kumchek tunakuta anakula mate na lishoga jamaa hajielewi hapo anajua kaopoa demu nikamwita bruno tukaenda pale cha kwanza hatujauliza tukampa yule shoga vibao vya maana ..akasepa

gafla karudi na mashoga wenzake kama sita wametujalia pale kwenye sofa wanaanzisha utata mmoja akasema au mnamuonea gere mwenzenu na nyie mnataka au? gafla akamrukia bruno akambusu mdomon mamaaeee akaachia bonge la ngumi yule shoga chali

hata mabaunsa walipotokea wakaanza kutupa za chemba mimi na bruno wakatubeba juu juu wakaenda kututupa nje hapo tumechezea za uso tumevimba

kumbe bwana meneja wa pale wantanshi anapenda mashoga yawepo mule ndan ili kuvutia wazungu waje pale...

kesho yake hatukwenda chuo maana bado tulikuwa tumevimba yule maasai pede tunamsimulia kisa kilichofanya tupigwe anabisha eti kuwa ajaliwa mate na shoga 😂😂😂

anasema aseee nyie jamaa makorofii sana jana itakuwa mmepata wababe yenu imewaonesa kazi
 
nakumbuka mwaka 2013 life la chuo na ujana damu inachemka kila weekend club..

tulikuwa washkaj watatu mimi gatsby..bruno..na masai mmoja tulikuwa tunamuita pede

tumekula bia za kutosha pale Club Wantansh kwa nje mida ya saa saba na nusu usiku tukasema ngoja tuzame ndani kubambia na ikiwezekana kung'oa wadada wa masaki (maana kama mara mbili mimi na bruno tulitunukiwa na wadada wakubwa wakubwa kiumri baada ya kudance nao)

ile tumezama ndani tukaanza kucheza huku tunaendelea kula bia ikafika mida ya saa 8 na nusu yule mwenzetu masai pede akazima tukamuweka kwenye sofa sisi tukaendelea kula maisha

gafla tunaenda kumchek tunakuta anakula mate na lishoga jamaa hajielewi hapo anajua kaopoa demu nikamwita bruno tukaenda pale cha kwanza hatujauliza tukampa yule shoga vibao vya maana ..akasepa

gafla karudi na mashoga wenzake kama sita wametujalia pale kwenye sofa wanaanzisha utata mmoja akasema au mnamuonea gere mwenzenu na nyir mnataka gafla akamrukie bruno akampusu mdomon mamaaeee tukaachia bonge la ngumi yule shoga chali

hata mabaunsa walipotokea wakaanza kutupa za chemba mimi na bruno wakatubeba juu juu wakaenda kututupa nje hapo tumechezea za uso tumevimba

kumbe bwana meneja wa pale wantanshi anapenda mashoga yawepo mule ndan ili kuvutia wazungu waje pale... kesho yake hatukwenda chuo maana bado tulikuwa tumevimba yule maasai pede tunamsimulia kisa kilichofanya tupigwe anabisha eti kuwa ajaliwa mate na shoga [emoji23][emoji23][emoji23]
Hahaha mngetoka nduki
 
Iyo inaitwa "KUNUNUA UGOMVI"
ebwana kuna jamaa alinunua ugomvi wa rafiki ake aliyekua anapata kichapo na raia wenye hasira kali...

Jamaa katokea from nowhere kanunua ugomvi...akitegemea ataungana na yule aliyekua anapigwa..

Basi bwana yule aliyekua anapigwa kapata lifetime chance akachomoka akamuacha mnunuzi......

Ebwana zile Raia zikamshuhulikia yule mnunuzi wa ugomvi kwa kipigo cha mbwa mwizi!

Akaapa kamwe hatakaa anunue ugomvi tena maana aliingia kwa nia njema ya kumuokoa rafiki ..rafiki akamkimbia..

Akazidi kusema kua ."......kwa kumsaidia mtu kama anapigwa eti ataenda kutoa taarifa nyumbani kwao kua ndugu yenu anakufa kule kaamueni.."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iyo inaitwa "KUNUNUA UGOMVI"
ebwana kuna jamaa alinunua ugomvi wa rafiki ake aliyekua anapata kichapo na raia wenye hasira kali...

Jamaa katokea from nowhere kanunua ugomvi...akitegemea ataungana na yule aliyekua anapigwa..

Basi bwana yule aliyekua anapigwa kapata lifetime chance akachomoka akamuacha mnunuzi......

Ebwana zile Raia zikamshuhulikia yule mnunuzi wa ugomvi kwa kipigo cha mbwa mwizi!

Akaapa kamwe hatakaa anunue ugomvi tena maana aliingia kwa nia njema ya kumuokoa rafiki ..rafiki akamkimbia..

Akazidi kusema kua ."......kwa kumsaidia mtu kama anapigwa eti ataenda kutoa taarifa nyumbani kwao kua ndugu yenu anakufa kule kaamueni.."

Sent using Jamii Forums mobile app
Halafu kipigo cha mtu anayeingilia hua kinakua cha mwana ukome ili siku nyingine usirudie
 
ilikuwa ambush kaka [emoji23][emoji23] sisi tupo bize tunawapiga wale mashoga gafla mbavu zimeingia bila hata kuuliza tukaanza kuchezea ...tulivyoona hawa hatuwawez tukajilaza chini ndio wakatubeba wakatutupa nje
[emoji23] [emoji23] [emoji23] hilo ambush si mchezo unaweza kuona unakimbia unawaponyoka kumbe ndo unaelekea upande wao
 
Kuna rafiki yangu anamiliki video library so anaburn miziki na watu wa ofisi hizi hua wanaweka sauti za muziki juu sana.

Basi tumekaa hapo mara akaja jamaa, mtu wa makamo kama miaka 45 hivi mfupi, mweusi, mwili mdogo mdogo, akauliza.
"Nani mhusika hapa?"
Mshkaji akajibu "Mimi"
Jamaa akaendelea "Watu wanasema wamekufuata kama mara nne upunguze sauti"
Mshkaji wangu akajibu "Hapana hapa hajaja mtu au Castr umemuona mtu?"
Nikajibu "Hapana" (Ni kweli hakuja mtu)
Akaendelea yule jamaa "Basi sawa, punguza sauti"
Mshkaji wangu akamjibu "Siwezi kupunguza, wateja wanatakiwa wajue kua nipo"

Yule jamaa akajibu sawa akaondoka, baadaye kidogo akarudi na mtu mwingine. Wa makamo pia ila ana mwili kumzidi huyu, mrefu na mweupe lakini anaonekana kalewa au ni mlevi wa kila siku.

Jamaa wakaanza tena utata juu ya sauti. Mimi nikasema kwani mbona mnamsumbua mshkaji wangu shida nini. Yule mwenye mwili mdogo akajibu "Haikuhusu kaa pembeni"
Nikasimama nikapeleka kitasa, kikampata yule mlevi wa kila siku akasema "Wewe unaipiga serikali?" Nikamwambia "We mwenyewe unasemaje?"

Hapo watu wakawa washajaa, si unajua uswazi? Kwahiyo nikawa nakula ujiko natamba. Nikamwambia "Toeni vitambulisho basi kama nyie serikali"

Nilikua sijui serikali hua inaajiri walevi mbwa kwa ajili ya kazi zao, hivyo sikudhania kuwa hawa wanaweza kua watumishi wa serikali.

Vitambulisho vikatoka.

Mweupe ni mtendaji wa kata ya Mwananyamala kwa Kopa na mweusi ni askari kanzu wa kituo kidogo cha Kwa Kopa.

Nilinywea.

Natamani kukimbia lakini nahofia watu wataona kumbe jamaa muoga.

Niliyempiga kitasa akatoa pingu,nikavalishwa mpaka kituo kidogo cha kwa Kopa.

Mizunguko miiiiiiingi lakini nikatoa hela ndiyo nikatoka.
Ulikuwa mdoogo km piriton

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku moja nipo ofisini. Kuna binti anarushia watu chupa obviously ilitakiwa azuiliwe kabla sijamfikia mlinzi mwenzangu akawa kashamfikia kambeba yule binti anaenda kumtoa nje.

Bwana ake akamkwida mlinzi mwenzangu huku anatukana "M**nge ku****ako unaingilia ugomvi wa mademu si uwaache wapigane?" Mimi nikamtight jamaa tukatoka hadi nje.

Jamaa brazamen tu kavaa jinzi inabana nyeupe fulana nyeupe kapelo nyeusi na converse nyekundu. Demu wake katia gauni fupi jeusi kama sundress hivi.

Kwahiyo hawakuonyesha kama ni threat kivyovyote. Yule mlinzi mwenzangu akaanza kumpaka jamaa "We ku*a tu nikiamua nato**ba wewe na huyo demu" mimi hapo namwambia mshkaji "Hoya jikatae hatutaki washamba wa starehe humu"

Mshkaji akajibu "Nyi was**nge tu, miili tu hiyo hamna kitu" hapo watu washajaa tayari.

Tukamwambia jaribu kutugusa basi.

Akageuka akaenda kwenye gari alivyorudi akachomoa pistol akaionyeshea upande wetu.
Hata sielewei ilikuaje nikajikuta nimeganda sauti haitoki mshkaji wangu kashapiga magoti mikono juu.

Binti akaanza "Was*nge nyinyi kelele nyingi mbona mpo kimya?" Kwa unyonge nikafunguka "Dada tafadhali mwambie braza atusamehe"

Mara kaja supavaiza akamplease jamaa akamuelewa yule supavaiza, akaingia kwenye ndinga akasepa.
Aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko form two naelekea shule kuna washkaji wanne wakawa wanataka kupanda gari konda anawazuia. Ugomvi ukalipuka na mimi nikaunga kwenye ugomvi..

Washkaji hawanijui siwajui. Tukamtembezea kichapo konda safi kabisa.

Safari inaendelea ndani ni kutemeana maneno ya shombo tu akatuambia subirini mtanielewa tu.

Gari kufika Tandale Kwa Mtogole. Konda akashuka akaanza kuita "Sele Bujeeee, wee Sele Bujeeee njoo huku" dereva akawasha gari akaanza kuondoka akawa kama hataki ile ishu. Konda akadandia gari.

Sele Buje akadandia carrier ya nyuma ya gari, kituo cha Sweet Corner watu wakashuka Sele Buje akaingia ndani kwenye gari.
Ana muonekano wa kibabe knuckles zimechacha vibaya.

Anamuuliza konda "Nani analeta vurugu?" Konda katuonyeshea sisi, akaanza kutusogelea. Mimi hapo nakokotoa namna gani naweza kuruka kutoka dirishani nitue kwenye lami bila kugongwa kisha nikimbilie mitaa ya Manzese.

Hesabu hazijakaa sawa. Sele Buje kafika tu anakutana na dogo kutoka wale wanne wanasalimiana "Master vipi?" Sele buje anajibu "Shwari mbona mnakua wakorofi?" Dogo anajibu "Tumechelewa master sasa jamaa akawa anatuzuia ndiyo tukalazimisha kuingia"

Sele Buje akamgeukia konda "Hawa wadogo zetu bwana hawana shida"

Turns out Sele Buje alikua ni mwalimu wa boxing wa yule dogo.

Ila nilitetemeshwa sana.
Sele bujeeee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom