Sitokaa nimsahau yule kenge, picha linaanza namwambia zima taa akanyoosha mguu tena umbali mrefu tu, nikastuka sana nikamwambia hebu washa tena akagoma! ulabu wote ulikata! Baada ya hapo nilianzisha vurumai ili nipate sababu ya kusepa, nikafanikiwa, niliumwa wiki nzima, ikawa kila nikienda mahali ananitokea, muda mwingine kama mhudumu wa bar, nesi nk..nilimtafuta nikampa black n white, akakiri kwamba alinipenda mno na nilimkwaza sababu tu nilimuahidi game[emoji23] , wakati naongea nae ilikua MRC Mikocheni, nyuma ya Shoppers, nikamwambia we nipotezee tu, asee from nowhere, waliibuka paka watatu chini ya miguu yangu, nilichukia ile nataka kunyanyuka ilipiga radi moja hatari na alikuwa amekasirika mm kumpiga chini, baadae nikawa na chat nae tu kama rafiki nikamwambia kwanini ushirikina wako usiutumie kutafuta hela? Akanambia ni kweli lakini nikitaka hela ni mpaka niwe nae kwenye mahusiano, alikua ana duka kariakoo, mshenzi sana, nikienda viwanja sijui Juliana , tripple 7 ,bulls park au fosters nikiagiza kinywaji ghafla namuona amekaa kwa mbali, nikiwa sina hela muamala huo na msg juu kwamba "najua huna hela" yani kila nikiwa na shida na pesa nikiwaza bila hata kumwambia mtu ghafla muamala unasoma, sasa sijui ni mchawi au jini yule ng'ombe, Dar isikie hivi hivi, yakikukuta utakaa kwa discipline!
Sent from my CPH2179 using
JamiiForums mobile app