Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
Good afternoon jamiiforums
Kumpa mfiwa pesa mkononi au kuandika kwenye daftari ni kipi bora zaidi emotionally? Jenga picha umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.
Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"
Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.
Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.
Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.
Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.
Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kumpa mfiwa pesa mkononi au kuandika kwenye daftari ni kipi bora zaidi emotionally? Jenga picha umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.
Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"
Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.
Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.
Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.
Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.
Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.