Ummy Mwalimu: Ruksa Madaktari kutumia hospitali za Serikali kama private clinic baada ya muda wa kazi

Ummy Mwalimu: Ruksa Madaktari kutumia hospitali za Serikali kama private clinic baada ya muda wa kazi

Yaani watumie rasilimali za umma kwa matumizi yao binafsi duh
Amekwambia watalipia kama wanavyofanya sasa hili wala sio kitu kipya. sio kila jambo kipinga tu haya mambo yanafanyika toka zamani. Namuona Dr baada ya kazi clinic yake anakupata appointment labda kufanya upasuaji anakuelekeza Hosp ya kwenda kwa maana private Hosp anakuja huyo Dr anafanya service zake wewe unamlipa kama yeye na unalipa gharama za Hosp. wakati mwingine inakuwa lump sum yeye Dr anakuwa na maelewano na hiyo Hosp kuhusu charges. Hakuna jipya katika hili.
 
Safi sana, ikiwezekana tutafute hata madaktari kutoka Dubei waje kuendesha suala zima la matibabu nchini😄
Acheni gubu nyinyi, mbona wakija ma Dr bingwa kutoka nchi za nje kama India tunawapokea kwa mikono miwlili hatusemei hatutaki wageni. Kila jambo nongwa tu hata kama unaichukia serikali sio kila jambo mengine hata kama hutaki kusifia nyamaza tu.
 
Au kama vipi, Kila mtumishi atumie ofisi ya serikali kujiongezea kipato baada ya muda wa kazi uliopangwa kuisha...😊
Ndio huku tunako elekea na tumefika, Mashuleni nako, waalimu nao! wana lao jambo
 
View attachment 2684415
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametoa ruhusa rasmi kwa Madaktari nchini walioajiriwa na serikali kufanya kazi Binafsi kwenye Hospitali za serikali baada ya muda wa kazi kuisha.

Waziri Ummy ametangaza uhamuzi huo leo Mkoani Simiyu, wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Simiyu katika ziara yake Mkoani humo.

Waziri Ummy amesema

"Tusiweke urasimu Daktari huyu baada ya saa kumi mruhusu afanye shughuli zake za Private hapa, atawaona mnakubaliana parcentage, Ocean Road nilifanya hivyo. Turuhusu hapa ni kuweka utaratibu tu, kuna Mgonjwa anataka aje wakati hakuna fujo.

Hata mimi kuna watu hawapendi kwenda hospitali za Serikali, mchukulie kama RC yupo busy aanze kupanga mafoleni, anataka akienda sehemu nimekuta chumba maalumu kimetengwa, kina makochi, kuna maji, kuna chai, kuna kahawa, kuna soda.

Daktari atamuita Muuguzi, Daktari atanisikiliza, Muuguzi atanichukua sampuli zangu kama nimeondoka ni kufanyiwa radiology tu lakini vitu vingine nitafanyiwa hapohapo."

Wataalamu wa Afya waonywa kupunguza Semina

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu Ummy Mwalimu amewataka Wataalamu wa Afya nchini kupunguza semina ili kuwa na muda zaidi wa kutoa huduma bora za matibabu kwa Wananchi.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo Julai 10, 2023 katika ziara yake Mkoani Simiyu wakati akiogea na Viongozi wa Mkoa huo chini ya Mkuu wa Mkoa Dkt. Yahaya Nawanda.

“Wataalamu wa Afya punguzeni semina maana mmekuwa na semina nyingi hadi kupelekea Wagonjwa kukosa huduma kwa wakati na kumekuwa na msomgamano mkubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya sababu ya semina”

Waziri Ummy pia amesema katika utolewaji wa huduma za afya nchini hakuna kilichosimama kwakuwa Serikali imejenga majengo ya Hospitali, imetoa dawa na vifaa tiba, hivyo ni jukumu la Wataalamu wa Afya ni kutoa huduma bora patika vituo hivyo.

“Tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia kila kitu katika Sekta ya Afya ikiwemo majengo, vifaa tiba, kuajiri Wataalamu na sasa ni jukumu letu Wataalau kutoa huduma bora kwa Wananchi kwani ndio dhamira ya Serikali”
Hapo mama yangu "umechemka"; tena umechemsha haswaa! Hospitali za Serikali zinakwenda kuharibika sasa. Kwa hiyo watumie vifaa na madawa ya Serikali kujinufaisha, Siyo?
Kumbukeni, madaktari wetu wamesomeshwa, wameajiriwa na wanalipwa na wananchi. Ni wajibu wao kuwatumikia wananchi usiku na mchana. Magonjwa hayana muda maalum. Tuige mfumo uendeshaji wa Sekta ya afya Botswana. Madaktari wa Nchi hii wanaogopwa na kusujudiwa kupita kiasi kwamba baadhi yao ni kama miungu watu wanafanyakazi wanavyotaka. Hapana.
 
Hapo mama yangu "umechemka"; tena umechemsha haswaa! Hospitali za Serikali zinakwenda kuharibika sasa. Kwa hiyo watumie vifaa na madawa ya Serikali kujinufaisha, Siyo?
Kumbukeni, madaktari wetu wamesomeshwa, wameajiriwa na wanalipwa na wananchi. Ni wajibu wao kuwatumikia wananchi usiku na mchana. Magonjwa hayana muda maalum. Tuige mfumo uendeshaji wa Sekta ya afya Botswana. Madaktari wa Nchi hii wanaogopwa na kusujudiwa kupita kiasi kwamba baadhi yao ni kama miungu watu wanafanyakazi wanavyotaka. Hapana.
Kwanza huyo Dokta kwenye hizo ‘after hours’ services, patients info anahifadhi wapi for medical history purposes; ni sawa na kufungua hospitali bubu na kuhatarisha maisha ya watu.

Only Ummy Mwalimu anaweza kuja na ubunifu kama huo.
 
"Mgonjwa nakuomba uje kwa ajili ya huduma za binafsi jioni-Daktari
"Kaka we njoo jioni nitakuwa natoa huduma binafsi nitakuwa na muda mzuri"

Tutegemee kauli kama hizi[emoji3]

Kama ambavyo shule zinawabakiza wanafunzi likizo ndivyo wagonjwa nao wanaenda kubakizwa kwa ajili ya huduma binafsi

Hii ndio Tanganyika,sijui inaongozwa na mtu au ipo autopilot
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hata walimu wanafundisha tuition tu shuleni. Sio kila kitu kipinga haya mambo hata hivi sasa yapo unaenda Hospital unataka fast track unalipia unataka kusubiri yapo tu, tusifanye mambo magumu na kuingiza ushabiki wa kisiasa kwa kila jambo.
Bora iwe sio halali, watu wafanye kwa kuibia, kuliko kuwapa uhuru sasa unawajua wabongoo vizuri lakini??
 
Bora iwe sio halali, watu wafanye kwa kuibia, kuliko kuwapa uhuru sasa unawajua wabongoo vizuri lakini??
Walikuwa hawafanyi kwa kuibia haya mambo yalikuwa wazi na kihalali kabisa. Ilikuwa unaenda kumuona Dr Hosp na anakuhudumia sio kwamba anafanya uzembe unapata huduma kama zote ila inajulikana baada ya kazi huyo huyo Dr ana clinic yake nje na anahudumia. Mimi binafsi sijawahi kuhudumiwa tofauti japo ukiwa Hosp ya serikali process zake ni tofauti. Lakini hata hizi Hosp za serikali ziko huduma za fast track ukitaka kuonana na Dr bingwa express bila foleni unalipa tu hutaki unapiga foleni haya mambo yapo kila siku.

Waziri nia yake ni nzuri kwamba hawa ma Dr nje ya kazi badala ya mfano kwenda kulipia xray nje wanaweza kutumia za Hosp na wakalipia mimi sidhani kama ni issue kubwa sababu tayari haya mambo yapo Hosp zote kubwa za serikali.
 
Amekwambia watalipia kama wanavyofanya sasa hili wala sio kitu kipya. sio kila jambo kipinga tu haya mambo yanafanyika toka zamani. Namuona Dr baada ya kazi clinic yake anakupata appointment labda kufanya upasuaji anakuelekeza Hosp ya kwenda kwa maana private Hosp anakuja huyo Dr anafanya service zake wewe unamlipa kama yeye na unalipa gharama za Hosp. wakati mwingine inakuwa lump sum yeye Dr anakuwa na maelewano na hiyo Hosp kuhusu charges. Hakuna jipya katika hili.
Basi tulichelewa sana wakanyage twende
 
Ukisoma comments nyingi humu watanzania wengi wana chuki na madaktari, they don't give a f*ck about doctors wellfare!!!
 
Huu uwamuzii bado hautotatua tatizo utaongeza tatizo wajomba watafanya sehemu ya biashara zaidi
 
Back
Top Bottom