Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Tabata to Manzese, hizi ruti nimefanya sasa nilipokuwa nasoma shule ya msingi zile siku za weekend nikipewa nauli sipandi daladala. Ila kubwa kuliko nilitoka Kiwanda cha Cement cha Wazo kule Tegeta hadi Mwenge nikiwa na miaka 12 tu. Ilikuwaje... Nilikuwa naishi Tabata nasoma Manzese na enzi hizo daladala zinatoka Buguruni zinapitia Tabata zinaishia Ubungo halafu napanda la Ubungo kwenda Kariakoo nashukia Manzese. Hivyo natakiwa kupanda Mabasi mawili, ile usumbufu wa makonda kuwakataa wanafunzi na kubadilisha magari muda unakwenda ikawa nikipata gari la lift napanda kuepuka huo usumbufu. Nikajenga mazoea, siku hiyo likaja basi la kiwanda cha Cement cha wazo nikapanda, kumbe lile gari likichukua wafanyakazi halisimani ni moja kwa moja hadi kiwandani. Nashangaa kufika Ubungo basi limeshika njia ya kwenda Mwenge na kwa utoto wangu sikuwa na ujasiri wa kuuliza gari inakwenda wapi au lisimame wanishushe. Aisee moja kwa moja hadi Kiwandani. Nashangaa watu wanashuka na kutawanyika na mimi sikuwa na jinsi nikashuka. Bahati nzuri basi ilisimama nje ya geti la kuingia kiwandani. Nikafuata barabara ya basi ilipotoka hadi Tegeta, nilikuwa sipajui kabisa Tegeta na nikawa na hofu nisipange gari nyingine nisije kupotea tena. Nikatembea kwa Miguu hadi Mwenge nikasikia wanatangaza magari ya Kariakoo nikapanda hadi Kariakoo kisha nikapanda basi la kwenda ubungo nikarudi nyumbani Tabata. Siku nzima nilimaliza na ilikuwa ni kipindi cha mitihani ya kufunga muhula. Sikusema nyumbani niliogopa ila shuleni nilidanganya nimefiwa wakanipa mitihani ya siku nisiokuja nikafanya peke yangu. SITOSAHAU!!!
Hahaha jomba[emoji23][emoji23]
 
[emoji3][emoji3][emoji3]taifa mpaka chanika

Kuna mwanangu mmoja baba yake alitupeleka kuangalia game ya Simba na yañga na tiketi akalipa Sasa yanga alivopigwa tu yule mzee alitukacha afu mfukoni Nina mia Saba ikabidi tule kashata za mia sita na maji ya kandoro ya hamsini hamsini kipindi hicho. Kisha tuanze kugonga one two
Aiseee.
Nawe umetisha
 
Humu sijaona ruti ndefu ya mtu hata moja, mimi nilikuwa natoka kibamba mpaka kibada na ni kila siku, nilikuwa natembea bila kujua kuwa ni mbali mpaka pale nilipozoea jiji zima nazunguka kwa miguu tu, sikuwahi kupanda daladala mpaka narudi kijijini kwetu Magera, Morogoro.
Ulimaliza pea ngapi za viatu kwa mwezi/mwaka?
 
road to road mzee mpaka tandika, hapo nikapata shortcut moja nikatokea stendi ya shamba mbele ya mtongani kidogo, baada ya hapo ni kunyooka mpaka mbagala.

safari ilianza saa 12 jioni nikafika saa 6 usiku nilikuwa napumzika pumzika njiani umo
Kipande cha Vetinari, Tandika Majaribio, Tandika kaburi moja, Kizinga mpaka msikitini hukupata bahati ya kukabwa?
Maana muda huo na maeneo hayo ni "Tuwa tugawe"
 
Ni kipaji alichonijalia Mungu mbali na mazoezi ninayofanyaga, ingawa sometimes nakimbiaga kwa zaidi ya dakika 70-75 lakini zoezi la kutembea huwa naenjoy sana.

NB:

Huwa naamka saa 8 au saa 9 usiku kutembea umbali namna hiyo.

Nilitokea Pugu, nikanyooka hadi Njiapanda Segerea, Kinyerezi hadi Magufuli Stand Mbezi mwisho na kugeuka.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Kwenye njia unazopita muda huo hali ya usalama inakuwaje ?
 
Mwaka 2018 kila jtano saa 12:00 asbh natoka pugu shule ya msingi hadi kivukoni. Kurud nilikuwa narud na bus. Nilijiwekea utaratibu huo kwa miezi 6
 
2015 Lowasa
Buguruni hadi Biafra kupitia Posta
 
Kawe adi mnazi mmoja Via Old bagamoyo road, Ali Hassan Mwinyi Rd na Bibi titi
 
Back
Top Bottom