Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Yaani wewe ndio umemaliza katika wote,ujue kutembea umbali flani kuna sababu tofauti na inategemea na hali ya kiuchumi kwa wakati husika mfano huyu mtu aliyeuliza je sisi machinga tunaruhusiwa kuchangia? Kiukweli hawa jamaa wanatembea sana na kwa ukaazi wangu nishawashuhudia wamachinga ambao wanauza bidhaa maeneo ya mbali sana mfano kuna mmoja alikuwa namkuta sana maeneo ya tmk sasa siku hyo nikamkuta maeneo ya Bonyokwa tena kabeba yale majiko ya mkaa yale yenye udongo ndani,ebu fikiria lilivyo zito tena na pima tmk to bonyokwa na hapo anapita kuelekea kimara!
Binafsi nimefanya uchinga...acha mze nilikuwa napiga route hizoo ni balaa jioni nikirudi gheto nanunua barafu naweka kwenye maji miguu ili ipoe
 
Mchakato wa kupata hati ya kusafiria ulinifanya nitembee kwa mguu kutoka Kurasini hadi Mlimani City mchana wa juakali.

Ilikua hivi:-
Tangu wakati niko chuo nilihangaikia sana suala la kuwa na passport ili niweze ku "access fursa za dunia." (Najichukulia kama mwananchi wa dunia, na sio mwananchi wa kipande kidogo cha dunia kiitwacho Tanzania pekee)

Kwangu mimi, kutokua na passport ilikua ni kama kifungo (nilijifananisha na mbuzi aliyefungwa kamba shingoni na kamba hiyo kufungwa kwenye mti). Hivyo kuwa na passport ingekua kama kuikata ile kamba na kuweza "kula majani" popote pale ambapo ningeweza kufika. A passport, was that important to me.

Kulingana na vigezo vya kuipata nyaraka hiyo ya kusafiria kuwa vingi, basi nilikumbana na "nenda rudi" nyingi sana hadi namaliza chuo sikufanikiwa kabisa kuipata hati hiyo.
Michakato hiyo (nenda rudi zisizozaa matunda) ilipelekea kupoteza pesa, kupoteza matumaini na furaha yangu.

Baada ya kupita kama mwaka mmoja na nusu hivi, kwa mbinde sana nilitimiza vigezo vya kuomba passport (japokua nilikua sina uhakika navyo sana kama "vitanivusha") na kwa mbinde zaidi nikapata pesa ya kugharamia mchakato huo.

Siku hiyo nimeenda pale uhamiaji makao makuu Kurasini, baada ya foleni kubwa, hatimaye nilifanikiwa kuhudumiwa majira ya saa saba mchana.
Nyaraka zangu zilipokelewa, zikakaguliwa, nikaambiwa nilipie, nikachukuliwa maelezo, nikapigwa picha na kuchukuliwa alama zangu za vidole na hatimaye nikaambiwa hati yangu itakua tayari baada ya siku 14.

Wakuu sikuamini, nilipata WEPESI WA AJABU. Yaani mwili ulikua soft, light and energetic. Namtabasamia kila mtu aliye mbele yangu.

Nikaanza tu kutembea, a joyful walk, napita tu vituo vya daladala sina habari, yaani nilikua ni kama kichaa mpya mjini. Juakali la saa saba kuelekea saa nane, saa tisa linaniwakia sina habari mimi.

Nilienda kusimama Mlimani City, Samaki Samaki kwa kaka mkubwa Carlito nilipoagiza Pepsi bariiiiiidi inayoambatana na glasi zenye mabarafu na vipande vya malimao.

Moral of the strory;-
Kufanikisha jambo (lolote lile) mara baada ya kulipambania kwa muda mrafu, kunaambatana na RAHA FULANI ambayo haielezeki.

Asanteni.

Pia aione Mwifwa
Sasa hv upo nchi gani??

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Kariakoo -Kawe, ilikuwaje ungana na mimi 2015 kuelekea 2016 sina ili wala lile hapo kula kulala kwa baba na mama,

Siku 1 nilikuwa na ahadi ya kumeet na demu wangu yeye anatoka pale kurasini ufundi kota enzi hyo anasoma marian girl alafu ni mwezi wa 6 likizo ndefu

Basi baba ako nikapanda gari fresh tu hadi kariakoo tukameet tukafanya mizunguko yetu pale balaa likaanza baby mm nataka tukapumzke sehemu nmechoka uzuri demu wangu hakuwa na Tamaa

Ila mm sasa Mr.misifa nikataka nimpeleke KFC pale kituo cha zamani bakhresa karbu na salama bearing opposite na sheli ya puma

Mfukoni nina 7K tu na pale ile portion ya kuku na chips ni 5K soda yao 1K jumla ni 6K nikabaki na 1K sasa uwezi kuwa na demu yeye ale ww usile lazma angalau ninywe chochote na nikajitusu kunywa soda ya buku weeh nikabaki empty

Tukaboll paleee kwa muda mm nawaza tuuu hapo narudi vp home kawe siwez kuomba nauli
Basi baada ya muda tukaagana yeye anarud kurasini ufundi mm kawe kilichotokea ni huu uzi hapa kwa sasa yule binti yupo IFM mwaka wa pili ni mjaluo anaitwa patricia ana akili balaaaa na mm ndo nilimvunja bikr***** pale Marian girls bagamoyo aligonga dvs 1 ya 9.

Sent from my iPhone 15 pro max.
 
Nakumbuka siku moja nikiwa Msasani alitokea kijana mmoja akaniomba nimtembeze kwenye mtumbwi.

Ila kwa bahati nzuri kukawa na boti linaenda Kigamboni siku hiyo, basi bhana nikamuunganisha akaniambia tuende wote mpaka taifa tukaangalie na Mpira kati ya Yanga na Mbeya city.

Alifurahi sana tulipofika Kigamboni tukapanda panton tukavuka posts tukaenda kupanda magari ya rangi tatu, basi bhana tulipofika akaenda kukata ticket kwenye gari akakata ya kwake tu akaniambia nimsubiri, anaenda kutoa hela kwenye simu, nikamuamini poa tu japo nilishashtuka ila nikawa najipa moyo.

Mpaka Mpira unaanza hakutokda ila bidi nianze kupiga ado ado na mguu mpaka msasani.
Coco beach - Mtoni Mtongani
 
Kariakoo -Kawe, ilikuwaje ungana na mimi 2015 kuelekea 2016 sina ili wala lile hapo kula kulala kwa baba na mama,

Siku 1 nilikuwa na ahadi ya kumeet na demu wangu yeye anatoka pale kurasini ufundi kota enzi hyo anasoma marian girl alafu ni mwezi wa 6 likizo ndefu

Basi baba ako nikapanda gari fresh tu hadi kariakoo tukameet tukafanya mizunguko yetu pale balaa likaanza baby mm nataka tukapumzke sehemu nmechoka uzuri demu wangu hakuwa na Tamaa

Ila mm sasa Mr.misifa nikataka nimpeleke KFC pale kituo cha zamani bakhresa karbu na salama bearing opposite na sheli ya puma

Mfukoni nina 7K tu na pale ile portion ya kuku na chips ni 5K soda yao 1K jumla ni 6K nikabaki na 1K sasa uwezi kuwa na demu yeye ale ww usile lazma angalau ninywe chochote na nikajitusu kunywa soda ya buku weeh nikabaki empty

Tukaboll paleee kwa muda mm nawaza tuuu hapo narudi vp home kawe siwez kuomba nauli
Basi baada ya muda tukaagana yeye anarud kurasini ufundi mm kawe kilichotokea ni huu uzi hapa kwa sasa yule binti yupo IFM mwaka wa pili ni mjaluo anaitwa patricia ana akili balaaaa na mm ndo nilimvunja bikr***** pale Marian girls bagamoyo aligonga dvs 1 ya 9.

Sent from my iPhone 15 pro max.
Dogo umefungua codes zote, jinga kabisa
 
Moro to Dom, kisha Rumonge to Bujumbura! Ngoja niishie hapa, safari ilikuwa kupata hati flani ya Ukimbizi watu wakajichanganye mbele mbele huko, nakumbuka nafasi zikatoka za Australia, Canada na Libya ( kipindi cha Gaddafi ) nikapangiwa Libya, Sikwenda.
 
Nakumbuka siku moja nikiwa Msasani alitokea kijana mmoja akaniomba nimtembeze kwenye mtumbwi.

Ila kwa bahati nzuri kukawa na boti linaenda Kigamboni siku hiyo, basi bhana nikamuunganisha akaniambia tuende wote mpaka taifa tukaangalie na Mpira kati ya Yanga na Mbeya city.

Alifurahi sana tulipofika Kigamboni tukapanda panton tukavuka posts tukaenda kupanda magari ya rangi tatu, basi bhana tulipofika akaenda kukata ticket kwenye gari akakata ya kwake tu akaniambia nimsubiri, anaenda kutoa hela kwenye simu, nikamuamini poa tu japo nilishashtuka ila nikawa najipa moyo.

Mpaka Mpira unaanza hakutokda ila bidi nianze kupiga ado ado na mguu mpaka msasani.
Bure ilikuponza. Kuna mwamba aliweka rekodi zake hapa za kukata mwendo kwa miguu
 
Nimewahi kutembea kwa miguu kutoka keko hadi kinondoni biafra na kurudi tena keko juu, pia kutoka makumbusho hadi ubungo kwenda na kurudi. Pia kutoka makumbusho hadi kivukoni kwenda na kurudi kupitia barabara ya bagamoyo/ally hasan mwinyi. Ruti nyingine ni makumbusho to kawe, makubusho to bunju bila kusahau ruti zingine za masafa ya kati na mafupi jijini dar. Jiji la dara nililiona kama kijiji fulani cha kwetu kwa kulitembea kwa miguu ndani ya miaka mitano nikawa nimelijua lote hadi vichochoro vya ushuani na uswahilini. Pale magogoni ilipo ikulu ya nchi nilikatiza sana kutalii kuzunguka nyumba hiyo yenye utukufu wa nchi kabla ya kuwa na ulinzi wa kutisha miaka hii sithubutu kukatiza maeneo hayo
 
Moro to Dom, kisha Rumonge to Bujumbura! Ngoja niishie hapa, safari ilikuwa kupata hati flani ya Ukimbizi watu wakajichanganye mbele mbele huko, nakumbuka nafasi zikatoka za Australia, Canada na Libya ( kipindi cha Gaddafi ) nikapangiwa Libya, Sikwenda.
Maeneo uliyoyataja yote yapo ndani ya Dar?
Duuuh! au unanena Kwa lugha mi ndo sikuelewi,waumini wengine ndo wanakuelewa?
Psych is real.
 
Mwananyamala A hadi bunju B nilitembea kuanzia saa9 alasiri hadi nafika bunju saa2 usiku
 
Back
Top Bottom