Umewahi kukutana ana kwa ana na mnyama gani mkali?

Miaka hiyo nipo darasa la nne kijijin. Nikajilimia mahindi ya maji. Yaan unalima mahindi baada ya msimu unayanyweshea kwa mfereji. Sasa maji mara nyingi ni ya kugombania. So mi nikawa naamka saa saba naenda kujifungulia maji namwagilia mahindi. Sasa ile namwagilia nimemaliza nikasema ngoja nikafunge maji. Mida hiyo saa tisa giza kama lote halafu kimyaa mbaya kabisa. Ile natoka kwenye mahindi ebwana kuna mdudu cjui alikuwa fisi au nini Anakimbia alishika break mguuni ile cjui nini kakatiza kwenye mahindi nilihic nywele zimesimama. Sasa Wakat natoka pale nafika tena barabaran mbele yangu nawaona wazee wa kaz wana mafurush kama yote wako mdogo mdogo Nikapiga kelele kamata hiyo Walirusha mafurush mbio kwenye mahindi na Mimi nikala kona home.
 
Kobla alinipitia kwa kifua nkiwa nmelala ghafla wakati anashuka Kuna jamaa yangu alikua macho anakula bange akawa amemuona akamuua ndo kuniamsha kumbe mwamba alimuona wakati anaingiza alikua anafukuza panya mpaka anapanda kitandani ananipita juu ya mwili wangu jamaa anamuona sema aliogopa kupiga kelele maana ningestuka angeningonga. Lilikua bonge la dude
 
Spitting Cobra
 
Kwenye kuchunga tunakutana na vitu vya kutisha sana.

Tuliendaga kuchunga polini( kuweka kambi )kwa wale wenzangu wa Kanda ya ziwa wanalijua hili, sasa mkifika huko mnachagua eneo mnamwaga dawa kwa kuzungushia na nyie mnaoga dawa,usiku simba na wanyama wakali wanakuja mpaka hapo kwenu halafu wanaunguruma ila hawawezi kuwaona ila ukitoka tu eneo lenye dawa umeisha.
 
Nishawah kuogelea sehem hivi.. kuzamia chini nikaona kitu sikielewi nimekipiga na mkono.. nikaibuka juu kimya.

Nikazamia tena nikagusana nacho miguuni.

Kuibuka juu, nikaona si kweli.. nikazamia huku macho nimeacha wazi nione kuna nini..

Kumbe Mamba yupo humo tunapishana tu..

Aisee sikumbuki nilipaa kwa kutumia mabawa ya aina gani.
 
Aisee kuna mnyama mkali zaidi ya mwanamke?
 
Usikutane na Mamba huyo ni mjusi tu, kutana na Chatu.
 
Tulikuwa tunawinda usiku, tumepaki landrover tunatembea kutafuta wanyama? Mwendo mrefu bila kuoma mnyama yeyote! , master akasema lazima kuna chui au simba anayewafukuza wanyama ili tusiwapate.

Ikabidi mission ibadilike! Tuanze kwanza kumuwimda huyu anaewafukuza wanyama!
Ni stor ndefu ila tulimuua chui mkubwa sijawai ona!
Baada ya hapo yulipata wanyama wakutosha!
 
Nyoka mwenye sumu zaidi duniani yupo Australia. Koboko (black mamba) ana sumu zaidi ya kifutu. Sumu ya kifutu hushambulia cells katika eneo alilong'ata, hii huweza kusababishwa mtu kukatwa eneo lililoathiriwa.
Black mamba wana sumu za aina tatu, inayoshambulia cells, neva za fahamu na moyo. Ndio maana inaelezwa kuwa, black akingata mara moja, ile sumu anayoachia inaweza ua hata watu 4 ikiwa hawatapata matibabu ya haraka.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Nimetoka kuua joka hili nyumbani
 

Attachments

  • 20211227_222814.jpg
    958.7 KB · Views: 8
Simba mara nyingi
Chatu
Majoko
Fisi
Nfuruwe pori mara nyingi
Nyani
Ngedere
Twiga
Tembo
Hao wanyama wote tulikutana.
Siku Wamarekani wakamtwanga risasi Nyati huko porini,wamemkosakosa.
Nyati kaja camp kuwatafuta.
Uliwaka moto ilibidi tuwaondoe pale porini.
Siku ingine tunachoma Nyama kumbe yuko hapo jirani tu anaskilizia harufu.

WaKaja fisi kadhaa kumsumbua aisee walipigwa pale sehemu tunachoma nyama wote tumekimbia.
Siku ingine jamaa walimjeruhi Simba huko porini wakarudi kulala.
Simba wakike si wakaja usiku camp,
Habari kutoka nje haipo
Wanaunguruma pale.
Siku ingine Simba na mbwa mwitu,
Simba anaogopa sana Mbwa mwitu watu hawajui tu.
Simba kazama kwenye tent letu kageuka
si wala hatuoni😂😂😂,
si hapo tunaangalia tutakimbia vipi,kumbe nae anakimbia kichapo cha mbwa mwitu.
Aisee kuna mambo humu duniani yanachekesha sana.
Ile movie
God Must be Crazy naielewa sana.
 

Hii ni kweli nimeshaangalia sana documentaries zinazohusu black mamba,pia kile kipindi cha Snake in the City kwa Africa Black Mamba ndio nyoka hatari zaidi akikuuma.
 
Sawa bro, umeeleweka kaka. Nashukuru kwa elimu hii mujarabu.
 
Hii ni kweli kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…