GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
Waafrika wanasoma vitabu, lakini Wazungu wana wasomaji wengi zaidi kuzidi Waafrika.
Kwa Wazungu, usomaji wa vitabu ni kama sehemu ya maisha ya wengi wao.
Unajua ni kwa nini? Naamini ni kwa sababu wamelelewa hivyo! Walijengewa hiyo tabia tokea wakiwa wadogo sana.
1. Wanaweza wasiwe wote, lakini nafahamu kuwa Wazungu wana kawaida ya kuwasomea watoto wao vitabu pindi wanapojiandaa kulala. Mtoto anapoingia kitandani kulala, mzazi huketi pembeni yake na kumsomea kitabu mpaka asinzie.
2. Wengine huanza kuwasomea watoto wao vitabu tokea wakiwa tumboni. Huamini kuwa kufanya hivyo kutasaidia kuifinyanga tabia ya mtoto tokea akiwa tumboni mwa mamaye.
3. Nao wenyewe ni wasomaji. Ni rahisi mtoto kuiga kile anachokiona kwa wazazi wake. Watoto wa wasomaji huishia kuwa wasomaji.
Hizo ni baadhi ya mbinu wanazozitumia. Yeyote anaweza kuzitumia kuwajengea watoto wake tabia ya kujisomea vitabu vizuri.
Kwa Wazungu, usomaji wa vitabu ni kama sehemu ya maisha ya wengi wao.
Unajua ni kwa nini? Naamini ni kwa sababu wamelelewa hivyo! Walijengewa hiyo tabia tokea wakiwa wadogo sana.
1. Wanaweza wasiwe wote, lakini nafahamu kuwa Wazungu wana kawaida ya kuwasomea watoto wao vitabu pindi wanapojiandaa kulala. Mtoto anapoingia kitandani kulala, mzazi huketi pembeni yake na kumsomea kitabu mpaka asinzie.
2. Wengine huanza kuwasomea watoto wao vitabu tokea wakiwa tumboni. Huamini kuwa kufanya hivyo kutasaidia kuifinyanga tabia ya mtoto tokea akiwa tumboni mwa mamaye.
3. Nao wenyewe ni wasomaji. Ni rahisi mtoto kuiga kile anachokiona kwa wazazi wake. Watoto wa wasomaji huishia kuwa wasomaji.
Hizo ni baadhi ya mbinu wanazozitumia. Yeyote anaweza kuzitumia kuwajengea watoto wake tabia ya kujisomea vitabu vizuri.