Unatumia mbinu gani usipigwe na mafundi kwenye ujenzi?

°Kuwa mwaminifu kwa fundi, mlipe stahiki zake vizuri kwa wakati. Usimpige sana kwenye ufundi(sijui hata unajua kumpiga ni kiaje ila usimpige sana), mlipe vizuri.
°Omba sana upate fundi mwaminifu, maana wapo wachache sana kwa sasa.
°Kuwa na ABCs za ujenzi hatua kwa hatua, walau basi ujue materials, ratio, hesabu za kujumlisha na kutoa.
°Simamia mwenyewe, kuanzia mwanzo hadi mwisho. Usiamini hata ndugu wa damu, unless unataka nae apate walau kidogo kuanza ujenzi wake.
°Fuatilia materials mwenyewe huko dukani, fanya due delegence ya vifaa na bei zake, ikiwezekana maduka tofauti ili upate kilicho bora kwa reasonable price.
°Usikurupuke, nenda step kwa step hasa wale ndugu zangu mnaojengea kwenye karatasi then mnahamishia site huku pesa ikiwepo tayari 100%.
°Wenye maduka wakitaka kumpa fundi asante usione wivu, ndivyo Tanzania inavyoenda. (Mf. Umeenda na fundi kununua mbao, bati nk, akipewa 20k usione wivu).
 
Kuna fundi umeme alinisisitiza kwenda duka flani kununua vifaa vya umeme ,tulivyofika yeye akaniona kama wa kuja mm namchola tu .
Anamwambia muuzaji nipe hiki nipe kile bila kuuliza bei mwisho nikamwambia muuzaji nipe main switch, metal box na conduit pipe vingine sichukui Dili lake likafia pale pale .
Akaenda kufanya kazi Kwa vifaa hivyo nikampa chake nikampiga chini .
 
Safi sana kiongozi
 
Hata Kama ishu Ni kutafuta pesa Kwanza ili tujenge ila sio kwa kunirudisha dukani, yaani ninunue materials alafu yafike site uyakatae?? Unataka material original Kwan nyumba Ni yako, Basi mwenye nyumba nimeyataka haya feki. We Jenga nikulipe pesa yako upite hivi. Hutaki nenda kaibie watu wengine. Labda Kama sikulipi unatoa tu msaada. Ila Hata Kama Ni msaada, mi uwezo wangu Ni huo, unanilazimishaje kununua materials unayoyataka wewe, kwani fundi Ni wewe mwenyewe. Tembea mbele huko mjivuni mkubwa weweeeee, eti Nina maisha yangu mengine. Maisha yako ungeenda kuning'nia kwenye gebo.
 
Hiyo Safi Sana mkuu. Ili usipigwe lazima uwe na ideas ya vifaa na ujenzi kwa ujumla
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mkuu ujue suala la kuiba buana ni kama hulka tu,, nikiwaza kuna mkurugenzi wa halmashauri kafutwa kazi kisa mil 2, kwann mm nsiibe misumali
Sasa unayetaka kumuibia hiyo misumari naye anaitaka misumari yake.😂😂
 
Kupigwa lazima
 
naomba iyo kazi ya wiring ya Umeme nikumalizie kazi
 
Simamia kazi yako, sio tu hofu ya kupigwa bali unahakikisha kazi inafanyika vile unavyotaka na unaridhika......
 
samahani mleta mada nipo nje ya mada kidogo,mimi ni fundi wa kufunga cctv camera,electric fence,gate motor pamoja na video door bell,kwa mwenye kuhitaji huduma naomba tuwasiliane kwa namba 0622667749 au 0674376787 nipo Dar es Salaam
 
Mkuu mimi ukiniambia hivi vifaa avifai mimi siwezi kukubali kirahisi yani ujipange kweli kweli na nikiona unamambo mengi kesho utakuta fundi mwingine huyo site, Huyo uliyekua unamwambi hiyo alikua mgeni wa vitu, Mimi nimenunua sink au Bati uniambie nirudushe, au Nimenunua frem ya Mninga na milango ya Mniga uniambie avifai.
 
Mkuu hakuna namna nyingine ni kusimamia mwenyewe!
Yaani bila hivyo uweke na ziada katika gharama za kujenga za kufidia kupigwa!
 
Kuna sehemu upo mbali wanaosimamia wanapiga simu tu.
Ukiwa mbali ukawaacha waendelee, hilo ni tatizo lako😂
Kama unasafiri si unamsimamisha tu ujenzi
Pia Kuna stage ambazo fundi hawezi kuiba hata usipokuwepo
 
Sifa za kijinga
 
Ukiwa mbali ukawaacha waendelee, hilo ni tatizo lako😂
Kama unasafiri si unamsimamisha tu ujenzi
Pia Kuna stage ambazo fundi hawezi kuiba hata usipokuwepo
Stage Gani hiyo?🙄 Au labda ni Mafundi wa Kuunganisha maji na Umeme. Zingine zote Maumivu tu.
Ila hili jukwaa limenisaidia sana sasahivi naweza kupigia hesabu idadi ya tiles na size kwa vyumba, idadi ya gypsum board , somo la vipimo vya Sqm nililifaidi sana humu, idadi ya tofari kwa kiramani, (nikafanya jaribio kwa Choo kidogo) kwa wazee ika work out. 😂😂
 
Akiwa anachimba msingi hawezi kuiba😂

Umeiva vizuri kwenye makadirio ya materials, maana hiyo ni profession kabisa wenyewe huitwa quantity surveyors

Vipi ile site yetu bado inaendelea au umesimama? 😂
Nataka kuwa inspired na hilo bungalow lako, nami nishushe langu😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…