Uchaguzi 2020 Umuhimu wa Mawakala wa Wagombea Urais, Ubunge na Udiwani kupatiwa nakala za matokeo ya uchaguzi katika vituo vya kupiga kura

Tume ya uchaguzi inaweza kuwa ndio chanzo Cha vurugu... Kipindi Cha kutoa matokeo ya uchaguzi...
 
Utata kama huu iwapo ni kweli tafsiri yake ni mahakama tu na zinauwezo wa kuzifuta kanuni batili
Vinginevyo maelezo yote hayo ni upotoshaji.
 
Elimu iliyoambatana na uchochezi wa chuki dhidi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, sawa rudi kwa huyo aliyekutuma mwambie umeshafanya kazi uliyotumwa.
Wezi utawajua tu....[emoji3][emoji3][emoji3]achen wizi...UNAOGOPA WATU KUFUNDISHWA HIYO ELIMU?[emoji16][emoji16][emoji16]

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
 
Elimu iliyoambatana na uchochezi wa chuki dhidi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, sawa rudi kwa huyo aliyekutuma mwambie umeshafanya kazi uliyotumwa.

Mimi nimefanya uchambuzi wa sheria tu, nimechambua na kujadili maswala ya kisheria bila kumjadili mtu binafsi na bila kutaja chama cha siasa au mgombea katika jitihada za kutoa elimu kwa wadau wa uchaguzi ikiwemo tume ya uchaguzi yenyewe na viongozi wake na watendaji wake hususani wasimamizi wa uchaguzi wa ngazi mbalimbali, wagombea, wapiga kura na vyama vya siasa.

Nimeandika makala hii kwa nia njema kabisa kutoa elimu kuhusu haki ya wagombea Urais, Ubunge na Udiwani wa vyama vya siasa vyote kupatiwa nakala za fomu za matokeo ya uchaguzi ikiwemo wagombea Urais, Ubunge na Udiwani wa Chadema, CCM, ACT-Wazalendo na wagombea wa vyama vingine.

Kusema ukweli umenionea sana kwa kauli yako hii, mima sijatumwa na mtu yoyote maana ni kawaida yangu kufanya uchambuzi wa sheria katika jukwaa hili na unaweza kufanya rejea katika threads zangu za nyuma.
 
Safi sana mkuu kwa uchambuzi ulioshiba.
 
Hiyo if achana nayo. Fomu zisitoshe kwa nini??
 
Kaka asante sana kwa jitihada zako. Wemye nia ovu hawatakubali hili.
 
Hiyo if achana nayo. Fomu zisitoshe kwa nini??

Kaka Pythagoras mwambie huyo Machomane haache papara na asome kwa makini sana nimeandika kila kitu, Sheria inataka kwa lazima ziwepo nakala za kutosha za fomu za matokeo ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na madiwani. Sheria inasema kuwa lazima kuwepo nakala 24 za fomu za matokeo katika kila kituo cha kupiga kura na kwa kila uchaguzi yaani uchaguzia wa Rais ni nakala 24, uchaguzi wa wabunge ni nakala 24 na uchaguzi wa diwani ni nakala 24, hii ni kwa mujibu wa Aya ya 9.19 ya Maelekezo ya Uchaguzi kwa Wasimamizi wa Uchaguzi, 2020 na Aya 3 (8) ya Maelekezo ya Uchaguzi kwa Wasimamizi wa Vituo vya Kupiga Kura, 2020. Kat Sherai pia inasema kati ya nakala hizo 24 za fomu za matokeo ya uchaguzi, nakala 21 ni kwa ajiri ya kuwapatia mawakala wa wagombea na nakala 3 zinazobaki ni kwa ajili ya matumizi ya kiofisi ya Tume ya Uchaguzi ambapo nakala moja (1) ni kwa ajiri ya kubandika Ukutani katika Kituo cha kupiga kura ili kuwajulisha wananchi matokeo ya uchaguzi na nakala ya pili ni Msimamizi ya Uchaguzi ambayo atatumia kujumlishia matokeo ya uchaguzi wa Rais au Mbunge na nakala ya tatu na mwisho ni kwa ajili ya matumizi ya kiofisi ya Tume ya Taifa hapo makao makuu.

Hivyo basi, kisheria lazima ziwepo nakala za utosha za fomu za matokeo ya uchaguzi wa Rais, Mbunge na diwani.
 

Uwazi kama ule wa akina gwa'jima na kina makondakta ulikuwa murua sana.

Hapo pasingekuwa na ubishi na tungemaliza salama.
 
Utata kama huu iwapo ni kweli tafsiri yake ni mahakama tu na zinauwezo wa kuzifuta kanuni batili
Vinginevyo maelezo yote hayo ni upotoshaji.

Mahakamani utapeleka nin? Mahakamani utapeleka maelezo haya haya na sio vinginevyo.

Kabla ya kwenda Mahakamani lazima upate legal opinion (ushauri wa kisheria) kwanza na haya maelezo ni sehemu muhimu ya legal opinion.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…