#COVID19 UN: Ukatili wa Kijinsia umeongezeka Afrika wakati wa COVID-19

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa, ukatili wa kijinsia barani Afrika umeongezeka maradufu katika kipindi hiki cha mlipuko wa UVIKO-19.

Kwa mfano imeelezwa kuwa huko nchini Kenya wanafunzi takribani 4000 walipachikwa mimba wakati shule zilipofungwa kipindi cha zuio la kutoka nje(lockdown), wengi wakifanyiwa ukatili huo na ndugu wa karibu au maofisa wa polisi.

Kwa Wanaume:

Utafiti uliofanywa na Chuo cha Saikolojia Afrika Kusini (SACAP) ulibaini kuwa, ukatili wa kijinsia kwa wanaume upo, lakini wengi hawatoi taarifa na hata wanapotoa taarifa basi hupewa uzito mdogo na hivyo kutofanyiwa kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…