Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?

Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?

mie nilikuwa napenda mambo ya Zena na Betina,afu Madenge ananiachaga hoi na vituko vyake
 
Kama unalikumbuka kipindi cha mwishoni mwa miaka ya 80 basi pole.
Kipindi hicho lilikuwa limeisha kufa likichorewa na ma bongo fleva kama Ibra.
Mzee, Sani ni la miaka ya mwishoni ya Sabini hadi 1986. baada ya hapo ni makapi tu!
Mchoraji halisi wa Sani alikuwa marehemu Philip Ndunguru.
Huyu ndiye aliyewavumbua kina Lodi Lofa, Dr Love pimbi, Kipepe na Ndumilakuwili.
Ndunguru pia alikuwa anamchora Ndumilakuwili kwenye gazeti la Kenya Leo la Nairobi kule akimuita Kazibure na alikuwa maarufu hadi akatoa kitabu maalum cha Kazibure kilichouzwa kwa maelfu nchini kenya.
Philip Ndunguru pia ndiye aliyekuwa akisanifu majalada ya vitabu vya riwaya vya akina Musiba au Willy Gamba na watunzi wengine.
Mhariri orijino wa Sani ni marehemu Said S Bawji ambaye pia alitunga vitabu kama Usiku wa Balaa, Kisiwa cha Mayuku na A love story between Tanganyika and Zanzibar.
Sani pia lilikuwa na kibonzo cha mlevi Sokomoko kikichorwa na Ted Marealle!
Gazeti hilo pia lilikuwa ndio chimbuko la misemo ya mitaani kama vile, Utajaza, Kisebu sebu na Kiroho papo etc.
Upo hapo mkuu?
 
Unakumbuka nini kuhusiana na gazeti la sani mwishoni mwa miaka ya themanini na mwazoni mwa miaka ya tisini?

Nimekumbuka enzi zile za gazeti la SANI, jamaa walikuwa wabunifu sana kwa matoleo yao,unamkumbuka kifimbo cheza na misemo mbalimbali(uchafuzi wa lugha?), kipepe na rungu lake, pimbi a.k.a dr. love yeye anatongoza kila demu! ndumila kuwili na wizi wake,aah wapi lodi lofa na kagari kake na kiko yake kitambi kule!madenge na vituko vyake akiwa na matanati yake !kuna mhusika moja hivi alikuwa chapombe sikumbuki alikuwa anaitwa nani vile?sukununu za babu sani je?wapi mechi ya bush star na born town?aah yale mazoezi kabla ya mechi hoiiii!uwanja wa fujo je? Hadithi za picha mambo ya kina Obi, Mzee Ole, Linda n.k ,wachapishaji walikuwa wabunifu kweli kweli, burudani zilizobebwa na wahusika wa kutengeneza lakini wanashambiiana na jamii!ilikuwa burudani sana kweli natamani ijirudie!


Wachoraji wa enzi zile ni kina John Kaduma(nasikia ni marehemu kweli?), Ibra Radi Washokera ndo ninaowakumbuka kama unakumbka wengine tukumbushane, watunzi wa hadithi pia walikua kina… aah km unakumbuka naomba tunikumbushe!

Jamaa walikuwa wakitoa toleo jipya basi wenye nazo wananunua then sisi wengine tunasubiria kuazima km ni shule basi utaona kikundi cha watu kibao wanasoma gazeti moja au km ni mtaani basi ndio kuazimana na ugomvi tele!natamani km nikusanye nakala za matoleo yale ya zamani!

Je wewe mdau unakumbuka nini katika gazeti la SANI?vipi kuhusu wahusika wake?hadithi na vituko je?




Naikumbuka makala ya 'Jambo limezua jambo'...
Pamoja na kuwa nilikuwa mdogo na makala ile ilikuwa na mabo ya kikubwa nilikuwa naipenda...
 
Kama unalikumbuka kipindi cha mwishoni mwa miaka ya 80 basi pole.
Kipindi hicho lilikuwa limeisha kufa likichorewa na ma bongo fleva kama Ibra.
Mzee, Sani ni la miaka ya mwishoni ya Sabini hadi 1986. baada ya hapo ni makapi tu!
Mchoraji halisi wa Sani alikuwa marehemu Philip Ndunguru.
Huyu ndiye aliyewavumbua kina Lodi Lofa, Dr Love pimbi, Kipepe na Ndumilakuwili.
Ndunguru pia alikuwa anamchora Ndumilakuwili kwenye gazeti la Kenya Leo la Nairobi kule akimuita Kazibure na alikuwa maarufu hadi akatoa kitabu maalum cha Kazibure kilichouzwa kwa maelfu nchini kenya.
Philip Ndunguru pia ndiye aliyekuwa akisanifu majalada ya vitabu vya riwaya vya akina Musiba au Willy Gamba na watunzi wengine.
Mhariri orijino wa Sani ni marehemu Said S Bawji ambaye pia alitunga vitabu kama Usiku wa Balaa, Kisiwa cha Mayuku na A love story between Tanganyika and Zanzibar.
Sani pia lilikuwa na kibonzo cha mlevi Sokomoko kikichorwa na Ted Marealle!
Gazeti hilo pia lilikuwa ndio chimbuko la misemo ya mitaani kama vile, Utajaza, Kisebu sebu na Kiroho papo etc.
Upo hapo mkuu?

Maelezo mazuri, tunashukuru kwa kuweka mabo sawa.
Ila, mashindano ya nini ndugu? Kama mtu amelikuta Sani la miaka ya 80 tatizo liko wapi? mwache aendeleze utamu mahala alikoukutia...
Tena bora huyo aliwahi, mimi nimelisoma kuanzia mwaka 96, na nililifurahia sana.
Sometimes being old does not mean everything in life, pay some respect to your amateur, since they do the same to you
 
Kuliuwa kuna zile hadithi za character mmoja anaitwa chino chino na mwingine anitwa zumo. Yaani enzi hizo kwa kuwa nyumba zenye TV zinahesabika gazeti la Sani iliuwa kama TV screen.
 
Kama unalikumbuka kipindi cha mwishoni mwa miaka ya 80 basi pole.
Kipindi hicho lilikuwa limeisha kufa likichorewa na ma bongo fleva kama Ibra.
Mzee, Sani ni la miaka ya mwishoni ya Sabini hadi 1986. baada ya hapo ni makapi tu!
Mchoraji halisi wa Sani alikuwa marehemu Philip Ndunguru.
Huyu ndiye aliyewavumbua kina Lodi Lofa, Dr Love pimbi, Kipepe na Ndumilakuwili.
Ndunguru pia alikuwa anamchora Ndumilakuwili kwenye gazeti la Kenya Leo la Nairobi kule akimuita Kazibure na alikuwa maarufu hadi akatoa kitabu maalum cha Kazibure kilichouzwa kwa maelfu nchini kenya.
Philip Ndunguru pia ndiye aliyekuwa akisanifu majalada ya vitabu vya riwaya vya akina Musiba au Willy Gamba na watunzi wengine.
Mhariri orijino wa Sani ni marehemu Said S Bawji ambaye pia alitunga vitabu kama Usiku wa Balaa, Kisiwa cha Mayuku na A love story between Tanganyika and Zanzibar.
Sani pia lilikuwa na kibonzo cha mlevi Sokomoko kikichorwa na Ted Marealle!
Gazeti hilo pia lilikuwa ndio chimbuko la misemo ya mitaani kama vile, Utajaza, Kisebu sebu na Kiroho papo etc.
Upo hapo mkuu?

mkuu umenikumbusha mbali sana usiku wa balaa namkumbuka kibibi gula na miujiza yake.hivi vitabu tunaweza kupata kwa ajili ya watoto wetu, maana vina mchango mkubwa sana wa kufundisha kiswahili, watoto wa siku hizi hawajui kiswahili fasaha,mfano kumekuwa na matumizi mabovu ya r na l hata kwenye magazeti haya tusomayo sasa hivi.Na ukitizama vizuri comments zote za uzi huu utagundua kitu,wachangiaji wote hawana shida ya r na l, majarida yale yalisaidia sana kwa kweli.siku hizi kila kitu kimechakachuliwa.
 
Unakumbuka nini kuhusiana na gazeti la sani mwishoni mwa miaka ya themanini na mwazoni mwa miaka ya tisini?

Nimekumbuka enzi zile za gazeti la SANI, jamaa walikuwa wabunifu sana kwa matoleo yao,unamkumbuka kifimbo cheza na misemo mbalimbali(uchafuzi wa lugha?), kipepe na rungu lake, pimbi a.k.a dr. love yeye anatongoza kila demu! ndumila kuwili na wizi wake,aah wapi lodi lofa na kagari kake na kiko yake kitambi kule!madenge na vituko vyake akiwa na matanati yake !kuna mhusika moja hivi alikuwa chapombe sikumbuki alikuwa anaitwa nani vile?sukununu za babu sani je?wapi mechi ya bush star na born town?aah yale mazoezi kabla ya mechi hoiiii!uwanja wa fujo je? Hadithi za picha mambo ya kina Obi, Mzee Ole, Linda n.k ,wachapishaji walikuwa wabunifu kweli kweli, burudani zilizobebwa na wahusika wa kutengeneza lakini wanashambiiana na jamii!ilikuwa burudani sana kweli natamani ijirudie!


Wachoraji wa enzi zile ni kina John Kaduma(nasikia ni marehemu kweli?), Ibra Radi Washokera ndo ninaowakumbuka kama unakumbka wengine tukumbushane, watunzi wa hadithi pia walikua kina… aah km unakumbuka naomba tunikumbushe!

Jamaa walikuwa wakitoa toleo jipya basi wenye nazo wananunua then sisi wengine tunasubiria kuazima km ni shule basi utaona kikundi cha watu kibao wanasoma gazeti moja au km ni mtaani basi ndio kuazimana na ugomvi tele!natamani km nikusanye nakala za matoleo yale ya zamani!

Je wewe mdau unakumbuka nini katika gazeti la SANI?vipi kuhusu wahusika wake?hadithi na vituko je?




kuna mzee meko, mapun'go,Bob mazishi, kobelo, udeze, na wengine wengi ktk timu za mpira kwenye hadithi za picha kulikuwa na obi, mayuku, zumo, linda, chino nk
 
dah..mwishoni mwa miaka ya themanini,..umenikumbusha mbali sana,nakumbuka lodilofa alitaka kupiga sadaka kanisani(kama nakumbuka vizuri)akajifanya anatafsiri kilatin....vova ili kuteliva it is molikuvai...duh,.childhood days pale mitaa ya migomigo life was stupid..i miss them
 
Bila kusahau na lile gazeti la Mzee MEKO? alitoka kijijini kauza mazao yake akaenda town kununua trekta lakini akakutana na watoto wa mjini je mnakumbuka?
 
shule ya msingi nilikuwa kibonge wakanipachika jina la lodi lofa japo sikuwa na vimiguu vyembamba. Mechi za born town na wa bush nilikuwa napenda hasa yale mazoezi yao.
 
Sani lilikuwa jarida la ukweli! Wakati huo bado watanzania ni wajamaa kweli maana gazeti moja linasomwa na kijiji kizima(kwa sie tuliozaliwa vijiji).

Sikuwahi kuona gazeti jipya la sani, sababu yatu wote kusoma kopi moja ilikuwa inazeeka haraka. Nakumbuka kaka zangu waliokuwa wanasoma Dar wakija likizo lazima waje na sani. Fotokopi hazikuwepo watu wa stationary wangefaidi
 
Bila kusahau na lile gazeti la Mzee MEKO? alitoka kijijini kauza mazao yake akaenda town kununua trekta lakini akakutana na watoto wa mjini je mnakumbuka?

Kilikuwa ni kitabu cha hadithi ya michoro.
Bob Mazishi aliibukia humo.
Ni kazi nzuri ya Marehemu Philip Ndunguru
 
Sani lilikuwa jarida la ukweli! Wakati huo bado watanzania ni wajamaa kweli maana gazeti moja linasomwa na kijiji kizima(kwa sie tuliozaliwa vijiji).

Sikuwahi kuona gazeti jipya la sani, sababu yatu wote kusoma kopi moja ilikuwa inazeeka haraka. Nakumbuka kaka zangu waliokuwa wanasoma Dar wakija likizo lazima waje na sani. Fotokopi hazikuwepo watu wa stationary wangefaidi

Mabinti wengi waliolewa kwa kufuata magazeti ya Sani nyumbani kwa manjemba!
Si ajabu some members humu walizaliwa kutokana na Sani
 
na yule aliekua anawinda hapati mawindo kila siku kipepe sijui.
Saivi so wanalitoa lile la juma5 na jumamosi halina hata mpango
 
Mimi nakumbuka hadithi za KIZAIZAI na MAJI MAZITO .kipindi hicho niko shule ya msingi,mwanafunzi akija na gazeti la sani tunamnunulia chipsi dume. Halafu mmesahau mzee mmoja alikuwa akiitwa MWINYI MPEKU KATIKA UPEKUZI. Mzee alikuwa na misemo ya busara sana.
 
Betina na nani yule bonge bonge...simkumbuki, walikuwa watu wa bifu kila wanapokutana..ila betina licha ya kuwa mwembamba alikuwa nammudu vizuri mwenzake bonge bonge
 
Ole kwenye na mzee kifimbo cheza...alikuwa anatembeza bakora mbaya....kwa waliokuwa wanaharibu kiswahili kwa maneno ya mtaani
 
Betina na nani yule bonge bonge...simkumbuki, walikuwa watu wa bifu kila wanapokutana..ila betina licha ya kuwa mwembamba alikuwa nammudu vizuri mwenzake bonge bonge


Bentina na zena hujambo wewe
 
Back
Top Bottom