Unafiki wa Marekani: Wakati Marekani ikishinikiza wengine kuitenga Urusi kiuchumi, yenyewe haiko tayari kuitenga Urusi maeneo inayofaidika nayo

Unafiki wa Marekani: Wakati Marekani ikishinikiza wengine kuitenga Urusi kiuchumi, yenyewe haiko tayari kuitenga Urusi maeneo inayofaidika nayo

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Marekani ni mnunuaji mkubwa sana wa mafuta yasiyosafishwa toka Urusi!! Hilo ni eneo nyeti sana kwake kiuchuni. Jana katika hotuba yake muhimu kwa Taifa, mataifa ya ulaya yalitegemea Biden kutangaza kususia ununuaji wa mafuta toka Urusi, na kwa mshangao wao hakugusia kabisa jambo hilo. Hata baadhi ya wabunge wa Democratic wameshangaa na kuamua kuandika barua ya kumkosoa Biden na bado Biden kala jiwe!

Marekani haiko tayari kuweka vikwazo ambavyo itajikuta inaumia sana pia kiuchumi, lakini inazikomalia nchi za ulaya kuiwekea vikwazo Urusi bila kujali zitaumia namna gani!! Hilo ndilo beberu baba lao! Mataifa ya India, China, Pakistani, Brazil, Mexico yamegoma wazi wazi kuunga mkono vikwazo dhidi ya Urusi ili mradi tu kuifurahisha Marekani!! Yameamua kuzingatia maslahi yao!

Huko tunakokwenda, si ajabu Marekani ikaanza kuzilazimisha nchi zetu hizi kuunga tela dhidi ya Urusi!! Tukifikia huko, kuna mwenye ubavu kama wa Baba wa Taifa mwalimu Nyerere wa kusimama kidete na kusema SISI HATUFUNGAMANI NA UPANDE WOWOTE? Karibuni tudadavue!
 
Putin alianza kumwadhibu kibaraka wa mabeberu (rais wa Ukraine) kwa kutumia fimbo inayotumika kwa watoto wa chekechea!! Ukraine ikastahimili na kusifiwa sana kuwa ni mashujaa, eti Putin kakutana na upinzani asioutarajia!! Jamaa akasema, ngoja nikuoneshe!! Sasa hivi ni kilio kila kona!! na kaweka kambi kubwa ya kufa mtu kama kilomita 24 toka mji mkuu wa Ukraine Kiev!! Amewaacha wajiharishie wenyewe kwanza!! Atakapotoa amri ya kuingia Kiev, kutakuwa na kilio hadi kwa Biden!!
 
Marekani Hana rafiki wa kudum,Wala adui wa kudum,Ila ana maslahi ya kudum! In Biden'$ voice.
 
Back
Top Bottom