Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Watatajirika waendelee kusubiri
Kusubiri nini?

Kusubiri hadi lini?

Huyo Yesu hajui wajibu wake kwamba anapaswa kuwapa watu utajiri bila wao kuhangaika kumuomba kila siku?

Au huyo Yesu ni msahaulifu sana hadi akumbushwe kwa kuombwa?

Kuna walokole wamemuomba huyo Yesu miaka nenda rudi na hakuna chochote walichopata wakafa maskini na ukapuku wao.
 
Mtu anasema Sema tu kwakua labda anataka kupata njia ya kwenda huko kutoka kwa wadau😀
Waniulize Mimi,nimewahi kuishi kwenye utajiri wa nguvu za kishirikina na Nina Wajua watu wangu wa karibu ambao wanaishi na utajiri huo!

Lakini pia,binafsi hadi hivi Sasa Nina Wajua watu wawili (wataalamu) ambao wanatoa utajiri wa nguvu za Giza,mmoja yupo Zanzibar na Mwingine yupo Malawi!

Mkuu maisha yangu ni simulizi tosha,sema kwasababu ya wapumbavu wa hapa JF huwa naamua tu kukaa kimya maana ukibishana na mjinga yawezekana ukawa mjinga zaidi yake!

Nimewahi hadi kulala na maiti hapo Malawi ili nifanikiwe na nilifanikiwa sema ndo hivyo maisha yangu yote ya mafanikio wanawake ndo huwa kikwazo kwangu !

Mtu anakuja hapa anabisha hata hajawahi Kutembea popote zaidi ya kutoka Mbeya kuja Dar au kutoka Dar kwenda Arusha !

Sihitaji kuuliza Kwa mtu Mimi mwenyewe ndiye ushuhuda !

Kama watabisha ngoja waendelee kubisha but for now Sina muda wa kubishana na Abharisya!
 
Ubongo wa binadamu huwa unaweza kufanya hallucinations katika mazingira fulani ikiwemo unapokuwa na njaa iliyopitiliza, uchovu uliopitiliza, ukitumia dawa za kulevya, ukifungiwa mwenyewe mahali muda mrefu, magic tricks au matatizo ya ubongo. Watu wanapouliza wanataka kufahamu ulikuwa na utimamu kiasi gani ili waweze kuipa uzito stahili story yako.
Elimu yako imekulimit kwenye kipengele Cha hallucination Kuna vitu vingine ni beyond hallucination ndio maana Kuna watu wanaona matukio flan kabla hayajatokea. Kuna brain alaf Kuna spirit Kila kimoja kinafanya kazi tofauti.
 
Mojawapo ya story huwa nazisikia sana na mtu kuwatoa watoto wake au ndugu zake kafara ili afanikiwe katika biashara au siasa. Utoaji kafara huwa unaelezewa kwa mtu huyo aliyoetolewa kafara kufariki kwa kinachodhaniwa kifo cha utata au kupatawa matatizo ya akili(kichaa).

Unaweza kuonyeshwa kichaa fulani ukaambiwa huu ni mtambo wa kutengeneza pesa wa tajiri fulani au ndio chanzo cha mafanikio cha mwanasiasa fulani.

Unajuaje au unathibitishaje kwamba fulani amefanikiwa kwa sababu ya kafara ya mtoto, mzazi, mke au ndugu yake?
USILOLIJUA NI SAWA NA KIZA KINENE !
 
Ufalme wa mbinguni haupo.

Habari za ufalme wa mbinguni ni habari za kuwafariji maskini na umaskini wao.

Heaven is the promise for the poor so that they don't demand happiness on earth.

A poor man who has Jesus is richer than the rich man without Jesus. Hivi ndivyo maskini wanafarijiwa na umaskini wao kupitia imani za kidini.

Yani watu maskini choka mbaya wanafarijiwa kwamba watamiliki utajiri wa kutosha mbinguni, Hivyo wasijihangaishe sana kuwekeza duniani.
Ukifa utathibitisha mwenyewe kama huo ufalme upo au haupo. Kuna vitu vingine kuvijadili ni kupoteza muda
 
Siwezi kupoteza muda kukujibu hayo maswali yako sababu mimi na wewe tayari tunaamini vitu viwili tofauti.

Ningekujibu kama ungekua unataka kueleweshwa na sio kushindana
Ila najiuliza swali Moja kwanini watu wengi ambao inasemekana wana utajiri wa kichawi, hawana utajiri mkubwa wa kumfikia bakhresa, mo dewji au hata Reginald Mengi 🤔 wengi utakuta Wana vighorofa viwili mjini, ndo utajiri wa kichawi huo ephen_
 
Mimi namjua mmoja alikua rafiki wa mama yangu utajiri wake ni wa kutumia nyota za wafanyakazi wake
Ila ilipofika mwaka 2018 ikabidi amtoe mtoto wake na akafanya hivyo

Ashawahi kumshawishi mama yangu ajiunge huko mama akakimbia nduki na urafiki ukaisha.

Alikuja dar kama housegirl kutoka Upareni ila sasa hivi ni tajiri.

Kwa hiyo kila mwenye matatizo ya akili ni chambo? Wewe ulijuaje?
Naomba umpinge na ephen.
 
Ila najiuliza swali Moja kwanini watu wengi ambao inasemekana wana utajiri wa kichawi, hawana utajiri mkubwa wa kumfikia bakhresa, mo dewji au hata Reginald Mengi 🤔 wengi utakuta Wana vighorofa viwili mjini, ndo utajiri wa kichawi huo ephen_
Watu weusi hawana roho ngumu kuliko hao waarabu na wahindi
 
Back
Top Bottom