Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Dunia hii kuna elimu kubwa zaidi ya elimu hii ya mashuleni na vyuoni. Kuna elimu inaitwa science beyond material ambayo ndiyo inaweza kuelezea mambo ya uchawi, freemason nk.
Ni kweli mkuu kuna kitabu kimoja nimekisahau jina nasikia ukikisoma lazima uchizike ni cha waturuki huko.
 
Huyo mama ni tajiri kabla ya kugundua pesa zake ni za madawa nilienda kukaa likizo kwake.
Hilo jumba la kifahari nilijihisi mtoto wa mfalme nikapewa chumba ghorofani kipo full kuanzia tv mpaka friji.

Kuna watu wanaishi kama wapo mbele vilee halafu kazi yake anayoifanya nikisema inachekesha

Niishie hapa labda yupo humu asije akaona akaunga dots usiku akanifata buree
Inawezekana anafanya kazi chafu pia kama za dawa za kulevya, utakatishaji fedha za wakubwa, magendo ya madini n.k Kwa nini ukimbilie moja kwa moja kuhisi ni ushirikina bila kufikiria haya mengine?
 
Inawezekana anafanya kazi chafu pia kama za dawa za kulevya, utakatishaji fedha za wakubwa, magendo ya madini n.k Kwa nini ukimbilie moja kwa moja kuhisi ni ushirikina bila kufikiria haya mengine?
Sasa nimuamini yeye au wewe?

Yeye alimuonea huruma mama yangu kama rafiki yake wa karibu akaamua ampe siri ya utajiri wake ili rafiki yake nae awe tajiri
Tena akamwambia ana mawazo sababu ameambiwa atoe kafara ya kijana wake aliyekua Canada chuo mwaka wa mwisho na kweli kijana akafa baada ya muda mchache karudishwa Tz akiwa Maiti
Lakini mama yangu akakataa
 
Mojawapo ya story huwa nazisikia sana na mtu kuwatoa watoto wake au ndugu zake kafara ili afanikiwe katika biashara au siasa. Utoaji kafara huwa unaelezewa kwa mtu huyo aliyoetolewa kafara kufariki kwa kinachodhaniwa kifo cha utata au kupatawa matatizo ya akili(kichaa).

Unaweza kuonyeshwa kichaa fulani ukaambiwa huu ni mtambo wa kutengeneza pesa wa tajiri fulani au ndio chanzo cha mafanikio cha mwanasiasa fulani.

Unajuaje au unathibitishaje kwamba fulani amefanikiwa kwa sababu ya kafara ya mtoto, mzazi, mke au ndugu yake?


Haya tena kwa anayetaka kubadilisha karatasi kuwa ni pesa anione mimi kwa wakati wake ili nimpe ujanja wa kuweza kupata pesa.
 
Kutafuta Uthibitisho Katika Inshu Za Mambo Ya Kiroho Inahitaji Juhudi.Kwa Mfano Mtu Anaweza Akawa Mchawi na Ni Kweli Mchawi Kweli Kweli Lakini Hauwezi Kuthibitisha Kirahisi.Mambo Ya Kiroho Ni Mambo Ya Sirini.
Kuna Siku Kwa Macho Yangu Naked Kabisa Nlishuhudia Mchawi Namuangalia Ananiangalia.Mwaka 2013 Hiyo Magomeni
Na ukieleza watu pia uliwahi kumuona mchawi bado kuna watakaosema umechanganyikiwa,wengine watasema ulikuwa na njaa,nina kubaliana na wewe kuwa mambo ya kiroho ni magumu kuyathititisha ni mpaka na wewe uwe kiroho zaidi...
 
Mimi namjua mmoja alikua rafiki wa mama yangu utajiri wake ni wa kutumia nyota za wafanyakazi wake
Nyota ni nini?

Ulijuaje na ulithibitisha vipi huo utajiri wa huyo mama ulipatikana kwa nyota za wafanyakazi wenzake?

Na ni kivipi?
Ila ilipofika mwaka 2018 ikabidi amtoe mtoto wake na akafanya hivyo
Alimtoa mtoto wake kwa nani?

Na huyo mtoto alifariki kwa namna gani?

Je baada ya huyo mtoto kutolewa, utajiri wa huyo mama uliongezeka kwa kiasi gani?

Na je una uthibitisho wa jinsi mali zilivyo ongezeka kabla ya mtoto kutolewa na baada ya mtoto kutolewa?

Tufanye ulinganisho wa mali kabla ya mtoto kutolewa na baada ya mtoto kutolewa.
Ashawahi kumshawishi mama yangu ajiunge huko mama akakimbia nduki na urafiki ukaisha.
Ajiunge huko wapi?

Sehemu gani?

Kwa nani?

Huko kwa kujiunga, Huyo anayeunga watu kwenye huo utajiri, Yeye ana utajiri wa namna gani?

Au ni mtu tu amekaa kwenye kibanda cha nyasi anawalaghai anaweza kuwapa utajiri?
Alikuja dar kama housegirl kutoka Upareni ila sasa hivi ni tajiri.
 
Nyota ni nini?

Ulijuaje na ulithibitisha vipi huo utajiri wa huyo mama ulipatikana kwa nyota za wafanyakazi wenzake?

Na ni kivipi?

Alimtoa mtoto wake kwa nani?

Na huyo mtoto alifariki kwa namna gani?

Je baada ya huyo mtoto kutolewa, utajiri wa huyo mama uliongezeka kwa kiasi gani?

Na je una uthibitisho wa jinsi mali zilivyo ongezeka kabla ya mtoto kutolewa na baada ya mtoto kutolewa?

Tufanye ulinganisho wa mali kabla ya mtoto kutolewa na baada ya mtoto kutolewa.

Ajiunge huko wapi?

Sehemu gani?

Kwa nani?

Huko kwa kujiunga, Huyo anayeunga watu kwenye huo utajiri, Yeye ana utajiri wa namna gani?

Au ni mtu tu amekaa kwenye kibanda cha nyasi anawalaghai anaweza kuwapa utajiri?
Siwezi kupoteza muda kukujibu hayo maswali yako sababu mimi na wewe tayari tunaamini vitu viwili tofauti.

Ningekujibu kama ungekua unataka kueleweshwa na sio kushindana
 
Ndugu yangu haya mabo yapo omba Mungu akuhepushilie mbali unaweza kutolewa kafara wewe..
Yapo wapi?

Na unathibitisha vipi yapo?

Au ni stori za kusimuliwa.

Wewe kama wewe Ulishawahi kufanya hayo mambo?

Eleza kwa ushahidi na uthibitisho mambo hayo yalivyo.
 
Utaamini siku nikikufanya msukule wa kufanikisha miradi yangu ,taja jina lako kamili nikunyooshe uwe msukule wangu ili uamini kwamba uchawi na kafara vipo
Kwa nini usiwe na misukule ya kutosha ikufanyie kazi uwe tajiri mkubwa nchini Tanzania Walau umzidi Bakhressa?

Kwa nini usiutumie huo uchawi kwa nguvu zako zote uwe tajiri mkubwa hapa nchini?

Toa kafara za kutosha ikiwezekana hata ukoo wako wote, Tuone kama utaweza hata kumzidi Dangote.
 
Ukiwa tajiri Africa hakikisha ndugu zako, HAWAUMWI, HAWAFI, pia WANAFANIKIWA,....vinginevyo utaambiwa UNAWAROGA, UNAWATOA KAFARA na KUWAIBIA NYOTA,....shity mindset 🚮🚮🚮
Ila mkuu kwa nini utajirike mwenyewe halafu ndugu zako wengine ni masikini na wanakufa vifo tata ? Halafu wakifa au wakichanganyiwa ndio utajiri wako unazidi kuongezeka
 
I did it and I made it .

Huwa nashangaa MTU anapokubali kuwa masikini while kuna njia nyingi za kufanikiwa.

Altar
Sacrifice

Is real .

Majengo yote marefu yamejengwa na damu za WATU .

Kinachowakwamisha WATU ni ile kutoelewa code
Wewe mwenye kuelewa hizo code, umezitumia vipi kukupa utajiri?

Hizo code zinaweza kukufanya uwe tajiri mkubwa hapa Afrika kama Dangote?

Toa kafara za kutosha, mwaga damu ya kutosha ukiweza hata za ukoo wako wote.

Ukifanikiwa kumzidi Elon musk tukasikia kweli wewe ndio tajiri mkubwa duniani, Ndio tutajua kwamba kweli ukitoa kafara unafanikiwa.
 
Na ukieleza watu pia uliwahi kumuona mchawi bado kuna watakaosema umechanganyikiwa,wengine watasema ulikuwa na njaa,nina kubaliana na wewe kuwa mambo ya kiroho ni magumu kuyathititisha ni mpaka na wewe uwe kiroho zaidi...
Ubongo wa binadamu huwa unaweza kufanya hallucinations katika mazingira fulani ikiwemo unapokuwa na njaa iliyopitiliza, uchovu uliopitiliza, ukitumia dawa za kulevya, ukifungiwa mwenyewe mahali muda mrefu, magic tricks au matatizo ya ubongo. Watu wanapouliza wanataka kufahamu ulikuwa na utimamu kiasi gani ili waweze kuipa uzito stahili story yako.
 
Siwezi kupoteza muda kukujibu hayo maswali yako sababu mimi na wewe tayari tunaamini vitu viwili tofauti.

Ningekujibu kama ungekua unataka kueleweshwa na sio kushindana
Ndio utoe maelezo ya kueleweka. Tuelewe.

Sasa tuta hakikisha vipi hichi unacho eleza ni ukweli?
 
Sasa nimuamini yeye au wewe?

Yeye alimuonea huruma mama yangu kama rafiki yake wa karibu akaamua ampe siri ya utajiri wake ili rafiki yake nae awe tajiri
Tena akamwambia ana mawazo sababu ameambiwa atoe kafara ya kijana wake aliyekua Canada chuo mwaka wa mwisho na kweli kijana akafa baada ya muda mchache karudishwa Tz akiwa Maiti
Lakini mama yangu akakataa
Ilibidi kufahamu kama kijana wake hakuwa na ugonjwa au tatizo lolote ambapo asingekuwa na muda mrefu wa kuishi na mganga akapitia humo, ilibidi kufahamu kama huyo kijana hakuja likizo au haketembelewa huko Canada halafu akapewa kitu kutoka kwa mganga ambacho kingeweza kuwa sumu, mambo yanaweza kuwa mengi.
 
Back
Top Bottom