Unaishi vipi na jirani anayependa dezo na kuombaomba?

Unaishi vipi na jirani anayependa dezo na kuombaomba?

Najua jirani ni ndugu wa karibu ila kuna mengine yamezidi.

Jirani alikuwa anakuja kuomba chaji nikaona sio kesi nimenunua nyingine nikamuachia atumie.

Bado basi yake imeharibika hana mpango wa kuitengeneza wala kununua nikaona sikesi usumbufu umezidi nichukue nyingine, sasa naona haajiongezi, chaji ile sijui imekuaje anakuja tena kugonga nimuwekee chaji, waungwana ujirani huu unafanyaje?
Mvumilie tu jirani ndio ndugu yako wa karibu hasa ukiwa uswahilini😂!

Kero ikizidi kuna Apartment Masaki hapa, nitafute nikupeleke kwa mwenyewe.
 
Najua jirani ni ndugu wa karibu ila kuna mengine yamezidi.

Jirani alikuwa anakuja kuomba chaji nikaona sio kesi nimenunua nyingine nikamuachia atumie.

Bado basi yake imeharibika hana mpango wa kuitengeneza wala kununua nikaona sikesi usumbufu umezidi nichukue nyingine, sasa naona haajiongezi, chaji ile sijui imekuaje anakuja tena kugonga nimuwekee chaji, waungwana ujirani huu unafanyaje?
Akiomba mpe fake atajifunza
 
Natengwa na majirani sababu ya mmea, kuna kisa fulani nikikumbuka mpaka nacheka kuna siku nilikuwa naelekea dukani usiku kununua mkate maana kesho yake nilikuwa nawahi asubuhi sana kutoka.

Kuna mama fulani wa makamo alikuwa anaelekea njia moja na mimi ila yupo mbele yangu ndio anaenda nyumbani kwake sasa nikiongeza mwendo na yeye anaongeza mwendo nisimkaribie mpaka akakata sandals alizokuwa amevaa.

Kumsemesha namuona ana hofu kama anatetemeka na hasira, alibahatisha kuna toyo ilikuwa inapita akaichukua na kwenda nayo umbali haufiki hata nusu kilomita kesho yake nilikuja kusikia stori mtaani eti alinusurika kukabwa na wavuta bangi wa mtaani duh nikajua kumbe najulikana mtaani na na kuogopwa kabisa,

hamna mtu mwenye time na mimi wanajua ni mhuni tu anayepuliza mmea kila saa, na mimi nawaacha wanichukulie hivyo hivyo sitaki mazoea🐒
Mzee wa Shada😂 unakula sana dawa!
 
Nakataa ndugu, mtu ambae kwa mwezi anaingiza 500,000tsh anashindwa chaji ya 10,000? Kitu anachotumia mara nyingi?
Aaaaaaaa....umenikumbusha mbali sana nilikuwaga na jirani yangu yeye n mwalimu wa secondary.....alikuwa anaomba kiberiti mpaka perfume.
 
Najua jirani ni ndugu wa karibu ila kuna mengine yamezidi.

Jirani alikuwa anakuja kuomba chaji nikaona sio kesi nimenunua nyingine nikamuachia atumie.

Bado basi yake imeharibika hana mpango wa kuitengeneza wala kununua nikaona sikesi usumbufu umezidi nichukue nyingine, sasa naona haajiongezi, chaji ile sijui imekuaje anakuja tena kugonga nimuwekee chaji, waungwana ujirani huu unafanyaje?
Ni kuwa bize na kazi ili asikukute Mara kwa Mara nyumbani!
 
maisha mepesi sana haya hasa ukijifunza kupuuza mambo,yaani kuwa mzungu tu.

unawezamkoromea huyo jamaa,akakuogopa kabisa mpaka siku umeanguka akaendelea kuogopa hata kukusogelea[emoji38][emoji38]
 
Aaaaaaaa....umenikumbusha mbali sana nilikuwaga na jirani yangu yeye n mwalimu wa secondary.....alikuwa anaomba kiberiti mpaka perfume.
Fikiria mtu mwenye mentality kama hiyo, yani ni kero sana
 
Mpe ujumbe kuwa hupendelei tabia yake hiyo kwa njia ya indirect... Mwekee chaji akiondoka zima switch akija kuchukua simu haijajaa ..ikitokea hivyo mara tatu harudi
Ukimuendekeza atakuja kuomba mpaka mboga na siku akiwa na wageni atakuomba pa kulala
Mkuu nitajiribu lakini naona kama hana mshipa wa aibu vile, siku unamuonesha kabisa umekasirika ila bado anarudi tena
 
Mimi jirani zangu tunaombana mbogamboga kwenye vibustani vyetu. Kama nimepanda mbogamboga hizi yeye hajapanda akiwa ana hamu nazo anakuja kuomba na mimi nikiwa na hamu na za mwenzangu namuomba.
Lakin sio kuombana vitu vingine.
Mi nataka nije niombe mboga mboga za mwilini zile jirani! Tuendelee na moyo wa mshikamano tu
 
Kuna mmoja alikuja kuazima pasi akaunguza waya nikakausha bahati nzuri nilikuanayo nyingine ambayo niliinunua nikiwa kwenye safari moja hivi, so kila akija kuomba nampa ile mbovu na sijui anaitumiaje!? Maana haipeleki moto
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukiweza kumsaidia jirani msaidie, kama huna uwezo au nafasi mueleze wazi na siyo kuja kumsimanga JF.

Unachopaswa kuelewa kila binadamu ana umuhimu wake hata anayezoa takataka ndio anakuokowa wewe nyumbani kwako pasinuke uvundo.

Tujifunze kuwaangalia wenzetu in positive way.

Kuna jamaa alipata tatizo kazini akajikuta yupo jela, kule lupango akakutana na mpiga debe wa daladala mtoto wa mtaani kazinguwa bararbarani wskamtia Segerea.

Baada ya yule jamaa kibosile wa mtaani kufika jela aliishi maisha salama na ya amani kupitia yule mpiga debe choka mbaya na akapewa na cheo gerezani kwa heshima tu.

Jamaa tangu ametoka jela alibadirisha mtazamo wake namna ya kuishi na binadamu.
 
Back
Top Bottom