Unamzungumziaje mchambuzi Geoff Lea

Unamzungumziaje mchambuzi Geoff Lea

Sasa unataka mashabiki ulazimishe wapende na vilabu vingine ?

Timu inapendwa kutokana na performance yake uwanjani na namna inavyovutia mashabiki.

Kama Simba na Yanga zimekamata mashabiki wa nchi nzima hiyo inapaswa zipongezwe kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuvutia mashabiki.
Timu iko nyumbani lakini inazidiwa mashabiki na timu ngeni, uliona wapi hiyo zaidi ya tz?
 
Sasa hilo ni tatizo la Simba/Yanga au ni tatizo la timu mwenyeji kutovutia mashabiki ?
Timu ya nyumbani kuishabikia haihitaji mvuto dhidi ya timu ngeni. Sidhani kama unaweza kuishabikia Argentina ya Messi dhidi ya Tanzania.
 
Ni tatizo la watu wanaojiita mashabiki wakati ni mashabiki uchwara. Mtu wa Namtumbo kuishabikia simba/ yanga dhidi ya Namtumbo united ni ushabiki uchwara.
Unajua kuwa Manchester united ina mashabiki hapa Tanzania ?
 
Unajua kuwa Manchester united ina mashabiki hapa Tanzania ?
Najua hilo ila hoja yangu haiendani na swali lako.Je Man u huwa ina mashabiki kuwazidi Everton , Norwich, West ham hata Brentford inapocheza ugenini? Sipingi yanga/simba kupendwa burundi.
 
Sielewi watu wanaposema ushabiki wa Simba na Yanga unaharibu mpira wa bongo ,leo Simba au Yanga ikicheza na timu yoyote kwenye ligi kunakuwa na mwamko ,Simba na Yanga wana mataji mengi na udhamini mzuri .

Hata timu zingine zimepata udhamini baada ya makampuni kuona mwamko.

Hivi tukisema Simba na Yanga wanaua wanaharibu mpira wa bongo je ni afadhali tuwe kama derby ya Gormahia na Leopards ambao ni derby lakini derby isiyo na mvuto hata wakicheza hakuna anayeweka attention ,Simba na Yanga wakicheza hadi nchi majirani wanakuja kuangalia mechi.Lakini kuna ligi Kama ya Zambia,DStv inaonyesha haina mwamko kila mechi mashabiki hawafiki hata 1000

Mpira wa bongo unaendelea kwa sababu ya Simba na Yanga ,hata utambulisho wa jezi miaka iliyopita ilikuwa siyo big deal kwa timu za bongo,leo hata Ruvu shooting wanazindua na kufanya press ,tuombe vilabu vingine vipate udhamini mnono wanunue wachezaji wazuri ili ligi ya bongo inoge zaidi.
 
Sasa hao waliobaki clouds wana uchambuzi gani zaidi ya unazi wa timu ya yanga tu?
Katika wachambuzi ambao wana uwezo mdogo ni huyu jamaa hua najiuliza anapataje chance za kuchambua kabumbu kwenye hizi radio zetu ila naona clouds FM walimtema maana uchambuzi wake ni hamna kitu
 
Back
Top Bottom