Umewahi kusoma kitabu, The Richest Man In Babylon? Ulijifunza nini? Kinasaidia?

Umewahi kusoma kitabu, The Richest Man In Babylon? Ulijifunza nini? Kinasaidia?

Baada ya karamu, baba yake na mama yake wakaketi vitini kama vile ni mfalme na malkia. Nomasir akasimama mbele yao ili kueleza yale aliyotimiza kwa kipindi cha miaka kumi.

"Mke wa Nomasir, wana wake wawili, rafiki zake na ndugu zake wengine wa ukoo walikaa kwenye zuria nyuma yake, wakisubiri kwa hamu kumsikiliza.

'''Baba yangu,' alianza kusema, ninainama kwa heshima ya busara zako. Miaka kumi iliyopita nilipoanza kuingia utu uzima, uliniagiza niende na nikapambane kuwa mwanaume kati ya wanaume badala ya kuwa mshirika na mrithi tu wa mali yako.

'''Ulinipatia dhahabu na hekima yako. Nikiri kuwa dhahabu uliyonipa sikuweza kuitumia vizuri, ilipukutika yote. Ilikimbia kama vile sungura hukimbia kutoka katika mikono ya mwindaji asiye na uzoefu.

"Baba yake akatabasamu na kusema,' endelea kusimulia, napenda kusikia kwa undani zaidi.'

'''Nilipotoka hapa nikaamua kwenda Ninawi. Kwa sababu ni mji uliokuwa unakua nilitumaini kutakuwa na fursa nyingi. Nilijiunga na msafara wa wafanyabiashara waliokuwa wakielekea huko. Njiani nilipata rafiki wengi na kati yao walikuwapo mabwana wawili wachangamfu. Walikuwa na farasi mweupe mzuri sana.

'''Tulipokuwa safarini, walinisimulia kuwa huko Ninawi kuna tajiri ambaye alikuwa na farasi ambaye hajawahi shindwa mashindanoni. Mmiliki wake alikuwa akijigamba kuwa hakuna farasi mwenye kasi kama wake. Alikuwa tayari kuweka kiasi chochote cha pesa dhidi ya farasi mwingine yoyote wa Babiloni. Rafiki zangu wale waliniambia kuwa, ukilinganisha na farasi waliyekuwa naye, farasi anayesifiwa ni kama punda tu na anaweza kushindwa kirahisi sana.

'''Wakaniambia kuwa kama nitapenda niungane nao katika kuweka pesa juu ya farasi wao dhidi ya farasi wa yule tajiri. Nilivutiwa sana na mpango ule.

'''Farasi wetu alishindwa vibaya na nilipoteza dhahabu nyingi sana.'
Baba yake akacheka baada ya kusikia hivyo.

'''Baadaye nikaja kugundua kuwa ulikuwa ni mpango wa kitapeli. Wale watu walikuwa wakisafiri na misafara ya wafanyabiashara wakitafuta watu wa kuwatapeli. Yule aliyedaiwa kuwa ni tajiri wa Ninawi alikuwa ni mshirika wao na waligawana pesa baada ya kushinda. Utapeli huu wa kijanja ulinifundisha somo la kuwa makini.

'''Baada ya muda mfupi nilipata funzo lingine lakini kwa uchungu vilevile. Kwenye ule msafara kulikuwa na kijana ambaye tulitokea kuwa marafiki wazuri sana. Alionekana kuwa ni mtoto wa kitajiri, alikuwa anaenda Ninawi kuangalia fursa, kama mimi tu. Muda mfupi baada ya kufika Ninawi akaniambia kuwa kuna mfanyabiashara amefariki na duka lake pamoja na bidhaa zake vinaweza kununuliwa kwa bei nafuu sana. Akaniambia tuwe washirika lakini kwanza inampasa kurudi Babiloni kuchukua pesa zake. Akanishawishi kununua biashara ile kwa pesa zangu na kuniambia pesa zake zitatumika kuongezea mtaji hapo baadaye.

'''Siku zilikwenda lakini hakurudi Babiloni kufuata pesa zake na mbaya zaidi alikuwa hajui biashara na ni mtu mwenye matumizi mabaya. Nilimfukuza kwenye biashara lakini tayari hali ya biashara ilikuwa mbaya sana. Bidhaa zilizobaki zilikuwa hazifai kuuzwa na sikuwa na pesa ya kununulia zingine. Niliamua kuuza ile biashara kwa muisraeli mmoja kwa bei ya hasara.

'''Baada ya hapo maisha yalikuwa magumu sana. Nilitafuta kazi lakini sikupata kwa sababu sikuwa na ujuzi wowote. Nililazimika kumuuza mtumwa wangu na baadhi ya nguo zangu ili nipate kula na sehemu ya kulala. Siku zilivyosonga ndivyo maisha yalivyozidi kuwa magumu.

'''Katika siku hizo ngumu nilikumbuka jinsi unavyiniamini. Ulinituma nikawe mtu wa maana na hilo ndilo nililopanga kutimiza.' Baada ya kusikia hayo mama yake alijiziba uso na kulia.
'''Muda huo ndipo nilipokumbuka kuhusu lile bamba ulilonipatia. Nikasoma maneno yake kwa umakini mkubwa, iwapo ningepata busara iliyokuwepo mule kabla ya kuanza kuwekeza basi nisingeweza kupoteza pesa zangu. Nilijifunza sheria zote na kuziweka akilini. Nikajiapisha kuwa iwapo Mungu wa bahati akinibariki tena nitaongozwa na busara iliyojengwa kwa miaka mingi badala ya kufanya mambo bila uzoefu kama ilivyo kawaida ya vijana.

'''Kwa faida ya nyote mliokusanyika hapa usiku wa leo, nitasoma hekima aliyonipa baba yangu kama ilivyoandikwa kwenye bamba alilonipa miaka kumi iliyopita.

Sheria tano za pesa

1. Pesa huja kwa wingi kwa yule ambaye huweka akiba moja ya kumi ya kipato chake. Na kuitumia kuwekeza kwa ajili ya wakati ujao.

2. Pesa hufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu iwapo itampata mtu anayeipatia kazi yenye faida. Hapo itaongezeka kama wanyama wa kufungwa.

3. Pesa hung'ang'ania kukaa kwa mtu mtu anayeilinda na mwenye tahadhari. Mtu anayeomba ushauri kutoka kwa watu wenye ujuzi na uzoefu wa kuitunza.

4. Pesa haikai na hupotea kwa mtu ambaye anawekeza kwenye biashara au mradi ambao haijui vizuri, au kwa mtu ambaye hapati ushauri kutoka kwa wale wenye uzoefu na ujuzi wa kuitunza.

5. Pesa haikai kwa mtu anayeiwekeza kwenye miradi inayodai kutoa faida kubwa kuliko kawaida, wala kwa wale wanaodanganywa na matapeli na watu wajanja wajanja na wale ambao wanawekeza bila kupata ushauri kutoka kwa wale wenye uzoefu, au wale wanaowekeza kwa sababu wanapenda tu miradi ya aina hiyo.

'''Hizi ndizo sheria tano za pesa kama zilivyoandikwa na baba yangu. Ninaweza kusema kuwa zina thamani kuliko pesa yenyewe, kama tu mtakavyoona kwenye kisa changu.
"Hapo Nomasir alimuangalia tena baba yake. 'Nimekusimulia jinsi kutokuwa na uzoefu kulivyonitumbukiza kwenye umaskini na taabu.
 
'''Lakini hakuna magumu yasiyo na mwisho. Nilipata kazi ya kusimamia watumwa waliokuwa wakijenga ukuta wa jiji.

'''Kwa kufuata sheria ya kwanza ya pesa nilitunza pesa kutoka kwenye pato langu. Niliendelea kutunza kadri nilivyopata hadi nilipofikisha kipande kimoja cha fedha. Nilipata shida kwa sababu kuna matumizi mengi ya maisha na niliishi kibahili sana. Nilipanga kuwa kabla miaka kumi haijaisha niwe nimepata kiasi cha dhahabu kama kile ulichonipatia.

'''Siku moja mmiliki wa wale watumwa ambaye sasa alikuwa rafiki yangu aliniambia. "Wewe ni kijana bahili sana, hutumii kabisa pesa zako, inamaana pesa zako umetunza tu, hazizalishi?"

'''Ndiyo,' nilimjibu, 'mpango wangu ni kutunza hadi kifike kiasi kama kile alichonipatia baba yangu nami nikakipoteza,'

'''Ni mpango mzuri, lakini unafahamu kuwa pesa unayoitunza inaweza kukuzalishia pesa nyingi zaidi?"

'''Nafahamu lakini naogopa kupoteza pesa zangu kama nilivyopoteza zile alizonipatia baba yangu.'
'''Kama unaniamini basi ninaweza kukufundisha jinsi ya kuwekeza pesa kwa faida,' aliniambia. "Ndani ya mwaka mmoja ukuta huu utakuwa umemalizika kujengwa. Utahitaji shaba kwaajili ya kutengenezea milango kwenye kila lango ili kulinda jiji dhidi ya maadui. Huu ndiyo mpango wangu: tujikusanye na tuchange pesa, kisha tukanunue shaba na tini kutoka migodini na kuileta hapa Ninawi kwaajili ya milango. Mfalme atakaposema 'milango itengenezwe,' basi sisi pekee ndiyo tutakuwa na shaba na tini na tutamuuzia kwa bei nzuri. Hata kama mfalme hatanunua kutoka kwetu tutaweza kuuza kwa watu wengine na kwa bei nzuri.

'''Kwa jinsi alivyonieleza nilikumbuka sheria ya tatu ya pesa. Sheria inayoshauri kuwekeza chini ya uongozi wa watu wenye ujuzi na uzoefu. Sikujutia uamuzi wangu, uwekezaji wetu ulikuwa wa mafanikio makubwa na pesa zangu chache ziliongezeka sana.
'''Baada ya hapo nikakaribishwa kuwa mshirika wa lile kundi na nilishiriki kwenye uwekezaji mwingine mwingi sana. Lilikuwa ni kundi la watu wanaojua jinsi ya kuwekeza pesa kwa faida. Kila mpango wa uwekezaji ulijadiliwa kwa kina kabla ya kuanza. Hawakuwekeza kwenye miradi ambayo kulikuwa na hatari ya kupoteza mtaji wala hawakuwekeza kwenye miradi ambayo haileti faida na ambayo ni ngumu kurejesha mtaji.

'''Vitu vya kipumbavu kama mashindano ya farasi au biashara yangu ya ushirika na yule tapeli hata visingefikiriwa na watu hawa. Mara moja wangejua ubaya wa miradi ile.
'''Kutokana na kushirikiana na watu hawa nilijifunza jinsi ya kuwekeza pesa kwenye miradi yenye faida na salama. Miaka ilivyokwenda ndivyo hazina yangu ilivyozidi kuongezeka kwa kasi. Nilifikisha kile kiasi nilichopoteza mwanzo na kupata na ziada.

'''kutokana na magumu niliyopitia na hatimaye mafanikio nilikuwa nimeona ukweli wa busara zilizokuwepo kwenye zile sheria tano za pesa, na ukweli wa busara ya baba yangu. Zilifanya kazi kila nilipozitumia.
'''Kwa asiyefahamu sheria hizi tano, pesa kwake haiji kirahisi na huondoka haraka. Lakini kwa yule anayezifahamu, pesa huja kirahisi na kumfanyia kazi kama mtumwa muaminifu.
"Nomasir alisimama na kumuonyeshea ishara mtumwa aliyekuwa amesimama nyuma ya kile chumba. Mtumwa alileta mifuko mitatu mizito ya ngozi, akibeba mmoja mmoja. Nomasir aliuchukua mmoja na kuuweka mbele ya baba yake na kusema:

'''Ulinipatia mfuko mmoja wa dhahabu, dhahabu ya Babiloni. Tazama, narudisha kwako dhahabu ya Ninawi yenye uzito uleule. Wote watakubaliana nami kuwa ni mabadilishano sawa.

'''Pia ulinipatia bamba la kigae lililokuwa limeandikwa mambo ya busara juu yake. Tazama! Narudisha mifuko miwili ya dhahabu,' baada ya kusema hayo, alichukua ile mifuko miwili na kuiweka mbele ya baba yake.
'''Nimefanya hivi ili kukuthibitishia ni jinsi gani nathamini hekima na busara zako kuliko dhahabu zako. Ni nani anaweza kupima thamani ya hekima? Bila hekima pesa hupotea haraka lakini mtu mwenye hekima hata kama hana pesa anaweza kuzipata. Mifuko hii mitatu ya dhahabu ni ushahidi kuhusu hilo.
 
'''Lakini hakuna magumu yasiyo na mwisho. Nilipata kazi ya kusimamia watumwa waliokuwa wakijenga ukuta wa jiji.

'''Kwa kufuata sheria ya kwanza ya pesa nilitunza pesa kutoka kwenye pato langu. Niliendelea kutunza kadri nilivyopata hadi nilipofikisha kipande kimoja cha fedha. Nilipata shida kwa sababu kuna matumizi mengi ya maisha na niliishi kibahili sana. Nilipanga kuwa kabla miaka kumi haijaisha niwe nimepata kiasi cha dhahabu kama kile ulichonipatia.

'''Siku moja mmiliki wa wale watumwa ambaye sasa alikuwa rafiki yangu aliniambia. "Wewe ni kijana bahili sana, hutumii kabisa pesa zako, inamaana pesa zako umetunza tu, hazizalishi?"

'''Ndiyo,' nilimjibu, 'mpango wangu ni kutunza hadi kifike kiasi kama kile alichonipatia baba yangu nami nikakipoteza,'

'''Ni mpango mzuri, lakini unafahamu kuwa pesa unayoitunza inaweza kukuzalishia pesa nyingi zaidi?"

'''Nafahamu lakini naogopa kupoteza pesa zangu kama nilivyopoteza zile alizonipatia baba yangu.'
'''Kama unaniamini basi ninaweza kukufundisha jinsi ya kuwekeza pesa kwa faida,' aliniambia. "Ndani ya mwaka mmoja ukuta huu utakuwa umemalizika kujengwa. Utahitaji shaba kwaajili ya kutengenezea milango kwenye kila lango ili kulinda jiji dhidi ya maadui. Huu ndiyo mpango wangu: tujikusanye na tuchange pesa, kisha tukanunue shaba na tini kutoka migodini na kuileta hapa Ninawi kwaajili ya milango. Mfalme atakaposema 'milango itengenezwe,' basi sisi pekee ndiyo tutakuwa na shaba na tini na tutamuuzia kwa bei nzuri. Hata kama mfalme hatanunua kutoka kwetu tutaweza kuuza kwa watu wengine na kwa bei nzuri.

'''Kwa jinsi alivyonieleza nilikumbuka sheria ya tatu ya pesa. Sheria inayoshauri kuwekeza chini ya uongozi wa watu wenye ujuzi na uzoefu. Sikujutia uamuzi wangu, uwekezaji wetu ulikuwa wa mafanikio makubwa na pesa zangu chache ziliongezeka sana.
'''Baada ya hapo nikakaribishwa kuwa mshirika wa lile kundi na nilishiriki kwenye uwekezaji mwingine mwingi sana. Lilikuwa ni kundi la watu wanaojua jinsi ya kuwekeza pesa kwa faida. Kila mpango wa uwekezaji ulijadiliwa kwa kina kabla ya kuanza. Hawakuwekeza kwenye miradi ambayo kulikuwa na hatari ya kupoteza mtaji wala hawakuwekeza kwenye miradi ambayo haileti faida na ambayo ni ngumu kurejesha mtaji.

'''Vitu vya kipumbavu kama mashindano ya farasi au biashara yangu ya ushirika na yule tapeli hata visingefikiriwa na watu hawa. Mara moja wangejua ubaya wa miradi ile.
'''Kutokana na kushirikiana na watu hawa nilijifunza jinsi ya kuwekeza pesa kwenye miradi yenye faida na salama. Miaka ilivyokwenda ndivyo hazina yangu ilivyozidi kuongezeka kwa kasi. Nilifikisha kile kiasi nilichopoteza mwanzo na kupata na ziada.

'''kutokana na magumu niliyopitia na hatimaye mafanikio nilikuwa nimeona ukweli wa busara zilizokuwepo kwenye zile sheria tano za pesa, na ukweli wa busara ya baba yangu. Zilifanya kazi kila nilipozitumia.
'''Kwa asiyefahamu sheria hizi tano, pesa kwake haiji kirahisi na huondoka haraka. Lakini kwa yule anayezifahamu, pesa huja kirahisi na kumfanyia kazi kama mtumwa muaminifu.
"Nomasir alisimama na kumuonyeshea ishara mtumwa aliyekuwa amesimama nyuma ya kile chumba. Mtumwa alileta mifuko mitatu mizito ya ngozi, akibeba mmoja mmoja. Nomasir aliuchukua mmoja na kuuweka mbele ya baba yake na kusema:

'''Ulinipatia mfuko mmoja wa dhahabu, dhahabu ya Babiloni. Tazama, narudisha kwako dhahabu ya Ninawi yenye uzito uleule. Wote watakubaliana nami kuwa ni mabadilishano sawa.

'''Pia ulinipatia bamba la kigae lililokuwa limeandikwa mambo ya busara juu yake. Tazama! Narudisha mifuko miwili ya dhahabu,' baada ya kusema hayo, alichukua ile mifuko miwili na kuiweka mbele ya baba yake.
'''Nimefanya hivi ili kukuthibitishia ni jinsi gani nathamini hekima na busara zako kuliko dhahabu zako. Ni nani anaweza kupima thamani ya hekima? Bila hekima pesa hupotea haraka lakini mtu mwenye hekima hata kama hana pesa anaweza kuzipata. Mifuko hii mitatu ya dhahabu ni ushahidi kuhusu hilo.
Kuwa mtumishi wa Mungu sio lazima uwe na kanisa Kama kina Masanja!! hata kwa kazi hii unayoifanya ni utumushi mkubwa sana!! Kwanza huhitaji sadaka Kama akina Masanja waganga njaa!! wewe unafanya utumishi ulioko moyoni mwako!! sio utumishi was kulazimisha Kama wafanyavyo wengine!!

Utumishi unatoka moyoni!! utumishi ni kipawa mtu anachopewa na Muumba wake!!
 
'''Ni jambo ninalojivunia sana kusimama hapa mbele yako na kusema kuwa hekima yako imeniwezesha kuwa tajiri na kuwa mtu katika watu.'

"Baba yake aliweka mikono yake juu ya kichwa cha Nomasir na kusema. 'Umejifunza masomo yako vizuri nami ni mtu mwenye bahati kwa kuwa na mwana ambaye ninaweza kumuamini juu ya mali yangu.'''

Kalabab alisimama kusimulia kisa chake na kuwaangalia wasikilizaji wake kwa makini.

'''Hadithi hii ya Nomasir ina maana gani kwenu?" Kisha akaendelea kusema.
"Nani kati yenu anaweza kwenda kwa baba yake au kwa baba mkwe wake na kumueleza jinsi alivyoweza kusimamia pesa zake vizuri?

"Watu huwa na pesa nyingi kwa sababu wanazijua sheria tano za pesa na wanazifuata.
"Kwa sababu nilijifunza sheria hizo nilipokuwa kijana na nikazifuata, nimeweza kuwa mfanyabiashara tajiri. Utajiri wangu haujaja kimiujiza.
"Utajiri unaokuja haraka hupotea haraka pia.

"Utajiri unaodumu na kumfurahisha anayeumiliki huja polepole. Huo ni mtoto aliyezaliwa kutokana na maarifa na uvumilivu.

"Kwa mtu mwenye kufikiri kwa kina, kupata utajiri si kazi ngumu wala mzigo mzito. Siri ni kubeba mzigo huo mwaka hadi mwaka na mwisho lengo lake litatimia.

"Sheria tano za pesa huwapatia utajiri wale wanaozichunguza. Kila moja ya sheria hizi tano ni ya maana sana. Msizidharau kwa sababu nimezieleza kwa hadithi fupi tu. Nitarudia kuwaeleza tena. Nimeziweka zote akilini mwangu kwa sababu nilizijua ningali kijana na niliona thamani yake. Nilijifunza kwa bidii hadi nilipozijua vizuri na kuzikariri.

Sheria ya kwanza ya pesa

Pesa huja kirahisi na kwa wingi kwa mtu ambaye anatunza si chini ya moja ya kumi ya pato lake kwajili ya kuwekeza. Kuwekeza kwaajili ya wakati wake ujao na wa familia yake.

"Mtu yeyote anayeweka akiba moja ya kumi ya pato lake bila kukoma, na akiziwekeza pesa hizo kwa hekima, atapata utajiri ambao utampatia kipato kwa wakati wake ujao na wa familia yake iwapo Miungu ikimchukua. Mara zote sheria hii husema kuwa pesa humfuata mtu huyo. Mimi mwenyewe nimeliona hilo maishani mwangu. Kadri nilivyozidi kutunza pesa ndivyo ilivyozidi kuja kwa urahisi na kwa wingi. Pesa niliyotunza ilizalisha zaidi, yenu pia itafanya hivyo. Na kilichozalishwa kinatakiwa kizalishe pia. Hivyo ndivyo sheria ya kwanza inavyofanya kazi.

Sheria ya pili ya pesa

Pesa hufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu kwa bosi anayeipatia kazi yenye faida. Hapo huongezeka kama wanyama wa kufugwa.

"Pesa ni mfanyakazi mwenye kujituma. Tamaa yake kubwa ni kuongezeka kila fursa ya kuongezeka inapopatikana. Mtu yeyote anayejiwekea akiba ya pesa ndiye hufuatwa na fursa zenye faida. Kila mwaka pesa itajizalisha kwa namna ya ajabu sana.

Sheria ya tatu ya pesa

Pesa hung'ang'ania kukaa kwa mtu mwenye kuitunza kwa tahadhari na anayeiwekeza baada ya kupata ushauri kutoka kwa wenye uzoefu wa masuala ya pesa.

"Ni kweli, pesa haiondoki kwa mtu mwenye kuchukua tahadhari na hukimbia kutoka kwa watu wasio makini. Mtu anayeomba ushauri kutoka kwa watu wenye ujuzi wa masuala ya pesa hujifunza kutohatarisha hazina yake bali kuilinda na kuitunza. Huyo hukaa na kufurahia inavyoongezeka kila siku.

Sheria ya nne ya pesa

Pesa huondoka kwa mtu anayewekeza kwenye miradi ambayo hana uzoefu nayo au ambayo haishauriwi na wale wenye uzoefu na masuala ya pesa.

"Kwa mtu mwenye pesa na ambaye hana uzoefu kila mradi utaonekana ni wenye faida. Lakini mingi yao huwa na hatari ya kuleta hasara. Na ikitokea watu wenye uzoefu wa kuwekeza wakaipitia miradi hiyo basi huikuta inauwezekano mdogo wa kuleta faida.

Mtu mwenye pesa ambaye hana uzoefu wa masuala ya pesa lakini akaamua kuwekeza mradi asioujua kwa kutegemea uelewaji wake mwenyewe, mara nyingi hukuta miradi hiyo haipo kama alivyotarajia na kuishia kupoteza hazina yake. Mtu mwenye busara ni yule anayewekeza hazina yake kwa kufuata ushauri kutoka kwa wenye ujuzi wa masuala ya pesa.

Sheria ya tano ya pesa

Pesa humkimbia mtu anayeilazimisha kuzalisha kiasi kikubwa kuliko inavyowezekana, anayefuata ushauri wa matapeli na wajanjawajanja, anayewekeza bila kupata ushauri wa wale wenye uzoefu wa masuala ya pesa na yule anayewekeza kwenye miradi kwa sababu tu anaipenda.

"Mara nyingi mtu akiwa na pesa mawazo mazuri ya jinsi ya kufanikiwa humjia. Anakuwa na mawazo ya kuwekeza na kupata faida kubwa kuliko kawaida. Mtu mwenye hekima anajua hatari ya kutaka kutengeneza pesa nyingi kwa haraka.
"Msiwasahau wale matajiri wa Ninawi ambao hawakuwekeza kwenye miradi iliyohatarisha mitaji yao wala hawakuzika mitaji yao kwenye miradi isiyoleta faida.

"Huu ndiyo mwisho wa simulizi langu kuhusu sheria tano za pesa. Hiyo ndiyo siri ya mafanikio yangu.
"Kwa kweli hakuna siri ya utajiri bali ukweli ulio wazi. Ukweli ambao kila mtu anayetaka kufanikiwa inampasa kujifunza na kuufuata. Mtu anayetamani kutokuwa kama hao mbwa mwitu ambao wanahangaika kupata chakula chao kila leo anatakiwa kufanya yale niliyowaeleza.

"Kesho tutaingia Babiloni, nadhani mnauona moto unaowaka daima juu ya hekalu la Beli? Kesho nitawalipa kila mmoja kwa kazi yake, mmekuwa waaminifu sana.
"Kila mmoja wenu yampasa kujiuliza, miaka kumi kutoka leo atazungumza nini juu ya pesa nitazomlipa?

"Kama kati yenu kuna watu kama Nomasir basi watatumia sehemu ya kumi ya pesa zao kuwekeza na watatumia hekima ya Arkad katika uwekezaji huo. Kama watafanya kama alivyofanya kijana wa Arkad basi miaka kumi kutoka sasa watakuwa matajiri wakubwa na watu wenye kuheshimika.

" Matendo ya hekima hutufuata maisha yetu yote. Hutuburudisha na kutusaidia. Hivyohivyo, matendo yasiyo na hekima hutufuata ili kutuumiza na kututesa. Sehemu kubwa ya mateso hayo huwa ni majuto juu ya mambo tuliyopaswa kufanya lakini hatukufanya. Majuto juu ya fursa zilizotutembelea lakini tukazipuuza.

"Babiloni ni mji tajiri kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kuhesabu dhahabu ulizonazo. Kila mwaka hazina yake inazidi kuongezeka. Kama hazina zingine hii ni zawadi, zawadi nzuri kwaajili ya wale wenye malengo ya kuipata.

Ndani ya nia zenu kuna nguvu kubwa. Chocheeni nia hizo kwa kutumia sheria tano za pesa nanyi mtashiriki utajiri wa Babiloni."


Mwisho wa sura ya Tano
 
MKOPESHA PESA WA BABILONI


Mtu mmoja anayeitwa Rodan aliyekuwa ni mtengeneza mikuki alikuwa ameshikilia kiasi kikubwa sana cha pesa. Maishani mwake hajawahi kushika kiasi kikubwa kama hicho. Vipande hamsini vya dhahabu! Alikuwa anatembea kwa furaha akishuka kwenye barabara pana inayotoka kwenye ikulu ya mfalme. Dhahabu kwenye pochi yake ililia kila alipotembea. Hajawahi kusikia sauti nzuri kama hiyo.

Hakuamini kuwa vipande vile hamsini vya dhahabu ni vyake. Mawazo ya nguvu ya vipande vile yalimzonga, viliweza kununua chochote alichotaka, nyumba nzuri, ardhi, ng'ombe, ngamia, farasi na magari yake; chochote alichotamani.

Azifanyie nini? Jioni hii alipokuwa anakatisha kuelekea kwa dada yake mawazo yake yote yalikuwa kwenye pesa yake.

Jioni kadhaa mbele Rodan alikuwa dukani kwa Mathon. Mathon alikuwa ni mkopesha pesa, muuza vito na vitambaa adimu. Bila kutizama pembeni alipita moja kwa moja hadi nyuma ya duka, ilipo nyumba ya kuishi Mathon. Huko alimkuta Mathon akila chakula alichoandaliwa na mtumwa wake.

"Naomba unisaidie ushauri juu ya jambo moja maana sielewi cha kufanya" alisema Rodan huku akiwa amesimama kizembe, miguu katanua na koti lake likiwa wazi na kuacha nywele za kifuani kuonekana.
Mathon alitabasamu kirafiki na kusema. "Umepatwa na nini hadi utake ushauri kutoka kwa mkopesha pesa?" Umepoteza pesa kwenye kamari? Au kuna mwanamke amekuchanganya? Nimekufahamu siku nyingi lakini hata siku moja hujawahi omba msaada wangu."
"Hapana, hapana, sijaja kukopa pesa, nimekuja tu kuomba ushauri wako,"

"Maajabu haya! Hakuna mtu anayeenda kwa mkopesha pesa kuomba ushauri. Au sijasikia vizuri?."

"Umesikia sahihi kabisa," alisema Rodan.

"Inawezekana kuwa hivyo,?" Isijekuwa una jambo lako. Watu huja kwangu kukopa pesa kwaajili ya mambo yao lakini si kupata ushauri. Lakini kiukweli ni nani anayeweza kutoa ushauri mzuri zaidi ya mkopesha pesa ambaye watu humtafuta wapatapo matatizo?!
"Sasa niambie, kitu gani kinakusumbua,"

"Karibu ule pamoja nami," alikaribishwa Rodan, karibu uwe mgeni wangu usiku wa leo...
"Andol" alimwita yule mtumwa mweusi, "Tandika zuria kwaajili ya rafiki yangu Rodan, amekuja kupata ushauri. Mletee chakula kizuri na mletee bilauri kubwa, pia chagua divai bora kabisa ndiyo umletee.

"Ni zawadi niliyopewa na mfalme."

"Zawadi ya mfalme? Yaani mfalme amekupa zawadi mbayo imekuletea matatizo! Zawadi gani hiyo?"

"Nilipewa kazi ya kuunda mikuki, mfalme alipendezwa sana na kazi yangu hivyo akanipatia zawadi ya vipande 50 vya dhahabu, vipande hivyo ndivyo vinavyonichanganya.

"Haipiti saa lazima nitaombwa na mmoja wa jamaa zangu."

"Hiyo ni kawaida watu hupenda kugawiwa pesa toka kwa mtu wanayefikiri amezipata kirahisi. Kwani huwezi kukataa? Inamaana huna roho ngumu kama mikono yako ilivyo migumu?"

"Wengi ninawakatalia lakini kuna wengine ni vigumu kuwakatalia. Mtu unawezaje kumnyima dada yako kipenzi?"

"Dada yako hawezi kukuzuia kufurahia zawadi yako."

"Lakini ni kwaajili ya mume wake, Araman. Anasema kuwa mume wake hajawahi pata fursa ya kutajirika hivyo ananibembeleza nimkopeshe ili afanye biashara na kutajirika, atanilipa kutokana na faida atakayo pata.

"Sikiliza rafiki yangu," akasema Mathon.

'''Hili ni jambo la maana sana umelileta, inatupasa kulijadili. Pesa inampa yule aliyenayo wajibu mkubwa na pia inabadili nafasi yake katika jamii. Inamfanya awe muoga wa kuipoteza au kutapeliwa. Na inamfanya ajihisi ana nguvu, lakini pia inaweza sababisha nia zake njema zimuingize matatizoni.
 
"Umewahi kusikia kisa cha mkulima wa Ninawi aliyekuwa na uwezo wa kuelewa lugha za wanyama? Natumaini hujawahi maana hizi siyo hadithi watu husimuliana wanapokuwa wanaunda mikuki na kuponda shaba. Nitakusimulia kisa hicho ili ujue kuwa kukopa ni zaidi ya kuhamisha fedha kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

"Mkulima aliyeweza kuelewa wanyama wanachosema alikuwa anakaa karibu na banda Kila jioni ili kusikiliza wakiongea.

"Jioni moja alimsikia ng'ombe dume akinung'unika na kumwambia punda kuwa anafanya kazi ngumu sana. 'Ninavuta jembe la kulimia toka asubuhi hadi usiku unapoingia. Haijalishi kuna joto kiasi gani, miguu yangu imechoka namna gani au nira imenichubua shingo kiasi gani, lazima nifanye kazi. Lakini wewe unaraha sana, umefungwa matandiko mazuri na kazi yako ni kumbeba bwana na kumpeleka atakako. Kama hana safari basi unapumzika siku nzima ukila nyasi.

"Punda alikuwa ni mnyama mwenye dharau lakini alikuwa na roho nzuri hivyo alimuonea huruma yule ng'ombe. 'Rafiki yangu,' akaanza kusema punda yule, 'unafanya kazi ngumu sana. Nitakusaidia kuipunguza. Nitakwambia jinsi unavyoweza kupata siku za mapumziko. Asubuhi mtumwa anapokuja kukuchukua kwenda kulima lala chini na gugumia kwa sauti kumfanya afikirie kuwa unaumwa hivyo hataweza kukupeleka kazini.'

"Fahali yule alichukua ushauri wa punda na kesho yake asubuhi mtumwa alienda kwa mwenye shamba na kumwambia kuwa ng'ombe wa kulimia anaumwa hivyo hataweza kufanya kazi.
"Mwenye shamba akasema. '''Basi mfunge punda kwenye jembe la kulimia sababu lazima kulima kuendelee.'

"Nia ya punda ilikuwa ni kumsaidia rafiki yake tu lakini siku hiyo alijikuta akilima siku nzima. Usiku ulipofika aliachiliwa lakini alikuwa amekasirika sana, miguu ilimuuma na shingo ilimuuma sababu nira ilikuwa imemchubua.
"Yule mwenye shamba akajibanza karibu na banda la wanyama ili aendelee kusikiliza.
"Wewe ni rafiki yangu mzuri sana. Sababu ya ushauri wako nimepumzika siku nzima,' alisema yule fahali.

'''Nimekuwa kama watu wengine wenye huruma ambao wanawasaidia rafiki zao na mwisho hushia kuwafanyia kazi. Kuanzia leo utafanya kazi zako mwenyewe. Tena nimemsikia bwana akisema kuwa ukiumwa tena atakuchinja, na natamani akuchinje tu maana umekuwa mvivu,' alisema punda kwa hasira.
Kuanzia siku hiyo urafiki wao uliisha na hawakusemezana tena.
"Rodan unafikiri kisa hiki kinatufundisha nini?"

"Ni hadithi nzuri," alijibu Rodan, "lakini sijaona inachofundisha."
"Sikufikiria kama utaona, lakini kuna somo zuri na ni rahisi kuliona, ni hili: kama unataka kumsaidia rafiki yako basi msaidie lakini hakikisha tatizo lake halihamii kwako."

"Sikufikiria hilo. Ni somo zuri sana. Kwakweli sina mpango wa kubeba mzigo wa shemeji yangu.
 
Lakini wewe hukopesha pesa kwa watu wengi, si huwa wanakulipa?"

Mathon akatabasamu. Tabasamu la mtu mwenye utajiri wa maarifa.

Je, mkopo unaweza kuwa mzuri iwapo aliyekopeshwa hawezi kulipa? Si ni lazima mkopesha pesa awe makini kujua iwapo mkopo wake utalipwa au utatapanywa na kumuacha na hasara?

Nitakuonyesha dhamana zilizopo kwenye sanduku langu la dhamana nazo zitakudimulia visa vyao."

Mathon akaingia chumbani na kutoka na sanduku lenye kama urefu wa mkono. Lilikuwa limezungushwa kwa ngozi na kupambwa kwa shaba. Aliliweka sakafuni na kuchuchumaa kulifungua. Kwa kila mkopo ninaotoa huwa nataka kitu fulani toka kwa wateja wangu. Wanapomaliza kulipa huwa nawarudishia, lakini wakishindwa kulipa mimi huviacha humu kama kumbukumbu ya kukosa kwao uaminifu.

Sanduku langu linaniambia kuwa mikopo salama ni ile ambayo wakopaji wanaweka vitu vya thamani kama dhamana. Wenye ardhi, vito, ngamia nk. Muda mwingine dhamana huwa na thamani kubwa kuliko mkopo niliotoa. Zingine huwa ni ahadi ambapo tunakubaliana kuwa wakishindwa kulipa basi watanipatia sehemu fulani ya mali zao. Kwa mikopo kama hiyo huwa nahakikisha mali hizo zinathamani ya juu kidogo kuliko mkopo ninaotoa.

"Wengine ni wafanyakazi kama ulivyo wewe. Hawa wana kipato cha uhakika, wasipopatwa na matatizo yoyote ninakuwa na uhakika wa kulipwa pesa zangu pamoja na riba. Mikopo hiyo hutegemea jitihada za watu.

"Wengine ni wale ambao hawana mali wala kazi ya kuwaingizia kipato. Maisha ni magumu lakini kuna watu wengi wasioweza kubadilika kulingana na nyakati.

Mathon alifungua sanduku lake na Rodan akasogea na kuinama karibu kwa shauku.

Alipofungua kulikuwa na kidani cha shaba kikiwa juu ya kitambaa chenye rangi nyekundu-angavu.

"Mathon alikichukuwa kile kidani na kukisugua taratibu. Hiki kitabaki kwenye sanduku langu siku zote, mwenye nacho alikwishafariki. Hiki ni kumbukumbu ya rafiki yangu yule mpendwa. Tulifanya biashara pamoja na kupata mafanikio makubwa. Alikutana na mwanamke mmoja mzuri kutoka mashariki na wakaoana, alikuwa ni mwanamke mnjanjamjanja sana. Rafiki yangu alitumia pesa zake nyingi ili kutimiza tamaa za mwanamke yule. Alipofirisika alinifuata, nilimshauri na kumwambia kuwa nitamsaidia kuweka mambo yake sawa. Alinihakikishia kuwa hata niangusha lakini haikuwa hivyo. Kuna siku waligombana na mkewe akaishia kuchomwa kisu na mkewe na kufariki."

"Nini kilimpata mke wake?" Akauliza Rodan.

"Hicho kipande cha kitambaa chekundu-angavu ni chake. Alijutia alichokifanya hivyo akajiua kwa kujitumbukiza kwenye mto Efrati. Mkopo huu hautakuja kulipwa kamwe. Sanduku hili linatufundisha kuwa mtu aliye kwenye msongo wa mawazo hafai kukopeshwa.

"Hapa kuna kitu kingine, hiki kisa chake ni tofauti." Alisema Mathon na kuchukua pete iliyokuwa imetengenezwa mifupa ya ng'ombe dume.

"Hii ilikuwa mali ya mkulima. Nilikuwa nanunua mazuria kutoka kwa wake zake. kuna kipindi baa la nzige lilitokea na hawakuwa na chakula. Nilimkopesha kwa makubaliano kuwa atanilipa atakapovuna msimu unaofuata. Lakini baada ya muda akaja na kuniomba kuwa kwenye nchi ya mbali kulikuwa na mbuzi bora sana. Aliniambia kuwa walikuwa ni wenye manyoya mengi na laini ambayo yangeweza kutengeneza mazuria bora kabisa.

Nilimkopesha pesa ili akanunue mbuzi hao na kuwaleta hapa Babeli. Mwaka ujao tutavuna manyoya na kuwashangaza matajiri wa Babeli kwa mazuria bora kabisa ambayo watanunua kwa pesa nyingi. Hapo ndipo nitamrudishia pete yake. Anasisitiza kuwa atanilipa haraka sana.

"He! Kuna wakopaji wanaosisitiza kulipa madeni yao haraka na kwa mkupuo?' alihoji Rodan.
"Kwa wale wanaokopa kwa malengo ya kuwekeza mara nyingi huwa hivyo, lakini wale wanaokopa kwa matumizi tu nakuonya dhidi yao iwapo unatak pesa yao irudi mikononi mwako."

"Vipi kuhusu hiki," alisema Rodan huku akishika bangili ya dhahabu iliyokuwa imepambwa na vito adimu na muundo wa pekee.
"Bado unatamani wanawake? " Alisema Mathon.
"Mimi bado ni kijana kuliko wewe," alijibu Rodan.
"Ni kweli lakini bangili hiyo isikufanye ufikirie mapenzi, mwenye nayo ni mwanamke mnene na mzee. Ni mwenye maneno mengi hadi huniudhi.

Mume wake alikuwa ni tajiri na walikuwa wateja wangu wazuri. Lakini baadaye hali yao haikuwa nzuri na wakafirisika. Akataka mwanawe awe mfanyabiashara hivyo alikuja na kukopa dhahabu na kumpa mwanawe ili aungane na wafanyabiashara wanaosafiri.

"Mfanyabiashara aliyeungana naye hakuwa mtu mzuri. Walipokuwa mji wa mbali alimtoroka kijana wakati wa asubuhi sana. Kijana hakuachwa na chochote. Labda kijana huyu akiwa mtu mzima ataweza kunilipa lakini mpaka sasa sijalipwa chochote zaidi ya maneno tu. Lakini bangili hii ni dhamana nzuri kwa ule mkopo.

"Huyu mama alikuomba ushauri wa juu cha kufanya na ule mkopo?"

"Hata kidogo. Alikuwa ana ndoto akimuona kijana wake akiwa tajiri na mtu mkubwa hapa Babiloni. Kumshauri vinginevyo ilikuwa ni kumkasirisha tu. Toka mwanzo nilikuwa na shaka na ile biashara kwa sababu kijana wake hakuwa na uzoefu wowote, lakini sababu aliweka dhamana sikuona sababu ya kumkatalia.
 
"Hiki hapa," aliendelea kusema Mathon huku akifungua kamba moja, 'Hii ni mali ya Nebaturi, mfanyabiashara ya ngamia. Kila atakapo kununua ngamia wengi kuliko pesa alizonazo huniletea kamba hii nami humkopesha kulingana na mahitaji yake. Ni mtu ninayemuamini sana. Ni mfanyabiashara mzuri na muaminifu hivyo hata bila dhamana mimi humkopesha. Ninawaamini wafanyabiashara wengi hapa Babiloni sababu ya uaminifu wao. Huweka mali zao kama dhamana na kuzikomboa mara tu wakamilishapo biashara. Wafanyabiashara wazuri ni hazina ya mji wetu na ni faida kwangu kuwasaidia kuendelea kufanya biashara na kuzidi kuneemesha mji wetu."

Mathon alichukua kito cha rangi ya ubluu na ukijani na kukitupa chini kwa dharau. "Mdudu kutoka Misri. Aliyekuwa anamiliki hiki hajali kabisa kunilipa. Nikimfuata kumdai anajibu, "nitakulipaje nami nimeandamwa na majanga kila leo? Hata hivyo wewe unapesa za kutosha! Unafikiri nitafanya nini?'

Dhamana ni ya baba yake. Baba yake si mtu tajiri lakini alijinyima na kuweka shamba na mifugo yake kama dhamana ili mwanae afanye biashara. Kijana wake alianza vizuri biashara zake na alikuwa akipata faida lakini akaingiwa na tamaa ya kutaka utajiri wa haraka. Kwa kuwa hakuwa na ujuzi mwingi, biashara yake ikafa.

"Vijana wana malengo makubwa sana. Mara zote wanatafuta njia ya mkato ya kuwa matajiri. Ili kupata utajiri haraka mara nyingi hukopa bila kufikiri.

Kwa kukosa kwao uzoefu hawatambui kuwa deni baya ni shimo refu ambalo unaweza kutumbukia kirahisi lakini ukahangaika kwa siku nyingi ili kutoka. Ni shimo la majuto na huzuni. Ni shimo ambalo jua la mchana huzibwa na mawingu na usiku hufanywa mchungu kwa usingizi wa mang'amung'amu.

Si kwamba nashauri watu wasikope, hapana! Nasisitiza watu wakope lakini iwe kwa jambo la maana. Mimi mwenyewe nilianza kufanya biashara kwa pesa za mkopo.

"Lakini mkopeshaji anapaswa kufanya nini kwa jambo kama la huyu kijana? Kijana mwenyewe amekata tamaa, hafanyi chochote wala hafanyi bidii yoyote kulipa deni. Moyo wangu unakuwa mzito kuchukua shamba na mifugo ya baba yake."

"Umeniambia habari nyingi na nimezifurahia ," alisema Rodan. "Lakini hujajibu swali langu iwapo nimkopeshe vipande vyangu hamsini vya dhahabu mume wa dada yangu? Kumbuka hawa ni ndugu zangu wa karibu sana.

"Dada yako ni mtu anayejitambua nami namheshimu kwa hilo. Lakini kama mume wake angekuja kwangu kuomba nimkopeshe vipande hamsini vya dhahabu lazima ningemuuliza anataka kufanyia nini?
"Kama akisema anataka kuwa mfanyabiashara kama mimi na kuuza vito na samani za gharama nitamuuliza. Unaujuzi gani kuhusiana na biashara? Unajua unakoweza kununua kwa bei rahisi ? Unajua unakoweza kuuza kwa bei nzuri?

Je, shemeji yako anafahamu vitu hivyo?

"Kwakweli hafahamu," akajibu Rodan. "Alikuwa msaidizi wangu kwenye kutengeneza mikuki na amewahi kuwa msaidizi wa dukani."

"Kama ni hivyo nitamwambia kuwa hajachagua kazi yake kwa busara. Mfanyabiashara anatakiwa kuwa na ujuzi wa kazi hiyo. Ana malengo mazuri lakini hayatimiziki, nisingeweza mkopesha pesa zangu.

"Tuseme angejibu kuwa, 'ninafahamu sababu nimekuwa msaidizi wa wafanyabiashara kwa muda mrefu. Ninajua jinsi ya kufika Smyrna na kununua mazuria yaliyoshonwa na wakinamama kwa bei ya chini. Pia nawajua matajiri wengi wa Babiloni ninaoweza kuwauzia kwa faida kubwa,' hapo ningemwambia kuwa 'lengo lako ni zuri na mpango wako unatekelezeka. Kwa hiyo ningekuwa tayari kumkopesha vipande hamsini vya dhahabu iwapo atakuwa na dhamana."

"Iwapo angesema 'sina dhamana yoyote lakini mimi ni muaminifu, nitalipa pesa yako vizuri,' ningemwambia; 'ninathamini kila kipande cha dhahabu nilichonacho. Inaweza tokea wanyang'anyi wakakupora pesa unapoenda Smyrna au kukupora mazuria unaporudi. Si unakuwa huna jinsi ya kunilipa na pesa yangu inakuwa imepotea?'
 
Safi sana
Baada ya karamu, baba yake na mama yake wakaketi vitini kama vile ni mfalme na malkia. Nomasir akasimama mbele yao ili kueleza yale aliyotimiza kwa kipindi cha miaka kumi.

"Mke wa Nomasir, wana wake wawili, rafiki zake na ndugu zake wengine wa ukoo walikaa kwenye zuria nyuma yake, wakisubiri kwa hamu kumsikiliza.

'''Baba yangu,' alianza kusema, ninainama kwa heshima ya busara zako. Miaka kumi iliyopita nilipoanza kuingia utu uzima, uliniagiza niende na nikapambane kuwa mwanaume kati ya wanaume badala ya kuwa mshirika na mrithi tu wa mali yako.

'''Ulinipatia dhahabu na hekima yako. Nikiri kuwa dhahabu uliyonipa sikuweza kuitumia vizuri, ilipukutika yote. Ilikimbia kama vile sungura hukimbia kutoka katika mikono ya mwindaji asiye na uzoefu.

"Baba yake akatabasamu na kusema,' endelea kusimulia, napenda kusikia kwa undani zaidi.'

'''Nilipotoka hapa nikaamua kwenda Ninawi. Kwa sababu ni mji uliokuwa unakua nilitumaini kutakuwa na fursa nyingi. Nilijiunga na msafara wa wafanyabiashara waliokuwa wakielekea huko. Njiani nilipata rafiki wengi na kati yao walikuwapo mabwana wawili wachangamfu. Walikuwa na farasi mweupe mzuri sana.

'''Tulipokuwa safarini, walinisimulia kuwa huko Ninawi kuna tajiri ambaye alikuwa na farasi ambaye hajawahi shindwa mashindanoni. Mmiliki wake alikuwa akijigamba kuwa hakuna farasi mwenye kasi kama wake. Alikuwa tayari kuweka kiasi chochote cha pesa dhidi ya farasi mwingine yoyote wa Babiloni. Rafiki zangu wale waliniambia kuwa, ukilinganisha na farasi waliyekuwa naye, farasi anayesifiwa ni kama punda tu na anaweza kushindwa kirahisi sana.

'''Wakaniambia kuwa kama nitapenda niungane nao katika kuweka pesa juu ya farasi wao dhidi ya farasi wa yule tajiri. Nilivutiwa sana na mpango ule.

'''Farasi wetu alishindwa vibaya na nilipoteza dhahabu nyingi sana.'
Baba yake akacheka baada ya kusikia hivyo.

'''Baadaye nikaja kugundua kuwa ulikuwa ni mpango wa kitapeli. Wale watu walikuwa wakisafiri na misafara ya wafanyabiashara wakitafuta watu wa kuwatapeli. Yule aliyedaiwa kuwa ni tajiri wa Ninawi alikuwa ni mshirika wao na waligawana pesa baada ya kushinda. Utapeli huu wa kijanja ulinifundisha somo la kuwa makini.

'''Baada ya muda mfupi nilipata funzo lingine lakini kwa uchungu vilevile. Kwenye ule msafara kulikuwa na kijana ambaye tulitokea kuwa marafiki wazuri sana. Alionekana kuwa ni mtoto wa kitajiri, alikuwa anaenda Ninawi kuangalia fursa, kama mimi tu. Muda mfupi baada ya kufika Ninawi akaniambia kuwa kuna mfanyabiashara amefariki na duka lake pamoja na bidhaa zake vinaweza kununuliwa kwa bei nafuu sana. Akaniambia tuwe washirika lakini kwanza inampasa kurudi Babiloni kuchukua pesa zake. Akanishawishi kununua biashara ile kwa pesa zangu na kuniambia pesa zake zitatumika kuongezea mtaji hapo baadaye.

'''Siku zilikwenda lakini hakurudi Babiloni kufuata pesa zake na mbaya zaidi alikuwa hajui biashara na ni mtu mwenye matumizi mabaya. Nilimfukuza kwenye biashara lakini tayari hali ya biashara ilikuwa mbaya sana. Bidhaa zilizobaki zilikuwa hazifai kuuzwa na sikuwa na pesa ya kununulia zingine. Niliamua kuuza ile biashara kwa muisraeli mmoja kwa bei ya hasara.

'''Baada ya hapo maisha yalikuwa magumu sana. Nilitafuta kazi lakini sikupata kwa sababu sikuwa na ujuzi wowote. Nililazimika kumuuza mtumwa wangu na baadhi ya nguo zangu ili nipate kula na sehemu ya kulala. Siku zilivyosonga ndivyo maisha yalivyozidi kuwa magumu.

'''Katika siku hizo ngumu nilikumbuka jinsi unavyiniamini. Ulinituma nikawe mtu wa maana na hilo ndilo nililopanga kutimiza.' Baada ya kusikia hayo mama yake alijiziba uso na kulia.
'''Muda huo ndipo nilipokumbuka kuhusu lile bamba ulilonipatia. Nikasoma maneno yake kwa umakini mkubwa, iwapo ningepata busara iliyokuwepo mule kabla ya kuanza kuwekeza basi nisingeweza kupoteza pesa zangu. Nilijifunza sheria zote na kuziweka akilini. Nikajiapisha kuwa iwapo Mungu wa bahati akinibariki tena nitaongozwa na busara iliyojengwa kwa miaka mingi badala ya kufanya mambo bila uzoefu kama ilivyo kawaida ya vijana.

'''Kwa faida ya nyote mliokusanyika hapa usiku wa leo, nitasoma hekima aliyonipa baba yangu kama ilivyoandikwa kwenye bamba alilonipa miaka kumi iliyopita.

Sheria tano za pesa

1. Pesa huja kwa wingi kwa yule ambaye huweka akiba moja ya kumi ya kipato chake. Na kuitumia kuwekeza kwa ajili ya wakati ujao.

2. Pesa hufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu iwapo itampata mtu anayeipatia kazi yenye faida. Hapo itaongezeka kama wanyama wa kufungwa.

3. Pesa hung'ang'ania kukaa kwa mtu mtu anayeilinda na mwenye tahadhari. Mtu anayeomba ushauri kutoka kwa watu wenye ujuzi na uzoefu wa kuitunza.

4. Pesa haikai na hupotea kwa mtu ambaye anawekeza kwenye biashara au mradi ambao haijui vizuri, au kwa mtu ambaye hapati ushauri kutoka kwa wale wenye uzoefu na ujuzi wa kuitunza.

5. Pesa haikai kwa mtu anayeiwekeza kwenye miradi inayodai kutoa faida kubwa kuliko kawaida, wala kwa wale wanaodanganywa na matapeli na watu wajanja wajanja na wale ambao wanawekeza bila kupata ushauri kutoka kwa wale wenye uzoefu, au wale wanaowekeza kwa sababu wanapenda tu miradi ya aina hiyo.

'''Hizi ndizo sheria tano za pesa kama zilivyoandikwa na baba yangu. Ninaweza kusema kuwa zina thamani kuliko pesa yenyewe, kama tu mtakavyoona kwenye kisa changu.
"Hapo Nomasir alimuangalia tena baba yake. 'Nimekusimulia jinsi kutokuwa na uzoefu kulivyonitumbukiza kwenye umaskini na taabu.
 
"Hiki hapa," aliendelea kusema Mathon huku akifungua kamba moja, 'Hii ni mali ya Nebaturi, mfanyabiashara ya ngamia. Kila atakapo kununua ngamia wengi kuliko pesa alizonazo huniletea kamba hii nami humkopesha kulingana na mahitaji yake. Ni mtu ninayemuamini sana. Ni mfanyabiashara mzuri na muaminifu hivyo hata bila dhamana mimi humkopesha. Ninawaamini wafanyabiashara wengi hapa Babiloni sababu ya uaminifu wao. Huweka mali zao kama dhamana na kuzikomboa mara tu wakamilishapo biashara. Wafanyabiashara wazuri ni hazina ya mji wetu na ni faida kwangu kuwasaidia kuendelea kufanya biashara na kuzidi kuneemesha mji wetu."

Mathon alichukua kito cha rangi ya ubluu na ukijani na kukitupa chini kwa dharau. "Mdudu kutoka Misri. Aliyekuwa anamiliki hiki hajali kabisa kunilipa. Nikimfuata kumdai anajibu, "nitakulipaje nami nimeandamwa na majanga kila leo? Hata hivyo wewe unapesa za kutosha! Unafikiri nitafanya nini?'

Dhamana ni ya baba yake. Baba yake si mtu tajiri lakini alijinyima na kuweka shamba na mifugo yake kama dhamana ili mwanae afanye biashara. Kijana wake alianza vizuri biashara zake na alikuwa akipata faida lakini akaingiwa na tamaa ya kutaka utajiri wa haraka. Kwa kuwa hakuwa na ujuzi mwingi, biashara yake ikafa.

"Vijana wana malengo makubwa sana. Mara zote wanatafuta njia ya mkato ya kuwa matajiri. Ili kupata utajiri haraka mara nyingi hukopa bila kufikiri.

Kwa kukosa kwao uzoefu hawatambui kuwa deni baya ni shimo refu ambalo unaweza kutumbukia kirahisi lakini ukahangaika kwa siku nyingi ili kutoka. Ni shimo la majuto na huzuni. Ni shimo ambalo jua la mchana huzibwa na mawingu na usiku hufanywa mchungu kwa usingizi wa mang'amung'amu.

Si kwamba nashauri watu wasikope, hapana! Nasisitiza watu wakope lakini iwe kwa jambo la maana. Mimi mwenyewe nilianza kufanya biashara kwa pesa za mkopo.

"Lakini mkopeshaji anapaswa kufanya nini kwa jambo kama la huyu kijana? Kijana mwenyewe amekata tamaa, hafanyi chochote wala hafanyi bidii yoyote kulipa deni. Moyo wangu unakuwa mzito kuchukua shamba na mifugo ya baba yake."

"Umeniambia habari nyingi na nimezifurahia ," alisema Rodan. "Lakini hujajibu swali langu iwapo nimkopeshe vipande vyangu hamsini vya dhahabu mume wa dada yangu? Kumbuka hawa ni ndugu zangu wa karibu sana.

"Dada yako ni mtu anayejitambua nami namheshimu kwa hilo. Lakini kama mume wake angekuja kwangu kuomba nimkopeshe vipande hamsini vya dhahabu lazima ningemuuliza anataka kufanyia nini?
"Kama akisema anataka kuwa mfanyabiashara kama mimi na kuuza vito na samani za gharama nitamuuliza. Unaujuzi gani kuhusiana na biashara? Unajua unakoweza kununua kwa bei rahisi ? Unajua unakoweza kuuza kwa bei nzuri?

Je, shemeji yako anafahamu vitu hivyo?

"Kwakweli hafahamu," akajibu Rodan. "Alikuwa msaidizi wangu kwenye kutengeneza mikuki na amewahi kuwa msaidizi wa dukani."

"Kama ni hivyo nitamwambia kuwa hajachagua kazi yake kwa busara. Mfanyabiashara anatakiwa kuwa na ujuzi wa kazi hiyo. Ana malengo mazuri lakini hayatimiziki, nisingeweza mkopesha pesa zangu.

"Tuseme angejibu kuwa, 'ninafahamu sababu nimekuwa msaidizi wa wafanyabiashara kwa muda mrefu. Ninajua jinsi ya kufika Smyrna na kununua mazuria yaliyoshonwa na wakinamama kwa bei ya chini. Pia nawajua matajiri wengi wa Babiloni ninaoweza kuwauzia kwa faida kubwa,' hapo ningemwambia kuwa 'lengo lako ni zuri na mpango wako unatekelezeka. Kwa hiyo ningekuwa tayari kumkopesha vipande hamsini vya dhahabu iwapo atakuwa na dhamana."

"Iwapo angesema 'sina dhamana yoyote lakini mimi ni muaminifu, nitalipa pesa yako vizuri,' ningemwambia; 'ninathamini kila kipande cha dhahabu nilichonacho. Inaweza tokea wanyang'anyi wakakupora pesa unapoenda Smyrna au kukupora mazuria unaporudi. Si unakuwa huna jinsi ya kunilipa na pesa yangu inakuwa imepotea?'
Mkuu tunashukuru sana hakika Mungu akubariki. Binafsi naomba uendelee na huduma hii hata kwa kutuwekea vitabu vingine zaidi ili tuendelee kupata madini ambayo hatukuyapata katika mfumo wetu wa elimu.
 
"Hiki hapa," aliendelea kusema Mathon huku akifungua kamba moja, 'Hii ni mali ya Nebaturi, mfanyabiashara ya ngamia. Kila atakapo kununua ngamia wengi kuliko pesa alizonazo huniletea kamba hii nami humkopesha kulingana na mahitaji yake. Ni mtu ninayemuamini sana. Ni mfanyabiashara mzuri na muaminifu hivyo hata bila dhamana mimi humkopesha. Ninawaamini wafanyabiashara wengi hapa Babiloni sababu ya uaminifu wao. Huweka mali zao kama dhamana na kuzikomboa mara tu wakamilishapo biashara. Wafanyabiashara wazuri ni hazina ya mji wetu na ni faida kwangu kuwasaidia kuendelea kufanya biashara na kuzidi kuneemesha mji wetu."

Mathon alichukua kito cha rangi ya ubluu na ukijani na kukitupa chini kwa dharau. "Mdudu kutoka Misri. Aliyekuwa anamiliki hiki hajali kabisa kunilipa. Nikimfuata kumdai anajibu, "nitakulipaje nami nimeandamwa na majanga kila leo? Hata hivyo wewe unapesa za kutosha! Unafikiri nitafanya nini?'

Dhamana ni ya baba yake. Baba yake si mtu tajiri lakini alijinyima na kuweka shamba na mifugo yake kama dhamana ili mwanae afanye biashara. Kijana wake alianza vizuri biashara zake na alikuwa akipata faida lakini akaingiwa na tamaa ya kutaka utajiri wa haraka. Kwa kuwa hakuwa na ujuzi mwingi, biashara yake ikafa.

"Vijana wana malengo makubwa sana. Mara zote wanatafuta njia ya mkato ya kuwa matajiri. Ili kupata utajiri haraka mara nyingi hukopa bila kufikiri.

Kwa kukosa kwao uzoefu hawatambui kuwa deni baya ni shimo refu ambalo unaweza kutumbukia kirahisi lakini ukahangaika kwa siku nyingi ili kutoka. Ni shimo la majuto na huzuni. Ni shimo ambalo jua la mchana huzibwa na mawingu na usiku hufanywa mchungu kwa usingizi wa mang'amung'amu.

Si kwamba nashauri watu wasikope, hapana! Nasisitiza watu wakope lakini iwe kwa jambo la maana. Mimi mwenyewe nilianza kufanya biashara kwa pesa za mkopo.

"Lakini mkopeshaji anapaswa kufanya nini kwa jambo kama la huyu kijana? Kijana mwenyewe amekata tamaa, hafanyi chochote wala hafanyi bidii yoyote kulipa deni. Moyo wangu unakuwa mzito kuchukua shamba na mifugo ya baba yake."

"Umeniambia habari nyingi na nimezifurahia ," alisema Rodan. "Lakini hujajibu swali langu iwapo nimkopeshe vipande vyangu hamsini vya dhahabu mume wa dada yangu? Kumbuka hawa ni ndugu zangu wa karibu sana.

"Dada yako ni mtu anayejitambua nami namheshimu kwa hilo. Lakini kama mume wake angekuja kwangu kuomba nimkopeshe vipande hamsini vya dhahabu lazima ningemuuliza anataka kufanyia nini?
"Kama akisema anataka kuwa mfanyabiashara kama mimi na kuuza vito na samani za gharama nitamuuliza. Unaujuzi gani kuhusiana na biashara? Unajua unakoweza kununua kwa bei rahisi ? Unajua unakoweza kuuza kwa bei nzuri?

Je, shemeji yako anafahamu vitu hivyo?

"Kwakweli hafahamu," akajibu Rodan. "Alikuwa msaidizi wangu kwenye kutengeneza mikuki na amewahi kuwa msaidizi wa dukani."

"Kama ni hivyo nitamwambia kuwa hajachagua kazi yake kwa busara. Mfanyabiashara anatakiwa kuwa na ujuzi wa kazi hiyo. Ana malengo mazuri lakini hayatimiziki, nisingeweza mkopesha pesa zangu.

"Tuseme angejibu kuwa, 'ninafahamu sababu nimekuwa msaidizi wa wafanyabiashara kwa muda mrefu. Ninajua jinsi ya kufika Smyrna na kununua mazuria yaliyoshonwa na wakinamama kwa bei ya chini. Pia nawajua matajiri wengi wa Babiloni ninaoweza kuwauzia kwa faida kubwa,' hapo ningemwambia kuwa 'lengo lako ni zuri na mpango wako unatekelezeka. Kwa hiyo ningekuwa tayari kumkopesha vipande hamsini vya dhahabu iwapo atakuwa na dhamana."

"Iwapo angesema 'sina dhamana yoyote lakini mimi ni muaminifu, nitalipa pesa yako vizuri,' ningemwambia; 'ninathamini kila kipande cha dhahabu nilichonacho. Inaweza tokea wanyang'anyi wakakupora pesa unapoenda Smyrna au kukupora mazuria unaporudi. Si unakuwa huna jinsi ya kunilipa na pesa yangu inakuwa imepotea?'
Asante Mtumishi wa Mungu!!
 
"Sikiliza Rodan, pesa ndiyo bidhaa ya mkopesha pesa. Ni rahisi kuikopesha lakini ukikopesha bila busara itakuwa vigumu sana kuirudisha. Mkopeshaji mwenye busara anahitaji kujihakikishia ulipwaji wa pesa yake.

'''Ni vizuri kuwasaidia wale walio kwenye matatizo, ni vizuri kuwasaidia wale wanaoanza ili baadaye waje kuwa watu wa maana. Lakini msaada unatakiwa kutolewa kwa hekima, isiwe kama yule punda wa mkulima, kumsaidia mtu na badala yake tuishie kubeba mzigo wake.

"Sasa bwana Rodan, kuhusiana na swali lako, hili ndilo jibu langu: baki na pesa zako, hakuna mtu atasema ana haki ya kupata sehemu ya pesa hiyo labda utake mwenyewe kumpa. Kama unataka kukopesha ili upate faida basi kopesha kwa tahadhari na kopesha watu wengi. Sipendi pesa ikae tu lakini hata zaidi, sipendi hatari ya kupoteza pesa.

"Umefanya kazi kama mtengeneza mikuki kwa miaka mingapi?"

"Miaka mitatu kamili,' alijibu Rodan.
"Mbali na zawadi uliyopewa na mfalme ni kiasi gani kingine umeweka kama akiba?"

"Vipande vitatu vya dhahabu."

"Kwahiyo kwa kila mwaka uliofanya kazi ulijinyima na kutunza kipande kimoja cha dhahabu?"

'''Inaonekana hivyo."

"Hivyo inamaana utahitaji kufanya kazi na kujinyima kwa miaka hamsini ili uweze kutunza vipande hamsini vya dhahabu. Kufanya kazi maisha yako yote."

"Fikiria hili, unaweza kumruhusu dada yako ahatarishe akiba yako uliyoifanyia kazi kwa miaka hamsini ukiungua kwenye tanuri la kuyeyusha shaba halafu mume wake aende kuitumia kujaribu kuwa mfanyabiashara?"

"Siwezi kwakweli." Alijibu Rodan kwa msisitizo.
"Basi nenda na kamwambie kuwa: 'Nimefanya kazi kwa miaka mitatu mfululizo isipokuwa siku za mfungo tu. Toka asubuhi hadi usiku nimefanya kazi, nimejinyima vitu vingi nilivyotamani ili niweze kutunza kipande kimoja cha dhahabu kwa mwaka. Wewe ni dada yangu mpendwa na ningependa mume wako aanze kufanya biashara na kufanikiwa. Sasa naomba uniletee mpango wake wa biashara yake ili rafiki yangu Mathon auchunguze kama ni mzuri na unatekelezeka. Kama upo sawa nitamkopesha akiba yangu ya mwaka mmoja na kumpa nafasi ya kuonyesha kama anaweza biashara.' Fanya hivyo na kama kweli ana nia ya kufanikiwa atafanikiwa. Hata akishindwa kiasi utakachokuwa umempatia ni kile ambacho anaweza kumudu kukulipa.

"Mimi nakopesha pesa kwasababu ninazo nyingi kuliko ninavyoweza kuzitumia katika biashara yangu. Nimeonelea pesa ya ziada ikafanyie kazi wengine na hivyo kuniletea faida. Sitaki kabisa kupoteza pesa yangu kwa sababu nimeifanyia kazi kwa bidii na nimejinyima vitu vingi kuipata. Siwezi kumkopesha mtu ambaye sina uhakika kama ni salama na itarudi. Pia sikopeshi watu ambao najua watachelewa kunilipa.

"Nimekuambia siri za sanduku langu la dhamana. Umejifunza udhaifu wa binadamu na tamaa ya kukopa huku wakijua hawana njia ya kulipia. Kutokana na hilo umeona jinsi watu wanavyokuwa na matumaini ya kuwekeza na kupata kipato kikubwa iwapo wakipata pesa lakini mara nyingi huwa ni matarajio hewa tu. Hii ni sababu wengi wao hawana uzoefu wala ujuzi wa kufikia malengo hayo.

"Wewe sasa una pesa, unatakiwa kuzifanyisha kazi ili zikuzalishie zaidi. Unaweza hata kuwa mkopesha pesa kama mimi.
Ukitumia pesa yako vizuri itakuzalishia na kukufanya uishi maisha ya furaha na kuridhika siku zako zote. Lakini ukiiacha ipotee itakuwa ni chanzo cha uchungu na majuto maisha yako yote.
"Kitu gani unatamani kuhusiana na dhahabu yako?"

"Natamani kuitunza isipotee," akajibu Rodan.

"Umejibu vyema," akasema Mathon. "Jambo la kwanza ni usalama wa pesa yako. Fikiria ikiwa mikononi mwa shemeji yako, itakuwa salama kama unavyotaka?"
"Nadhani haiwezi maana shemeji yangu si mwenye hekima katika utunzaji wa pesa."

"Basi usiyumbishwe na huruma za kijinga kuwa una wajibu wa kuwasaidia wengine na hivyo ukagawa hazina yako. Kama unataka kuwasaidia jamaa zako au watu wa ukoo wako tafuta njia nyingine lakini si kuhatarisha hazina yako. Kumbuka kuwa pesa hupotea kwa njia isiyotegemewa kutoka kwa wale wasio na uzoefu wa kuitunza. Ni bora kupoteza pesa kwenye anasa na starehe kuliko kuwapa wengine waipoteze.
"Baada ya kuhakikisha usalama wa pesa zako, nini kinafuata?"

"Kuifanya izalishe," akajibu Rodan.

"Umejibu vyema pia. Inatakiwa izalishe na kukua. Pesa ikikopeshwa kwa hekima inaweza kukua na kuwa mara mbili hata kabla ya kuwa mzee. Ukiiweka katika hatari ya kupotea unakuwa unahatarisha si tu pesa hiyo bali hata kile ambacho ingezalisha.

"Kwa hiyo Rodan, Usidanganywe na mipango kabambe isiyotimizika inayotolewa na watu ambao wanafikiri wana ujuzi wa kuifanya pesa izalishe kiasi kikubwa sana. Hiyo ni mipango ya waota ndoto ambao hawajui kanuni za biashara. Usitarajie kupata faida kubwa kuliko kawaida. Kukopesha au kuwekeza kwa matarajio makubwa kupita kiasi ni kukaribisha hasara.

Kuwapa watu pesa yako na kutegemea faida kubwa kupita kawaida ni kukaribisha hasara.
"Shirikiana na watu wenye uzoefu na waliofanikiwa. Acha pesa yako ilindwe na hekima na uzoefu wao. Pia wekeza kwenye miradi iliyojithibitisha kuwa ina faida.

"Kwa mtindo huo utaepuka hasara ambazo huwapata vijana wengi wapatapo pesa."

Rodan alipoanza kumshukuru kwa ushauri wake, Mathon hakusikiliza bali aliendelea kusema

"Zawadi uliyopewa na mfalme inatakiwa kukufundisha hekima. Ukitaka kubaki na vipande vyako hamsini vya dhahabu, unatakiwa kuwa makini. Utavutiwa na vitu vingi na utapata ushauri mwingi sana. Utaambiwa fursa nyingi zinazodaiwa kutoa faida kubwa. Habari na hadithi kutoka kwenye sanduku langu la dhamana zinatakiwa kuwa onyo kwako. Kabla hujaruhusu pesa yako kutoka kwenye pochi hakikisha utaweza kuirudisha. Kama utahitaji ushauri zaidi unaweza kurudi nami nitafurahi kukupatia.

'''Mwisho naomba usome nilichoandika. Chini ya mfuniko wa sanduku la dhamana. Maneno haya yana faida kwa mkopeshaji na mkopaji pia.


Bora tahadhari kidogo kuliko majuto makubwa.

Mwisho wa sura ya sita.
 
KUTA ZA BABILONI


Mzee Banzar, shujaa mkongwe na shupavu wa enzi zake. Alikuwa amesimama akilinda njia ya kuelekea sehemu ya juu ya ukuta wa Babiloni. Huko juu, wanajeshi shupavu walikuwa wakipambana kulinda ukuta. Wakati ujao wa jiji hili kubwa na ule wa malaki ya wakazi wake ulikuwa mikononi mwao.

Nje ya ukuta, kelele za majeshi ya wavamizi zilisikika, kelele za watu wengi sana. Vishindo vya maelfu ya farasi na kelele zenye kutia uziwi za magogo ya kubomolea milango zilisikika zikipiga milango ya shaba.

Ndani ya milango walisimama wanajeshi waliotumia mikuki, walijiandaa kulinda lango iwapo milango ingebomolewa. Walikuwa ni wachache tu. Jeshi kubwa la Babiloni lilikuwa pamoja na mfalme wao, sehemu za mbali huko mashariki likipigana vita dhidi ya waelami. Hawakutarajia jiji lao kuvamiwa kipindi hiki hivyo waliacha kikosi kidogo kulinda jiji. Ghafla, jeshi kubwa la waashuru lilishuka kutoka kaskazini. Kuta za jiji zilitakiwa kusimama au sivyo jiji la Babiloni lingeangamizwa.

Pembeni ya Banzar kulikuwa na umati mkubwa wa raia. Walikuwa na nyuso zilizopauka na zenye kujawa na uoga. Kwa shauku walikuwa wakiuliza habari za mwenendo wa vita.
Walikuwa kimya kwa mshangao huku wakiangalia msururu wa majeruhi na maiti wakitolewa njiani. Siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya pambano. Baada ya kuzingira jiji kwa siku tatu, ghafla adui akawa ameelekeza nguvu zake zote kwenye hili eneo na kwenye lango hili.

Walinzi waliokuwa juu ya ukuta Walipambana na maadui waliokuwa kwenye minara ya kupandia kuta na wale waliopanda kwa ngazi. Walitumia mishale, mafuta yanayowaka na mikuki kwa wale maadui waliofika juu ya ukuta. Maelfu ya adui walirusha mishale mingi sana dhidi ya walinzi hao.

Banzar alikuwa amekaa eneo ambalo alikuwa ni wa kwanza kupata habari kuhusu vita inayoendelea.

Mfanyabiashara mmoja mzee alimkaribia huku akitetemeka. "Niambie! Niambie!" Alimsihi Banzar,"hawataweza kuingia. Wana wangu wako pamoja na mfalme. Hakuna wa kumlinda mke wangu mzee. Mali zangu watapora zote. Chakula changu pia, hawatatuacha na kitu chochote. Sisi ni wazee, hatuwezi kujilinda wala kuwa watumwa. Tutapatwa na njaa na kufa. Niambie kuwa hawataweza kuingia."

"Tulia ndugu yangu," akajibu Banzar. "Kuta za Babiloni ni imara. Nenda sokoni na mwambie mke wako kuwa kuta zitamlinda na mali zenu zipo salama kama inavyolindwa hazina ya mfalme. Tembea pembeni ya kuta ili mishale inayorushwa isije kukupata."

Mwanamke mmoja akiwa amebeba mtoto akamfuata baada ya yule mzee kuondoka.
"Sajenti, kuna habari gani toka huko juu ya ukuta? Niambie ukweli ili nikamwambie mume wangu. Yuko kitandani kwa homa iliyotokana na majeraha lakini anasisitiza kuvaa mavazi ya vita na kubeba mkuki ili anilinde, mimi ni mjamzito. Anasema maadui wakifanikiwa kuingia watalipa kisasi kwa ukatili wa kutisha."

"Uwe na amani moyoni mama. Kuta za Babiloni zitakulinda wewe na wanao. Ni ndefu na imara. Husikii kelele za mashujaa wetu wanapokuwa wanamimina mafuta yanayowaka juu ya adui wanaopanda kuta kwa ngazi?"

"Nasikio hilo lakini pia nasikia sauti ya gogo likipiga lango la jiji."

"Nenda kwa mumeo, mwambie milango ni imara na haitaweza kuvunjwa. Hata hao maadui wanaopanda ukutani hukutana na mikuki ikiwasubiri. Nenda kwa uangalifu. Na tembea pembeni ya majengo."

Banzar alisogea pembeni ili kuruhusu kikosi cha jeshi kilichokuwa na silaha nzito kupita. Walipokuwa wakipita binti mmoja mdogo alimvuta mkanda na kusema.
"Askari naomba uniambie, tupo salama?" Aliuliza. "Nimesikia sauti za kuogopesha na naona watu wakivuja damu. Ninaogopa sana. Nini kitaipata familia yangu, mama yangu na wadogo zangu?"

Banzar akainama na kumsogelea yule ntoto.

"Usiogope mtoto mzuri,"
alimhakikishia. "Kuta za Babiloni zitakulinda wewe na, mama yako na wadogo zako. Malkia Semiramisi alizijenga hizi kuta miaka mia moja iliyopita kwa ajili ya usalama wa watu kama wewe. Hakuna aliyewahi kuzipenya. Nenda na mwambie mama na wadogo zako kuwa kuta za Babeli zitamlinda na hawana sababu za kuwa na wasiwasi."

Siku baada ya siku, Banzar alisimama kwenye kituo chake akisalimia vikosi vikipanda juu ukutani. Walishuka walipokuwa wamejuruhiwa au wamekufa tu. Banzar alikuwa amezungukwa na raia wengi waliokuwa wamejawa na woga huku wakitaka kujua iwapo kuta zitahimili.
Kwa heshima aliwajibu wote kuwa,
"Kuta za Babiloni zitawalinda."
 
Kwa wiki tatu na siku tano mashambulizi yaliendelea bila kukoma. Sehemu aliyokuwa amekaa Banzar iligeuka matope kutokana na damu na wanajeshi kupita walipokuwa wanaenda juu ya ukuta au walipokuwa wanajikokota kushuka. Kila siku maiti za wavamizi zilijazana nje ya ukuta. Usiku, wenzao walizitoa na kwenda kuzizika. Kwenye siku ya tano ya wiki ya nne vita iliendelea usiku kucha bila kukoma. Kulipopambazuka vumbi lililotimuliwa na adui aliyekuwa anaondoka lilionekana.

Walinzi wa kuta za jiji walipiga kelele kwa shangwe. Wanajeshi waliokuwa ndani nao wakapiga kelele, na raia vilevile. Jiji zima likashangilia.

Watu walitoka majumbani mwao na mitaa ikajaa umati wa watu. Wasiwasi uliowajaa kwa wiki kadhaa ukageuka nyimbo za furaha. Kutoka kwenye mnara wa hekalu la Beli moto wa ushindi uliwashwa. Moshi ulipanda juu kupeleka taarifa hadi sehemu za mbali.

Kwa mara nyingine kuta za Babiloni zilikuwa zimemzuia adui mwenye nguvu. Adui aliyepanga kupora hazina yake, kutesa na kufanya watu wake kuwa watumwa.

Jiji la Babaliloni lilidumu karne na karne kwa sababu lilikuwa na ulinzi thabiti. Gharama ya kutojilinda ilikuwa ni kubwa sana kwake.

Kuta za Babiloni zilikuwa ni mfano bora juu ya tamaa ya mwanadamu ya kujilinda. Hii ni tamaa ya asili ya mwanadamu. Tamaa ina nguvu leo kama ilivyokuwa enzi za kale. Tofauti ni kuwa leo tuna njia bora za kuitimiza.

Leo tuna kuta zisizopenywa za bima, akaunti za akiba na miradi mingi salama tunayoweza kuwekeza. Leo tunaweza kujilinda dhidi ya majanga yasiyotarajiwa, yanayoweza kuingia katika nyumba zetu na kuweka makazi.

Gharama ya kutokuwa na ulinzi wa kutosha ni kubwa sana.

Mwisho wa sura ya saba.
 
Back
Top Bottom