Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 590
- 1,648
Mimi nishawahi kula Ada na mtihani unakaribia.Katika harakati za kusaka elimu vyuoni wanafunzi wanakutana na kashikashi nyingi sana zinazosababisha wakati mwingine mpaka mtu kuachana na mambo elimu, mfano kujikuta uko kwenye mgogoro na mwalimu wako sababu wote mnamfukuzia binti fulani, kufanya starehe kwa kupitiliza mpaka unasahau kilichokupeka ni baadhi ya kati ya mengi.
Je ulishawahi kukutana na kisanga gani mpaka ukapaona chuoni kama uwanja wa vita? Uliweza kurudi kwenye mstari au mpaka leo bado ni majuto tu?
Nasoma komentiKatika harakati za kusaka elimu vyuoni wanafunzi wanakutana na kashikashi nyingi sana zinazosababisha wakati mwingine mpaka mtu kuachana na mambo elimu, mfano kujikuta uko kwenye mgogoro na mwalimu wako sababu wote mnamfukuzia binti fulani, kufanya starehe kwa kupitiliza mpaka unasahau kilichokupeleka ni baadhi ya kati ya mengi.
Je ulishawahi kukutana na kisanga gani mpaka ukapaona chuoni kama uwanja wa vita? Uliweza kurudi kwenye mstari au mpaka leo bado ni majuto tu?
π π Tutakuwa wasoma commentWa darasa la saba tunahusika kwel hapa
Hongera kwa kuchomokaNilipata sup ya negotiation n mediation alafu mkufunzi mtata ukikata rufaa anaku mind mara 2
Mwamba nikakata rufaa, jamaa wakija kwangu wanasema mkufunzi haniachi aseeh lazima anile kichwa tena na tena
Nilikuja kuchomoka, tangu hapo nikaacha ubwege
ππ wazee wa staki shuleMimi nilikua mtu nisiependa kusoma tokea niko mdogo mpaka kufika chuo kikuu japo nilipokua mdogo nilikua sipendi kusoma na sikiwahi kufeli..
Nilivyofika chuo na ule u free mwingi Mimi ndio nilikua mtaalamu wa movie mpya mpya, nikapanga gheto nje yani habari za chuo sina quiz washikaji wananifanyia. Naenda chuo usiku kudownload movie tu.
Chuo niligraduate na GPA ya 1.9 hata sijutii.
Gpa ya 1.9 si umedisco?Mimi nilikua mtu nisiependa kusoma tokea niko mdogo mpaka kufika chuo kikuu japo nilipokua mdogo nilikua sipendi kusoma na sikiwahi kufeli..
Nilivyofika chuo na ule u free mwingi Mimi ndio nilikua mtaalamu wa movie mpya mpya, nikapanga gheto nje yani habari za chuo sina quiz washikaji wananifanyia. Naenda chuo usiku kudownload movie tu.
Chuo niligraduate na GPA ya 1.9 hata sijutii.
Dah, pole sanaMimi tukio la chuo ambalo sitolisahau ni mwaka wa kwanza.
Hostel room tulipangwa wa 4. Sasa mambo ya kike tena roommates wangu watatu wakaungana wakaninunia halafu wakawa wananipiga vijembe live.
Wakavuka mipaka wakawa wananiharibia vitu vyangu. Mfano, nikitanyika kitanda wanatoa shuka na kuvuruga nikiwa sipo.
Sasa hiyo siku kama Mungu. Naenda class nikawa nimesahau notes room. Nikarudi kabla hata sijamaliza kushuka ngazi. Nikavikuta vinavuruga vitu vyangu.
Hasira ilinipanda nikaona liwalo liwe. Nikakamata mmoja nikamtembezea kichapo wakaingilia wale wawili. Nikawachanganya wote. Nikawapiga wote. Yaani walinichangia watatu lakini walichapika haswa hadi vikakimbia nje vingine havijavaa hata nguo.
Baadae warden akatuita tukatakiwa tufukuzwe hostel.
Kunidsco ni 1.8<Gpa ya 1.9 si umedisco?
π π π mjini mipangoTulipogundua kwamba chuoni hawana kawaida ya kufuatilia watu walio feli(discontinue) tukaunda team ya watu kama saba na kutengeneza vitambulisho fake vya watu walifeli kuendelea na masomo mara tu baada ya orodha kutoka ubaoni kuonyesha kweli wamefeli.Kweli tukafaniki kuchukua zile pesa dirishani (enzi hizo pesa haitumwi kwenye benki account) na kugawana kadri ya ushiriki wa kila mmoja wetu.Kasheshe ilikuja baada ya mmoja wa waliofeli kujitokeza kupinga kuwa hajafeli (kukata rufaa) na kukuta pesa yake imechukuliwa.....ilikuwa mbaya maana yule aliyechuykua pesa alikuja kujulikana na kusimamishwa masomo na kutakiwa kuzirudisha pesa zote
Wa darasa la saba tunahusika kwel hapa
Ukapata tabu sanaππNilimtongoza Mkufunzi. Sitokaa nisahau japo tulikuja kumalizana vizuri hapo baadaye ila baada ya kuteseka sana kwa Kuweka wazi mambo yoote