Unahitaji mtoto wa Kambo au Kumuasili?

Vyema.
Ila bado kuna vijiswali pale juu.
Nasubiri Dkt aje kunifafanulia.
Ndiyo Sasa nimepata fursa ngoja niyakusanye sasa hivi nimpe kamishna wa ustawi anipe majibu nirudi hapa sasa nikupe. Mambo mengi ndugu zangu, kuna wakati napotea kuendelea na mengine narejea tena. Subiri tafadhali, shukrani
 
Utaratibu wa kuasili watoto mapacha unafana na watoto wengine. Kanuni ya kuasili 3(e) hairuhusiwi kuwatenganisha watoto ndugu.

Kuhusu vigezo vikuu; vigezo vyote kuasili ni vikuu kwa ulinzi na usalama wa mtoto na ni njia mojawapo ya kujiridhisha kwamba mtu ametimiza vigezo

Umri wa kuasili mtoto ni umri wowote chini ya miaka 18. Kigezo cha umri pia kimewekwa kwa mwombaji wa kuasili. Sheria ya Mtoto kifungu cha 56(a) kinasema, mwombaji awe na umri wa miaka 25 kupanda na amzidi mtoto miaka 21. Mwombaji mwenye miaka 50 atapewa mtoto mwenye umri wa kuanzia miaka 10

Unaweza kuasili watoto wawili kwa wakati mmoja (kanuni iliyopo kwenye mapitio imepunguza idadi ya watoto kutoka 3 mpaka 2)

Tanzania haijaridhia uasili baina ya mataifa hivyo, watoto wanaoasiliwa ni Watanzania tu. Kama ni mtoto raia wa nchi nyingine sheria haijamtambua kwenye suala la kuasili (ipo kimya). Kwa watoto wa makabila ya Tanzania unaweza kuasili mtoto wa kabila lolote.

Shukrani sana kwa mchango wako kwenye mjadala huu. Iko siku tutawaleta wataalamu kwenye mkutano online Ili mpate elimu na ufafanuzi mpana zaidi.
 
Dr asalaam aleyqum
Kidogoo naomba unieleweshe
Umesema kwamba ruksa imetoka kwa watanzania tu kuadapt watoto,

Naomba kuuliza swali tunafahamu tz ni bara na visiwani
Swali langu linakuja ,je mwananchi kutoka zanzibar ambae saiv anaishi huku bara kwa. miaka 5

Je hakuna masharti yoyote yale atakayopata ambapo akiamua kuchukuwa mtoto wa kambo hapa bara?

je kama akiruhusiwa kupewa huyo mtoto hakuna tatizo kwenda nae kuishi znz ? Ahsante
 
Hii ni habari njema sana, watu wengi walikuwa wanaisubiri kwa shauku kubwa sana ujio wa jambo hili.
Ila Dkt., naomba utusaidie kuhusu mambo haya kuhusiana na suala hili:-
1. Je, suala hili kwa hapa Tanzania linasimamiwa na Sheria gani/zipi katika nchi hii? Kanuni zipi za Sheria hiyo /hizo??
2.Je, historia kamili (historical background) za hao watoto wanaoasiliwa mmezitunza vyema kwa maandishi na kuwapatia hao "wazazi wapya" wanaowaasili hao watoto? Nimewahi kushuhudia kesi /mgogoro mmoja mzito ktk nchi fulani (nisingependa kuitaja jina hapa) ambayo niliwahi kuishi, mgogoro wenyewe unahusiana moja kwa moja na suala hili.
Historia kamili za hao watoto pamoja na upatikanaji wao hadi kufikia hatua za kuasiliwa na 'wazazi wapya' zipo???? Je, Hao wazazi wapya wanapokabidhiwa hao watoto pia huwa wanakabidhiwa na nyaraka rasmi za Serikali sambamba na nyaraka za historia za maiisha za hao watoto ?
 
Ndiyo Sasa nimepata fursa ngoja niyakusanye sasa hivi nimpe kamishna wa ustawi anipe majibu nirudi hapa sasa nikupe. Mambo mengi ndugu zangu, kuna wakati napotea kuendelea na mengine narejea tena. Subiri tafadhali, shukrani
Haya mkuu.
Pole sana kwa majukumu, si unajua wizara yako inabeba majukumu mengi sana, sana.
Haya Dkt tunakusubiri....
 
Asante sana mkuu,umenifumbua macho kwa yale ambayo nilikuwa sina uelewa nayo, hasa hili la mapacha, kumzidi miaka 21 pamoja na uraia mwingine kwa mtoto unayetaka kumuasili.

Na pia wengine wamejifunza na kuelimika kupitia maelezo yako.

Kumbe huku mtaani huwa tunapotoshana sana kuhusu suala zima la kuasili mtoto na masharti yake, ni afadhali umetuweka wazi kwa maelezo nyoofu na yenye kueleweka.

Nakushukuru sana waziri kwa kunijibu na kunipa ufafanuzi yamkini.

Asante na nikutakie kila la kheri kwenye majukumu yako
🀝🀝🀝
 
Dkt Kuna mtu anaitwa cocastic Ni tapeli asipewe mtoto huyu mtu hatari tupu wala asikuzogeleee mtajuta endapo mtampa mtoto akamlee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…