Unapozidishiwa chenji huwa unarudisha au ndio wimbo wa Albert Mangwear "kimya kimya" mwendo wa haraka mbele

Nishawahi kurudisha hizi 1000 au 2000.

Nikipata mtihani mkubwa zaidi labda laki 2 na kuendelea nitaleta mrejesho
 
Nimecheka sana
 
ticha mpumbavu
hawezi kutajirika kwa 18000
 
Mie niliwai kumuambia wakala niwekee elf 7 ye akaweka elf 70 maeneo ya mwenge yangu nilipogeuka tu nilichukua bodaboda chaaap kuelekea Ubungo, hyo pesa iliyozid nikaibetia na ikaliwa Yote
 
Katika mihangaiko ya hapa na pale unaweza kwenda dukani ama sokoni inapotokea muuzaji kakuzidishia 'chenji" unachukua hatua gani!??

Binafsi huwa narudisha
Wewe je? Wafanyabiashara wanapitia changamoto sana
Kuja tajiri flan tunafanya naye biashara sasa alitakiwa kufanya malipo ya tsh laki8 na 50.

Nipo ofisini kwake na kuna watu kadhaa pembeni wanasubiri huduma kanihesabia pesa harakaharaka kaniwekea mezani.

Nilipohesabu nikakuta ni million moja na elf50 nikahesabu zangu laki8 na nusu then nikampa laki2 zake then nikamwambia boss umezidisha pesa imezd laki2.

Boss alishukuru kinoma na wake jamaa wa pembeni wakaanza kunipa maua yangu.

Mpka leo Boss kanipa acc number yake ya bank nikitaka kudepozit naweka tu napeleka slip na hata hakagui namimi hata simuibii nafanya kazi comfortably na najiamini na yeye anasema ananiamin nisije kumuangusha.

Kifupi now naenjoy matunda ya uaminifu wangu.

Nawashauri muwe na utaratibu wa kurudisha pesa mnapozidishiwa kwani kuna faida nyingi sana kuliko hasara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…