Umewahi kupigwa roba mtaani? Weka kisa chako

Umewahi kupigwa roba mtaani? Weka kisa chako

Yes 2010
Fainali uefa baina ya asernal na Barcelona kumbukumbu golikipa asernal alipata kadi nyekundu mapema sana alimgusa unyayo samueli eto akienda kufunga goli

Najamaa yangu tunasiku mbili panaitwa bagamoyo unaelekea stend kuu yatukuyu panadispensari na bar moja hivi nalakitano kwenye waleti ,simu Samsung

Kumbe kunajamaa ananiwinda mana natumia pombe balaa
Ukafika muda wamechi bwana ukumbini nilazima upite kaunta ,upande wakulia kunachoo unavoelekea ukumbini
Niliingia choo gent kama kawa kumbe kibaka alikuja nyumayangu akaingia cha ke ili ufike choo cha wanaume nilazima uvuke mlango wa ke
Natoka hivi nataka kukunja niingie baa niliguswa begani kugeuka nikasukumwa kidogo ukutani nikanata pale

Jamaa akatoa kisu vile vyakufyatua akaniambia unaona watu wanapita kuingia kuangalia mechi nikasema ndio
Ukipiga kelele wananiua naomba zilehela zote na simu kila kitu tumeona kwanza mgeni hapa tokajana unakunywa tu bia hapa ukikaa hata kuinuka huinuki

Nikasema nimekwisha ghafla akili ikija yule jamaa niponae alikua ametoka bwana mungu mwema akili ikaja nilegeze mwili na kauli hapo kichwani nipo nahisi damu inamwagika nimeloa mwiliwote
Watu wanapita nawanamwita jamaa jinalake(),anaitikia poa napiga stories na big yetu hapa

Basi ,nikamuangalia alivo nikipande cha MTU mweusi harufu pia yabangi kwambali nasikia toka kwake
Kimo chake urefu kidogo tunalingana

Nawaza nipige wapi huyu usoni jibu ikawahapa
Ghafla wazo likaja nitagonga kichwa changuvu eneo lapua nilazima ainame kidogo niifaidi pua yake
Nikamwambia naomba laini nitoe nikuachie simu napesa zote nakupa

Jibu likawa
Sawa brother nyie ndo mabrother tunawataka hamna bugdha
Nikatoa laini ingia mfuko wanyuma to a waleti

Wakati natoa waleti aliinama ili aifadhi kisu anavoinuka niligonga kichwa puani alilia kwasauti kubwa mamaaaaa nakufa akadondoka chini paaa

RAIA kwenye ukumbi na bar wakatoka wanauliza imekuaje nikawambia wakati mnapita hapa nilikua nimepigwa tero amesema nimpe simu napesa pia Mimi mgeni nakaaje sikumbili nakunywa tu pombe

ndo nikasikia najina lake anaitwa God ,dereva vigali beba mizigo soko LA tukuyu stend pale



Kutoka ilesiku sijawahi kusekana nyumbani sambili kamili usiku labda niwe safarini

Usiombee ukutwe au ubananishwe na kibaka sikiaga tu

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
Fainali ya UCL kati ya Arsenal na Barcelona ilichezwa mwaka 2006, fainali ya mwaka 2010 ilikuwa kati ya Inter Milan ya Jose Morinho na Bayern Munich ya Lois Van Gaal.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Mimi nilipigwa ngwara [emoji23][emoji23][emoji1732]enzi za chuo,njaa za usiku nikajifanya kutoka hostel kwenda kununua chips jomonii woiii mitaa ya bonanza area c Dom... ile ngwara siji isahau asee japo nilitoka mkuku ni Mungu tuu maana walikuwa vijana kama wanne na ndio kipindi ambacho matukio ya mauaji yalikuwa yamepamba moto hasa kwa wanafunzi....lile tukio ni moja wapo lilinifanya niokoke asee maana ukiniuliza nilivukaje nabaki kusema ni Mungu wa mbinguni tuu,daah!!![emoji119][emoji119]
Mkuu ulienda maisha plus nini kupata na matunda [emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka nikiwa Arusha nasoma chuo cha uhasibu miaka ya 2013 kama sijakosea, kuna siku nlishuka kituo cha SDA pale Njiro ili niende ghetto.

Basi nimetembea kama mita kumi hivi njia nzima nipo peke yangu mara nasikia kuna mtu kama anatembeaa ila kwa vishindo kidogo sana, kucheki nyuma kuna njemba hata sijui ilikotokea, kwa hatua za kiusalama akili ilifunguka nikaongeza mwendo ila nikienda kushoto nae anakuja kushoto nikienda kulia nae ni kulia anakuja kwa kuongeza mwendo, mara mbele yangu akatokea mwengine kama anataka anizibe flani hivi.

Nilitoka mbio, sikuruhusu kuwa ndani ya 18 zao maana kwa stori tulizokuwa tukiskia ni kwamba wale vijana ni hatari tupu, nlijidai kama nmesimama flani hivi, akilini nikawa nachora ramani nikimbilie wapi, basi ile nakariba kuwa ndani ya 18 nlitoka spidi nadhani ile siku ndio nlikimbia tangu nizaliwe, wakati nataka nianze kukimbia moja wao alinipiga na kitu kama ubao, nilivyofika geto nilikuwa na kanundu kwa mbali, walinifukuza kidogo ila kwa mbio nilizotoka naona walisanda huku wakinisindikiza na matusi mazito ila nashukuru niliwakwepa.
Hongeraa pale kwenye ile sehemu ilikuwa hatari sanaa ziku zote
 
Hyo ndo kanuni muhim tena kama njia unayopita kuna wahun mbele vua kabisa shat weka begani tembea kwa kutuna uku ukijiongelea kwa nguvu kibabe Zaidi tena mwendo nao tembea wa kibaharia na ukipita Kwny kona usijitokeze mzimamzima ikibidi inamisha kichwa kidogo alaf pita apo unaweza kwepa roba ya Koo.
Kuvua shati na kutembea bega juu bega chini hizo ni code mkuu kuna mitaa ukipita hvyo hata iwe sa tisa usiku uwezi kukabwa
 
Kipindi hiko maisha ya kuunga unga, 2015 baada ya dili zangu kufeli kkoo, nikaona niingie ilala, nikadaka daladala fasta hadi amana pale

Napo pale Amana mambo hayakua upande wangu, ilibidi safari ya kugeuka ubungo geto ianze rasmi
Daladala za kutokea mnazi mmoja zinazoenda ubungo (hii route ina daladala chache sana) zimejaza kiasi cha kwamba mimi ni masikini lakini wale ni masikini zaidi[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Nikaona hapa kubalance hesabu inabidi niue winga hadi buguruni then nipande dalala pale hadi ubungo
Tena naweza nikalia nikapanda kwa 300/=

Safari ikaanza, kutoka ilala nikaona hapa niitafute buguruni kwa kuprint mokomoko (kutembea kwa miguu) hiyo mishale ya saa 4

Katika kula mitaa hapa na pale hatua kama 40 nikapata company ya watu kama 3 "vibaka"

Sijakaa sawa raia hawa hapa, mmoja akaja kwa mbele mwingine akaniwai roba aisee. Nikawa mpole
Mwingine anajifanya kama father hivi huku anavuta fegi, "dogo tulia atutaki kuuza gazet hapa"
Akanipiga search akapata buku, hapo nimewapa ushirikiano 90%

Wakaniacha wao wanatembea na mimi natembea uelekeo tofauti, ila niliwachana
Nikawaambia wanangu sio fresh haya maisha tu,

Nikaona Kwa usalama wangu sasa ngoja nikatembee along the road, hapo nipo malapa napandisha kimwinuko upande wa kulia opposite yangu kuna makaburi around za saa 5 kasoro
Mara nashangaa miguu haigusi chini alafu upumuaji haupo kama unavyotakiwa
Nikagundua nipo kwenye kitanzi cha wahuni hapa
Mikiki mikiki nikapate ahueni ya kupumua,
alafu walikua machalii tu
Nikaona hawa acha niwapange kishikaji, nikawaambia wanangu nimetoka kukabwa mtaa wa nyuma hapa sina kitu, mtaniua bure kamanda wenu
Kumbuka bado nipo kwenye roba [emoji3][emoji3]

Madogo wamevuta mibangi hawana ata time ya kucheka, walivyomaliza inspection bila kupata kitu wakaniacha

Pale kinyonge hadi buguruni chama, nikaingia mifuko ya siri, hii mifuko ya kibahari zaidi nikatoka na buku 8000, nikanunua soda takeaway huku nawashangaa wazarendo pale "KAMBOKI"
Huku najisemea moyoni, oneday tutafurahi pamoja[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]


Sasa ntakuja kuelezea nusura Niue mtu kwenye haya haya mambo ya kukabwa[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Mitaa yangu hiyo mkuu, dah way back nimesizi sana malapa hapo. Umenikumbusha mbali sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes 2010
Fainali uefa baina ya asernal na Barcelona kumbukumbu golikipa asernal alipata kadi nyekundu mapema sana alimgusa unyayo samueli eto akienda kufunga goli

Najamaa yangu tunasiku mbili panaitwa bagamoyo unaelekea stend kuu yatukuyu panadispensari na bar moja hivi nalakitano kwenye waleti ,simu Samsung

Kumbe kunajamaa ananiwinda mana natumia pombe balaa
Ukafika muda wamechi bwana ukumbini nilazima upite kaunta ,upande wakulia kunachoo unavoelekea ukumbini
Niliingia choo gent kama kawa kumbe kibaka alikuja nyumayangu akaingia cha ke ili ufike choo cha wanaume nilazima uvuke mlango wa ke
Natoka hivi nataka kukunja niingie baa niliguswa begani kugeuka nikasukumwa kidogo ukutani nikanata pale

Jamaa akatoa kisu vile vyakufyatua akaniambia unaona watu wanapita kuingia kuangalia mechi nikasema ndio
Ukipiga kelele wananiua naomba zilehela zote na simu kila kitu tumeona kwanza mgeni hapa tokajana unakunywa tu bia hapa ukikaa hata kuinuka huinuki

Nikasema nimekwisha ghafla akili ikija yule jamaa niponae alikua ametoka bwana mungu mwema akili ikaja nilegeze mwili na kauli hapo kichwani nipo nahisi damu inamwagika nimeloa mwiliwote
Watu wanapita nawanamwita jamaa jinalake(),anaitikia poa napiga stories na big yetu hapa

Basi ,nikamuangalia alivo nikipande cha MTU mweusi harufu pia yabangi kwambali nasikia toka kwake
Kimo chake urefu kidogo tunalingana

Nawaza nipige wapi huyu usoni jibu ikawahapa
Ghafla wazo likaja nitagonga kichwa changuvu eneo lapua nilazima ainame kidogo niifaidi pua yake
Nikamwambia naomba laini nitoe nikuachie simu napesa zote nakupa

Jibu likawa
Sawa brother nyie ndo mabrother tunawataka hamna bugdha
Nikatoa laini ingia mfuko wanyuma to a waleti

Wakati natoa waleti aliinama ili aifadhi kisu anavoinuka niligonga kichwa puani alilia kwasauti kubwa mamaaaaa nakufa akadondoka chini paaa

RAIA kwenye ukumbi na bar wakatoka wanauliza imekuaje nikawambia wakati mnapita hapa nilikua nimepigwa tero amesema nimpe simu napesa pia Mimi mgeni nakaaje sikumbili nakunywa tu pombe

ndo nikasikia najina lake anaitwa God ,dereva vigali beba mizigo soko LA tukuyu stend pale



Kutoka ilesiku sijawahi kusekana nyumbani sambili kamili usiku labda niwe safarini

Usiombee ukutwe au ubananishwe na kibaka sikiaga tu

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
Ghwandike kinyakyusa khitupu nkamu,,,,,huu mwandiko una lafudhi ya Kinyakyusa mkuu...
 
Nilipigwa ROBA kichochoro cha Mbagala Kiburugwa....

Kanuni ya ROBA si kung'ang'ania uutoe mkono....bali bila ya kupoteza muda nilijikunja na kuweka mikono katika mkono wake ulio shingoni mwangu na "kuning'inia"....

Kama umecheza MARTIAL ARTS hii ndio salama yako....

Kikanuni.....hakuna mkono unaoweza kuhimili UZITO WA KILO 70 za mwanadamu....

Yuke Sakala hakuhimili UZITO WA MNING'INIO WA MWILI WANGU ,miguu nimeikunja pia ili niongeze uzito chini(gravity)....mkono wake ulichoka na akaniachia....Kama angeujua "mchezo" basi wakati NILIPOJIKUNJA NA KUINAMA angekwenda nami chini(naye angeinama).....angefanya hivyo NISINGEWEZA KUJIOKOA....

Baada ya kuchoka mkono wake ,nilimgeukia kwa haraka na KUMTIA VIDOLE VYA MACHO....huku nikikamata "MBUPU"zake na kuzivuta.... Alitoa ukelele mmoja matata....SIKUMSUBIRI NIKAKIMBIA MBIO ZA USAIN BOLT....🤣🤣
 
Kilimanjaro,Moshi vijijini,Kibosho mtaa wa Kombo, Tumekaa kwenye gogo tunakula "kaya" na wanangu wawili mmoja mtoto wa Tandika (M'bongo) na (Nzige) huyu kwao Chunya-Mbeya , majira ya saa 12 jioni ghafla bin vuu ikatokea njemba moja hivi mbavu sana ikachomoa panga, hapo mi ndo nilikuwa naroli kitu, Nzige akataka kukimbia kwa uoga "oya chini ya ulinzi, kaa chini" mimi na huyo dogo wa Dsm ndo tulikuwa hatuna kitete, mi kwanza nikalipua "kitu" punde si punde zikaibuka njemba mbili kwa mtindo ule ule wa mapanga , sasa kati ya wale wawili waliokuja mmoja wao nilikuwa nakutana nae kwa pusha mara ingine namnunulia ganja au namuachia fegi, alivoniona tu akaja akatoa "tano" wale wenzake wawili wakakosa nguvu ya kutukaba, alafu mi hapo nishasizi siogopi chochote, nikamtembezea ganja yule mbavu nikawasha na fegi wakashusha mapanga yao tukaanza kupiga nao na stori nikawapa na ganja wakanyonga....

Wahuni hatukabwi kizembe, labda ukosee code
 
Vaa buti LA kihuni,jins mtumba mnyonyo,kunja suruali mguu mmoja na mwingine achia kawaida,vua shati au T-shirt kisha tupia begani ubaki na vest kisha badili Mwendo na bega moja bonyeza chini,dundika km mla ngada,nunua sigara hata 3 vuta hadi uvuke sehemu hiyo Mbaya na puliza moshi Wa kutosha hewani,hakuna kibaka atakugusa
 
Kipindi hiko maisha ya kuunga unga, 2015 baada ya dili zangu kufeli kkoo, nikaona niingie ilala, nikadaka daladala fasta hadi amana pale

Napo pale Amana mambo hayakua upande wangu, ilibidi safari ya kugeuka ubungo geto ianze rasmi
Daladala za kutokea mnazi mmoja zinazoenda ubungo (hii route ina daladala chache sana) zimejaza kiasi cha kwamba mimi ni masikini lakini wale ni masikini zaidi[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Nikaona hapa kubalance hesabu inabidi niue winga hadi buguruni then nipande dalala pale hadi ubungo
Tena naweza nikalia nikapanda kwa 300/=

Safari ikaanza, kutoka ilala nikaona hapa niitafute buguruni kwa kuprint mokomoko (kutembea kwa miguu) hiyo mishale ya saa 4

Katika kula mitaa hapa na pale hatua kama 40 nikapata company ya watu kama 3 "vibaka"

Sijakaa sawa raia hawa hapa, mmoja akaja kwa mbele mwingine akaniwai roba aisee. Nikawa mpole
Mwingine anajifanya kama father hivi huku anavuta fegi, "dogo tulia atutaki kuuza gazet hapa"
Akanipiga search akapata buku, hapo nimewapa ushirikiano 90%

Wakaniacha wao wanatembea na mimi natembea uelekeo tofauti, ila niliwachana
Nikawaambia wanangu sio fresh haya maisha tu,

Nikaona Kwa usalama wangu sasa ngoja nikatembee along the road, hapo nipo malapa napandisha kimwinuko upande wa kulia opposite yangu kuna makaburi around za saa 5 kasoro
Mara nashangaa miguu haigusi chini alafu upumuaji haupo kama unavyotakiwa
Nikagundua nipo kwenye kitanzi cha wahuni hapa
Mikiki mikiki nikapate ahueni ya kupumua,
alafu walikua machalii tu
Nikaona hawa acha niwapange kishikaji, nikawaambia wanangu nimetoka kukabwa mtaa wa nyuma hapa sina kitu, mtaniua bure kamanda wenu
Kumbuka bado nipo kwenye roba [emoji3][emoji3]

Madogo wamevuta mibangi hawana ata time ya kucheka, walivyomaliza inspection bila kupata kitu wakaniacha

Pale kinyonge hadi buguruni chama, nikaingia mifuko ya siri, hii mifuko ya kibahari zaidi nikatoka na buku 8000, nikanunua soda takeaway huku nawashangaa wazarendo pale "KAMBOKI"
Huku najisemea moyoni, oneday tutafurahi pamoja[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]


Sasa ntakuja kuelezea nusura Niue mtu kwenye haya haya mambo ya kukabwa[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Ulikabwa mara 2 wakati mmoja ? Hawana huruma 😀
 
Miaka ya 2013 naishi kigamboni ferry.
Nilikuwa nafanya shughuli za umeme Goba.
Siku Moja nimerudi ghetto mida ya night huku nimeweka tester (Screwdriver) flat mfuko wa shati.
Sasa wakati nakatizq chochoro za magenge ya urasa, mara ghafla , kibaka akanipiga roba matata. Pasipo kupoteza muda nikawahi ile pisipisi yangu iliyo mfuko wa shati. Nikamdunga nayo mitaa ya Mbavu. Ile anashituka kuniachia, mie nikakurupuka kukimbilia huku sokoni chini, kibaka akakimbilia kule juu.
Pisipisi nayo ilipotelea pale pale.
Tangu siku hiyo, mtaani wananiogopa , kwa kitendo kile. Nilichomfanya yule kibaka.

Mara zote Jaribu kuwa na zana shirikishi. Pindi inapofika usiku.
 
Nilipigwa ROBA kichochoro cha Mbagala Kiburugwa....

Kanuni ya ROBA si kung'ang'ania uutoe mkono....bali bila ya kupoteza muda nilijikunja na kuweka mikono katika mkono wake ulio shingoni mwangu na "kuning'ania"....

Kama umecheza MARTIAL ARTS hii ndio salama yako....

Kikanuni.....hakuna mkono unaoweza kuhimili UZITO WA KILO 70 za mwanadamu....

Yuke Sakala hakuhimili UZITO WA MNING'INIO WA MWILI WANGU....mkono wake ulichoka na akaniachia....Kama angeujua "mchezo" basi wakati NILIPOJIKUNJA NA KUINAMA angekwenda nami chini(naye angeinama).....angefanya hivyo NISINGEWEZA KUJIOKOA....

Baada ya kuchoka mkono wake ,nilimgeukia kwa haraka na KUMTIA VIDOLE VYA MACHO....huku nikikamata "MBUPU"zake na kuzifuvuta.... Alitoa ukelele mmoja matata....SIKUMSUBIRI NIKAKIMBIA MBIO ZA USAIN BOLT....[emoji1787][emoji1787]
Hawa wajinga wa Mbagala wasijichanganye kwangu nitawaua.
 
Back
Top Bottom