Unafungua daftari la michango ya rambirambi unakuta mtu wa kwanza kaandika 1,200,000/=

Unafungua daftari la michango ya rambirambi unakuta mtu wa kwanza kaandika 1,200,000/=

Hyo huwa jambisha jambisha ili watu watoe kiasi kikubwa,back to me nilikuta jina la mwanangu ninayemfahamu kabsa eti katoa 100k nikasema aaaah wap...wakati huyo mwanangu mbahili wa kutupwa mpaka akitoa sadaka kanisani anachukua chenchi kwenye kikapu[emoji23][emoji23]
 
Mi nilikuwa na buku nikaandika 900.0 na chenji nikadai
 
Hiyo ni bosheni tu kuwafanya wasijielewa kuingia mkenge kufuata mkumbo [emoji108][emoji108][emoji108]
 
Kama uliwai kuhudhuria vikao vya harusi utakua unaelewa maana yake, Kwenye hivi vikao vya michango wanakuwepo waropokaji walioandaliwa wawe wa kwanza kutoa ahadi. Unashangaa anasimama mtu huko nyuma anachangia milion kadhaa, hawa wengine ni lazima wajiongeze, Lakini hawa waliondaliwa kuropoka si kweli kwamba wanatoa hizo ela walizoahidi hio inakua siri ya Kamati.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Kwani Magige daftari lake mtu wa kwanza hadi tatu waliandika sh ngapi...

Misiba kwa mijini nayo imekuwa upigaji, ila kijijini mambo ya rambirambi ni mara chache sana
 
Good afternoon jamiiforums

Umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.

Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"

Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.

Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.

Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.

Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.

Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Rambi rambi haimpozi machungu mfiwa msibani
 
Kama uliwai kuhudhuria vikao vya harusi utakua unaelewa maana yake, Kwenye hivi vikao vya michango wanakuwepo waropokaji walioandaliwa wawe wa kwanza kutoa ahadi. Unashangaa anasimama mtu huko nyuma anachangia milion kadhaa, hawa wengine ni lazima wajiongeze, Lakini hawa waliondaliwa kuropoka si kweli kwamba wanatoa hizo ela walizoahidi hio inakua siri ya Kamati.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Hata kwenye kutoa zawadi utasikia mtu anasimama mbele anasema,nimejitolea kuwapa maharusi gari,kiwanja,nyumba kumbe ile ni uzushi tu😂😂

Ova
 
Unatoa hiyo 15,000 yako then unaongeza zero mbili mbele...
 
Good afternoon jamiiforums

Umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.

Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"

Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.

Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.

Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.

Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.

Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kwanza jua Mazishi na Misiba ni ghali. Tofauti na wale wanaofukia lakini kwa tunaozika Mazishi ya kawaida sana na mwili haujasafirishwa ni milioni 5

Sent from my vivo 1915 using JamiiForums mobile app
 
Good afternoon jamiiforums

Umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.

Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"

Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.

Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.

Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.

Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.

Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
..."Toa ndugu, toa ndugu,
Ulicho nacho Wewe,
Mungu atakuona, Mpaka rohoni mwako"...
 
Changia kwa uwezo wako, isikutishe kiasi alichochangia aliekutangulia
 
Back
Top Bottom