Umoja Party walikuja kuzima harakati halali

Umoja Party walikuja kuzima harakati halali

RingaRinga

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2015
Posts
1,047
Reaction score
521
Enyi viongozi wa vyama na wanasiasa,
Nataka niwaambie ukweli mchungu:

Mpaka sasa hakuna chama kilichojipambanua kuwakilisha mawazo ya wananchi wengi,
Kama wananchi watapiga kura 2025 watapiga kura za visilani tu, usishangae hata vyama visivyopata kura nyingi vikapata kura nyingi kuliko wakati wowote.
Lakini ni juu ya wanasiasa kulijua hilo, na kama wanaweza kuchukua jukumu la kuwasimamia wananchi walio wengi basi watazipata kura halali.

Kwa sasa kiasi kikubwa wananchi waliowengi hawana uongozi, wamemeza uchungu na hakuna wakuwatapisha, mnawaangalia kama hamjui kwa kuwa siasa za wanasiasa wengi ni siasa za uongo na wizi zikitanguliwa na sura ya uzalendo kumbe ni ujanja'ujanja tu.

2025 itaongea.

Hawa Umoja Party nilidhani wamekuja kuweka rekodi sawa na kuendeleza uzalendo wa kweli lakini nadhani lilikuwa tawi la wahuni kwa ajili ya kuchota akili za watu na kuwaacha kwenye mataa ikiwa ni jitihada za kuzima harakati halali za kuondokana na uhuni ambazo kwa vyovyote zingeweza kuibuka kipindi hicho.

Nchi inahitaji chama kilicho na wanasiasa wenye mioyo yenye uchungu, na wasiopepesa macho, wawazi na wakweli.

R.I.P JPM ulionyesha njia na legacy yako ipo, ulipendwa na wengi na kuchukiwa na wahuni.
Walioumia katika kipindi chako kimakosa lilikuwa ni jambo lisilokwepeka kwa kuwa ilikuwa ni vita na tulishaelewa hivyo, hata kama mimi ningeumia pia ningeelewa ni ajali vitani.
Maisha yako yalikuwa somo kubwa,
Bwawa lilijaa viumbe wa kila aina, halali na wasiohalali,
Hakukuwa na namna yoyote isipokuwa kulivurugavuruga ili kila mmoja aijue nguvu ya asili inavyofanya kazi.
Ilikuwa kama nyakati za Nuhu ambapo ililazimika kushusha mvua ambayo ilitafuna wema na waovu japo kizazi kingine kilisalimishwa.
Haikuwa bahati mbaya, yalikuwa makusudi ya Mungu kukuleta na kukuchukua,

Somo lilishaeleweka.

Yapo yaliyofanyika maalum kwa ajili ya kipindi cha operation hiyo tu, kwa uwezo na kipawa chako tu, ambayo mwingine hawawezi kufanya na labda hatuwezi hata kuwaelewa kwa kuwa sio muktadha wake.
Watu kama wewe ni baada ya miaka nenda rudi kutokea tena.

Lakini pia kwa kuwa somo lililoachwa na JPM lilisomwa na wenye uchungu na nchi na wahuni, maana yake ni kuwa ajaye hawezi kufanya km JPM kwa kuwa hawatamwacha aende mbali,
Atapaswa kuwa na style yake kama atapenda kuishi kwa raha,
La awe tayari kwa lolote ndio atakidhi mahitaji ya walio wengi.

Awe tayari na ajue ni vita.

Kwa sasa sioni yeyote kati ya waliojitokeza, sioni 🤷

Wapo ndani ya CCM na CHADEMA, wakitaka kujitokeza tunawatambua, maana tunawajua,
Labda ni swala la wakati,

Katiba mpya sawa lakini isiandaliwe ku'intertain wahuni.
 
Kuna mantiki inapotoshwa kuhusu Chadema na kulamba asali, hasa nichukulie mfano wa viongozi wakuu wawili wa chama hicho, Lissu, na Mbowe.

Nikianza na Mbowe, huyu tunatambua fika madhila yote aliyofanyiwa wakati wa JPM, kuanzia wakati ule DC wa Hai akiwa Mnyeti, huyu alihakikisha anaharibu mashamba ya Mbowe kwa namna alivyopenda, ajabu JPM akampa Ukuu wa Mkoa kama zawadi kwa kazi aliyofanya.

Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".

Kuonesha Magufuli alivyokuwa na hasira na chuki kwa Mbowe, hata asset zake nje ya Kilimanjaro kama Club Billicanas hazikuachwa salama..

Tukija kwa Lissu, lile shambulio dhidi yake, risasi zaidi ya kumi na sita, lililomuacha na kilema cha maisha ni mfano tosha, hawa watu wanastahili kufidiwa kwa maumivu waliyosababishiwa na utawala uliopita, na wakifanyiwa hivyo, huko sio kulambishwa asali kama wengi mnavyodai, wale wamepewa haki zao, huu ndio uhalisia wa mambo.
 
Maskinii. I can see the sadness in your eyes.
Kazi yake Mola haina makosa. Mungu hufanya yale yanayompendeza yeye. Sifa na utukufu ni kwake Yehova. Yeye aliyesema nayo ikawa, ahimidiwe daima...
 
Kuna mantiki inapotoshwa kuhusu Chadema na kulamba asali, hasa nichukulie mfano wa viongozi wakuu wawili wa chama hicho, Lissu, na Mbowe.

Nikianza na Mbowe, huyu tunatambua fika madhila yote aliyofanyiwa wakati wa JPM, kuanzia wakati ule DC wa Hai akiwa Mnyeti, huyu alihakikisha anaharibu mashamba ya Mbowe kwa namna alivyopenda, ajabu JPM akampa Ukuu wa Mkoa kama zawadi kwa kazi aliyofanya.

Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".
We lini mnyeti alikuwa dc hai?
 
Enyi viongozi wa vyama na wanasiasa,
Nataka niwaambie ukweli mchungu:

Mpaka sasa hakuna chama kilichojipambanua kuwakilisha mawazo ya wananchi wengi,
Kama wananchi watapiga kura 2025 watapiga kura za visilani tu, usishangae hata vyama visivyopata kura nyingi vikapata kura nyingi kuliko wakati wowote.
Lakini ni juu ya wanasiasa kulijua hilo, na kama wanaweza kuchukua jukumu la kuwasimamia wananchi walio wengi basi watazipata kura halali.

Kwa sasa kiasi kikubwa wananchi waliowengi hawana uongozi, wamemeza uchungu na hakuna wakuwatapisha, mnawaangalia kama hamjui kwa kuwa siasa za wanasiasa wengi ni siasa za uongo na wizi zikitanguliwa na sura ya uzalendo kumbe ni ujanja'ujanja tu.

2025 itaongea.

Hawa Umoja Party nilidhani wamekuja kuweka rekodi sawa na kuendeleza uzalendo wa kweli lakini nadhani lilikuwa tawi la wahuni kwa ajili ya kuchota akili za watu na kuwaacha kwenye mataa ikiwa ni jitihada za kuzima harakati halali za kuondokana na uhuni ambazo kwa vyovyote zingeweza kuibuka kipindi hicho.

Nchi inahitaji chama kilicho na wanasiasa wenye mioyo yenye uchungu, na wasiopepesa macho, wawazi na wakweli.

R.I.P JPM ulionyesha njia na legacy yako ipo, ulipendwa na wengi na kuchukiwa na wahuni.
Walioumia katika kipindi chako kimakosa lilikuwa ni jambo lisilokwepeka kwa kuwa ilikuwa ni vita na tulishaelewa hivyo, hata kama mimi ningeumia pia ningeelewa ni ajali vitani.
Maisha yako yalikuwa somo kubwa,
Bwawa lilijaa viumbe wa kila aina, halali na wasiohalali,
Hakukuwa na namna yoyote isipokuwa kulivurugavuruga ili kila mmoja aijue nguvu ya asili inavyofanya kazi.
Ilikuwa kama nyakati za Nuhu ambapo ililazimika kushusha mvua ambayo ilitafuna wema na waovu japo kizazi kingine kilisalimishwa.
Haikuwa bahati mbaya, yalikuwa makusudi ya Mungu kukuleta na kukuchukua,

Somo lilishaeleweka.

Yapo yaliyofanyika maalum kwa ajili ya kipindi cha operation hiyo tu, kwa uwezo na kipawa chako tu, ambayo mwingine hawawezi kufanya na labda hatuwezi hata kuwaelewa kwa kuwa sio muktadha wake.
Watu kama wewe ni baada ya miaka nenda rudi kutokea tena.

Lakini pia kwa kuwa somo lililoachwa na JPM lilisomwa na wenye uchungu na nchi na wahuni, maana yake ni kuwa ajaye hawezi kufanya km JPM kwa kuwa hawatamwacha aende mbali,
Atapaswa kuwa na style yake kama atapenda kuishi kwa raha,
La awe tayari kwa lolote ndio atakidhi mahitaji ya walio wengi.

Awe tayari na ajue ni vita.

Kwa sasa sioni yeyote kati ya waliojitokeza, sioni 🤷

Wapo ndani ya CCM na CHADEMA, wakitaka kujitokeza tunawatambua, maana tunawajua,
Labda ni swala la wakati,

Katiba mpya sawa lakini isiandaliwe ku'intertain wahuni.
Utasubiri sana na vyama vyako vya kwenye makaratasi
 
Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".
Hata uwaziri angepewa
 
Maskinii. I can see the sadness in your eyes.
Kazi yake Mola haina makosa. Mungu hufanya yale yanayompendeza yeye. Sifa na utukufu ni kwake Yehova. Yeye aliyesema nayo ikawa, ahimidiwe daima...
Sadness ipi kiongoz,
Kupumzika kwake kwa style hiyo ilikuwa sawa kabisa, ili legacy yake iwe na nguvu halisi.
Sasa nasikitika kufariki kwake?
Hapana,.. nasikitishwa na somo kutoeleweka ma kumpuuza mwalimu wa somo,

Nasemaje..
Kuna kitu hakiko sawa na siasa za Tanzania, labda tusubiri 2025 tutaconclude.
 
Kuna mantiki inapotoshwa kuhusu Chadema na kulamba asali, hasa nichukulie mfano wa viongozi wakuu wawili wa chama hicho, Lissu, na Mbowe.

Nikianza na Mbowe, huyu tunatambua fika madhila yote aliyofanyiwa wakati wa JPM, kuanzia wakati ule DC wa Hai akiwa Mnyeti, huyu alihakikisha anaharibu mashamba ya Mbowe kwa namna alivyopenda, ajabu JPM akampa Ukuu wa Mkoa kama zawadi kwa kazi aliyofanya.

Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".

Kuonesha Magufuli alivyokuwa na hasira na chuki kwa Mbowe, hata asset zake nje ya Kilimanjaro kama Club Billicanas hazikuachwa salama..

Tukija kwa Lissu, lile shambulio dhidi yake, risasi zaidi ya kumi na sita, lililomuacha na kilema cha maisha ni mfano tosha, hawa watu wanastahili kufidiwa kwa maumivu waliyosababishiwa na utawala uliopita, na wakifanyiwa hivyo, huko sio kulambishwa asali kama wengi mnavyodai, wale wamepewa haki zao, huu ndio uhalisia wa mambo.
Hujaelewa alichosema jamaa. Amesema nchi ilikuwa kama bwawa lililojaa viumbe vya kila aina na kila kimoja kiliishi kwa staili yake.

Mbowe alijua sheria za mazingira lakini alikiuka makusudi kwa kuendeleza mashamba mita chache kutoka chanzo cha maji kwa kuwa aliamini yupo juu ya sheria na hakuna watakaomgusa. Uamuzi wa kuharibu mashamba utaokoa vizazi na vizazi. Juzi hapa ukame ulipozidi tuliona watu wanatafuta wachawi wanaolima mashamba makubwa kwenye vyanzo vya maji.

Suala la Lissu la kulobby na watu waliokuwa na mgogoro na serikali kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo halikubaliki popote duniani. Lissu ye aliamini anapambana na Magufuli, wakati Magufuli ye alikuwa anapambana kwa ajili ya taifa lake. Suala la Lissu libaki hivyo hivyo. Lissu anachopaswa kufahamu ni kuwa kuna haki na sheria ila dunia nayo ina kanuni zake.
 
Kila may hata duniani ameletwa kwa sababu zake na akikamilisha anaondoka ba mbao badly hatujakamilisha kusudio letu tupo hapag sasaki JPM Alikamilisha ba sasaki ni zamu yak inakujatutaumbuana Sana maana makati ni Hakim mzuri sana
 
Kuna mantiki inapotoshwa kuhusu Chadema na kulamba asali, hasa nichukulie mfano wa viongozi wakuu wawili wa chama hicho, Lissu, na Mbowe.

Nikianza na Mbowe, huyu tunatambua fika madhila yote aliyofanyiwa wakati wa JPM, kuanzia wakati ule DC wa Hai akiwa Mnyeti, huyu alihakikisha anaharibu mashamba ya Mbowe kwa namna alivyopenda, ajabu JPM akampa Ukuu wa Mkoa kama zawadi kwa kazi aliyofanya.

Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".

Kuonesha Magufuli alivyokuwa na hasira na chuki kwa Mbowe, hata asset zake nje ya Kilimanjaro kama Club Billicanas hazikuachwa salama..

Tukija kwa Lissu, lile shambulio dhidi yake, risasi zaidi ya kumi na sita, lililomuacha na kilema cha maisha ni mfano tosha, hawa watu wanastahili kufidiwa kwa maumivu waliyosababishiwa na utawala uliopita, na wakifanyiwa hivyo, huko sio kulambishwa asali kama wengi mnavyodai, wale wamepewa haki zao, huu ndio uhalisia wa mambo.
Mnyeti hajawahi kuwa DC wa Hai... alikuwa DC Arumeru...
 
Kuna mantiki inapotoshwa kuhusu Chadema na kulamba asali, hasa nichukulie mfano wa viongozi wakuu wawili wa chama hicho, Lissu, na Mbowe.

Nikianza na Mbowe, huyu tunatambua fika madhila yote aliyofanyiwa wakati wa JPM, kuanzia wakati ule DC wa Hai akiwa Mnyeti, huyu alihakikisha anaharibu mashamba ya Mbowe kwa namna alivyopenda, ajabu JPM akampa Ukuu wa Mkoa kama zawadi kwa kazi aliyofanya.

Akaja DC Sabaya, huyu nae alifanya uharibu kwa asset za Mbowe kwa makusudi, tena kinyume cha sheria, alivamia hoteli ya Mbowe usiku akiwa na silaha, akaharibu mashamba yake kwa visingizio tofauti, inawezekana huyu nae alikuwa anakaribia kupewa zawadi ya Ukuu wa Mkoa, kama sio Mungu "kuingilia kati".

Kuonesha Magufuli alivyokuwa na hasira na chuki kwa Mbowe, hata asset zake nje ya Kilimanjaro kama Club Billicanas hazikuachwa salama..

Tukija kwa Lissu, lile shambulio dhidi yake, risasi zaidi ya kumi na sita, lililomuacha na kilema cha maisha ni mfano tosha, hawa watu wanastahili kufidiwa kwa maumivu waliyosababishiwa na utawala uliopita, na wakifanyiwa hivyo, huko sio kulambishwa asali kama wengi mnavyodai, wale wamepewa haki zao, huu ndio uhalisia wa mambo.
Huna lolote wewe pia mbabaishaji
 
Hujaelewa alichosema jamaa. Amesema nchi ilikuwa kama bwawa lililojaa viumbe vya kila aina na kila kimoja kiliishi kwa staili yake.

Mbowe alijua sheria za mazingira lakini alikiuka makusudi kwa kuendeleza mashamba mita chache kutoka chanzo cha maji kwa kuwa aliamini yupo juu ya sheria na hakuna watakaomgusa. Uamuzi wa kuharibu mashamba utaokoa vizazi na vizazi. Juzi hapa ukame ulipozidi tuliona watu wanatafuta wachawi wanaolima mashamba makubwa kwenye vyanzo vya maji.

Suala la Lissu la kulobby na watu waliokuwa na mgogoro na serikali kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo halikubaliki popote duniani. Lissu ye aliamini anapambana na Magufuli, wakati Magufuli ye alikuwa anapambana kwa ajili ya taifa lake. Suala la Lissu libaki hivyo hivyo. Lissu anachopaswa kufahamu ni kuwa kuna haki na sheria ila dunia nayo ina kanuni zake.
Wewe hujatembelea maeneo ya milimani tangu ukoloni mashamba ya wenyeji yako mpaka kwenye chemichemi miwa kahawa migomba majani ya ngombe iwe kwa mbowe ambaye kwakwe Jirani na sehemu kame lambo na mshara mwisho Wa wenyeji kuishi ambako ni umbali sana na nkweseko ambako ni vijiji Vya juu mlimani kwanza green house tangu lini ikawa na uharibifu Wa maji wakati anatumia derep mbona Shamba LA mkukufi ndizi wameotesha mpaka karibu na maji ?mnyeti Mungu atamwona kwa jicho lingine
 
Kujaribu kumchafua JPM ni sawa na mtu aliyejipakaa samuli halafu aogeshwe tope!

Ni kutwanga maji kwenye kinu, ni shariti anaetwanga aoge hayo maji!

JPM atabaki kuwa yuleyule
So what? Anagombea 2025? Ulie usilie 2025 itabidi uchague either fisadi CCM au Chadema usiowapenda. Na wote hao hawampendi JPM so upige usipige kura yeyote atakayeshinda ni anti JPM and there's nothing you can do about it.
 
Sadness ipi kiongoz,
Kupumzika kwake kwa style hiyo ilikuwa sawa kabisa, ili legacy yake iwe na nguvu halisi.
Sasa nasikitika kufariki kwake?
Hapana,.. nasikitishwa na somo kutoeleweka ma kumpuuza mwalimu wa somo,

Nasemaje..
Kuna kitu hakiko sawa na siasa za Tanzania, labda tusubiri 2025 tutaconclude.
2025 ni Lissu vs Samia ambao wote ni anti JPM so kazi kwako kususa au kupiga kura but JPM is no more so kumtaja hakutobadilisha kitu.
 
Natamani sana kije chama kitakachokiri na kufuata falsafa za JPM, kimuenzi katika harakati zake, kifanye siasa kama za Dr Mwinyi kule Zanzbar, mbona tutakielewa sana..
Wala hakutahitaji kuwa na viongozi wakali sana kama JPM, maana ile ilikuwa kazi maalum, wafanye tu km ananvyofanya Dr Mwinyi.. lakini kisifanye makosa ya kukaribisha vinasaba vya watu toka CCM ambao wameonyesha kuwa na chuki na JPM, wananchi wanawafahamu na hawataki kuwaona katika siasa.

Wananchi tuliowengi haturidhiki na namna viongozi wa siasa wanavyosajisahaulisha kulitaja jina la JPM kwa mazuri yake.
AU watuambie wazi bas iwapo katika misaada tunayopokea sasa ipo yenye masharti ya kuhakikisha jina la JPM halitajwitajwi km jina la kuenzi harakati zake kipindi cha utawala wake..
 
2025 ni Lissu vs Samia ambao wote ni anti JPM so kazi kwako kususa au kupiga kura but JPM is no more so kumtaja hakutobadilisha kitu.
Hali haiko hivyo unavyodhani, utakutana na mazingira tofauti sana na unavyofikiri, jina la JPM litatajwa na sana kwa mazuri na mabaya, lakini jina litatamalaki kwa mazuri
 
So what? Anagombea 2025? Ulie usilie 2025 itabidi uchague either fisadi CCM au Chadema usiowapenda. Na wote hao hawampendi JPM so upige usipige kura yeyote atakayeshinda ni anti JPM and there's nothing you can do about it.
Kuandika kwangu huko kumekukera mkuu! Na ama unataka Mimi na wewe tuwe sawa kimtazamo kuhusu hayati JPM?

Ni jambo ambalo halitawezekana!

Bakia kwa msimamo wako na nitauheshimu na wangu uuheshimu

Mengine sasa uliyonayo kunihusu nitayaita ujinga na upumbufu!
 
Hali haiko hivyo unavyodhani, utakutana na mazingira tofauti sana na unavyofikiri, jina la JPM litatajwa na sana kwa mazuri na mabaya, lakini jina litatamalaki kwa mazuri
Twende taratibu..... Yaani mgombea akiwa lIssu alafu CCM akagombea Samia (maana fomu itaprintiwa Moja) je magufuli factor inaingiaje hapo??

Yaani mama akimtolea povu mwendazake na Lissu akimtolea povu mwendazake nani atakaye anguka kwa kumpuuza JPM?!

Tuanzie hapo
 
Kuandika kwangu huko kumekukera mkuu! Na ama unataka Mimi na wewe tuwe sawa kimtazamo kuhusu hayati JPM?

Ni jambo ambalo halitawezekana!

Bakia kwa msimamo wako na nitauheshimu na wangu uuheshimu

Mengine sasa uliyonayo kunihusu nitayaita ujinga na upumbufu!
Ndio hivo Samia na Lissu wote hawampendi JPM na ndio watakaogombea so wewe endelea kupiga kelele Mitandaoni ila hamna utakachobadilisha
 
Back
Top Bottom