Unafanyaje kuishi maisha ya kigeto geto bila kupika?

Unafanyaje kuishi maisha ya kigeto geto bila kupika?

Unaweza kupika wali nyama, maharage na mboga za majani pembeni na vidagaa vya kutia hamasa pembeni kwa 2000?
Haujawahi kula kwa gharama hii! Hata robo ya nyama mpaka iive siyo elf 2, na sikuizi wengine hawapimi ¼ ya nyama ni kanzia ½ nakuendelea
 
Fanya kama mimi. Nachemsha nyama, nakaanga dagaa na samaki. Naweka kwenye friji. Maharage nikitaka nanunua ya kuchemsha yanapimwa kwa mamantilie. Sasa wewe eti ukitaka kula nyama ndio unanunua buchani hapo lazima uumie.

Nina viungo kama mdalasini, hiriki na tangawizi na maziwa ya kopo. Nachemsha chai nikitaka.

Nanunua nyanya na vitunguu na mara chache nanunua viazi vitamu au magimbi ila mihogo huwa siipendi. Napata vitafunwa. Unga, mchele, mayai, ngano visikose.

Napika sio sababu nishibe mimi hula chakula kidogo tu. Napika sababu ni mbaguzi mkubwa wa vyakula na mapishi, siwezi kama wewe hapo kula popote ninapokuta mgahawa. Pia quality na style kwamba nikimiss kitu fulani nipike au nipikiwe. Mfano huwa natamani 'supu' ya karanga za kusaga, sasa mamantilie gani akupikie hivyo si anakucheka.
 
Kupika Inategemea na mood na ratiba zitakavyokua mfano mwezi wa tano nilipika sana,cost za kununua mazaga zaga zilifika %45 ya budget kwa mwezi wa tano [emoji116]

IMG_3869.jpg


Ila mwezi huu wa sita ulioisha sikuwa kabisa na mzuka wa kupika nilikua napika kwa manati na cost za hayo mazaga zaga zilishuka hadi %15.9

IMG_3867.jpg


Nasubiri nione huu mwezi wa saba utakavyokua upande wa maskolodinyo
 
Ukipika mwenyewe siyo kwamba gharama inapungua hata uwe unakula vitu basic tu ila kama wengine walivyosema kwa kiasi kikubwa utakuwa unakula vyakula fresh. Huko migahawani mazingira siyo safi na wapikaji siyo wasafi ni kwamba huwa tunafumba macho tu vyakula vipite kwenye koo.

Kuhusu kuosha vyombo, anza kuosha wakati unapika. Chakula kikiiva hakikisha vyombo vyote ulivyotumia kupika tayari ni safi inakupunguzia mzigo baadae. Ukimaliza kula utajikuja umebaki kuosha vitu vichache sana ulivyotumia kama sahani, vijiko na vikombe. Osha hivyo fasta kabla uvivu haujakuingia.
 
Kupika Inategemea na mood na ratiba zitakavyokua mfano mwezi wa tano nilipika sana,cost za kununua mazaga zaga zilifika %45 ya budget kwa mwezi wa tano [emoji116]

View attachment 3030977

Ila mwezi huu wa sita ulioisha sikuwa kabisa na mzuka wa kupika nilikua napika kwa manati na cost za hayo mazaga zaga zilishuka hadi %15.9

View attachment 3030978

Nasubiri nione huu mwezi wa saba utakavyokua upande wa maskolodinyo
Hesabu kali sana hizi 😂😂 umenishinda 🙌
 
Pika mwenyewe unakula kitu moyo unashangiliaa. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Sawa ila mpaka ule moyo unashangilia, kumbuka hapo lazima itumie si chini ya bajeti ya mboga 8,000 na zaidi hapo utakuwa umeokoa matumizi au umeongeza tumizi
 
Ukipika mwenyewe siyo kwamba gharama inapungua hata uwe unakula vitu basic tu ila kama wengine walivyosema kwa kiasi kikubwa utakuwa unakula vyakula fresh. Huko migahawani mazingira siyo safi na wapikaji siyo wasafi ni kwamba huwa tunafumba macho tu vyakula vipite kwenye koo.

Kuhusu kuosha vyombo, anza kuosha wakati unapika. Chakula kikiiva hakikisha vyombo vyote ulivyotumia kupika tayari ni safi inakupunguzia mzigo baadae. Ukimaliza kula utajikuja umebaki kuosha vitu vichache sana ulivyotumia kama sahani, vijiko na vikombe. Osha hivyo fasta kabla uvivu haujakuingia.
Sahihi 🤝🤝
 
Kwa miaka 4 sasa na mwezi mmoja nimeishi bila kujipikia nikila kwa migahawa nfanya hivi kwa maisha haya ya kutojipikia kwa sababu mimi siyo mtu wa kukaa sehemu moja nikatulia hii ni sababu ya mazingira yangu ya utafutaji nakaa sehemu kwa muda mfupi baadae naenda eneo jingine nikiridishe kwenye mada leo bhana nimeona naumia kwa siku natumia chai 1,000 hadi 1500 inategemea nimepita wapi siku hiyo maana sina kasumba ya kula sehemu moja nikazoeleka.

Mfano: Chakula cha mchana natumia 2,000 hadi 2500 nikijilipua sana labda 3000 siku zingine.

Sasa leo nikaenda nilikozoea wanasema chakula nilichokuwa nakula 2,000 leo wamepandisha ni elf 2500 hivyo hivyo hadi chai mpaka vyakula vingine!

Imebidi niulize hivi nyie kwanini imekuwa ghafla sana na hizi bei za vyakula wanasema vitu vimepanda bei na wanasema hata bajeti imekuja na mabadiliko ya vitu kupanda hivyo tuzoee!

Nimeishiwa nguvu ya kuendelea kusema chochote imebidi nilipie tu nijipange kununua vitu na mimi nianze kujipikilisha, na kupika ndio mvivu wa kwanza katika sekta hii ya kijipikia hasa kuosha vyombo ni mtihani kwangu siyo kwamba najiona hapana, sijui wengine wasema wanaona "aibu" hapana kitu nachokuwa nazembea nipale nimekula nimeshiba nikimaliza vyombo vinaniangalia tena yaani kikifikia hatua hii ndio naona kupika kazi bwana.

Kwa wenzangu ambao mnaishi maisha ya kigeto geto bila kupika, mna ushauri gani juu ya hili? Je, kuna njia rahisi za kupika ambazo hazihitaji jitihada kubwa au muda mwingi? Na je, ni vipi mnavyopambana na gharama hizi za juu za chakula nazungumzia wewe kwa wale ambao hampiki huku mkiendelea kuishi bila kujipikia? Naomba uzoefu na mawazo yenu.

Karibuni kwa mjadala!
Wee endelea na hayo maisha mzeya. Mambo ya kupika pika ni ya kike.
Kwanza unapoteza muda tuu. Wee lengo lako sii tumbo lishibe.
Hamna kitu kinakera kama kuosha vyombo
 
Fanya kama mimi. Nachemsha nyama, nakaanga dagaa na samaki. Naweka kwenye friji. Maharage nikitaka nanunua ya kuchemsha yanapimwa kwa mamantilie. Sasa wewe eti ukitaka kula nyama ndio unanunua buchani hapo lazima uumie.

Nina viungo kama mdalasini, hiriki na tangawizi na maziwa ya kopo. Nachemsha chai nikitaka.

Nanunua nyanya na vitunguu na mara chache nanunua viazi vitamu au magimbi ila mihogo huwa siipendi. Napata vitafunwa. Unga, mchele, mayai, ngano visikose.

Napika sio sababu nishibe mimi hula chakula kidogo tu. Napika sababu ni mbaguzi mkubwa wa vyakula na mapishi, siwezi kama wewe hapo kula popote ninapokuta mgahawa. Pia quality na style kwamba nikimiss kitu fulani nipike au nipikiwe. Mfano huwa natamani 'supu' ya karanga za kusaga, sasa mamantilie gani akupikie hivyo si anakucheka.
Ni wazo zuri sema muda wa kununua fridge/ freezer ndio sina maana naishi kama ndege kesho mkoa huu mwezi ujao wilaya ile hapo utanunua vitu kweli labda ununue vitu hivi ukiwa umesimika kambi kabisa sehemu moja
 
Wee endelea na hayo maisha mzeya. Mambo ya kupika pika ni ya kike.
Kwanza unapoteza muda tuu. Wee lengo lako sii tumbo lishibe.
Hamna kitu kinakera kama kuosha vyombo
Kumbr tuko wengi aisee nikajua niko peke yangu kuhusu hili suala 😂😂😂
 
Mama ntilie yuko blid akajikuna kunako akaedelea kukatakata kachumbari,mtoto kajisaidia akamtawaza kwenye beseni lakukandia maandazi,ukinikuta kwa mama ntilie niite mbwa
Hata nyumbani hili unalosema linaweza kufanywa na mkeo au mfanyakazi wako, kikubwa uwe mzima tu basi mengine hayo ni matokeo.

Kuna wanawake wachafu ajabu yaani unaona kabisa hapa hamna kitu kupika, hata ndani ni holela sema kama ukiangukia kwenye mtego huu omba isiwe utajuta. Ukitaka kuja na mgeni mpaka utangulie kwanza ukahakiki kama mazingira ni salama ndio umpokee mgeni uliyepanga kuja nae kwa pamoja
 
Hata nyumbani hili unalosema linaweza kufanywa na mkeo au mfanyakazi wako, kikubwa uwe mzima tu basi mengine hayo ni matokeo.

Kuna wanawake wachafu ajabu yaani unaona kabisa hapa hamna kitu kupika, hata ndani ni holela sema kama ukiangukia kwenye mtego huu omba isiwe utajuta. Ukitaka kuja na mgeni mpaka utangulie kwanza ukahakiki kama mazingira ni salama ndio umpokee mgeni uliyepanga kuja nae kwa pamoja
Kigezo changu cha kwanza kwa wife material ni mwanamke msafi,kinyume chake hafai kuweka ndani
 
We hakikisha una sufuria zako 2 tu.
Moja ya mboga moja ya ugali. Ukinaliza kupika unakula humo humo.
Kwaio ukitaka kupika tena lazma uyaoshe. Automatically unakua umeondoa jam ya kuosha vyombo.
Sufuria la ugali ndo litatumika kuchemsha hadi chai. Unaacha ipoe unainywa from sufuria kistaarabu kabisa.
 
Back
Top Bottom