Unaiona wapi Tanzania ya kesho kupitia malezi ya watoto wa leo?

Unaiona wapi Tanzania ya kesho kupitia malezi ya watoto wa leo?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Mwandishi maarufu wa vitabu, Robert T. Kiyosaki, kaandika kuwa mahali sahihi pa somo la mafanikio kufundishwa ni nyumbani. Kwa msingi huo, makuzi ya mtoto yatakuja kumwathiri si yeye peke yake tu, bali pia familia yake, Jamii yake na Taifa lake kwa ujumla.

Je! Malezi yetu ya Kitanzania yanamuandaa mtoto kuja kuwa mtu mwenye mafanikio kibinafsi na katika nafasi atakazozishika kwenye Jamii au Serikalini?

Ikiwa maisha ya utotoni ni kama msingi wa maisha ya utu uzima, namna watoto wa sasa wanavyolelewa kunatia matumaini kuwa kesho Taifa litakuwa na watu "potential?"

Kumbuka, watu wazima walio kwenye nafasi mbalimbali leo Serikalini, kwenye dini, Jamii, biashara, taaluma, n.k. ni watoto wa "Jana".

Ukiangalia Mataifa yaliyoendelea, na hapa, walengwa wakuu ni "Wazungu ", ingawa hawana ngozi ngumu na zinazostahilimili mazingira mbalimbali kama ngozi zetu, ni wazi kuwa fikra zao zimechochea sana maendeleo ya nchi zao.

Wanajulikana kuwa ni:
1. Wazalendo sana kwa nchi zao

2. Ni wajasiri hivyo hupenda kujaribu mambo mpya hata kama yanaonekana ni hatari.

3. Wabunifu

4. Wanajiamini

5. Watu waliozoeshwa kujitegemea tokea wakiwa wadogo

6. Hujiwekea malengo ya maisha mapema sana tokea wakiwa watoto wadogo

7. Huzoeshwa tabia ya usomaji vitabu tokea wakiwa wadogo sana.

Kupitia malezi ya "sasa" ya watoto wa Watanzania wanaoishi Tanzania, unaionaje Tanzania ya "kesho?"
 
Tz ya kesho niionayo mm n Ile ilee tu ikiendelea kuongozwa na ccm hakuna mabadiliko yyt km CCM itaendelea kuongozwa nchi.

N hayo tu Kwa Leo Asante[emoji120]
 
Kuna giza sana.
Mkuu, unajua kuwa ukimbadilisha mtoto mmoja huyo mtoto anaweza kuja kuubadilisha ulimwengu?

Unafanya jitihada zo zote "kuwekeza" mtazamo chanya kwa watoto ili waje kuwa msaada kwa Taifa la "kesho"?
 
Tz ya kesho niionayo mm n Ile ilee tu ikiendelea kuongozwa na ccm hakuna mabadiliko yyt km CCM itaendelea kuongozwa nchi.

N hayo tu Kwa Leo Asante[emoji120]
Aisee!
 
Tatizo sio la Tanzania (inagawa Tanzania ni wazembe; with all potential and resources hiki nachosema kinachofuatia huenda kisingetuletea shida sana)

Issue kubwa ni Automation na Teknolojia - Hata watu wawe wabunifu kiasi gani (mmoja mmoja) wengine wanaweza waka-copy na kupaste...; Tatizo la dunia ya kesho ni kwamba Nguvu kazi haiitajiki kama zamani hivyo Dunia ya kesho lazima itafute namna ya kuweza / kuhakikisha massive production capability ni vipi inaweza ikawanufaisha majority (wasio na kitu) angalau kupata basic needs.....

Its going to get worse and the current political / economical system will disintegrate....
 
Tatizo sio la Tanzania (inagawa Tanzania ni wazembe; with all potential and resources hiki nachosema kinachofuatia huenda kisingetuletea shida sana)

Issue kubwa ni Automation na Teknolojia - Hata watu wawe wabunifu kiasi gani (mmoja mmoja) wengine wanaweza waka-copy na kupaste...; Tatizo la dunia ya kesho ni kwamba Nguvu kazi haiitajiki kama zamani hivyo Dunia ya kesho lazima itafute namna ya kuweza / kuhakikisha massive production capability ni vipi inaweza ikawanufaisha majority (wasio na kitu) angalau kupata basic needs.....

Its going to get worse and the current political / economical system will disintegrate....
Aisee!
 
Ngazi ya serikali na familia zimelala usingizi mzito..kizazi Cha mtandao, kizazi za kudanga, kizazi Cha kubeti. Kizazi Cha starehe ...kwanza tutaenda kuwa na vijana wengi wenye matatizo ya afya, wengi watapoteza Imani kabisa Kwa Mungu, matukio ya ajabu kwenye jamii yataongezeka..Kuna vitu Sasa vinaonekana ni vya aibu kuvifanya ila kadiri miaka inavokwenda jamii itavikubali..watu watakuwa wakaidi.etc..
 
Back
Top Bottom